Tuesday, April 23, 2013

ZIARA YA KICHAMA YA DKT SHEIN KUTEMBELEA MIKOA YA ZANZIBAR


19
Na Maelezo Zanzibar
Makamo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar Dkt Ali Muhammed Shein amesema kuwa ataendelea kukiimarisha na kukienzi Chama Cha Mapinduzi pamoja na kuulinda Muungano wa Serikali mbili uliopo.
Kauli hiyo ameitoa leo huko katika ukumbi wa CCM Mkoa Amani wakati akizindua ziara yake ya Mikoa mitano ya Zanzibar.
 Dkt Shein ambaye pia ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar amesema kuwa kuna kila sababu ya kukiimarisha chama hicho kutokana na umuhimu wake na kwamba Muungano uliopo wa Serikali mbili ndio njia bora ya kuendeleza mashirikiano ya kidugu yaliyodumu kwa muda mrefu.
 Amesema kuwa lengo kuu la ziara hiyo ni kupata taarifa za matukio mbali mbali pamoja na changamoto zilizopo katika mikoa hiyo zinazohusu CCM.

 Aidha amewataka viongozi wa CCM kuwa  na mashirikano mazuri katika kukiimarisha Chama na kuhakikisha kwamba kinapata ushindi katika kila uchaguzi unaokuja.
 Dkt. shein amesema kuwa ana imani na Chama chake kuibuka mshindi katika chaguzi kutokana Chama hicho kuchagua uongozi makini ambao utahimili vishindo vya uchaguzi ujao.
 Katika hatua nyingine Dkt Shein aliwataka Wananchi kuendelea kujishughulisha na harakati zao za kujiletea maendeleo na kuepuka kuvunja sheria za nchi.
 “Serikali inataka amani na utulivu kwa Wananchi wake sambamba na kuimarisha maendeleo kama Malengo ya Mapinduzi yalivyoelekeza na kwa njia hiyo hatuna budi kuyaenzi Mapinduzi” alieleza Makamo Mwenyekiti wa CCM.
Katika ziara hiyo Makamo Mwenyekiti amezindua Tawi jipya la CCM la Vikokotoni, Kikwajuni SACCOS BANK pamoja na kutoa kadi 270 kwa wanachama wapya wa Chama cha Mapinduzi.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...