Thursday, March 07, 2013

CHADEMA WAZUA GHASIA MAZISHI YA MOLLEL

Wafuasi wa Chadema, wameibua tafrani ya aina yake wakati wa mazishi ya aliyekuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), marehemu Benson Mollel baada ya kung’oa bendera za chama hicho na kuamsha hasira za 
waombolezaji wafuasi wa chama tawala. 

Mollel alikutwa amefariki mwanzoni mwa wiki, katika Hoteli ya Lush Garden Business, Mtaa wa Jacaranda Arusha huku mwili wake ukiwa mtupu.Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana na baadhi ya makada wa CCM walionekana wakiwasaka wafuasi hao wa Chadema. 

Mashuhuda walisema tukio hilo lilitokea saa 8:30 usiku na baadhi ya wafuasi wanaosadikika kutoka Chadema walichukizwa na kuwapo kwa bendera hizo msibani na hivyo kuanza kuzing’oa.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...