Monday, September 08, 2014

MORIS AREJEA MAZOEZINI TAYARI KWA KUIKABILI YANGA


BEKI tegemezi wa Azam FC,Aggrey Moris leo ameanza mazoezi na timu yake kujiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga uliopangwa kufanyika Jumapili hii uwanja wa taifa..
Meneja wa Azam FC,Jemedari Said amesemeiambia Father Kidevu Blog kuwa Moris ameanza mazoezi na kikosi hicho baada ya kupona Malaria iliyomsumbua kwa wiki moja.
Moris hakuweza kusafiri na kikosi cha Taifa Stars juzi kutokana na kusumbuliwa na maradhi hayo na baada ya kupona anatarajiwa kuwemo kwenye kikosi cha Azam kitakacho pambana na Yanga Jumapili. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

OKWI HURU KUCHEZA SIMBA


Wajumbe wa Kamati ya Sheria na Hadhi ya Wachezaji ya TFF wakiwa katika mkutano jijini Dar es Salaam jana. 


Utata wa Emmanuel Okwi umemalizwa rasmi na mchezaji huyo wa Uganda sasa yupo huru.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ilikutana jana na kupitia masuala mbalimbali ikiwamo mgogoro wa kimkataba kati ya klabu ya Yanga na mchezaji Emmanuel Okwi.

Mkataba huo ulipitiwa na kamati ikiwamo kumsikiliza mchezaji mwenyewe pamoja na upande wa Yanga na kuridhika kuwa mkataba kati ya pande hizo umevunjika.

Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Boniface Wambura alisema jana kuwa mkataba wa pande mbili haupo kwa sababu Yanga ilikiuka kipengele namba 8 kuhusu malipo ya ada ya usajili.

“Yanga ikiwa mwajiri, haikutekeleza kipengele hicho cha kimkataba hadi kufikia Juni 27 mwaka huu ilipoandika barua TFF kuomba mkataba huo uvunjwe. Kwa maana hiyo Okwi ni mchezaji huru, hivyo yuko huru kujiunga na timu yoyote,” alisema Wambura.

Alifafanua kuwa mkataba ni uhusiano kati ya mwajiri (Yanga) na mwajiriwa (Okwi), ambapo Kamati imebaini kuwa uhusiano huo haupo, hivyo hakuna mazingira ya pande hizo mbili kuendelea kufanya kazi pamoja. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Sunday, September 07, 2014

HAYA NDIO MAAMUZI YA WAZIRI MWAKYEMBE KUFUATIA AJALI ILIYOTOKEA MUSOMA NA KUUA WATU 39

Waziri wa uchukuzi, Mhe Harrison Mwakyembe
Kufuatia ajali ya mabasi iliyoua takbriban watu 39 Musoma, Waziri wa uchukuzi, Mhe Harrison Mwakyembe amefanya maamuzi kadhaa, kupunguza ajali za barabarani. Ifuatayo ni kauli yake:
1.Tunaanza na hawa waliopata ajali, nimeelekeza na najua vyombo vinavyohusika Polisi pamoja na SUMATRA watatekeleza… kwanza kuzifungia kampuni za haya mabasi ya J4 na Mwanza Coach wasijihusishe na usafirishaji wa abiria tena, hatuwezi kuwa tunapata ajali za kijingajinga namna hiyo, nimeliona eneo lenyewe liko wazi kabisa lakini ni watu tu wameamua, dereva wa huku anamuona mwenzake na kusema mimi lazima anipishe’ – Dr. Mwakyembe
2. Tumeelekeza Wafanye uhakiki wa madereva wao wote na tunahitaji picha zao lakini vilevile tunahitaji mikataba ya kazi, hatutaki mabasi ya kupeleka abiria yaendeshwe na watu tu kwa majaribio, nataka ushahidi wa kila dereva kwamba amejiunga na hii mifuko ya akiba ya Wafanyakazi, tuone kabisa mchango wa Mwajiri na mfanyakazi kila mwezi’
3. Nimeagiza lazima tuangalie BIMA ya hiyo gari, unajifikiria mwenyewe tu ukipoteza gari ulipwe kidogo gari yako lakini hufikirii kuhusu binadamu…. bila comprehensive haendeshi mtu gari kuchukua abiria.
Tamasha la Fiesta lililokua lifanyike Ijumaa hapa Musoma sasa imefahamika litafanyika Jumapili ya kesho September 7 2014 ambapo pia imehamasishwa kwa wingi watu kujitokeza ili mapato hayo yapelekwe kwa ndugu waliopoteza watu na majeruhi ajalini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

'SHEMEJI' AELEZA JINSI MBASHA ALIVYOMBAKA...!!!

  Mwimbaji wa nyimbo za Injili, Emmanuel Mbasha

Shahidi wa kwanza katika kesi ya kubaka inayomkabili mwimbaji wa nyimbo za Injili, Emmanuel Mbasha, ameieleza mahakama jinsi mshtakiwa alivyomkaba shingo na kumziba mdomo kwa kutumia nguo, kisha kumbaka.
Shahidi huyo ambaye ni shemeji yake, mwenye umri wa miaka 17, aliyasema hayo jana wakati akitoa ushahidi wake katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala.
Hata hivyo, kesi hiyo ilisikilizwa kwa faragha (Chamber Cort) baada ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali Nassoro Katuga kuiomba mahakama kesi hiyo kuendeshwa kwa faragha kwa kuwa imefikia hatua ya kusikilizwa na sheria inaonyesha kuwa mtoto huyo yupo chini ya miaka 18.
Ombi hilo lilikubaliwa na pande zote mbili na kesi hiyo kuendeshwa katika mahakama ya faragha na Hakimu, Wilbaforce Luhwago aliomba watu wote walikuwepo ndani ya mahakama hiyo kutoka nje ili kupisha upande wa mashtaka kutoa ushahidi.
Akiongozwa na mwendesha Mashtaka wa Serikali Nassoro Katuga, shahidi huyo alidai siku ya tukio, Mei 23, mwaka huu, mshtakiwa aliondoka na mke wake kwenda kufuatilia mkanda wa video lakini ghafla alirudi nyumbani kwake Tabata Kimanga akiwa peke yake.
Alidai siku hiyo ya tukio mshtakiwa alifanikiwa kufanya mapenzi na binti huyo na kumwambia asimwambie mtu wakati mke wake akiwa hayupo nyumbani hapo.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 12,2014. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na Mwananchi

AL-SHABAAB WATHIBITISHA KIFO CHA KIONGOZI WAO

Wapiganaji wa Alshabaab

Kundi la wapiganaji wa kisomali Al-shabaab limethibitisha kuwa kiongozi wake Ahmed Abdi Godane aliuawa siku ya jumatatu katika shambulizi la angani lililotekelezwa na wanajeshi wa Marekani.
Msemaji wa Alshabaab amesema kuwa wanachama wengine wawili wa kundi hilo pia walifariki katika shambulizi hilo ,yapata kilomita 170 kusini mwa mji mkuu wa Mogadishu .
Ripoti zinasema kuwa kundi la Alshabaab limemchagua kiongozi mpya Ahmad Omar,katika mkutano uliofanyika katika eneo lisilojulikana.
Mwandishi wa BBC mjini Nairobi amesema kuwa kiongozi huyo hafahamiki vyema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

LOIC REMY: BADO SIELEWI KWANINI SIO MCHEZAJI WA LIVERPOOL…LAKINI NINA FURAHA KUWA CHELSEA

1410045801087_wps_63_France_s_forward_Loic_Rem
Tatizo: Loic Remy  alikaribia kusajiliwa Liverpool kabla ya dili kushindikana.
MSHAMBULIAJI wa Chelsea,  Loic Remy amesema bado haelewi kwanini dili la kujiunga na Liverpool majira ya kiangazi lilivunjika.
Nyota huyo mwenye miaka 27 alitazamiwa kujiunga Anfield kwa dau la paundi milioni 8 kabla ya wekundu hao kulitupilia mbali dili hilo wakidai mchezaji huyo ameshindwa kufuzu vipimo vya afya.
Remy alishindwa kufuzu vipimo vya afya kutokana na matatizo ya moyo na goti, lakini alishangazwa na tangazo hilo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
“Binafsi sikuelewa. Tatizo wakati wa vipimo vya afya? sijui. Walitengenezea, lazima itakuwa hivyo,” aliwaambia Daily Star.
Mfaransa huyo alirejea QPR na alionekana katika mechi ya ligi kuu kabla ya kujiunga na Chelsea wiki ya mwisho ya usajili ambapo atacheza kumsaidia Diego Costa ambaye amepata majeraha ya nyama za paja katika majukumu ya kimataifa.
Delight: Remy signed for Chelsea on final week of the transfer window
 
Remy, ambaye aliifungia Ufaransa bao la ushindi dhidi ya Hispania siku ya alhamisi, alisema; “Kichwani mwangu, nilitaka kuendelea kukaa QPR, lakini sikuogopa kwa sababu nyingi  nilizonazo: Kwa jinsi nilivyojiimarisha, kujiamini kwangu na kwa namna Chelsea walivyonihitaji, nilikubali kwasababu hii ni moja ya klabu kubwa duniani.
“Nina furaha ya kujiunga na klabu hii” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

LOUIS VAN GAAL HANA LA KUJITETEA KWA MANCHESTER UNITED, KIKOSI CHAKE KINA THAMANI YA PAUNDI MILIONI 379

1410038770007_Image_galleryImage_MILTON_KEYNES_ENGLAND_AUG
Hakuna kujitetea:Kikosi cha Manchester United chini ya Louis van Gaal kina thamani inayofikia paundi milioni 379
LOUIS van Gaal hatakuwa na la kujitetea kama Manchester United itashindwa kupambana kusaka ubingwa msimu huu.
Hii inatokana na ukweli kwamba Van Gaal ndiye kocha mwenye kikosi ghali zaidi katika ligi ya England kwa sasa.
Baada ya usajili mkubwa majira ya kiangazi, tafiti zinaonesha kuwa bosi huyo wa United ana kikosi chenye thamani ya paundi milioni 379.4.
Thamani hiyo haifikiwi na Manchester City ya Manuel Pellegrini na Chelsea ya Jose Mourinho.
Tangu kustaafu kwa Sir Alex Ferguson mwaka mmoja uliopita kampeni za kuwania ubingwa ziliisha na United wamejaribu kutumia paundi milioni 215 kusajili wachezaji ili kurudi katika kiwango cha juu.
Big deals: Angel di Maria and Radamel Falcao both arrived at Old Trafford in big-money moves this summer

JUAN MATA SOKONI JANUARI, ARTURO VIDAL, MATS HUMMELS KWENYE RADA, RONALDO NAYE ANAWEZA KURUDI OLD TRAFFORD

1410046545686_Image_galleryImage_VERONA_ITALY_AUGUST_30_Ar
Siku zijazo: Manchester United  bado wanaiwinda saini ya  Arturo Vidal (pichani juu)
MANCHESTER United bado hawajamaliza matumizi makubwa ya fedha katika dirisha la usajili.
Katika dirisha dogo la usajili mwezi januari mwakani wametenga paundi nyingine milioni 50  kwa ajili ya kunasa saini za wachezaji wengine.
Tayari United imeshatumia paundi milioni 150 katika dirisha la usajili majira ya kiangazi jumlisha kumsajili Radamel Falcao.
Arturo Vidal, Mats Hummels na Sami Khedira ndio wachezaji wanaowaniwa zaidi na United.
Jaun Mata Garcia atauzwa mwezi januari kama sehemu ya kuongeza wachezaji wapya ili kuimarisha kikosi cha Louis van Gaal.
Pia kuna taarifa kuwa mwanasoka bora wa dunia na Ulaya, Cristiano Ronaldo anaweza kurejea Manchester United.
Nyota huyo anayekipiga Real Madrid ana mapenzi makubwa na klabu yake hiyo ya zamani na anasema anaipenda toka moyoni.
On the move: United will look to sell Juan Mata as Louis van Gaal continues his rebuilding process
Atletico Madrid, Roma na Juventus  zipo tayari kumsajili Mata aliyesajiliwa na United kutoka Chelsea mwezi januari kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 37.
United inatarajia kukubali ofa ya paundi milioni 20. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, September 06, 2014

MORSI ASHTAKIWA KWA KUTOA SIRI ZA MISRI

Mohammed Morsi akiwa Kizimbani

Kiongozi mkuu wa mashtaka nchini Misri amemfungulia mashtaka aliyekuwa rais wa taifa hilo Mohammed Morsi kwa kupeleka stakhabadhi za siri kutoka idara ya usalama nchini Qatar.
Bwana Morsi amekuwa akizuiliwa jela tangu jeshi limuondoe madarakani mwaka uliopita wakati wa maandamano ya kumtaka ajiuzulu.
Tayari kiongozi huyo anakabiliwa na hukumu ya kifo katika mahakama nyengine tofauti.
Kundi la Muslim Brotherhood ambalo ni mwanachama wa maisha limepigwa marufuku na viongozi wake wengi huku wengine wakihukumiwa kifo.
Qatar imekuwa ikimuunga mkono Bwana Morsi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

DAMU YA WALIOPONA EBOLA KUTIBU UGONJWA HUO

Mkutano wa WHO kuhusu Ebola mjini Geneva.

Shirika la afya duniani WHO limesema kuwa damu ya watu ambao wameponea ugonjwa wa Ebola inaweza kutumiwa kuwauguza wagonjwa wengine.
Katika mkutano mjini Geneva, wataalam wa shirika hilo walikubaliana kwamba hii itakuwa njia ya haraka na ilio salama dhidi ya ugonjwa wa Ebola,sababu kuu ikiwa kwamba kinga ya mwili katika damu ya mtu aliyepona inaweza kukabiliana na virusi hivyo.
Wataalam hao pia wanataka matibabu mengine kuharakishwa ikiwemo dawa ya Zmapp pamoja na chanjo zengine mbili.
Idadi ya watu wanaodaiwa kufariki kutokana na ugonjwa wa Ebola imepita elfu mbili.
Zaidi ya watu elfu nne wameambukizwa ugonjwa huo huku tiba yake ikiwa bado haijajulikana. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, September 05, 2014

TAZAMA PICHA ZA AJALI ILIYOTOKEA MUSOMA NA KUUA WATU ZAIDI YA 40

 Basi la Kampuni ya J4 EXPRESS lenye nambari za usajili T 677 CYC lililokuwa likitoka Musoma kuelekea Silari Mkoani Mara likiwa limeumia vibaya sana baada ya kugongana uso kwa uso na Basi lingine la Kampuni ya MWANZA COACH lenye nambari za usajili T 736 AWJ katika eneo la SabaSaba, Mjini Musoma mchana wa leo.
Watu zaidi ya 40 wamepoteza maisha papo hapo na wengine kujeruhiwa vibaya kwa mujibu wa Ripota wetu aliopo eneo la tukio, ilielezwa kuwa chanzo cha ajali hiyo ni Basi la J4 ambalo lilikuwa likijaribu kuipita gari ndogo aina ya Nissan Terano lenye nambari za usajili T 332 AKK katika sehemu ambayo mbele kuna daraja linaloweza kupitisha gari moja kwa wakati huo, kutokana na kuwa basi hilo lilikuwa kwenye mwendo kasi liliweza kuisukuma kwa ubavuni gari hiyo ndogo ambayo haikuweza kuhimili nguvu ya Basi hilo na kutoka kwenye njia na kwenda kuingia mtoni hali iliyoipelekea dereva wa basi hilo kuamini kuwa atawahi kupita katika daraja hilo bila kufahamu kuwa Basi lingine linalokuja mbele nalo liko kwenye mwendo kasi huku nalo likitaka kuwahi kupita kwenye daraja hilo. Ndani ya gari hiyo ndogo kulikuwa na watu watatu, ambapo wawili wamefariki na mmoja amejeruhiwa.
Basi la Kampuni ya MWANZA COACH lililokuwa likitokea Musoma kwenda Mwanza linavyoonekana baada ya kugongana uso kwa uso na Basi la Kampuni ya J4 EXPRESS.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz 

BUNGE LA KATIBA LAKATAA ELIMU YA KIDATO CHA NNE KWA WABUNGE


Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Pandu Amir Kificho (kulia) akiwaeleza jambo wajumbe wa bunge hilo walipohudhuria kikao cha 32 cha Bunge mjini Dodoma jana.

Pendekezo la Rasimu ya Katiba kuwa wabunge walau wawe na elimu ya kidato cha nne limetupiliwa mbali na wajumbe wa Bunge Maalumu, baada ya Kamati karibu zote kulikataa.
Kamati hizo zimependekeza kigezo cha elimu kuanzia walau kidato cha nne kama sharti muhimu la mtu anayetaka kugombea Ubunge kiondolewe, badala yake mgombea ama ajue tu kusoma na kuandika, au ajue kusoma na kuandika Lugha ya Kiswahili au Kiingereza kama ilivyo kwenye Katiba ya sasa.Mbali na pendekezo hilo, kamati hizo zimegawanyika kuhusu Ibara ya 129 ya Rasimu ya Katiba inayowapa wananchi nguvu ya kumuondoa mbunge wao madarakani kabla ya miaka mitano kumalizika.
Hayo yalijitokeza bungeni Dodoma jana, wakati kamati hizo zikiwasilisha taarifa zake kuhusu Sura ya 9 na 10 ya Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa bungeni na Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NISHA AZUA TAHARUKI HEKALU LA FREEMASON...!!!


STAA wa sinema za Kibongo, Salma Jabu 'Nisha', Jumanne iliyopita alijikuta akizua taharuki kufuatia kuegesha gari lake nje ya Hekalu la Freemason lililopo nyuma ya Hyatt Regency Dar es Salaam The Kilimanjaro Hotel jijini Dar es Salaam.


Staa wa sinema za Kibongo, Salma Jabu 'Nisha'.

Taharuki hiyo ilikuja pale Nisha alipoegesha gari lake eneo hilo na kushuka kisha wanafunzi na watu wengine kusitisha shughuli na kumzunguka kutaka kujua kulikoni staa huyo kufika eneo hilo linaloaminika kuwa kila anayekwenda ni muumini wa imani ya Freemason.

Baadhi ya watu walimuuliza Nisha alichofuata kwenye hekalu hilo huku mwenyewe akishindwa kujibu kwani alitupiwa maswali mfululizo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

DIAMOND AELEZA JINSI ALIVYODHALILISHWA UJERUMANI


SIKU chache baada ya kufanyiwa fujo katika shoo yake nchini Ujerumani, staa wa Mdogo Mdogo, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ameibuka na kueleza namna ambavyo alidhalilishwa nchini humo.
Diamond aliponea chupuchupu kupewa kipigo baada ya kuchelewa kwenye shoo iliyokuwa ifanyike katika Ukumbi wa Sindelfingen katika mji wa Stuttgart, Ujerumani.
Staa wa Mdogo Mdogo, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Akizungumza na paparazi wetu baada ya kutua Bongo Jumanne iliyopita, Diamond alisema anasikitika kwani alidhalilishwa wakati alipokuwa akidai haki ya kumaliziwa malipo yake ya shoo euro 250 (zaidi ya sh 500,000). Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SULUHU: HUYU NDIYE SHIBUDA ORIJINO

Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samia Suluhu.

WAKATI Mbunge wa Bariadi Magharibi (Chadema), John Shibuda akiwasilisha maoni ya wachache ya Kamati namba 8 ya Bunge Maalum la Katiba linaloendelea na vikao vyake mjini Dodoma Jumatano mchana, Makamu Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samia Suluhu alimsifu na kusema kuwa mwakilishi huyo wa wananchi ndiye orijino, ukimuona mwingine ni photokopi.
Shibuda aliyeingia katika ukumbi huo akipingana na msimamo wa chama chake kilichoamua kususia vikao hivyo kwa kushirikiana na vyama vya CUF na NCCR-Mageuzi, alitumia pia nafasi hiyo kuwapiga vijembe viongozi wake, akisema hana matatizo na Chadema, isipokuwa ana ‘bifu’ na mfumo wa utumishi wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini.
Akifafanua kauli yake hiyo, Shibuda anayefahamika kwa mbwembwe na mikogo ya lugha, alisema yeye ni kama mchezaji wa mpira aliye staa, akiwatolea mfano Cristiano Ronaldo na Lionel Messi, ambao wanaponunuliwa na timu yoyote, huenda kwa ajili ya kuiimarisha na si vinginevyo.
Mbunge wa Bariadi Magharibi (Chadema), John Shibuda.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 05, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MCHEKESHAJI MAARUFU DUNIANI 'JOAN RIVERS' AFARIKI


Enzi za uhai wake Joan Rivers
Mchekeshaji maarufu nchini Marekani Joan Rivers amefariki dunia akiwa na umri wa miaka themanini na na mmoja.
Joan alikua amelazwa katika hospitali moja mjini New York kwa wiki kadhaa sasa akisumbuliwa na maradhi ya moyo.
Melissa binti wa Joan,Akitangaza juu ya kifo cha mamake alimuelezea mama yake kua maishani mwake alikua akipenda kuona watu wana tabasamu usoni ama vicheko.
Joan River alianza shughuli zake za ucheshi kama muigizaji wa kawaida tu nusu karne iliyopita, na anatajwa kua mwanamke maarufu na bora katika ucheshi jukwaani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAJANGA: BOKO HARAM WAZUIA WATU KUZIKA MAITI...!!!

Wapiganaji wa Boko Haram wamesababisha maafa Kaskazini ya Nigeria ngome yao ya vita
Taarifa za kutisha zimeibuka kutoka mjini Bama moja ya miji ambayo ilitekwa na wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram Kaskazini Mashariki ya Nigeria
Seneta mmoja wa eneo hilo,Ahmed Zanna, aliambia BBC kwamba wakazi hawaruhusiwi kuwazika jamaa wao waliouawa na wapiganaji hao.

Inaarifiwa miili imetapakaa katika barabara za mji huo ambao Boko Haram imeuteka.
Kundi hilo linasemekana kuuteka mji huo huku wapiganaji wa kundi hilo wakishika doria katika barabara zake.
Maelfu ya watu wametoroka huku idadi kubwa ya wengine wakiuawa.
Seneta huyo ameitaka serikali ya Nigeria kupeleka wanajeshi mjini Maiduguri ambao ni mji mkuu wa jimbo hilo ili kuulinda dhidi ya wapiganaji hao.
Mnamo siku ya Jumatano serikali ya jimbo hilo ilikanusha madai kuwa jimbo hilo limetekwa na wapiganaji hao.
Maafisa wakuu wanakisia kuwa watu 26,000 wameachwa bila makao kutfuatia mapigano katika mji wa Bama.
Bwana Zanna anasema kuwa barabara za mji huo zimejaa miili ya watu na Boko Harama imewakata wakazi kuwazika jamaa wao. ''Kwa hivyo hali ni mbaya na inaendelea kuzorota,'' asema bwana zANNA
Boko Haram wameteka miji kadhaa Kaskazini Mashariki ya Nigeria, katika miezi ya hivi karibuni na kusababisha hofu kuwa huenda wakaufikia mji mkuu Maiduguri.
Bwana Zanna amesema kuwa itakuwa janga kubwa ikiwa Boko Haram wataushambulia mji wa Maidiguri ambao una watu zaidi ya milioni mbili. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WATOTOMILIONI 120 WAFANYIWA UKATILI DUNIANI

Mtoto akijilia nyama
Umoja wa mataifa umetoa kauli kwamba wasichana zaidi ya milioni 120 duniani kote,sawa na msichana mmoja kati ya kumi atakua amaebakwa ama amewahi kufanyiwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kabla hajatimiza umri wa miaka 20.
Kitengo cha umoja wa mataifa kinachoshughulikia masuala ya watoto UNICEF kimegundua mnamo mwaka 2012 pekee watoto na mabinti wapatao elfu tisini na watano waliuawa,wengi wao ni kutoka Marekani kusini na Caribbean.
Ripoti hiyo ya UNICEF iliangazia nchi zipatazo mia moja na tisini, na kusema kwamba duniani kote watoto wametendewa ukatili,mauaji na mashambulizi ya kingono ikiwemo kuonewa na uadabishaji watoto unaokiuka haki zao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

Wednesday, September 03, 2014

SITTA AKANA KUTUMIA BUNGE LA KATIBA KUSAKA URAIS 2015, TAZAMA VIDEO

Wakati joto la Urais mwakani likizidi kuongezeka nchini, Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samwel Sitta ameweka wazi kuwa hana nia ya kuwania Urais kwa kutumia kigezo cha kuongoza Bunge hilo maalum.
Akizungumza wakati wa kufungua kikao cha thelathini na moja cha Bunge Maalum la Katiba ambalo limeanza kupokea taarifa za kamati zake, Sitta hata hivyo alisema atakuwa tayari kufanya hivyo kama wananchi wataona anafaa kwani wao ndio wenye dhamana ya kuchagua mtu wanayetaka awaongoza.
“Wengine wananikejeli, wanasema kwa shughuli hii naonesha sifai Urais, me sijaomba Urais,” alisema Sitta na kufuatiwa na idadi kubwa ya makofi bungeni hapo.
Sitta aliongeza: “Naifanya kazi hii kama Mwenyekiti wa Bunge la Katiba basi, lakini nasema wanaochagua ni wananchi, inawezekana mwakani, wananchi wa Tanzania wakatamani mtu mzima, aliyetulia na muadilifu, kama itakuwa hivyo wajue tupo na sisi wengine.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

HARUSI YA KIPEKEE YAFANYIKA NDANI YA MAJI

Katika mtaa, mdogo wa Shanghai, kilichokuwa kiwanda cha kushona nguo sasa kimegeuka, ishara ya mabadiliko ya kuchumi yanayoshuhudiwa nchini China.
Katika eneo hili, wafanyakazi walikuwa wanafanya kazi ndogondogo kujikimu kimaisha na hata kuuza bidhaa zao nje , lakini kazi mpya imeanza kufanyika hapa.
Biashara hii ni moja ya biashara ambazo zinasukuma uchumi wa China kwa kuwafanya watu kutumia pesa zao.
Duka lililofunguliwa hapa linaitwa Mr Wedding ...Biashara ndogo ambayo inawaajiri watu 16 ni sehemu ya sekta ambayo imekuwa ikinawiri kuliko nyinginezo katika historia ya nchi hii.
Kulingana na taarifa za serikali, soko la biashara za bidhaa za harusi , pesa zinazotumika kwa sherehe aina zote za harusi imekuwa kwa kasi na kuwa na thamani ya dola bilioni 130 kila mwaka.
Duka hili la Mr Wedding halijaachwa nyuma kwani nalo linataka kipande cha mapato kutoka kwa sekta hiyo. Tofauti ya biashara yake ni kwamba maharushi hupata huduma ya kipekee kutoka kwa duka lake.
'Mtindo tofauti wa picha'
''Watu wanaweza kupigwa picha ndani maji wakiwa katika hali yoyote, '' asema mmiliki wa duka hili Tina Liu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 03, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC_0041

DSC_0039
DSC_0042
DSC_0043 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

OBAMA KUONGEZA VIKOSI IRAQ

Rais Barack Obama
Rais Barack Obama wa Marekani ameidhinisha kupelekwa vikosi vya wanajeshi wapatao 350 kwa lengo la kuwalinda wanadiplomasia na wafanyakazi raia wa nchi hiyo waishio mji mkuu wa Iraq Baghdad.
Ikulu ya Marekani imesema wanajeshi hao watakaopelekwa baadhi yao ni wale wanaojihusisha na diplomasia ya ulinzi ya iraq ambao ni zaidi ya mia nane.
Hata hivyo Marekani inatarajia kuwatuma maofisa waandamizi akiwemo John kerry katibu mkuu wa marekani na Chuck Hagel katibu wa ulinzi ambao watakwenda mashariki ya kati katika harakati za kuimarisha ushirikiano.
Hatua hiyo inafuatia vitendo vya mashambulizi na mauaji yanayoendelea Iraq ikiwa ni matokeo ya utofauti kati ya Marekani na makundi ya wapiganaji ambao wamekuwa wakiwalenga raia wa Marekani waliopo nchini humo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MWANDISHI WA HABARI MWINGINE "ACHINJWA"


Mwandishi aliyechinjwa na IS Steven Sotloff
Wapiganaji wa dola ya Kiislam IS wamesambaza picha za video katika mitandao kwa lengo la kuonyesha kuchinjwa kwa mwandishi wa habari raia Marekani Steven Sotloff ambaye ni mmoja wa mateka wanaoshikiliwa na wapiganaji hao.
Mwandishi huyo Sotloff, mwenye umri wa miaka 31 ambaye alitekwa na wapiganaji hao mwezi August mwakajana.
Mwezi uliopita Sotloff alionekana mwishoni katika picha za video zilizoonyeshwa kuhusiana na kuchinjwa kwa mwandishi mwingine wa Marekani James Foley.
Wapiganaji hao wa katika picha hizo pia wameonekana wakimtishia kumuua mateka mwingine anayedhaniwa kuwa ni raia wa Uingereza.
Baada ya mauaji ya mwandishi wa awali Foley, mama mzazi wa mwandiashi wa Sotloff alitoa ombi maalumu kwa kiongozi wa wanajeshi hao Abu Bakr al-Baghdadi kutoa muua mtoto wake.
Msemaji wa Ikulu ya White House Josh Earnest amesema kuwa maofisa wa Marekani wanaendelea na uchunguzi wa ripoti hiyo.
Marekani hivi karibuni ilifanya mashambulizi ya anga dhidi ya IS nchini Iraq.
Mwandishi wa masuala ya usalama wa BBC Frank Gardner amesema hatua hiyo ya wapiganaji wa IS ni kulipa kisasi kwa Marekani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

Tuesday, September 02, 2014

SASA UKICHUKUA FEDHA BENKI ROHO MKONONI


Katuni inayoonyesha ujambazi wa kutumia pikipiki na bastola unavyoshika kasi jijini Dar es Salaam. 

Ni roho mkononi. Hayo ndiyo maneno matatu yanayofaa kuelezea hali ilivyo jijini Dar es Salaam na maeneo kadhaa nchini kwa sasa, hasa pale mtu anapobeba fedha nyingi.
Matukio ya ujambazi kwa kutumia silaha yamekuwa sugu na kusababisha wananchi wanaopeleka au kutoa fedha benki kuvamiwa, kujeruhiwa au kuuawa mchana kweupe na majambazi wanaotumia pikipiki.
Wananchi wamekuwa wakihoji ni kwa jinsi gani majambazi hao hupata taarifa za mtu aliyekwenda benki ama kuweka au kuchukua fedha.
Mkazi wa Tabata Kimanga, Dar es Salaam, Salum Mashati alisema: “Haiingii akilini, utasikia mtu kaporwa fedha akitoka benki. Eti majambazi wanasema kabisa toa hizo milioni 20, wanajuaje kuwa una kiwango hicho? Huenda watu wa benki wanashiriki uhalifu huu.”
Hata hivyo, meneja wa tawi moja la benki lililopo Mlimani City, ambaye hakupenda jina lake litajwe alikanusha madai hayo... “Si kweli kwamba benki zinashirikiana na majambazi kufanya uhalifu huu. Kwanza wahudumu (bank tellers) hawaruhusiwi kuingia na simu wanapohudumia wateja.
“Hata mteja anapoingia benki hukatazwa kuongea na simu au kuandika ujumbe. Mazingira tuliyojiwekea hayaruhusu kabisa mawasiliano kati ya benki yetu na watu wa nje wakati wa kazi. Nadhani vitendo hivi vya ujambazi vinaanzia kwa wateja wenyewe kutoa taarifa juu ya mipango yao kwa watu ambao si waaminifu,” alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

JAY DEE "MAADUI ZANGU WAMEBADILISHA WIMBO"


Malkia wa muziki wa R&B, Lady Jay Dee  

 Malkia wa muziki wa R&B, Lady Jay Dee amedai kuwa maadui zake wamebuni njia mpya ya kumwangusha, baada ya zile za awali kutofanikiwa.
Katika waraka mrefu aliouandika katika mtandao wa facebook, Lady Jay Dee alisema watu wasiopenda mafanikio yake wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali kumwangusha, lakini hata hivyo wameshindwa.
Jay Dee analalamikia habari iliyoandikwa juu yake kuwa amekuwa katika uhusiano mpya na kijana aliyemzidi umri, jambo analosema halina ukweli.
Habari hiyo inahusishwa na kile kilichodaiwa kuwa mwanamuziki huyo ameachana na mume wake, Gadner G Habash, ambaye ni mtangazaji wa kituo cha redio Times FM. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NDEGE YA KENYA YAANGUKA TANZANIA


Masalia ya ndege ya Kampuni ya Safari Express Limited iliyoanguka katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuua watu watatu jana.
Ndege ya Kampuni ya Safari Express Limited imeanguka katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuwateketeza watu watatu waliokuwamo ndani.
Ndege hiyo yenye namba za usajili 5Y-SXP iliruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza Jumapili saa 1:26 usiku ikielekea Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta (JKIA) Kenya ambako ilitakiwa kutua saa 2:36 usiku.
Meneja Uhusiano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa), Paschal Shelutete alikiri ndege hiyo kuanguka kwenye hifadhi hiyo na walikuwa katika harakati za kuitafuta.
Mkaguzi Mkuu wa Ajali za Ndege nchini, kutoka Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi, David Nyamwihura alisema ajali hiyo ilitokea takriban maili 20 kutoka Serengeti, katika eneo la Kogatembe na watu wote watatu waliokuwamo wamefariki dunia.
Meneja wa Udhibiti wa JKIA, Clever Davor aliliambia gazeti la Daily Nation la Kenya kuwa ndege hiyo ilipoteza mawasiliano na rada ya uwanja huo ikiwa imeruka angani urefu wa futi 14,000. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BOKO HARAM WAUTEKA MJI MUHIMU NIGERIA

Wanajeshi wa serikali ya Nigeria.
Kundi la Boko haram limefanya mashambulizi katika mji wa Bama na kusababisha mauaji ya watu wengi huku wengine wakitoroka.
Wanamgambo hao waliuteka mji wa Bama ,ambao ni wa pili kwa ukubwa katika jimbo la Borno siku ya Jumatatu baada ya jaribio la awali la kutaka kuuteka mji huo kuzimwa na vikosi vya serikali.
Akizungumza na BBC ,wakaazi wamethibitisha kuwa mji huo umetekwa na kundi hilo na kwamba maelfu ya watu sasa wameachwa bila makao.
Mamlaka ya Nigeria bado haijatoa tamko lolote kuhusu shambulizi hilo.
Taarifa zinasema kuwa watu wengi wametoroka wakiwemo wanajeshi.
Zana za kivita zinazotumiwa na wapiganaji wa Boko Haram
Hapo awali jeshi la Nigeria lilitoa ripoti kuonyesha kuwa mpaka sasa limewaua wapiganaji 70 wa Boko Haram ,kutokana na mapigano kati ya kikundi hicho na wanajeshi Kaskazini -Mashariki mwa mji wa Bama.
Boko Haram walifika mapema asubuhi katika mji huo kwa magari ya kivita.Taarifa kutoka katika mji huo zinaeleza kwamba mashambulizi yalianzishwa na vikosi vya jeshi la Nigeria.
Msemaji wa kundi hilo la Boko Haram ameelezea hali ya mji huo kwa sasa kuwa wakaazi wa mji wa Bama wamekimbilia katika mji mwingine wa Borno na Maiduguri .
Nalo shirika la Amnesty International limetoa takwimu kuwa raia wapatao milioni nne wamekufa mwaka huu katika mgogoro huo kati ya Boko Haram na vikosi vya ulinzi vya Nigeria.

KIONGOZI WA AL-SHABAB ASHAMBULIWA

Haijulikani ikiwa Ahmed Abdi Godane aliuawa kwenye shambulizi hilo
Wanajeshi wa Mreakani wamefanya mashambulizi ya angani dhidi ya msafara wa magari ya mmoja wa viongozi wa kundi la Al Shabaab nchini Somalia.
Haijulikani ikiwa kiongozi wa kundi hilo, Ahmed Abdi Godane aliuawa kwenye shambulizi hilo lililofanyika umbali wa kilomita 240 kusini ya mjini mkuu Mogadishu.
Mwandishi wa BBC anasema kuwa wanajeshi wa Marekani walionekana wakishuka katika eneo hilo kwa helikopta na kuchukua miili ya wapiganaji waliouawa.
Msemaji wa idara ya ulinzi ya Marekani, (Rear Admiral John Kirby) alisema bado inadurusu matokeo ya shambulizi hilo.
Baadhi ya taarifa zinasema kuwa wapiganaji waliwakamata wakazi walioshukiwa kutoa taarifa kwa Marekani.

Na BBC

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...