Friday, March 27, 2015
KILIMANJARO KINARA WA POMBE YA VIROBA
Mji wa Moshi, Tanzania
Utafiti mpya umebaini kuwa wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro wanaongoza kwa unywaji wa pombe hasa ya viroba, ikiwa ni mara nne zaidi ya wakazi wanaokunywa pombe katika mikoa ya Mwanza na Geita.
Utafiti mpya umebaini kuwa wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro wanaongoza kwa unywaji wa pombe hasa ya viroba, ikiwa ni mara nne zaidi ya wakazi wanaokunywa pombe katika mikoa ya Mwanza na Geita.
Katika utafiti huo uliofanywa na Taasisi ya Taifa
ya Utafiri wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kupitia mradi wa Strive
ulibaini kuwa idadi kubwa ya wanaokunywa pombe ni vijana wenye umri wa
kati ya miaka 15 hadi 24.
Utafiti huo wa NIMR ulilenga kujua ukubwa wa
Matumizi ya Pombe kwa vijana katika mikoa ya Kilimanjaro, Mwanza,
Geita na Kahama umebaini kuwa mkoa wa Kilimanjaro unaongoza kwa unywaji
wa pombe kwa vijana wenye umri kutokana na utamaduni uliopo mkoa huo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
LIL WAYNE AMTANGAZA CHRISTINA MILIAN KUWA MPENZI WAKE MPYA
BOSI wa kundi la Young Money, Lil Wayne, amemuweka wazi mpenzi wake mpya, Christina Milian, ambaye ni mmoja wa wanachama wa kundi hilo analoliongoza.
Baada ya kuweka wazi habari hiyo, Wayne kupitia mtandao wa Twitter, aliandika, “Samahani kwa kusubiri muda mrefu kujua nini kinaendelea, kwa sasa hakuna tena maswali nikiwa na Christina, huyu ni mpenzi wangu.”
Wayne ni baba wa watoto watano, na sasa yeye, mpenzi wake huyo na mtoto wake wa kwanza, Regina aliyezaa na mama mwingine wanafanya kazi pamoja katika kundi hilo.
Thursday, March 26, 2015
LOWASSA AKUBALI YAISHE URAIS CCM
Aliyekuwa
Waziri Mkuu Edward Lowassa
SIKU moja baada ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kumuonya aliyekuwa
Waziri Mkuu Edward Lowassa, kwa tuhuma za kukiuka Katiba na kuanza
kampeni za Urais kabla ya muda, kiongozi huyo ameibuka na kudai kuwa
hana njia ya kuwazuia watu wasimuombe agombee Urais.
Pia Lowassa ametumia nafasi hiyo na kuwaomba wale wote ambao bado
wana nia ya kumshawishi agombee nafasi hiyo ya urais, wasubiri kwanza
hadi pale chama chake hicho kitakapotoa maelekezo.
Akizungumza na vijana 60 wa bodaboda kutoka wilaya ya Mbarali, Mbeya
waliokwenda pia kumshawishi agombee nafasi hiyo, mjini Dodoma jana,
alisema si vyema kwa maofisa wa chama kuzungumzia masuala ya wanachama
wao kwenye vyombo vya habari wakati kuna vikao vya chama.
Alisema watu waliojitokeza na kumshawishi kuchukua fomu za kuwania
nafasi hiyo ya Urais, hajawaita wala kuwalipa chochote kama inavyodaiwa
na kwamba walikuwa wakifuata maneno ya Rais Jakaya Kikwete aliyoyatoa
mkoani Ruvuma katika sherehe za maadhimisho ya miaka 38 ya Uhuru.
Alisema katika siku hiyo, Rais Kikwete aliwataka watanzania
wawashawishi viongozi wanaoona wanafaa ili wajitokeze kugombea nafasi
hiyo ya Urais. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
'VIJANA WENGI HAWANA NGUVU ZA KIUME'
Mkurugenzi wa NIMR, Dk. Mwele Malecela
TAASISI ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR),imesema vijana wenye umri wa kuanzia miaka 30 na kuendelea, wanaongoza kwa kutumia dawa za kuongeza nguvu za kiume.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa NIMR, Dk. Mwele Malecela alisema kwa sasa tatizo hilo ni kubwa ambalo linawakumba vijana wengi hususan barani Afrika.
Alisema hali hiyo,imesababisha vijana hao kutafuta dawa za kuongeza nguvu za kiume aina ya Mundex, AAili waweze kupunguza ukubwa wa tatizo hilo.
“Vijana wengi wenye umri wa kuanzia miaka 30 na kuendelea wana matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume, jambo ambalo limewafanya kutafuta dawa za kuongeza nguvu ili waweze kuzitumia na kupunguza ukubwa wa tatizo.
“Tangu tugundue dawa hii, idadi kubwa ya wanaokuja kununua ni vijana hasa wenye umri wa miaka 30, hali ambayo inaonesha wazi kuwa tatizo hili linakua kwa kasi,” alisema Dk Mwele.
Alisema kipindi kilichopita, matatizo hayo yalikuwa yanawapata wanaume wenye umri wa kuanzia miaka 50 na kuendelea, lakini sasa hivi ni tofauti kabisa ambapo vijana wenye umri huo ndiyo wenye matatizo hayo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
ASKARI WAWILI MBARONI KWA FEDHA BANDIA
Jeshi la Polisi mkoani Simiyu linawashikilia
askari wawili wa magereza na polisi kwa kukutwa na noti bandia ikiwa
pamoja na sare za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Charles Mkumbo
alisema askari hao walikamatwa juzi saa tisa mchana katika Mtaa wa Old
Maswa, Kata ya Nyakabindi, wilayani Bariadi.
Alisema askari hao walifika kwenye kibanda cha
M-pesa kinachomilikiwa na Mwalimu wa Shule ya Sekondari Old Maswa,
Kassian Luhende (29) wakiwa na pikipiki aina ya Sunlg kwa lengo la
kuweka fedha hizo katika simu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
BABA MBARONI KWA KUWABAKA WATOTO WAKE...!!!
Mkazi mmoja wa Miembe Saba wilayani Kibaha
mkoani Pwani amekamatwa na polisi akituhumiwa kuwabaka watoto wake
wawili wadogo kwa zaidi ya miaka miwili sasa.
Habari zilizolifikia gazeti hili, zilisema kuwa
katika tukio hilo ambalo limethibitishwa na polisi na watoto wenyewe,
baba huyo alianza kuwafanyia binti zake vitendo hivyo mwaka 2013 kwa
siku ambazo mkewe ambaye nimama wa wasichana hao hakuwapo hadi usiku wa
Machi 19, mwaka huu. Kwa sasa tunayahifadhi majina ya familia hiyo.
Watoto hao mmoja mwenye umri wa miaka 15 anayesoma
darasa la saba na mdogo wake mwenye umri wa miaka 11 aliyeanza kubakwa
akiwa darasa la tatu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
MAREKANI: UGANDA HATARINI KUSHAMBULIWA
Ubalozi wa Marekani nchini Uganda, umesema una taarifa za uwezekano wa shambulio la kigaidi nchini humo.
Aidha Marekani pia imetoa tahadhari kwa raia wake. Taarifa
ya ubalozi huo umebainisha kwamba shambulio hilo linaweza kutekelezwa
wakati wowote, katika maeneo ambayo raia wa mataifa ya Magharibi na
Marekani hukutana.
Katika kipindi kilichopita, kundi la Al-Shaabab lenye makao yake Nchini Somalia, limetekeleza mashambulio Nchini Uganda. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
JESHI LA SAUDIA LASHAMBULIA WAASI, YEMEN
Saud Arabia imeanza operesheni zake za kijeshi nchini Yemen, ikiwa ni kujibu ombi la Rais wa nchi hiyo Abd Rabbuh Mansour Hadi. Balozi
wa Saudi Arabia Nchini Marekani amesema kuwa, taifa lake na washirika
wao wa ghuba wanatumia mashambulizi ya angani katika harakati za kuunga
mkono serikali halali ya Yemen, ili isichukuliwe na kundi wa waasi la
Houthi.
Awali duru zasema kuwa wapiganaji wa Houthi walikuwa wakikaribia kuutwa mji wa Aden, ulioko kusini mwa Nchi hiyo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
HODGSON KUONGEA ULAJI ENGLAND
Shirikisho
la kandanda nchini Uingereza limesema lina mpango wa kuwa na mazunguzo
na Kocha mkuu wa timu ya England Roy Hodgon mapema mwaka ujao.
Hodgon
mwenye miaka 67 alipokea mikoba ya kuifundisha England mwaka 2012
kutoka kwa Fabio Capello lakini timu ikatolewa mapema katika hatua ya
makundi kwenye kombe la dunia. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Tuesday, March 24, 2015
CCM WATOANA MACHO URAIS...!!!
JOTO la Uchaguzi wa Rais ndani ya CCM linazidi kupanda huku makada na viongozi wa chama hicho wakipigana vijembe hadharani.
Hali hiyo inatokana na kile kinachojitokeza sasa, kuibuka kwa makundi ya
jamii, wakiwamo wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu, kuwashawishi makada
kadhaa wa CCM wawanie nafasi hiyo ya uongozi wa nchi katika Uchaguzi
Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba.
Makada ambao wamekuwa wakishawishiwa kuwania nafasi hiyo ni Mbunge wa
Monduli, Edward Lowassa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu),
Profesa Mark Mwandosya na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa
Sospeter Muhongo.
Wakati baadhi ya makada wengine wanaotajwa kutaka kuwania urais ndani ya
CCM wakimlalamikia Lowassa, wachambuzi wa siasa wamekuwa wakihoji
mpango wa Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January
Makamba, alipochapisha vitabu na kugawa kwa wajumbe wote wa mkutano
mkuu, lakini makada wenzake wamekuwa kimya, hawajalalamikia kitendo
chake hicho.
KIKWETE AIONYA POLISI MATUMIZI YA NGUVU
RAIS Jakaya Kikwete amelitaka Jeshi la Polisi nchini kuacha kutumia
nguvu kupita kiasi kwa wananchi wakati linapotekeleza majukumu yake ya
kazi.
Pia amelitaka kuwa makini kutokana na nchi kukabiliwa na mambo matatu
muhimu ya uandikishaji Daftari la Kudumu la Wapigakura, kura ya maoni ya
Katiba Inayopendekezwa na Uchaguzi Mkuu.
Rais Kikwete aliyasema hayo Dar es Salaam jana alipofunga mafunzo ya
uongozi katika ngazi ya urakibu katika Chuo Cha Taaluma ya Polisi
Kurasini (DPA).
Alisema polisi wanayo haki ya kuwachukulia hatua wananchi wanapodai haki lakini wafuate utaratibu ili wasivunje amani.
Hata hivyo, Rais Kikwete aliwaonya wananchi kutokujichukulia sheria
mkononi akisema jeshi la polisi halitawafumbia macho watakaovunja
sheria. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
TOFAUTI YA ADA VYUO VIKUU SASA BASI
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
Anne Kilango
MWONGOZO wa ada elekezi utakaondoa utata wa utofauti wa kulipa ada
baina vyuo na vyuo nchini, unatarajiwa kukamilika na kuanza rasmi
kutumika mwezi ujao.
Kwa sasa mwongozo huo umeshaandaliwa na kinachosubiriwa ni mfumo wa
kompyuta utakaosaidia kukokotolea ada zitakazotumika katika vyuo vikuu
nchini ambao ndio utakamilika rasmi Aprili mwaka huu.
Hayo yalibainishwa na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
Anne Kilango, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Amina
Makilagi (CCM), aliyetaka kujua mchanganuo wa ada baina ya Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na endapo
unaendana na hali halisi.
Akijibu swali hilo, Kilango alikiri kuwa kumekuwa na tatizo hilo la
utofauti wa utozaji ada katika vyuo mbalimbali nchini kwa muda mrefu, na
kwa sasa Tanzania ina vyuo vikuu 53 na taasisi 21 zinazotoa shahada. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
DAVID CAMERON: AWAMU MBILII ZATOSHA...!!!
Waziri mkuu wa Uingereza, hataendelea tena na wadhfa wake huo, iwapo atarudi madarakani katika uchaguzi mkuu wa mwezi Mei. David
Cameron, ameiambia BBC kuwa, anadhani awamu ya tatu inaweza kuwa ni
kipindi kirefu kwake kukaa madarakani na kiongozi mpya ni vizuri
kuchaguliwa.
Chama kikuu cha upinzani cha Leba kimemshutumu Bwana
Cameron kwa kuonyesha uzembe na kushinikiza muhula wa tatu, kwa chama
chake cha Conservative, hata kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu ujao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
KAVUMBAGU: UWANJA ULITUKWAMISHA TANGA
Mshambuliaji wa Azam FC, Didier Kavumbagu
amesema walihitaji ushindi wa zaidi ya bao moja dhidi ya Coastal Union
ila walikwamishwa na uwanja mbovu wa Mkwakwani na kushindwa kuonyesha
kiwango chao cha juu.
Mechi hiyo iliyochezwa juzi ilimalizika kwa
ushindi wa bao 1-0 kwa Azam na kuendelea kukaa katika nafasi ya pili
kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi 36 nyuma ya pointi moja
dhidi ya Yanga wenye 37.
Bao pekee la Azam lilifungwa na mshambuliaji wao,
John Bocco, na Kavumbagu alilazimika kutolewa nje huku nafasi yake
ikichukuliwa na Gaudence Mwaikimba. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
CANNAVARO ATAKA MABAO MENGI YANGA
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’
amewataka wachezaji wenzake kuhakikisha wanafunga mabao mengi na
kutoruhusu bao katika kila mechi watakayocheza kama wana nia ya
kuipokonya ubingwa Azam FC.
Cannavaro alisema katika kipindi hiki ambacho
Yanga na Azam FC zinaeendelea kushindana kileleni mwa msimamo wa Ligi
Kuu kitu pekee kinachotakiwa ni kufunga mabao mengi ili mwisho tofauti
ya mabao inaweza kuamua bingwa.
Cannavaro alisema kwa hatua ambayo ligi imefikia
ni lazima kila mchezaji apambane kuhakikisha timu inamaliza ikiwa bingwa
na si vinginevyo kwani malengo yao msimu huu yalikuwa ni kutwaa taji.
“Inapotokea nafasi ya kufunga tunatakiwa tufunge
pasipo kuangalia kuwa mfungaji ni beki, kiungo au mshambuliaji. Pia
wakati wa kujilinda inatakiwa kila mchezaji ashiriki kuzuia na kulinda
magoli, hapo tunaweza kuwa mabingwa bila wasiwasi.
Njia nzuri zaidi ya kuonyesha hilo ni angalau kufunga mabao mawili kwenye kila mechi mpaka mwisho wa msimu,” alisema Cannavaro.
Cannavaro alisema ushindi walioupata dhidi ya
Mgambo JKT juzi Jumapili, umerudisha morali ya kikosi chao kuelekea
mechi za mwishoni mwa ligi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
MOICT YA KENYA WAIBUKA MABINGWA WA NETIBOLI
Michuano
ya netball ya Afrika ya Mashariki imemalizika Zanzibar huku timu ya
MOICT ya Kenya ikitwaa ubingwa kwa upande wa wanawake baada ya kuifunga
timu ya NIC ya Uganda kwa mabao 32-29.
NIC ndio walikuwa mabingwa
watetezi baada ya kulinyakua kombe hilo mwaka jana katika michuano
iliyofanyika Dar es Salaam. Hii ni mara ya pili kwa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania kuandaa michuano hiyo mara mbili mfululizo, zamu hii ikiwa
ni upande wa Tanzania Zanzibar (visiwani) katika viwanja vya Gymkhana.
Netball,
au mpira wa pete ni mchezo ambao kwa miaka mingi umekuwa ukihusisha
timu za wanawake pekee, lakini katika kuleta usawa (gender balance) kama
ilivyo kwa michezo mingine kama vile mpira wa kikapu (basketball), wavu
na mingineyo, mchezo huo katika miaka ya hivi karibuni, umekuwa
ukishirikisha timu za wanaume katika kuleta hamasa na ushindani.
Kwa
upande wa wanaume, wenyeji Polisi ya Zanzibar waliibuka washindi wa
michuano hiyo ya Afrika Mashariki, baada ya kuwafunga wenzao wa JKU (pia
ya Zanzibar) kwa mabao 38-34 katika mechi ya vuta nikuvute.
Michuano
hiyo hufanyika kila mwaka kwa nchi wanachama kupeana zamu za kuandaa
mashindano hayo. Nchi zilizoshiriki ni wenyeji Zanzibar, Kenya, Uganda
na Tanzania Bara.
Rwanda na Burundi ni sehemu ya jumuiya hiyo ya Afrika
ya Mashariki lakini hawana historia kubwa ya kuwa sehemu ya kuwa nchi
shiriki. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
WANASOKA WA NJE KUPUNGUZWA ENGLAND
Shirikisho
la kanda kanda nchini England FA sasa linakusudia kuandaa sheria
itakayo kupunguza idadi ya wachezaji kutoka nje ya nchi za Umoja wa
Ulaya watakaosajiliwa katika ligi za nchi hiyo.
Mwenyekiti wa
shirikisho hilo Greg Dyke asema kwamba ligi kuu ya England ipo kwenye
hatari ya kutowasaidia wachezaji raia wa Uingereza kama hatua
hazitachukuliwa.
Katika mpango pia itaweka sheria ngumu kwa wachazaji wenye vipaji waliokulia nchini humo.
Mikakati hiyo yote ni ya kuimarisha timu ya taifa ya England ambayo imekuwa haifanyi vizuri kwenye mechi za kimataifa. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Thursday, March 19, 2015
UKAWA WAGAWANA MAJIMBO 211
KAMATI maalumu ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), imekamilisha kazi ya ugawaji wa majimbo 211 ambayo ni sawa na asilimia 88 kati ya majimbo yote 239, imefahamika.
Wakati hayo yakiendelea, kamati hiyo imeshindwa kuafikiana katika majimbo 28 ambayo yanasubiri uamuzi wa wenyeviti wa vyama vinavyounda Ukawa, ambao watamaliza kiporo hicho mwezi huu.
Hatua hiyo imekuja baada ya viongozi wa juu wa umoja huo, kutangaza mkakati wa kusimamisha mgombea mmoja wa urais na kuachiana majimbo ya uchaguzi katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba. Ukawa ni umoja ulioanzishwa Februari mwaka jana wakati wa Bunge Maalumu la Katiba, ukiundwa na vyama vya NCCR-Mageuzi, Chadema, CUF na NLD.
Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya kamati hiyo maalumu ya Ukawa, kiliiambia MTANZANIA jana kuwa kwa muda wa wiki moja sasa, kamati hiyo imekamilisha kazi hiyo kwa kiwango kikubwa jambo ambalo limeelezwa linaweza kutoa upinzani mkali kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
KIKWETE AWAONYA WANAOHUJUMU KATIBA MPYA
Rais
Jakaya Kikwete akiwa na wakuu wa wilaya wapya walioteuliwa hivi karibuni.
RAIS
Jakaya Kikwete ameziagiza mamlaka za ulinzi na usalama kuhakikisha
shughuli ya kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura, upigaji kura ya
Katiba Inayopendekezwa unafanyika kwa amani na wasioitakia mema nchi
wasibadilishe matukio hayo kuwa fujo na kuingiza nchi kwenye vurugu.
Alitoa kauli hiyo juzi wakati akifungua mafunzo elekezi kwa wakuu
wapya 27 wa wilaya walioteuliwa hivi karibuni huku akiwataka kuwa na
ushirikiano na vyama vyote vya siasa.
Alisema kazi ya kuboresha daftari la wapiga kura, imeanzia Njombe na
itaendelea mikoa mingine na kuwataka viongozi hao kuhamasisha wananchi
kujitokeza kwa wingi na kukumbusha maana ya kuwa na kitambulisho cha
kura ambacho kitamwezesha kupiga kura ya maoni na katika uchaguzi mkuu
mwaka huu.
“Wananchi wasipoteze fursa waone haja ya kujiandikisha na watakaokosa
fursa ya kupiga kura hawataipata fursa hiyo tena. Tunataka Watanzania
wenye sifa washiriki kikamilifu kuhimiza wananchi wajiandikishe, na
kupiga kura,” alisema. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
WAMILIKI WA MABASI WACHARUKIA NAULI...!!!
WAKATI
wadau wa usafiri nchini wakipendekeza kushuka kwa nauli za daladala na
mabasi yaendayo mikoani, wamiliki wa mabasi wametishia kufuta utaratibu
wa kutowatoza nauli askari na kuongeza kuwa, hata nauli pungufu za
wanafunzi sasa zitakuwa historia.
Wadau wamependekeza kupunguzwa kwa nauli za mabasi yaendayo mikoani
kwa viwango vya kati ya asilimia 15 na 25 huku wakitaka nauli za
daladala zipungue kutoka Sh 400 hadi Sh 300 kwa njia ya umbali wa
kilometa 10.
Hayo yaliibuka jana wakati wa mkutano wa wadau kukusanya maoni kuhusu
mapitio ya viwango vya nauli za mabasi ya mikoani na daladala kupungua
kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta ulioandaliwa na Mamlaka ya
Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra). Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
WANAZUONI WA KIISLAMU WAJIBU HOJA YA MAASKOFU
Taasisi ya Masheikh na Wanazuoni
wa Kiislamu Tanzania imejibu hoja zilizotolewa wiki iliyopita na Jukwaa
la Wakristo nchini kuhusu Katiba Inayopendekezwa, Mahakama ya Kadhi na
hali ya usalama na amani ya nchi.
Machi 10, mwaka huu maaskofu kupitia Jukwaa la
Wakristo Tanzania walitoa tamko na kuwataka waumini wao kuipigia kura ya
hapana, Katiba Inayopendekezwa kwa sababu imepatikana kwa njia za hila
na kibabe, jambo ambalo sasa limesababisha mvutano.
Katika tamko hilo lililosainiwa na Mwenyekiti wa
Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT),
Askofu Dk Alex Malasusa, Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Tarcicius Ngalalekumtwa na Mwenyekiti wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (CPCT), Askofu Daniel Awet, maaskofu hao walisema uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi ni uvunjifu wa Katiba na kuwa unahatarisha amani ya nchi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Askofu Dk Alex Malasusa, Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Tarcicius Ngalalekumtwa na Mwenyekiti wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (CPCT), Askofu Daniel Awet, maaskofu hao walisema uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi ni uvunjifu wa Katiba na kuwa unahatarisha amani ya nchi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
FDLR TISHIO MASHARIKI MWA DRC
Wajumbe
wa mashirika ya kiraia wa vijiji vya Tama na Itala kusini mwa tarafa la
Lubero jimboni kivu kaskazini, wanasema kutishiwa na kundi la waasi wa
kihutu toka Rwanda wa FDLR kundi wanao ongozwa na Kanali Kizito.
Vitisho
hivyo vinakuja kutoka uchapishaji wa ripoti wa mashirika ya kiraia
katika sekta hio inayo bainisha hali ya harakati makundi ya waasi na
wanamgambo katika maeneo hayo ambao wanahusika naunyanyasaji dhidi ya
raia.
Baadhi ya wanachama wa vyama vya kiraia katika vijiji vya
Tama na Itala wanasema kua raia katika maeneo hayo wanaishi katika hali
ya mafichoni kwa siku tano sasa kulingana na unyanyasaji kutoka waasi
wanao hishi maeneo hayo hasa FDLR huku wakisema nawaishi kwa tabu
wakilala usiku misituni. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
MAN CITY WATOLEWA LIGI YA MABINGWA
Timu
za England zimetolewa katika kinyang'anyiro cha michuano klabu bingwa
barani Ulaya,baada ya Man City kuchabangwa bao 1-0 dhidi ya Barcelona na
kuondolewa katika mashindano hayo, ilikuwa zamu ya Manchester City
kufuata nyayo za waingereza wenzao kutupwa nje ya mashindano na miamba
ya soka ya Hispania Barcelona. Katika kipute hicho kilichopigwa katika
dimba la Nou Camp.
Na huko nchini Ujerumani vijana wa Jurgen Klopp Borussia Dotmund, ilikiona cha moto baada ya kutandikwa bao 3 kwa mshangao dhidi ya Juventus ya Italia,katika mtanange huo uliopigwa katika dimba la Sigunal Iduna Park, mchezaji Carlos Tevez ndiye aliyepeleka msiba kwa Wajerumani hao kwa kutumbukiza kimiani mabao mawili.
Dakika tatu tu za mchezo huo zilimtosha Tevezi kufunga bao la kuongoza kabla ya Morata kuandika bao la pili dakika ya 70 na kisha Tevez kutikisa tena nyavu katika dakika ya 79. Matokeo ya jumla kati ya timu hizo mbili yanakuwa ni 5-1 baada ya Juventus kushinda 2-1 katika mchezo wa awali. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Wednesday, March 18, 2015
BAADA YA VURUGU KUDUMU KWA SIKU TATU MFURULIZO, HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA TUNDUMA LEO MCHANA
Mkazi wa Tunduma ambae jina lake halikufahamika mara moja akionyesha bomu la machozi ambalo halijatumika alilomnyang'anya askari na kukimbia nalo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz. |
NYALANDU AMJIBU KINANA; 'SASA NITAZURURA ANGANI KUPAMBANA NA MAJANGILI'
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akielekezwa kitu na wataalam wa ndege hiyo aliyozindua jana.
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu jana alionekana kumpiga kijembe Katibu MKuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana aliposema kuwa sasa atakuwa anazurura angani.
Nyalandu alitoa kauli hiyo Dar es Salaam alipozindua ndege nyepesi (Micro-Light, 5H – Hel), ambayo itatumika kupambana na ujangili katika Hifadhi ya Taifa ya Selous.
“Karibuni wote, leo tunazururia hapa uwanja wa ndege na ninazindua ndege hii nyepesi ambayo imetengenezwa Ufaransa, itatumika kupambana na majangili katika Mbuga ya Selous.
“Kwa maana hiyo sasa tunaanza kuzururia angani kupambana na majangili na nasisitiza kwamba ndege hii ni mpya kabisa na gharama za uendeshaji wake ni ndogo kwa vile inatumia petroli,” alisema.
Hivi karibuni Kinana akiwa ziarani mkoani Arusha alimsifia Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa (CCM) kuwa ni mchapakazi lakini Waziri Nyalandu ni mzururaji.
Akizungumza jana wakati wa uzinduzi wa ndege hiyo ya kupambana na ujangili, Nyalandu alisema imetengenezwa kwa gharama ya Dola za Marekani 2,040,000 na ina uwezo wa kubeba askari mmoja na rubani.
Waziri Nyalandu alisema ndege hiyo imeundwa kwa usalama wa hali ya juu kwa kuwekewa puto (parachute) ambalo litatumika kushuka chini iwapo ndege itaishiwa mafuta angani.
“Itakapoanza kutumika itasaidia kuwabaini majangili, inakwenda kwa mwendo mdogo iwapo angani hali ambayo inawezesha kuwaona majangili na kila kinachoendelea ardhini kwa wepesi,”alisema Nyalandu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
UBUNGE WA ZITTO WANING'INIA...!!!
Kitendo cha kutupiana mpira kati ya Ofisi ya Bunge, Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuhusu
hatima ya Zitto Kabwe, kimeufanya ubunge wa mbunge huyo kuendelea
kuning’inia huku mwenyewe akitazamiwa leo kueleza anachoita ‘maamuzi
magumu’.
Kutupiana mpira kulijitokeza jana baada ya Spika
wa Bunge, Anne Makinda kusema Bunge linasubiri taarifa rasmi ya
kufukuzwa uanachama kwa mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kutoka NEC,
ambayo hata hivyo, nayo ilisema inasubiri taarifa kutoka Chadema huku
chama hicho kikisema kinashughulikia kwanza kesi zinazowakabili
wanachama wake wanaotuhumiwa kumpiga aliyekuwa mlinzi wa Katibu Mkuu
wake, Dk Willibrod Slaa.
Wakati Makinda akieleza hayo, taarifa kutoka kwa
watu wa karibu wa mbunge Zitto zilieleza kuwa leo ataibuka bungeni kwa
nia ya kuwaaga wabunge kama alivyoahidi wiki iliyopita. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
'KURA YA MAONI IPO PALE PALE'
Kaimu kiongozi wa shughuli za serikali bungeni Mh. Samuel Sitta.
SERIKALI imesema haiwezi kubadili msimamo wake kuhusu upigaji wa Kura
ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa, licha ya kuwepo maoni ya viongozi
wa dini ambao wanataka jambo hilo lisitishwe.
Kaimu Kiongozi wa shughuli za Serikali bungeni, Samuel Sitta alisema
jana mjini hapa kuwa pamoja na kuwepo kwa tofauti kati ya Jukwaa la
Wakristo na Kiongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam,
Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, msimamo wa Serikali uko pale pale.
Sitta, ambaye anakaimu shughuli za serikali bungeni kutokana na
kutokuwepo kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alisema Serikali inakubaliana
na maoni ya Kardinali Pengo kuwa waumini waachwe waamue wenyewe kuhusu
Katiba Inayopendekezwa.
Alisema kama viongozi wa dini wamegawanyika hakuna namna ya kuwafanya
wawe na kauli moja, lakini akasisitiza kuwa jambo la msingi ni kuachwa
kwa mtu aamue mwenyewe aina ya kura atakayopiga.
Hivi karibuni Pengo alitofautiana na Baraza la Maaskofu (TEC) na
Jukwaa la Wakristo ambao wanataka upigaji wa kura ya maoni usitishwe,
kwa maelezo kuwa wananchi hawajapewa muda wa kuisoma na kuielewa katiba
hiyo na kama Serikali itang’ang’ania ni vyema waumini wa kanisa wapige
kura ya hapana. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
MAASKOFU WA JUKWAA LA WAKRISTO WAMEKOLEZA MOTO KUIKATAA KATIBA
Gazeti la Mwananchi la Machi 13, 2015 lilibeba
ujumbe mzito kwa Watanzania. Kichwa cha habari kimoja kilisomeka:
“Maaskofu: Pigieni Katiba kura ya hapana.”
Maaskofu wa Jukwaa la Wakristo ambao ni Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Kikristo (CCT), Askofu Dk Alex Malasusa, Mwenyekiti wa
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Askofu Tarcicius
Ngalalekumtwa na Mwenyekiti wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (CPCT)
Askofu Daniel Awet, kwa sauti moja wamewataka waumini wao kujiandikisha
kwa wingi katika Daftari la Wapigakura, kuisoma vyema Katiba
Inayopendekezwa na hatimaye kuikataa kwa kuipigia kura ya ‘hapana.’
Sababu kuu za kuwahamasisha waumini wao na
Watanzania kuikataa Katiba Pendekezwa ni mbili. Mosi ni kulazimisha kura
ya maoni ya katiba mpya kufanyika bila maandalizi ya kutosha, yakiwamo
maridhiano ambayo yameligawa Taifa katika vipande vipande. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
AL SHABAAB YAUA WATU WATATU NCHINI KENYA
Maafisa wa polisi nchini Kenya wanasema kuwa takriban watu watatu
wameuawa katika mji wa kazkazini wa Wajir, yapata kilomita 100 kutoka
mpaka na Somalia. Watu waliofunika nyuso zao walishambulia duka moja na kufyatua risasi, kulirushia magurunedi kabla ya kulichoma.
Kundi
la wapiganaji wa Al-Shabaab limeongeza mashambulizi yake kazkazini
mashariki mwa Kenya katika siku za hivi karibuni ,na kufanya
mashambulizi mawili katika mji wa Mandera ambao una pakana na Somali.
Kundi hilo linadhibiti eneo kubwa la Somalia la mashambani na limesajili idadi kubwa ya raia Wakenya. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Na BBC
MAKAMU WA RAIS WA S LEONE AFUTWA KAZI
Rais wa Sierra Leone Ernest Bai Koroma amemfuta kazi makamu wa rais kwa kutafuta hifadhi katika ubalozi wa kigeni nchini humo. Siku
ya jumamosi ,Samuel Sam Sumana amesema kuwa alimtaka balozi wa Marekani
kumpatia hifadhi ndani ya ubalozi wa Marekani nchini humo akihofia
maisha yake.
Awali wanajeshi waliizunguka nyumbani yake na kumpokonya silaha mlinzi wake .
Kumekuwa na wasiwasi kati ya rais na bwana Sam Sumana. Hivi majuzi aliondolewa katika chama tawala cha All People Congress kwa udanganyifu na kuchochea ghasia. Hatahivyo amekana madai hayo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Na BBC
MONACO HAWAKUSTAHILI KUSONGA MBELE
Meneja
wa klabu ya soka ya Arsenal Mfaransa Arsene Wenger anaamini timu ya
Monaco haikustahili kusonga mbele kwenye hatua ya nane bora ya ligi ya
mabigwa ulaya.
Licha ya Arsenal kuibuka na ushindi wa mabao 2-0
dhidi ya Monaco walishindwa kufuzu kwa nane bora baada ya kupoteza
mchezo wa kwanza kwa kuchapwa 3-1.
Kocha Wenger amesema haamini
kama timu hiyo ilitakiwa kusonga mbele “ukiangalia idadi ya mashuti
yaliyolenga goli utashangaa, kupoteza mchezo kunauma ila hatujapoteza."
Hii imekua ni mara ya tano mfululizo kwa washika bunduki hao wa London kushindwa kufuzu hatua ya nane bora. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
SERENA WILLIAMS ATINGA NANE BORA
Nyota wa mchezo wa tenesi Serena Williams ametinga katika hatua ya nane bora ya michuano ya BNP huko Indian Wells. Serena
amefanikiwa kufanya vizuri kwa kumshinda Sloane Stephens anayeshika
nafasi ya 33 kwa ubora wa dunia kwa seti 6-7 (7-3) 6-2 6-2,
Sloane alipoteza mchezo huu baada ya kushindwa kuhimili mikiki miki ya mpinzani wake aliekua anacheza kwa juhudi kubwa.
Williams alikataa kucheza hapo baada ya kufanyiwa vitembo vya kudharauriwa mwaka 2001. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Monday, March 16, 2015
WAHAMIAJI 64 KUTOKA ETHIOPIA WAKAMATWA
Polisi
mkoa wa Dodoma nchini Tanzania wanawashikilia wahamiaji haram 64 raia
wa Ethiopia, huku mmoja wao akipatikana akiwa amekufa.
Kamanda wa
Polisi mkoa wa Dodoma amenukuliwa akisema wanamshikilia dereva wa gari
lililokuwa limewabeba watu hao ambao inaaminika walikuwa njiani kuelekea
kusini mwa Afrika.
Hii si mara ya kwanza kwa wahamiaji wa aina hiyo kukamatwa katika mazingira hayo.
Mwaka
2012 watu 42 kutoka Eritrea walikutwa wamekufa katika lori mkoa wa
Dodoma kwa kile kinachosemekana ni kukosa hewa kutokana na kufichwa
ndani ya lori hilo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Subscribe to:
Posts (Atom)