Sunday, September 28, 2014

YANGA ‘WAKITAITIWA’ SAFU YA KIUNGO..JAJA ATAISHIA KUZUNGUKA TU!

Jaja akipambana

Jaja alishindwa kufunga dhidi ya Mtibwa na kwa bahati mbaya alikosa mkwaju wa penalti
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
0712461976
YANGA SC wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kufungwa 2-0 katika mechi ya ufunguzi wa ligi kuu soka Tanzania bara, septemba 20 mwaka huu uwanja wa Jamhuri Morogoro dhidi ya Mtibwa Sugar, leo jioni wanaikaribisha Tanzania Prisons katika mtanange wa raundi ya pili uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
Prisons wanaingia katika mechi hiyo wakiwa na kumbukumbu ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting waliopata katika mechi ya ufunguzi iliyopigwa wikiendi ya septemba 20 mwaka huu uwanja wa Mabatini, Mlandizi, mkoani Pwani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Kocha mkuu wa Yanga, Mbrazil, Marcio Maximo bila shaka atatumia mbinu ya kushambulia zaidi kwa lengo la kufunga mabao mengi, lakini akijaza viungo wengi  kwa ajili ya kujilinda.
Maximo hupendelea kuchezesha viungo wengi na kumsimamisha mshambuliaji wa Kibrazil, Genilson Santos Santana ‘Jaja’. Ni kocha ambaye huwa hahitaji mabao mengi, anapenda kufunga goli moja au mawili, halafu anaimarisha ulinzi ili kuvuna pointi tatu.
Habari njema kwa mashabiki wa Yanga ni kwamba washambuliaji wawili, Mtanzania, Jerryson John Tegete na Andrey Coutinho wamerejea baada ya kushindwa kucheza mechi iliyopita kwasababu ya majeruhi.
Coutinho kipenzi cha mashabiki wa Yanga ana asilimia ‘200’ za kuanza katika mechi ya leo kuliko Tegete na maana yake atacheza nyuma ya Jaja.
Kutokana na aina ya uchezaji wake, amekuwa mwiba kwa mabeki wa timu pinzani kwasababu ana vitu vingi. Anaweza kupiga chenga, anamiliki mpira, anapiga pasi za mwisho, ana mashuti ya mbali na kasi nzuri.
Coutinho (kulia) yako fiti kuivaa Prisons leo
Itakuwa mechi yake ya kwanza ya ligi kuu, lakini alishaonesha uwezo mzuri kwenye mechi za kirafiki wakati wa maandalizi ya kabla ya msimu.
Kama ataendelea kuwa katika ubora wake, mabeki wa Prisons wanatakiwa kujipanga kuhakikisha hawampi nafasi ya kucheza atakavyo. Wakimuachia, anaweza kuwafunga au kumtengenezea nafasi Jaja.
Jaja alianza msimu kwa kufunga mabao mawili kwenye mechi ya ngao ya jamii dhidi ya Azam fc Yanga ikishinda 3-0 . Alitukuzwa na mashabiki wa Yanga na kugeuka kuwa habari ya mjini. Lakini hakufanikiwa kufunga kwenye mechi ya ufunguzi dhidi ya Mtibwa Sugar.
Kwa bahati  mbaya zaidi alikosa penalti katika mechi hiyo, hivyo leo anahitaji kufuta makosa hayo na kurudisha imani kwa mashabiki wa Yanga.
Jaja ataingia uwanjani akiwa na wazo moja tu la kutikisa nyavu. Uchezaji wake haukubaliki kwa mashabiki wa Yanga, lakini mabao mawili aliyoifunga Azam yalimpa sifa kubwa, hususani goli la pili ambalo alipiga mpira kiufundi mno.
Jaja anacheza ‘kivivu’,  hana uwezo wa kupiga rangi mpira,sio mkali wa kumiliki mpira, Jaja hana kasi uwanjani, lakini ni mtu hatari sana anapofika golini kama atapigiwa pasi za mwisho.
Katika mechi ya Mtibwa Sugar, hukugusa sana mpira, lakini pasi nne alizopigiwa almanusura afunge magoli. Tatu alipiga vichwa vya hatari, lakini kipa wa Mtibwa, Said Mohammed aliendelea kuwa katika ubora wa kuokoa hatari hizo.
Moja alifunga goli, lakini mwamuzi alikataa akidai nahodha wa Mtibwa, Shaaban Nditi alishika kwa mkono mpira kabla na akatoa penalti ambayo Mbrazil huyo alikosa. Kwa takwimu hizo, unaweza kuona jinsi gani Jaja anaona lango na anajua kujipanga maeneo sahihi.
Tegete (kushoto) amerejea tayari kwa kuanza kazi
Kama Prisons wanahitaji kushinda leo au kutoa sare, wanahitaji kuzuia mipira ya Yanga kuanzia katikati.
Uhai wa Jaja unatokana na viungo wa kati na pembeni. Kama Mrisho Ngassa ataanza winga ya kushoto na Saimon Msuva winga ya kulia, halafu kiungo mchezeshaji akaanza Haruna Niyonzima na kiungo mshambuliaji (namba 10 ) akaanza Coutinho na bahati mbaya wakawa katika kiwango chao, nina uhakika Jaja atafunga.
Bila shaka Mbuyu Twite atacheza nafasi ya kiungo wa ulinzi, yaani mbele kidogo ya Yondani na Cannavaro. Nyota huyu amekuwa akifanya vizuri eneo hili na mipira mirefu inayorusha, inawasaidia sana Yanga kutengeneza hatari kwa wapinzani.
Yanga wamekuwa bora zaidi katikati japokuwa staili ya uchezaji wa Niyonzima imebaki kuwa ile ile. Anapenda kugeuka na kupiga pasi za nyuma , anapenda kupiga chenga na wakati fulani hupunguza kasi ya kupanga mashambuliaji.
Niyonzima ndivyo alivyo, kumbadilisha sio rahisi, lakini ni mtu anayeweza kupiga pasi nzuri na zikafika maeneo sahihi. Kama hatachungwa leo, anaweza kutengeneza hatari kubwa kwani anaweza kuwapa mipira mizuri akina Ngassa, Msuva, na Coutinho ambao watampa pasi za mwisho au krosi nzuri mshambuliaji wa kati, Jaja au kufunga wenyewe.
Mrisho Ngassa (kulia) ni mtu hatari sana na anapaswa kuchungwa na Prisons
Prisons wanatakiwa kuja na mpango mkakati wa kuzuia mipira yote ya katikati. Staili ninayoona inaweza kuwasaidia ni kutowafanya Yanga wawe huru kucheza mpira wao.
Wanatakiwa kukaba mtu kwa mtu na kurudi wengi nyuma kama timu. Haitawafaa kupaki basi, lakini timu inatakiwa kukaba kwa pamoja.
Wakipoteza mpira wanatakiwa kurudi wote nyuma ili kuweka ngome imara ya ulinzi. Kama wataamua kupaki basi moja kwa moja itakuwa hatari zaidi kwao kwasababu watawaruhusu Yanga kukaa zaidi katika eneo lao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Ikitokea hivyo, watashambuliwa sana na wanaweza kujikuta wanapoteza umakini na hatimaye kufungwa magoli mengi.
Prisons wana marali kubwa baada ya kushinda 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting
Mfumo wa kujilinda na kushambulia kwa kushitukiza unaweza kuwasaidia zaidi Prisons. Lakini kama wataingia na mfumo wa kucheza mpira wa wazi (open football), naamini itakuwa ngumu kwao kutokana na mazingira halisi ya Yanga.
Nina uhakika Yanga watapiga mpira mwingi na wana hasira za kuanza vibaya, watashambulia sana, lakini hiyo itakuwa faida kwa Prisons kama watatumia mashambulizi ya kushitukiza.
Kama watapiga mipira mirefu inaweza kuwasaidia kwasababu Yanga wana tatizo la kujisahau. Kama wana mpira basi wanauchezea sana, lakini wakipokonywa na kukimbizwa kwa mipira mirefu, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Yondani wanajikuta katika wakati mgumu. (kumbuka mechi na Mtibwa).
Inawezekana Maximo amerekebisha tatizo hilo, lakini mpira wa miguu ni mchezo wa makosa, wanaweza kufanya makosa tena. Hivyo Prisons wajiandae.
Mpira umebadilika, timu yoyote inaweza kupata matokeo nyumbani na ugenini.
Prisons walishinda ugenini dhidi ya timu ngumu ya Ruvu Shooting. Hii imewaongezea morali kubwa . Wanaweza kushindana na kupata matokeo mazuri.
Polisi Morogoro  walicheza vizuri mno jana. Waliinyanyasa Simba hususani kipindi cha pili na kuambulia sare ya 1-1. Wengi waliwachukulia poa, lakini wakaonesha kuwa wanaweza kufanya lolote.
Hata Prisons ambao ni wakongwe na ligi kuu wanaweza kuwazuia Yanga leo, lakini itawabidi wafanye kazi ya ziada.
Hata historia inawahukumu wanapocheza na Yanga uwanja wa Taifa. Mechi mbili za mwisho walifungwa 3-1 na 5-0.
Licha ya kufungwa, hawakucheza kabisa mpira. Lakini sahizi wamejijenga upya chini ya kocha David Mwamwaja. Wana morali kubwa, wana wachezaji mchanganyiko, nadhani wanaweza kutoa changamoto.
Yanga wanaweza kuifunga Prisons, lakini ikitokea sare au kufungwa wasishangae. Ni matokeo yanayoweza kutokea kabisa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...