Wednesday, September 03, 2014

OBAMA KUONGEZA VIKOSI IRAQ

Rais Barack Obama
Rais Barack Obama wa Marekani ameidhinisha kupelekwa vikosi vya wanajeshi wapatao 350 kwa lengo la kuwalinda wanadiplomasia na wafanyakazi raia wa nchi hiyo waishio mji mkuu wa Iraq Baghdad.
Ikulu ya Marekani imesema wanajeshi hao watakaopelekwa baadhi yao ni wale wanaojihusisha na diplomasia ya ulinzi ya iraq ambao ni zaidi ya mia nane.
Hata hivyo Marekani inatarajia kuwatuma maofisa waandamizi akiwemo John kerry katibu mkuu wa marekani na Chuck Hagel katibu wa ulinzi ambao watakwenda mashariki ya kati katika harakati za kuimarisha ushirikiano.
Hatua hiyo inafuatia vitendo vya mashambulizi na mauaji yanayoendelea Iraq ikiwa ni matokeo ya utofauti kati ya Marekani na makundi ya wapiganaji ambao wamekuwa wakiwalenga raia wa Marekani waliopo nchini humo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...