Wednesday, September 03, 2014

SITTA AKANA KUTUMIA BUNGE LA KATIBA KUSAKA URAIS 2015, TAZAMA VIDEO

Wakati joto la Urais mwakani likizidi kuongezeka nchini, Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samwel Sitta ameweka wazi kuwa hana nia ya kuwania Urais kwa kutumia kigezo cha kuongoza Bunge hilo maalum.
Akizungumza wakati wa kufungua kikao cha thelathini na moja cha Bunge Maalum la Katiba ambalo limeanza kupokea taarifa za kamati zake, Sitta hata hivyo alisema atakuwa tayari kufanya hivyo kama wananchi wataona anafaa kwani wao ndio wenye dhamana ya kuchagua mtu wanayetaka awaongoza.
“Wengine wananikejeli, wanasema kwa shughuli hii naonesha sifai Urais, me sijaomba Urais,” alisema Sitta na kufuatiwa na idadi kubwa ya makofi bungeni hapo.
Sitta aliongeza: “Naifanya kazi hii kama Mwenyekiti wa Bunge la Katiba basi, lakini nasema wanaochagua ni wananchi, inawezekana mwakani, wananchi wa Tanzania wakatamani mtu mzima, aliyetulia na muadilifu, kama itakuwa hivyo wajue tupo na sisi wengine.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Wajumbe wa Bunge hilo wameanza kuwasilisha taarifa za kamati zao ambazo zimekaa kwa siku 15 wakijadili sura zilizokuwa zimebaki za Rasimu ya Katiba Mpya ambapo kulikuwa na maoni ya wajumbe wengi na wale wachache katika ibara mbalimbali za sura walizokuwa wakijadili.
Akiwasilisha maoni ya Kamati namba 12, mtoa maoni ya wengi, Thwaiba Kissasi alisema kamati yake pamoja na mambo mengine imependekeza kuongezwa kwa neno rangi na kutoa neno jinsi katika Ibara ndogo ya 3(a) (i) kutokana na kile walichokisema ni kukithiri kwa baadhi ya watu kubaguliwa kutokana na rangi zao.
Kamati 12 za Bunge hilo maalum zimeanza kuwasilisha taarifa zake kwenye Bunge hilo, baada ya kukaa kwa muda wa siku 15, wakijadili na kuichambua Rasimu ya Pili ya Katiba, ambapo kumekuwa na mabadiliko ya katika Sura mbalimbali huku baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo wakiwa wamesusia mchakato mzima unaoendelea. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na Mwananchi

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...