Thursday, March 07, 2013

WAUGUZI MOROGORO WAPOKEZANA KUWASHIKIA DRIPU WAGONJWA BAADA YA KUKOSA VITANDA



BAADHI ya wananchi wa mkoani  MOROGORO  wameshangaza na kitendo cha waunguzi wa hospital ya rufaa ya mkoa wa Morogoro,kupokezana kuwashika madripu ya dawa wagonjwa waliolaza chini ya wodi za hospital hiyo ya rufaa nya mkoa wa Morogoro baada ya kukosa vitanda.
 .
Skendo zinazidi kuiandama hospital hiyo ambayo imepandishwa hadhi ya kuwa hospital ya rufaa hivi karibuni ambapo ljumaa iliyopita mtangazaji wa Top redio ya mkoani hapa Edward Abed Mganga aliyevamiwa na majambazi na kukimwizwa kwenye hospital hiyo imeilalamikia hospital hiyo kwakumtelekeza bila kumpa huduma kwa zaidi ya masaa matano na kuladhimika kuondoka kwenye hospital hiyo ya serikali na kwenda kutibiwa hospital za watu binafsi. 


Mtandao huu umeibua Skendo nyingine ndani ya hospital hiyo baada ya kushuhudia waunguzi wa hospital hiyo wakipokeza kuwashikia  madripu ya dawa wagonjwa waliolazwa chini ya sakafu baada ya hospital hiyo kukosa wodi na vitanda vya kutosha. 
Juzikati hospital hiyo ilivamiwa na majeruhi zaidi ya 60 waliopoteza fahamu baada ya kiwanda  cha kutengeza nguo za michezo cha Mazava kukumbwa na shoti ya umeme na kukimbizwa kwenye hospital hiyo,hivyo uongozi wa hospital hiyo baada ya kuelemewa na wingi wa majeruhi hao ulilazimia kutoa magodoro stoo na kuwalaza chini baadhi ya majeruhi hao kufuatia hospital hiyo kukosa wodi na vitanda vya kutosha.

 " Hii ni aibu kubwa kwa hospitali ya rufaa ya mkoa kuwalaza chini wagonjwa hata kama wakijitetea kwamba wagonjwa wamekuja kwa mkupo. hospital inapopewa hadhi ya rufaa inamaana inamudu kukabiliana na majanga yoyote kwa maana wa kuhudumua majeruhi zaidi ya mia watakaofika kwa mkupuo kwenye hospital hiyo"alisema Bi Asha Abdallah aliyekuwepo ndani ya wodi namba 3 walipolazwa majeruhi hao. 

Vile vile mwandishi wa matandao huu mbali ya kushudia wauguzi hao wakipokezana kuwashikia madripu wagonjwa hao pia walishuhudia wahudumu hao wakilazimika kupita juu ya wagonjwa waliolazwa kwenye eneo la njia za wodi hizo  
Ili kupata ufafanuzi wa jambo hilo Mtandao huu ulimsaka Mganga Mfawidhi wa hospital hiyo kwa zaidi ya siku tano na kufanikiwa kumpata leo asubuhi ambapo alipotakiwa kueleza hali hiyo Mganga huyo mfawidhi Bi Rita Lyamuya alikuwa na haya ya kusema 
" Nikweli siku ile ya tukio la kiwanda cha Mazava tulitoa magodolo stoo na kuwatandikia chini baadhi ya majeruhi .kiukweli kwa ishu kama ile tulikosa namna ya kukabiliana  nayo kwani walikuja kwa mkupua zaidi ya majeruhi 65 hivyo tulichofanya tuliwapokea na baadhi kuwalaza chini na kuwapatia hudumu ya kwanza huku tukitafuta sehemu muafaka ya kuwalaza"alisema Dr Rita
dustanshekidele blog

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...