Wednesday, April 24, 2013

BINTI ANUSURIKA KUBAKWA BAADA YA KUKATIZA MITAA YA SINZA AKIWA AMEVAA KIMINI

Wanawake ambao majina yao hayakupatikana, wakazi wa Sinza, Dar es Salaam wamekumbana na sekeseke  la aina yake la ubakaji kisa kikiwa ni uvaaji wa vimini ambao kwa sasa umeshika kasi kila kona Bongo...
Mwanahabari wetu mwishoni mwa wiki iliyopita usiku wa manane, alinyetishiwa tukio la wanawake watatu kuvamiwa na midume na kufanyiwa kitu mbaya baada ya  kuchaniwa vimini vyao maeneo ya Barabara ya Shekilango, Dar kabla ya kuokolewa na wasamaria wema.
Wasichana hao, wakiwa wamejipodoa vilivyo na kutinga vimini vilivyoonesha sawia maungo yao nyeti bila ‘makufuli’, walijikuta  katika hali hiyo mbaya baada ya kurushiana maneno na vijana hao wahuni hivyo wakaonja joto ya jiwe.

Warembo hao ambao walikuwa wakitokea Sinza kuelekea Manzese, Dar walivamiwa na vijana hao ambao wengi wao ni waendesha  pikipiki maarufu kama bodaboda,  walipokaribia Makutano ya Barabara ya Shekilango na Morogoro, Dar.

“Kila siku wanapita hapa wakiwa nusu utupu, sasa leo tumewakomesha, serikali inatangaza Ukimwi ni hatari, wao hawajali,  wanatutia majaribuni,” alisikika akisema mwendesha bodaboda mmoja ambaye alikuwa miongoni mwa waliowavamia wasichana
hao.

Mwendesha bodaboda mwingine alimwambia  mwandishi wetu  kuwa waliwaeleza wasichana hao kuacha tabia ya kutembea nusu utupu kwani ni hatari kwa maisha yao na ni kinyume cha maadili ya Watanzania lakini walijifanya jeuri ndiyo maana wakawaadabisha.
Aliweka wazi kuwa baada ya kuelezwa hivyo akina dada hao hawakufurahishwa na maneno hayo na badala yake
wakawaporomoshea matusi mazito madereva hao, hali iliyowafanya wapandwe na hasira.
“Madereva wale baada ya kusikia wakitukanwa waliwavamia wasichana hao na kuanza kuwachania nguo kwa maelezo kwamba badala ya kuwa nusu utupu, ni vema wakakaa uchi wa mnyama kabisa.

“Warembo wawili walifanikiwa kutimua mbio licha ya kuchaniwa vimini vyao lakini mmoja aliyekuwa na ‘mdomo mchafu’ 

“Shukrani ziwaendee wasamaria wema waliomukoa kwa sababu kwa vyovyote lazima angebakwa kwani alikuwa  ameshachaniwachaniwa nguo na ku... ,” alisema shuhuda mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake.

Shuhuda huyo aliongeza kuwa binti huyo alifanyiwa kitu mbaya kwa kushikwa sehemu nyeti kabla ya wale wenzake waliokimbia kurudi wakiwa kwenye Bajaj na mabaunsa wao kisha kutokomea na mwenzao aliyekuwa amehenyeshwa vya kutosha na wanaume
hao.

“Wale wasichana wawili walirudi wakiwa na Bajaj na mabaunsa, wakasaidiwa na raia wema ndipo wakafanikiwa kumuokoa  mwenzao na kutokomea naye kusikojulikana,” alisema shuhuda huyo.

Credit: GPL

SUALA LA JUMA NATURE KUTIMULIWA CHANNEL 5 ALIPOINGIA NA NDALA LACHUKUA SURA MPYA ....


Kitendo cha mtangazaji wa EATV Sam Misago kumtoa nje ya studio Sir Juma Nature weekend iliyopita baada ya kwenda studio kwenye kipindi cha Saturday Night Live akiwa na ndala na kaoshi, hajakichukulia poa staa huyo.
  
Licha ya kuwasilisha malalamiko yake kwenye Facebook kutokana na kitendo hicho, Nature hajaishia hapo na sasa amemchana mtangazaji wa kipindi hicho kwenye wimbo mpya wa TMK Halisi, Fitina.
Katika wimbo huo Nature anachana, “Halafu watu wengine sijui wanakuwaga ni mapimbi, eti msanii kaingia studio na ndala na amevaa pensi hakujua anayosema kwenye Facebook na Twitter sijui kisa hela alizopewa na mameneja feki wasiopenda wa Uswazi, mzomeeni huyo, sasa kazi kwake na raia wake.”

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 24.04.2013

.
.
.
.
.
.

Mdogo wa Wema aibukia Redds Miss Hai.

WAREMBO 14 kutoka vitongoji vitano vya wilaya za Siha na Hai, Kilimanjaro, akiwemo mdogo wake Wema Sepetu, wamejitokeza kushiriki shindano la kumsaka mrembo wa Hai, ‘Redds Miss Hai 2013.
Shindano hilo linalotarajiwa kulindima Hoteli ya Snow View Bomang’ombe Hai, Ijumaa.Akizungumza mjini hapa jana, muandaaji wa mashindano hayo, Grace 

Mmari, kupitia kampuni ya ulinzi ya FEM ya jijini Arusha, alisema maandalizi ya mashindano hayo yamekamilika na tayari warembo hao wako kambini kwa wiki mbili sasa katika hoteli ya Sinza B.

Alisema warembo hao wamepatikana kutoka vitongoji vya Kwa Sadala, Bomang’ombe, Sanya Juu, Machame na KIA, ambao wana vigezo vyote huku akitamba mwaka huu, Mrembo wa Tanzania atatoka wilaya ya Hai.

“Warembo wangu ni wazuri, warefu, wanajiamini na wana uwezo wa kuwakilisha vyema wilaya ya Hai, mkoa wa Kilimanjaro na hata taifa, kwa kuwa tunao kina Wolper wengine hapa na kina Sepetu wapo pia,“ alisema.

Alisema miongoni mwa warembo waliojitokeza kushiriki shindano hilo ni pamoja na mdogo wa mrembo wa zamani wa Miss Tanzania (2006), Wema Sepetu, Weru Sepetu, ambaye alidai kuwa huenda akafuata nyayo za dada yake.

Aliwataja warembo watakaoshiriki shindano hilo kuwa ni Sharon Abdalah, Zena Ally, Ivony Steven, na Winny Shayo wanaotoka Machame na Sanya Juu.
Wengine ni Julieth Kimaro, Rehema John, Mary Chemponda, Catherine Leonard na Modesta Joseph.

Mmari alisema shindano hilo litapambwa na msanii wa muziki wa kizazi kipya, Rich Mavoko pamoja na Jambo Squad, ambako mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Novatus Makunga.

Kwa upande wake, mwalimu wa warembo hao, Evameri Gamba, alisema warembo wanaendelea na mazoezi ya mwisho pamoja na kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii, ikiwemo uoteshaji wa miti na kutembelea wagonjwa katika hospitali ya wilaya ya Hai.
Shindano hilo linafanyika kwa mara ya pili sasa, huku wadhamini wakiwa ni TBL kupitia kinywaji chake cha Redds, Fem Security, Bonite Bottlers, Snow View Hotel, Panone pamoja migodi ya madini ya Anglo America Mining na Manga Germ.

Zitto Kabwe atoa majibu kwa Umma kuhusu Habari za mama yake Mzazi Bi. Shida kuvamiwa na kutishiwa bastola.


Mh.Zitto Kabwe.
Nimekuwa naulizwa kuhusu Habari za mama yangu Mzazi Bi. Shida kuvamiwa na kutishiwa bastola. Nawajibu watu Kwa ujumla kwamba 
“Moja, mie sio msemaji wa familia. Ni basi tu katika watoto wa mama yetu mie najulikana zaidi na hivyo mama anaitwa Mama Zitto. Kwetu Kigoma haitwi hivyo, ama Ni mama Salum au mama Lulu. 
Pili, hili Ni suala la polisi. Lipo polisi na linashughulikiwa na polisi. Nisingependa kulisemea wakati Ni suala linalochunguzwa na polisi. Mama yangu Ni mama wa kawaida wa kitanzania kama mama mwingine yeyote yule. Matukio ya namna hii yamezagaa nchi nzima. Hivyo suala lake litashughulikiwa kama yanavyoshughulikiwa masuala mengine yote ya Watanzania. Polisi wakimaliza uchunguzi wao naamini hatua mwafaka zitachukuliwa. 
Ushauri- tuwe makini na “Agente provocatuers” au in English “provocation agents” nyakati kama hizi. Calmness is the best protection against provocations. Nadhani mmenipata”
Nawatakia Kila la kheri katika kazi za ujenzi wa Taifa letu na kuimarisha Umoja na mshikamano wa Watanzania dhidi ya ufisadi, umasikini na ugandamizaji.
Majibu haya  ameandika kupitia mtandao wa Kijamii wa facebook.

POMBE YAMTOA MADEE...ANADAI IMEMPA HESHIMA KUBWA MTAANI......!!


Msanii wa Kundi la Tip Top Connection, Madee au Rais wa Manzese ameeleza kuwa wimbo wake wa Nani Kamwaga Pombe Yangu umempa heshima kubwa.
  
Akiongea  na  mwandishi  wetu, Madee, ambaye jina lake halisi ni Hamad Ally Seneda alisema licha ya kupata shoo nyingi, lakini pia ni wimbo ambao unapigwa sana kwenye klabu mbalimbali na kila unapopigwa hakuna anayekaa kitini.
Alisema kuwa kufuatia kutoa wimbo huo ameshakusanya Shilingi 16 milioni.
Alisema pamoja na kupata fedha nyingi kupitia wimbo huo bado hajaamua azifanyie nini ila ameamua atulie kwanza akitafakari nini kinafuata.
“Wimbo bado upo juu na unafanya vizuri, hivyo ninachofanya kwa sasa ni kuendelea kukusanya fedha kutokana na shoo ambazo nitapata kutoka kwenye wimbo huo baada ya hapo ndio nitajua nifanyie nini,” alieleza.
Aidha, Madee alisema kuwa anafurahi kuona amefanya kitu ambacho kila mpenda burudani kinamfurahisha kwani sio wasanii wengi ambao wanaweza kufanya kitu kama hicho hasa kwa wale waliopo kwenye usanii kwa muda mrefu. Kalunde Jamal

Tuesday, April 23, 2013

RAIS KIKWETE AKUTANA NA VIONGOZI WA MADHEHEBU MBALIMBALI YA KIKRISTO LEO IKULU

 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mkutano na viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini ya Kikristo alipokutana nao leo April 23, 2013 Ikulu jijini Dar es salaam katika kukutana na makundi mbalimbali ya kidini ili kuondoa changamoto za kiimani zilizojitokeza nchini hivi karibuni.
 Raisi akiwa katika picha ya Pamoja na viongozi wa dini mbalimbali
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini ya Kikristo alipokutana nao leo April 23, 2013 Ikulu jijini Dar es salaam katika kukutana na makundi mbalimbali ya kidini ili kuondoa changamoto za kiimani zilizojitokeza nchini hivi karibuni.
PICHA NA IKULU

HII NDIO STYLE MPYA YA NYWELE YA TUNDA MAN

Msanii kutoka kundi la Tip Top Connection maarufu kama Tunda Manameonekana kubadili muonekano wake wa zamani na sasa kuja na mpya ....

Muonekano huo mpya wa style ya nywele zake [pichani] umeonekana kuwashangaza watu kwa jinsi ulivyokuwa wa kipekee ...

Haijafahamika ameutoa wapi na ni kwa ajili gani anautumia, ila hivi ndivyo anavyoonekana sasa Tunda Man kichwani kwake ...

MCHINA AJA NA SIMU MPYA INAYOCHAJIWA KWA SODA

HII NDO SIM INAYOCHAJIWA KWAKUTUMIA SODA YA COCA COLA

Wanasema hii dunia kilichoshindikana ni kumtengeneza binadamu peke yake, kuna vitu vingine ni ngumu kuamini lakini ni ukweli vimetokea, hiyo ni simu ambayo chaji yake inatokana na soda ya Cocacola.

MAAFANDE WACHEZEA NYETI ZA MTUHUMIWA KWA KISINGIZIO CHA UKAGUZI.......!!

Pengine hizi  ndo  starehe  pekee  wanazozipa  "maafande" hasa  wale  wanahusika  na  ulinzi  wa  mageti.....
Miongoni  mwa  majukumu  yao  ni  "kuwapapasa"   na "kuwashika- shika" watu wanaofika  katika  maeneo  hayo  yenye  ulinzi  mkali  ili  kujiridhisha  kwamba  hawana  silaha  au  kitu  chochote  kibaya....
Kinachoshangaza  zaidi  ni  kitendo  cha mafande   kukomaa  na  nyeti  za  akina  mama  wakati  kuna  sehemu  zingine  kibao  za  mwili  ambazo  walitakiwa  wazikague.....
 
Hata  hivyo, kwa  dunia  ya  leo, ukaguzi  kama  huu  umepitwa  na  wakati  kwa  sababu  kuna  vifaa vingi  sana  vya  kitaalam  ambavyo  vinaweza  kufanya  kazi  hizi  badala  ya  maafande  kushinda  wakicheza  na  makalio  ya  watu.
Sourec Gumzo la Jiji

RAIS MASKINI KULIKO WOTE DUNIANI


NCHI ya Uruguay yenye raia takribani milioni 4, inatajwa kuwa na bahati ya kuwa na Rais asiye na chembe ya tamaa. Hana makuu, kiasi kwamba anatajwa kuwa ndiye Rais masikini zaidi kuwahi kutokea duniani.
Huyu si mwingine, bali ni Jose Mujica, Rais wa sasa wa Uruguay ambaye pia ni Rais wa 40 wa nchi hiyo. Tangu aingie madarakani Machi mosi mwaka 2010, amekuwa akionekana kuwa kiongozi wa tofauti kabisa, tofauti na waliomtangulia.
Mathalan, baada ya kufanikiwa kuishika nchini, hakuwa na tamaa ya kukimbilia Ikulu, yeye alichokifanya ni kuamua kuishi katika makazi yake yaleyale, katika nyumba ya mkewe iliyoko shambani, nje ya Jiji la Montevideo.

Kwa ujumla, anapenda maisha ya kawaida, maisha ya kuwahurumia wengine na kujitahidi kuonesha kwa vitendo.
Ni vigumu kuamini, licha ya kuwa ni Rais wa nchi, amejishusha mno kiasi cha mara kadhaa kuonekana akijichanganya na raia wake katika shughuli za ujenzi wa taifa, ikiwamo ujenzi wa barabara, kulima mashamba ya mfano.

WALIMU WAPIGWA MAWE NA WANAFUNZI WA SHULE YA MIZENGO PINDA KWA MADAI KUWA NI WACHAWI

WANAFUNZI wa shule ya sekondari ya Mizengo Pinda  kata ya Kibaoni  Wilayani Mlele mkoani Katavi, wamemshambulia kwa mawe na matofali mkuu wa shule hiyo na mwalimu wa taaluma na kuharibu jengo la utawala na nyumba za walimu hao baada ya kuwatuhumu walimu hao kuwa ni washirikina.

Kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa katavi, Joseph Myovela, alisema tukio hilo limetokea juzi saa 2:30 usiku shuleni hapo baada ya kuzuka kwa tafrani iliyodumu kwa zaidi ya saa 1:30.

Habari kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa chanzo cha tukio hilo kilitokana na mwanafunzi mmoja aitwaye Jofley Pinda kushikwa na ugonjwa wa mapepo uliomfanya aanguke chini ambapo tukio hilo lilitokea mchana wa saa saba.

Alisema wakati akiwa ameshikwa na mapepo hayo aliwataja Alico Kamyoge (36) ambaye ni Mkuu wa shule hiyo ya sekondari ya Mizengo Pinda na mwalimu wa taaluma Bonifasi Nsalamba (35) kuwa ndio wamemroga ugonjwa huu wa mapepo.

MAKAHABA WAILALAMIKIA POLISI NA KUDAI KUWA IMEWAGEUZA "ATM MASHINE"

Kamanda wa polisi mkoani wa Kinondoni (RPC), Charles Kenyela.

Jeshi la Polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni, limelalamikiwa kwa vitendo vya baadhi ya askari wake kuvamia vyumba vinavyodaiwa kupangwa na watu wanaodaiwa kuwa makahaba (madanguro) na kuwapora fedha, simu na vitu vingine vya thamani nyakati za usiku.

Aidha, askari hao wamedaiwa kuwageuza wanawake hao mashine za kutolea fedha (Atm) ambapo hufika katika vyumba vyao kila baada ya wiki moja na kuwadai fedha kati ya Sh.30,000 na 50,000 kila mmoja kama hongo ili wasiwafikishe polisi.

Malalamiko hayo yametolewa na baadhi ya akina mama wanaoishi eneo la Mwananyamala walipozungumza na NIPASHE baada ya askari hao kukamata wanawake zaidi ya 87.

Kiongozi wa wanawake hao, Judith Rugamwa alidai kuwa, askari hao kutoka vituo vya Oysterbay na Mabatini wamekuwa wakiwanyanyasa kwa kuwapiga, jambo ambalo ni kinyume cha haki zao binadamu.

Upelelezi kesi ya Lwakatare umekamilika - Mkurugenzi

Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini, Issaya Mulungu, amesema upelelezi kuhusu tuhuma za vitendo vya ugaidi zinazomkabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatale na mwenzake Joseph Ludovick umekamilika.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mulungu alisema kwa sasa jalada linaandaliwa kwenda kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya hatua zaidi.

Lwakatare na mwenzake, Ludovick, wanakabiliwa na kesi ya ugaidi, katika Mahakama ya Kisutu.

Watu hao wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kufanya mipango ya kumteka na kutaka kumdhuru kwa sumu, Dennis Msacky.

Kuhusu kesi ya kumwagiwa tindikali Kada wa CCM, Mussa Tesha katika uchaguzi mdogo wa ubunge wa Igunga Septemba 2011, alisema tayari watuhumiwa wawili wamekwishafikishwa mahakamani.

Mulungu alisema kuhusu kuvamiwa, kupigwa na kujeruhiwa kwa Mhariri Mtendaji wa New Habari 2006, Absalom Kibanda, tukio la kutekwa na kujeruhiwa kwa Dk Ulimboka na matukio mengine yaliyotokea Zanzibar, upelelezi bado unaendelea na kwamba upo katika hatua mbalimbali. Aliwataka watu kuwa na subira.

"Lady Jay Dee, mnafiki wa miaka 10, shujaa wa siku 30.....!!" asema Saleh Ally


Imeandikwa na Saleh Ally wa  www.salehjembe.blogspot.com
MGOGORO wa kimuziki kati ya msanii Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’ na kituo kimoja cha redio umezidi kuchukua kasi huku makundi mawili, kila moja likitengeneza ngome yake na kuamini linachoamini.
Kundi ambalo linamuunga mkono Jaydee na kumuona ni mkombozi, anazungumza kwa niaba yake na wasanii wengine, la pili ni lile linalobaki upande unaoshambuliwa, linatetea ngome yake.
Jaydee anashutumu kubaniwa nyimbo zake na kituo hicho ambacho kupitia mitandao kadhaa ya kijamii ameeleza wazi kuwa wanambania, wanaziponda lakini hata watangazaji wake wamekuwa wakionyesha chuki binafsi dhidi yake.
Jaydee pia aliwaponda wasanii Ben Pol na Linah anayetokea THT kwamba walishindwa kutokea kwenye uzinduzi wa video ya wimbo wake wa Joto Hasira, kwa madai walizuiwa na bosi wao.

Samata aziponda Yanga, Simba

Lubumbashi, DR Congo. Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayechezea TP Mazembe ya DR Congo, Mbwana Samata amesema viongozi wa klabu za Tanzania hawana malengo ya kutwaa ubingwa wa Afrika ila wanapigania kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu tu.
Samata alisema hayo wakati alipokuwa akihojiwa na waandishi wa mtandao wa klabu ya TP Mazembe wakati timu hiyo ilipokuwa imeweka kambi mjini Ndola, Zambia kwa ajili ya kujiandaa na mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini.
Alisema,”Viongozi wa klabu kubwa za Tanzania, Simba na Yanga hawana malengo ya kutaka kushinda ubingwa wa Afrika na kucheza mashindano ya FIFA ya klabu bingwa ya dunia, viongozi wanapigania kushinda Ligi Kuu tu.”
Samata alisema,”Viongozi wa TP Mazembe wana malengo ya juu, wapo tofauti na viongozi wa klabu kubwa za Tanzania, ndiyo maana TP Mazembe inakuwa klabu kubwa.
“TP Mazembe haionei wivu klabu nyingine za Afrika, ila zipo klabu nyingi za Afrika zinazoionea wivu, TP Mazembe ina vifaa vyote muhimu vya kuwaandaa wachezaji, ina miundombinu ya soka, ina wafanyakazi wanaoijua soka na ina wachezaji wenye kiwango cha juu,”alisema Samata.
Alisema, “TP Mazembe ina wachezaji nyota kutoka DR Congo, Ghana, Zambia, Tanzania na Uganda, naona faraja kuchezea klabu hii, nataka mwaka huu nitwae ubingwa wa Afrika nikiwa na klabu yangu ya TP Mazembe.
Nataka nicheze mashindano ya FIFA ya Klabu Bingwa ya Dunia, ambapo naweza kucheza dhidi ya Barcelona na kuonyesha uwezo wangu.”
Mwanacnhi

MATUSI YATAISHA BUNGENI ENDAPO SPIKA ATAACHA UPENDELEO"........TUNDU LISSU





Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, amesema fujo zitaisha bungeni ikiwa Spika wa Bunge, Naibu na Wenyeviti watafuata na kusimamia kanuni za Bunge bila kupendelea upande wowote.

Lissu, ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani bungeni, aliyasema jijini Dar es Salaam jana wakati akihojiwa na kituo cha televisheni cha ITV.

Alisema fujo hazitaisha kama watu hawatafuata kanuni na Spika kusimamia na kuzingatia mamlaka yake bila ya upendeleo wowote. 
“Tatizo kubwa Spika anafanya kazi bila kufuata kanuni za Bunge. Kuna mambo mengine anayatolea maamuzi bila kufuata kanuni za Bunge. Mfano suala letu la adhabu tuliyopewa wabunge watano wa Chadema ya kutohudhuria vikao vitano. Hakuna katika kanuni za Bunge. 
Spika alipaswa kupeleka majina yetu katika Kamati ya Maadili ili ichunguze na kupendekeza adhabu kisha ipeleke taarifa bungeni na Bunge ndilo litoe adhabu," alisema.

ZIARA YA KICHAMA YA DKT SHEIN KUTEMBELEA MIKOA YA ZANZIBAR


19
Na Maelezo Zanzibar
Makamo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar Dkt Ali Muhammed Shein amesema kuwa ataendelea kukiimarisha na kukienzi Chama Cha Mapinduzi pamoja na kuulinda Muungano wa Serikali mbili uliopo.
Kauli hiyo ameitoa leo huko katika ukumbi wa CCM Mkoa Amani wakati akizindua ziara yake ya Mikoa mitano ya Zanzibar.
 Dkt Shein ambaye pia ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar amesema kuwa kuna kila sababu ya kukiimarisha chama hicho kutokana na umuhimu wake na kwamba Muungano uliopo wa Serikali mbili ndio njia bora ya kuendeleza mashirikiano ya kidugu yaliyodumu kwa muda mrefu.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 23.04.2013

.
.
.
.

Monday, April 22, 2013

WANAWAKE WATANO WANASWA WAKIGAWA URODA KWA WANAUME WAWILI NDANI YA CHUMBA KIMOJA HUKO MWANANYAMALA

Kwa tukio hili, vijana wa mjini wanasema; kimenuka! Hivi karibuni wanawake watano ambao majina yao hayakuweza kufahamika mara moja walinaswa usiku mnene wakifanya mapenzi na wanaume wawili kwenye chumba kimoja kilichopo Mwananyamala jijini Dar.

Watu hao walinaswa katika oparesheni kabambe iliyoongozwa na Kamanda Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kinondoni, OCD Wilbroad Mtafungwa pamoja na Ofisa wa Oparesheni, Inspekta Jacob Swai.


Katika zoezi hilo, polisi walivamia kambi kuu inayotajwa kusheheni wanawake wanaojiuza iliyopo Mwananyamala A ambapo ‘wauza sukari’ hao hutumia vyumba vyao kufanya ufuska huo.
Polisi hao walipofika kwenye chumba kimoja kilichopo eneo hilo, walikumbana na upinzani mkubwa wa watu waliokuwa ndani na baada ya kufanikiwa kuufungua mlango, waliwakuta wanawake watano na wanaume wawili wakiwa kimahaba.
Mbali na hao, polisi walifanikiwa kuwanasa wanawake wengine kwenye vyumba vyao na baadhi mtaani wakijiuza ambapo walipewa kibano cha hali ya juu.
Imeelezwa kuwa, wanawake hao wamekuwa na tabia ya kujiuza na wakati mwingine hukubali kufanya mapenzi na wanaume zaidi ya mmoja, hali ambayo ni hatari sana.
Mkazi mmoja wa eneo hilo, Husein Juma alisema: “Kwanza tunampongeza Kamanda Mtafungwa kwa operesheni hii, wanawake hawa wamekuwa ni tatizo kwani wamekuwa wakijiuza waziwazi na kutupa ovyo kondomu.
 Naye Inspekta Swai alisema wamekuwa wakipokea malalamiko kutoka kwa wananchi wa eneo hilo wakaona ni vyema kuyafanyia kazi ambapo waliwakamata zaidi ya watu 35, wanawake kwa wanaume wanaohusika.

BI KIDUDE UMEKWENDA, UMEACHA MAJANGA YA WASANII WA KIKE BONGO!, WAJUE BAADHI YAO HAPA

Kishindo cha kuondoka kwako kwenye uso wa dunia tunayoishi kinaweza kuwa kikubwa ama kidogo au hakuna kabisa kutokana na mazingira au heshima uliyojijengea katika jamii.
Fatma Binti Baraka maarufu kwa jina la Bi Kidude aliaga dunia wiki iliyopita akiwa na zaidi ya miaka 100. Bado jina lake linatamkwa kwenye vinywa vya wengi na linaweza kuendelea kutamkwa kwa miaka mingi zaidi.
Bi Kidude, mwanamke shujaa mzaliwa wa Visiwani Zanzibar alileta mapinduzi katika muziki asilia wa mwambao. Aliitangaza Zanzibar, Tanzania na Bara la Afrika sehemu mbalimbali duniani alipokwenda kwa ziara za kimuziki. Inaaminika alifanya kazi hiyo ya muziki, mafunzo ya unyago na biashara ya hina na wanja kwa zaidi ya miaka 90. Katika kipindi chote, Bi Kidude hakushuka kimuziki hadi pale mdomo ulipoanza kuwa mzito kutokana na uzee miaka 10 kabla ya kifo chake Aprili 17, mwaka huu baada ya kuugua maradhi ya kisukari na kongosho kwa muda mrefu.
Pia inaaminika kuwa ndiye msanii mkongwe zaidi aliyekuwa akipanda jukwaani na umri mkubwa ukilinganisha na wengine unaowajua.

Mpango wa bunge kuidhinisha Sheria ya ndoa za jinsia moja Ufaransa wazua kizazaa mjini Paris.

Siku mbili kabla ya bunge la Ufaransa kuidhinisha sheria inayohalalisha ndoa za jinsia moja kumetokea maandamano ya dakika za mwisho mwisho mjini Paris.
Watu wanaopinga sheria hiyo wamekusanyika katika eneo la Montparnasse la mji mkuu katika juhudi za mwisho za kuizuia sheria hiyo, huku maandamano mengine ya kundi hasimu pia yaliandaliwa kuiunga mkono sheria hiyo.
 Zaidi ya watu 100 wamekamatwa katika kipindi cha wiki moja iliyopita katika maandamano mengine ya kupinga ndoa za jinsia moja.
Makundi ya kutetea haki za binadamu pia yameripoti ongezeko la matusi na mashambulizi ya kimwili dhidi ya jamii ya mashoga na wasagaji nchini Ufaransa.
Ufaransa inatarajiwa kuwa nchi ya 14 kuhalalisha ndoa za jinsia moja, kufuatia kuidhinishwa sheria hiyo nchini New Zealand wiki iliyopita.

Liewig akabidhi majina ya anaowabakiza Simba.

WAKATI Ligi Kuu Tanzania Bara ikielekea ukingoni, Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Liewig, tayari ametoa mapendekezo ya wachezaji watakaobaki Msimbazi.
Kocha huyo alijiunga na klabu hiyo katikati ya msimu huu akichukua mikoba ya Mserbia, Milovan Cirkovic, aliyetimuliwa.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Ofisa Habari wa timu hiyo, Ezekiel Kamwaga, alisema wachezaji wengi waliopendekezwa na Liewig ni vijana.
 
“Ni mapema kuzungumzia usajili katika kipindi hiki, lakini kikubwa ni kwamba kocha tayari amekabidhi orodha ya wachezaji anaowahitaji watakaoendelea kuichezea Simba katika msimu ujao.
“Wachezaji hao aliowapendekeza wengi wao ni vijana tuliowapandisha msimu huu na wachache wa timu ya wakubwa ambao amepanga kuwaandaa zaidi,” alisema Kamwaga.

TAPELI ANAYETUMIA JINA LA WAZIRI LUKUVI AMTAPELI LOWASSA IRINGA

maofisa  wa  polisi mkoa wa  Iringa
wakiweka mtego katika nje ya
 ukumbi wa St Dominic  ili kumnasa
  tapeli  huyo anayejiita ni mtoto  wa
  waziri Lukuvi  na kutapeli  watu
Tapeli  anayetapeli  watu maeneo
 mbali mbali ya Tanzania  kupitia jina
 la  waziri Lukuvi akiingizwa ktk  gari maalum leo
Tapeli  Jonathan Wiliam Lukuvi
feki akitiwa matatani askari kanzu  Iringa
Mkuu  wa  mkoa  wa Iringa Dkt
 Christina  Ishengoma ,askofu Dkt
Boaz Sollo na Waziri mkuu wa
  zamani Edward  Lowassa akimsikiliza
 tapeli huyo akimpa maneno ya kitapeli  Lowassa
Kijana  huyo Tapeli akimsomesha
waziri Lowassa ukumbini kwa
kuahidi kuchangia 100,000 huku
akimwomba  kumsaidia misaada  zaidi
Hapa akipelekwa  katika gari
 maalum Hapa akiingizwa katika
Taxi tayari  kwenda  polisi

MAGAZETI YA LEO APRILI 22, 2013

11 6fa4e
13 d676614 a60d6

LADY JAYDEE AWACHANA TENA CLOUDS..... ANADAI KWAMBA MUNGU SI "RUGE" WALA "KUSAGA"

Baada ya kipindi kirefu cha kuongea kwa mafumbo dhidi ya wamiliki wa Clouds FM kuwanyonya wanamuziki akianzia na wimbo wake waJoto Hasira, mwanamuziki Judith Wambura ameendelea kuishambulia redio hiyo na leo Jumapili ameamua kufunguka kwa kuwachana live wamiliki wa redio hiyo.

Hii ni post yake aliyoipost twitter:

Lady JayDee ‏@JideJaydee 1h Naamini kabisa kuwa Mungu sio Ruge wala Kusaga. Atanisimamia kwenye hili #Confidence
\

BABY MADAHA: NTAWACHANGANYA WANAUME KAMA DIAMOND

STAA wa muziki na filamu Bongo, Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’ amesema mwaka huu atawachanganya wanaume kama afanyavyo Nasibu Abdul ‘Diamond’ ili kwenda sawa.
Akifafanua kauli yake kwa paparazi wa Stori 3, Baby Madaha aliweka bayana kuwa haoni tatizo kunaswa na Mwisho Mwampamba kama ilivyoripotiwa hivi karibuni wakati huohuo anatoka kisela na mkali wa Bongo Fleva, Juma Kassim ‘Nature’.
“Watakoma mwaka huu, lazima niwachanganye sana, mbona wao wanatuchanganya sana kama Diamond vile anavyofanya!” alisema Baby.

Sunday, April 21, 2013

WASOMI:::SPIKA ANAVURUGA BUNGE

Baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kutoa mwongozo na kuunga mkono uamuzi wa Naibu wake, Job Ndugai kuwasimamisha wabunge sita wa Chadema, wasomi, wanasiasa na wanaharakati wamesema Kiti cha Spika ndiyo chanzo cha mvutano bungeni kwa kuwa kinapendelea wabunge wa chama tawala (CCM).
Wamesema licha ya Bunge kuongozwa na kanuni, wakati mwingine viongozi hao wa Bunge wanatumia kanuni hizo kuwapendelea wabunge wa CCM, huku wakieleza kuwa licha ya wabunge wa chama hicho kutukana, hawakupewa adhabu yoyote.
Jumatano ya wiki hii, Ndugai aliwasimamisha Tundu Lissu (Singida Mashariki), Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Ezekiah Wenje (Nyamagana) na Godbless Lema wa Arusha Mjini kutohudhuria Bunge kwa siku tano kutokana na alichokiita kufanya vurugu ndani ya Bunge.
Uamuzi huo wa Spika Makinda ulikuja baada ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kumtaka Ndugai aeleze alitumia kanuni gani kuwasimamisha wabunge hao.

DAWA ZA KUONGEZA AKILI ZATUA NCHINI

Mtindo wa maisha, ulaji na msongo wa mawazo, vimewasababishia Watanzani wengi maradhi lukuki hata vifo.Hata hivyo, wataalamu wa afya kutoka Afrika Kusini wamekuja na dawa maalumu, zilizo na uwezo wa kurudisha kumbukumbu, kuongeza upeo darasani, kuondoa sumu mwilini na kumfanya mzee kuonekana kijana.

 Dawa hizo zinazotumia vitamini zilizomo kwenye vyakula vya kila siku, zina uwezo wa kuongeza kiwango cha uelewa kwa mwanafunzi au mfanyakazi.
Kiwango hicho cha uelewa kitaalamu unatambulika kama ‘IQ’.
Mratibu wa dawa hizo hapa nchini, John Haule anasema kuwa dawa hizo zina uwezo wa kufanya kazi kwa haraka.
“Virutubisho hivi ni vizuri kwa wale wanaokwenda katika
mitihani au wanataka kufanya kazi inayohitaji umakini wa hali ya juu,” anasema Haule na kuongeza: “Zimetengenezwa kwa vyakula tunavyotumia na siyo kemikali.”
Haule ambaye ni mtaalamu wa tiba asili na mimea anasema kwamba mtindo wa maisha na vyakula vinavyoliwa na watu mara kwa mara kwa sasa huufanya mwili kuhifadhi sumu nyingi mwilini.

MUME WA MTU ATIWA MBARONI KWA KOSA LA KUFANYA MAPENZI NA MBUZI MWENYE MIMBA NA KUHARIBU MIMBA YA MBUZI HUYO

Marcel ambaye ni mume wa mtu, alifunguliwa kesi namba 29/2013 katika Mahakama ya Mwanzo ya Bashneti mkoani Babati kwa kosa la kuiingilia kimwili mifugo, kinyume na kifungu cha 325 kanuni ya adhabu, sura ya 16 na kesi hiyo ilisomwa hivi karibuni.
Mshitakiwa aliwekewa dhamana lakini siku chache baadaye kesi ilipotakiwa kuendelea, hakuonekana na imebainika mahakamani hapo kuwa ametoroka.

Kesi hiyo ipo mbele ya Hakimu Julius Dagharo wa mahakama hiyo na aliyethibitisha mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa ametoroka ni Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Bashneti, Omari Mwanditi.
Akizungumza mwishoni mwa wiki iliyopita, mmiliki wa mbuzi anayedaiwa kuingiliwa,  Clementina Masay alidai kuwa mtuhumiwa huyo amemsababishia hasara kwani mbuzi wake alikuwa na mimba lakini baada ya kitendo hicho, imeharibika.
Jamii ya wafugaji wa Kiiraq wa eneo hilo wamesikitishwa na kitendo cha mtuhumiwa kudaiwa kuiingilia mifugo yao kimwili mara kwa mara na wameahidi kumsaka hadi wamkamate.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Babati, ACP Akili Mpwapwa amekiri kutokea kwa tukio hilo na ametoa wito kwa wananchi kutoa taarifa wakimuona mtuhumiwa huyo ili afikishwe mahakamani.

AMA kweli dunia imekwisha kwani mtu mmoja, Daniel Marcel (27), mkazi wa Kijiji cha Madunga, wilayani Babati, Manyara, amekamatwa na kufikishwa mahakamani kwa madai ya kufanya mapenzi.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...