Tuesday, March 24, 2015

KIKWETE AIONYA POLISI MATUMIZI YA NGUVU

jk
RAIS Jakaya Kikwete amelitaka Jeshi la Polisi nchini kuacha kutumia nguvu kupita kiasi kwa wananchi wakati linapotekeleza majukumu yake ya kazi.

Pia amelitaka kuwa makini kutokana na nchi kukabiliwa na mambo matatu muhimu ya uandikishaji Daftari la Kudumu la Wapigakura, kura ya maoni ya Katiba Inayopendekezwa na Uchaguzi Mkuu.

Rais Kikwete aliyasema hayo Dar es Salaam jana alipofunga mafunzo ya uongozi katika ngazi ya urakibu katika Chuo Cha Taaluma ya Polisi Kurasini (DPA).
Alisema polisi wanayo haki ya kuwachukulia hatua wananchi wanapodai haki lakini wafuate utaratibu ili wasivunje amani.

Hata hivyo, Rais Kikwete aliwaonya wananchi kutokujichukulia sheria mkononi akisema jeshi la polisi halitawafumbia macho watakaovunja sheria. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TOFAUTI YA ADA VYUO VIKUU SASA BASI

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango

MWONGOZO wa ada elekezi utakaondoa utata wa utofauti wa kulipa ada baina vyuo na vyuo nchini, unatarajiwa kukamilika na kuanza rasmi kutumika mwezi ujao.
Kwa sasa mwongozo huo umeshaandaliwa na kinachosubiriwa ni mfumo wa kompyuta utakaosaidia kukokotolea ada zitakazotumika katika vyuo vikuu nchini ambao ndio utakamilika rasmi Aprili mwaka huu.
Hayo yalibainishwa na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Amina Makilagi (CCM), aliyetaka kujua mchanganuo wa ada baina ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na endapo unaendana na hali halisi.
Akijibu swali hilo, Kilango alikiri kuwa kumekuwa na tatizo hilo la utofauti wa utozaji ada katika vyuo mbalimbali nchini kwa muda mrefu, na kwa sasa Tanzania ina vyuo vikuu 53 na taasisi 21 zinazotoa shahada. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MARCHI 24, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.

.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

DAVID CAMERON: AWAMU MBILII ZATOSHA...!!!

David Cameron
Waziri mkuu wa Uingereza, hataendelea tena na wadhfa wake huo, iwapo atarudi madarakani katika uchaguzi mkuu wa mwezi Mei. David Cameron, ameiambia BBC kuwa, anadhani awamu ya tatu inaweza kuwa ni kipindi kirefu kwake kukaa madarakani na kiongozi mpya ni vizuri kuchaguliwa.

Chama kikuu cha upinzani cha Leba kimemshutumu Bwana Cameron kwa kuonyesha uzembe na kushinikiza muhula wa tatu, kwa chama chake cha Conservative, hata kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu ujao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KAVUMBAGU: UWANJA ULITUKWAMISHA TANGA

 

Mabeki wa Coastal Union wakiwahani mpira na wachezaji waAzam wakati wa mchezo wa Ligi kuu Tanzania Bara uliochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani ,Tangajuzi.Azam ilishinda 1-0.

Mshambuliaji wa Azam FC, Didier Kavumbagu amesema walihitaji ushindi wa zaidi ya bao moja dhidi ya Coastal Union ila walikwamishwa na uwanja mbovu wa Mkwakwani na kushindwa kuonyesha kiwango chao cha juu.

Mechi hiyo iliyochezwa juzi ilimalizika kwa ushindi wa bao 1-0 kwa Azam na kuendelea kukaa katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi 36 nyuma ya pointi moja dhidi ya Yanga wenye 37.

Bao pekee la Azam lilifungwa na mshambuliaji wao, John Bocco, na Kavumbagu alilazimika kutolewa nje huku nafasi yake ikichukuliwa na Gaudence Mwaikimba. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

CANNAVARO ATAKA MABAO MENGI YANGA

 Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro
 
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amewataka wachezaji wenzake kuhakikisha wanafunga mabao mengi na kutoruhusu bao katika kila mechi watakayocheza kama wana nia ya kuipokonya ubingwa Azam FC.
Cannavaro alisema katika kipindi hiki ambacho Yanga na Azam FC zinaeendelea kushindana kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu kitu pekee kinachotakiwa ni kufunga mabao mengi ili mwisho tofauti ya mabao inaweza kuamua bingwa.
Cannavaro alisema kwa hatua ambayo ligi imefikia ni lazima kila mchezaji apambane kuhakikisha timu inamaliza ikiwa bingwa na si vinginevyo kwani malengo yao msimu huu yalikuwa ni kutwaa taji.
“Inapotokea nafasi ya kufunga tunatakiwa tufunge pasipo kuangalia kuwa mfungaji ni beki, kiungo au mshambuliaji. Pia wakati wa kujilinda inatakiwa kila mchezaji ashiriki kuzuia na kulinda magoli, hapo tunaweza kuwa mabingwa bila wasiwasi.
Njia nzuri zaidi ya kuonyesha hilo ni angalau kufunga mabao mawili kwenye kila mechi mpaka mwisho wa msimu,” alisema Cannavaro.
Cannavaro alisema ushindi walioupata dhidi ya Mgambo JKT juzi Jumapili, umerudisha morali ya kikosi chao kuelekea mechi za mwishoni mwa ligi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MOICT YA KENYA WAIBUKA MABINGWA WA NETIBOLI

Raisi wa TFF Jamal Malinzi
Michuano ya netball ya Afrika ya Mashariki imemalizika Zanzibar huku timu ya MOICT ya Kenya ikitwaa ubingwa kwa upande wa wanawake baada ya kuifunga timu ya NIC ya Uganda kwa mabao 32-29.

NIC ndio walikuwa mabingwa watetezi baada ya kulinyakua kombe hilo mwaka jana katika michuano iliyofanyika Dar es Salaam. Hii ni mara ya pili kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuandaa michuano hiyo mara mbili mfululizo, zamu hii ikiwa ni upande wa Tanzania Zanzibar (visiwani) katika viwanja vya Gymkhana.

Netball, au mpira wa pete ni mchezo ambao kwa miaka mingi umekuwa ukihusisha timu za wanawake pekee, lakini katika kuleta usawa (gender balance) kama ilivyo kwa michezo mingine kama vile mpira wa kikapu (basketball), wavu na mingineyo, mchezo huo katika miaka ya hivi karibuni, umekuwa ukishirikisha timu za wanaume katika kuleta hamasa na ushindani.

Kwa upande wa wanaume, wenyeji Polisi ya Zanzibar waliibuka washindi wa michuano hiyo ya Afrika Mashariki, baada ya kuwafunga wenzao wa JKU (pia ya Zanzibar) kwa mabao 38-34 katika mechi ya vuta nikuvute.

Michuano hiyo hufanyika kila mwaka kwa nchi wanachama kupeana zamu za kuandaa mashindano hayo. Nchi zilizoshiriki ni wenyeji Zanzibar, Kenya, Uganda na Tanzania Bara. 

Rwanda na Burundi ni sehemu ya jumuiya hiyo ya Afrika ya Mashariki lakini hawana historia kubwa ya kuwa sehemu ya kuwa nchi shiriki. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WANASOKA WA NJE KUPUNGUZWA ENGLAND


Baadhi ya wachezaji wa kiafrika watakaathirika na sheria hiyo.
Shirikisho la kanda kanda nchini England FA sasa linakusudia kuandaa sheria itakayo kupunguza idadi ya wachezaji kutoka nje ya nchi za Umoja wa Ulaya watakaosajiliwa katika ligi za nchi hiyo.
Mwenyekiti wa shirikisho hilo Greg Dyke asema kwamba ligi kuu ya England ipo kwenye hatari ya kutowasaidia wachezaji raia wa Uingereza kama hatua hazitachukuliwa.
Katika mpango pia itaweka sheria ngumu kwa wachazaji wenye vipaji waliokulia nchini humo.
Mikakati hiyo yote ni ya kuimarisha timu ya taifa ya England ambayo imekuwa haifanyi vizuri kwenye mechi za kimataifa. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Thursday, March 19, 2015

UKAWA WAGAWANA MAJIMBO 211

ukawa
 KAMATI maalumu ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), imekamilisha kazi ya ugawaji wa majimbo 211 ambayo ni sawa na asilimia 88 kati ya majimbo yote 239, imefahamika.

Wakati hayo yakiendelea, kamati hiyo imeshindwa kuafikiana katika majimbo 28 ambayo yanasubiri uamuzi wa wenyeviti wa vyama vinavyounda Ukawa, ambao watamaliza kiporo hicho mwezi huu.

Hatua hiyo imekuja baada ya viongozi wa juu wa umoja huo, kutangaza mkakati wa kusimamisha mgombea mmoja wa urais na kuachiana majimbo ya uchaguzi katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba. Ukawa ni umoja ulioanzishwa Februari mwaka jana wakati wa Bunge Maalumu la Katiba, ukiundwa na vyama vya NCCR-Mageuzi, Chadema, CUF na NLD. 

Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya kamati hiyo maalumu ya Ukawa, kiliiambia MTANZANIA jana kuwa kwa muda wa wiki moja sasa, kamati hiyo imekamilisha kazi hiyo kwa kiwango kikubwa jambo ambalo limeelezwa linaweza kutoa upinzani mkali kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KIKWETE AWAONYA WANAOHUJUMU KATIBA MPYA

Rais Jakaya Kikwete akiwa na wakuu wa wilaya wapya walioteuliwa hivi karibuni.

RAIS Jakaya Kikwete ameziagiza mamlaka za ulinzi na usalama kuhakikisha shughuli ya kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura, upigaji kura ya Katiba Inayopendekezwa unafanyika kwa amani na wasioitakia mema nchi wasibadilishe matukio hayo kuwa fujo na kuingiza nchi kwenye vurugu.

Alitoa kauli hiyo juzi wakati akifungua mafunzo elekezi kwa wakuu wapya 27 wa wilaya walioteuliwa hivi karibuni huku akiwataka kuwa na ushirikiano na vyama vyote vya siasa.

Alisema kazi ya kuboresha daftari la wapiga kura, imeanzia Njombe na itaendelea mikoa mingine na kuwataka viongozi hao kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi na kukumbusha maana ya kuwa na kitambulisho cha kura ambacho kitamwezesha kupiga kura ya maoni na katika uchaguzi mkuu mwaka huu.

“Wananchi wasipoteze fursa waone haja ya kujiandikisha na watakaokosa fursa ya kupiga kura hawataipata fursa hiyo tena. Tunataka Watanzania wenye sifa washiriki kikamilifu kuhimiza wananchi wajiandikishe, na kupiga kura,” alisema. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WAMILIKI WA MABASI WACHARUKIA NAULI...!!!

WAKATI wadau wa usafiri nchini wakipendekeza kushuka kwa nauli za daladala na mabasi yaendayo mikoani, wamiliki wa mabasi wametishia kufuta utaratibu wa kutowatoza nauli askari na kuongeza kuwa, hata nauli pungufu za wanafunzi sasa zitakuwa historia.

Wadau wamependekeza kupunguzwa kwa nauli za mabasi yaendayo mikoani kwa viwango vya kati ya asilimia 15 na 25 huku wakitaka nauli za daladala zipungue kutoka Sh 400 hadi Sh 300 kwa njia ya umbali wa kilometa 10.

Hayo yaliibuka jana wakati wa mkutano wa wadau kukusanya maoni kuhusu mapitio ya viwango vya nauli za mabasi ya mikoani na daladala kupungua kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta ulioandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra). Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WANAZUONI WA KIISLAMU WAJIBU HOJA YA MAASKOFU

Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Masheikh na wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Khamis Mataka akizungumza jijini Dar es Salaam jana kuhusu msimamo wa taasisi hiyo kuhusu Mahakama ya Kadhi, kuli ni Sheikh Mohamed Id

Taasisi ya Masheikh na Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania imejibu hoja zilizotolewa wiki iliyopita na Jukwaa la Wakristo nchini kuhusu Katiba Inayopendekezwa, Mahakama ya Kadhi na hali ya usalama na amani ya nchi.

Machi 10, mwaka huu maaskofu kupitia Jukwaa la Wakristo Tanzania walitoa tamko na kuwataka waumini wao kuipigia kura ya hapana, Katiba Inayopendekezwa kwa sababu imepatikana kwa njia za hila na kibabe, jambo ambalo sasa limesababisha mvutano.
Katika tamko hilo lililosainiwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), 

Askofu Dk Alex Malasusa, Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Tarcicius Ngalalekumtwa na Mwenyekiti wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (CPCT), Askofu Daniel Awet, maaskofu hao walisema uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi ni uvunjifu wa Katiba na kuwa unahatarisha amani ya nchi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

FDLR TISHIO MASHARIKI MWA DRC

 Wapiganaji wa FDLR
Wajumbe wa mashirika ya kiraia wa vijiji vya Tama na Itala kusini mwa tarafa la Lubero jimboni kivu kaskazini, wanasema kutishiwa na kundi la waasi wa kihutu toka Rwanda wa FDLR kundi wanao ongozwa na Kanali Kizito.

Vitisho hivyo vinakuja kutoka uchapishaji wa ripoti wa mashirika ya kiraia katika sekta hio inayo bainisha hali ya harakati makundi ya waasi na wanamgambo katika maeneo hayo ambao wanahusika naunyanyasaji dhidi ya raia.

Baadhi ya wanachama wa vyama vya kiraia katika vijiji vya Tama na Itala wanasema kua raia katika maeneo hayo wanaishi katika hali ya mafichoni kwa siku tano sasa kulingana na unyanyasaji kutoka waasi wanao hishi maeneo hayo hasa FDLR huku wakisema nawaishi kwa tabu wakilala usiku misituni. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MARCHI 19, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAN CITY WATOLEWA LIGI YA MABINGWA

Barcelona na Manchester city
Timu za England zimetolewa katika kinyang'anyiro cha michuano klabu bingwa barani Ulaya,baada ya Man City kuchabangwa bao 1-0 dhidi ya Barcelona na kuondolewa katika mashindano hayo, ilikuwa zamu ya Manchester City kufuata nyayo za waingereza wenzao kutupwa nje ya mashindano na miamba ya soka ya Hispania Barcelona. Katika kipute hicho kilichopigwa katika dimba la Nou Camp.

Wenyeji Barcelona walijipatia bao lao katika dakika ya 31 baada mchezaji Ivan Rakitic kuitumia vema pasi maridadi kutoka kwa Leonel Mess. Hadi mwisho wa mchezo Barcelona 1 Man City hawakupata kitu na kufanya jumla ya matokeo kuwa ni 3-1 baada ya mchezo wao wa awali vijana wa Manuel Pellegrini kuanguka nyumbani kwa jumla ya mabao 2-1.

Na huko nchini Ujerumani vijana wa Jurgen Klopp Borussia Dotmund, ilikiona cha moto baada ya kutandikwa bao 3 kwa mshangao dhidi ya Juventus ya Italia,katika mtanange huo uliopigwa katika dimba la Sigunal Iduna Park, mchezaji Carlos Tevez ndiye aliyepeleka msiba kwa Wajerumani hao kwa kutumbukiza kimiani mabao mawili. 

Dakika tatu tu za mchezo huo zilimtosha Tevezi kufunga bao la kuongoza kabla ya Morata kuandika bao la pili dakika ya 70 na kisha Tevez kutikisa tena nyavu katika dakika ya 79. Matokeo ya jumla kati ya timu hizo mbili yanakuwa ni 5-1 baada ya Juventus kushinda 2-1 katika mchezo wa awali. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Wednesday, March 18, 2015

BAADA YA VURUGU KUDUMU KWA SIKU TATU MFURULIZO, HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA TUNDUMA LEO MCHANA

  Wakinawa uso kufuta moshi wa mabomu.

Mkazi wa Tunduma ambae jina lake halikufahamika mara moja akionyesha bomu la machozi ambalo halijatumika alilomnyang'anya askari na kukimbia nalo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

NYALANDU AMJIBU KINANA; 'SASA NITAZURURA ANGANI KUPAMBANA NA MAJANGILI'

 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akielekezwa kitu na wataalam wa ndege hiyo aliyozindua jana.

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu jana alionekana kumpiga kijembe Katibu MKuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana aliposema kuwa sasa atakuwa anazurura angani.
Nyalandu alitoa kauli hiyo Dar es Salaam alipozindua ndege nyepesi (Micro-Light, 5H – Hel), ambayo itatumika kupambana na ujangili katika Hifadhi ya Taifa ya Selous.
“Karibuni wote, leo tunazururia hapa uwanja wa ndege na ninazindua ndege hii nyepesi ambayo imetengenezwa Ufaransa, itatumika kupambana na majangili katika Mbuga ya Selous.
“Kwa maana hiyo sasa tunaanza kuzururia angani kupambana na majangili na nasisitiza kwamba ndege hii ni mpya kabisa na gharama za uendeshaji wake ni ndogo kwa vile inatumia petroli,” alisema.
Hivi karibuni Kinana akiwa ziarani mkoani Arusha alimsifia Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa (CCM) kuwa ni mchapakazi lakini Waziri Nyalandu ni mzururaji.


Akizungumza jana wakati wa uzinduzi wa ndege hiyo ya kupambana na ujangili, Nyalandu alisema imetengenezwa kwa gharama ya Dola za Marekani 2,040,000 na ina uwezo wa kubeba askari mmoja na rubani.


Waziri Nyalandu alisema ndege hiyo imeundwa kwa usalama wa hali ya juu kwa kuwekewa puto (parachute) ambalo litatumika kushuka chini iwapo ndege itaishiwa mafuta angani.


“Itakapoanza kutumika itasaidia kuwabaini majangili, inakwenda kwa mwendo mdogo iwapo angani hali ambayo inawezesha kuwaona majangili na kila kinachoendelea ardhini kwa wepesi,”alisema Nyalandu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

UBUNGE WA ZITTO WANING'INIA...!!!

Zitto Kabwe 

Kitendo cha kutupiana mpira kati ya Ofisi ya Bunge, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuhusu hatima ya Zitto Kabwe, kimeufanya ubunge wa mbunge huyo kuendelea kuning’inia huku mwenyewe akitazamiwa leo kueleza anachoita ‘maamuzi magumu’.

Kutupiana mpira kulijitokeza jana baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kusema Bunge linasubiri taarifa rasmi ya kufukuzwa uanachama kwa mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kutoka NEC, ambayo hata hivyo, nayo ilisema inasubiri taarifa kutoka Chadema huku chama hicho kikisema kinashughulikia kwanza kesi zinazowakabili wanachama wake wanaotuhumiwa kumpiga aliyekuwa mlinzi wa Katibu Mkuu wake, Dk Willibrod Slaa.
Wakati Makinda akieleza hayo, taarifa kutoka kwa watu wa karibu wa mbunge Zitto zilieleza kuwa leo ataibuka bungeni kwa nia ya kuwaaga wabunge kama alivyoahidi wiki iliyopita. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

'KURA YA MAONI IPO PALE PALE'

Kaimu kiongozi wa shughuli za serikali bungeni Mh. Samuel Sitta.
SERIKALI imesema haiwezi kubadili msimamo wake kuhusu upigaji wa Kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa, licha ya kuwepo maoni ya viongozi wa dini ambao wanataka jambo hilo lisitishwe.

Kaimu Kiongozi wa shughuli za Serikali bungeni, Samuel Sitta alisema jana mjini hapa kuwa pamoja na kuwepo kwa tofauti kati ya Jukwaa la Wakristo na Kiongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, msimamo wa Serikali uko pale pale.

Sitta, ambaye anakaimu shughuli za serikali bungeni kutokana na kutokuwepo kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alisema Serikali inakubaliana na maoni ya Kardinali Pengo kuwa waumini waachwe waamue wenyewe kuhusu Katiba Inayopendekezwa.

Alisema kama viongozi wa dini wamegawanyika hakuna namna ya kuwafanya wawe na kauli moja, lakini akasisitiza kuwa jambo la msingi ni kuachwa kwa mtu aamue mwenyewe aina ya kura atakayopiga.

Hivi karibuni Pengo alitofautiana na Baraza la Maaskofu (TEC) na Jukwaa la Wakristo ambao wanataka upigaji wa kura ya maoni usitishwe, kwa maelezo kuwa wananchi hawajapewa muda wa kuisoma na kuielewa katiba hiyo na kama Serikali itang’ang’ania ni vyema waumini wa kanisa wapige kura ya hapana. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO MARCHI 18, 2015

.
.
.
.
.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAASKOFU WA JUKWAA LA WAKRISTO WAMEKOLEZA MOTO KUIKATAA KATIBA

Pichani ni  Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri la Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa

Gazeti la Mwananchi la Machi 13, 2015 lilibeba ujumbe mzito kwa Watanzania. Kichwa cha habari kimoja kilisomeka: “Maaskofu: Pigieni Katiba kura ya hapana.”
Maaskofu wa Jukwaa la Wakristo ambao ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo (CCT), Askofu Dk Alex Malasusa, Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Askofu Tarcicius Ngalalekumtwa na Mwenyekiti wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (CPCT) Askofu Daniel Awet, kwa sauti moja wamewataka waumini wao kujiandikisha kwa wingi katika Daftari la Wapigakura, kuisoma vyema Katiba Inayopendekezwa na hatimaye kuikataa kwa kuipigia kura ya ‘hapana.’
Sababu kuu za kuwahamasisha waumini wao na Watanzania kuikataa Katiba Pendekezwa ni mbili. Mosi ni kulazimisha kura ya maoni ya katiba mpya kufanyika bila maandalizi ya kutosha, yakiwamo maridhiano ambayo yameligawa Taifa katika vipande vipande. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

AL SHABAAB YAUA WATU WATATU NCHINI KENYA

Alshabaab
Maafisa wa polisi nchini Kenya wanasema kuwa takriban watu watatu wameuawa katika mji wa kazkazini wa Wajir, yapata kilomita 100 kutoka mpaka na Somalia. Watu waliofunika nyuso zao walishambulia duka moja na kufyatua risasi, kulirushia magurunedi kabla ya kulichoma.

Kundi la wapiganaji wa Al-Shabaab limeongeza mashambulizi yake kazkazini mashariki mwa Kenya katika siku za hivi karibuni ,na kufanya mashambulizi mawili katika mji wa Mandera ambao una pakana na Somali.

Kundi hilo linadhibiti eneo kubwa la Somalia la mashambani na limesajili idadi kubwa ya raia Wakenya. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

MAKAMU WA RAIS WA S LEONE AFUTWA KAZI

Rais wa Sierra Leone Ernest Koroma kushoto na makamu wake Sam Sumana Kulia
Rais wa Sierra Leone Ernest Bai Koroma amemfuta kazi makamu wa rais kwa kutafuta hifadhi katika ubalozi wa kigeni nchini humo. Siku ya jumamosi ,Samuel Sam Sumana amesema kuwa alimtaka balozi wa Marekani kumpatia hifadhi ndani ya ubalozi wa Marekani nchini humo akihofia maisha yake.

Awali wanajeshi waliizunguka nyumbani yake na kumpokonya silaha mlinzi wake .
Kumekuwa na wasiwasi kati ya rais na bwana Sam Sumana. Hivi majuzi aliondolewa katika chama tawala cha All People Congress kwa udanganyifu na kuchochea ghasia. Hatahivyo amekana madai hayo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

MONACO HAWAKUSTAHILI KUSONGA MBELE

Arsene Wenger,meneja wa klabu ya Arsenal.
Meneja wa klabu ya soka ya Arsenal Mfaransa Arsene Wenger anaamini timu ya Monaco haikustahili kusonga mbele kwenye hatua ya nane bora ya ligi ya mabigwa ulaya.
Licha ya Arsenal kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Monaco walishindwa kufuzu kwa nane bora baada ya kupoteza mchezo wa kwanza kwa kuchapwa 3-1.

Kocha Wenger amesema haamini kama timu hiyo ilitakiwa kusonga mbele “ukiangalia idadi ya mashuti yaliyolenga goli utashangaa, kupoteza mchezo kunauma ila hatujapoteza."
Hii imekua ni mara ya tano mfululizo kwa washika bunduki hao wa London kushindwa kufuzu hatua ya nane bora. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SERENA WILLIAMS ATINGA NANE BORA

Serena Williams
Nyota wa mchezo wa tenesi Serena Williams ametinga katika hatua ya nane bora ya michuano ya BNP huko Indian Wells. Serena amefanikiwa kufanya vizuri kwa kumshinda Sloane Stephens anayeshika nafasi ya 33 kwa ubora wa dunia kwa seti 6-7 (7-3) 6-2 6-2,
Sloane alipoteza mchezo huu baada ya kushindwa kuhimili mikiki miki ya mpinzani wake aliekua anacheza kwa juhudi kubwa.

Williams alikataa kucheza hapo baada ya kufanyiwa vitembo vya kudharauriwa mwaka 2001. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Monday, March 16, 2015

WAHAMIAJI 64 KUTOKA ETHIOPIA WAKAMATWA

Ramani ya Tanzania
Polisi mkoa wa Dodoma nchini Tanzania wanawashikilia wahamiaji haram 64 raia wa Ethiopia, huku mmoja wao akipatikana akiwa amekufa.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma amenukuliwa akisema wanamshikilia dereva wa gari lililokuwa limewabeba watu hao ambao inaaminika walikuwa njiani kuelekea kusini mwa Afrika.
Hii si mara ya kwanza kwa wahamiaji wa aina hiyo kukamatwa katika mazingira hayo.
Mwaka 2012 watu 42 kutoka Eritrea walikutwa wamekufa katika lori mkoa wa Dodoma kwa kile kinachosemekana ni kukosa hewa kutokana na kufichwa ndani ya lori hilo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAMILIONI WAANDAMANA BRAZIL

Rais Dilma Roussef wa Brazil
Zaidi ya watu milioni moja kutoka nchini Brazil wameandamana dhidi ya rais wa nchi hiyo Dilma Rousseff, huku wengi wao wakitaka rais huyo afunguliwe mashtaka ya ufisadi mkubwa uliofanyika katika shirika la mafuta la serikali, Petrobras.
Maandamano kama hayo yamefanyika katika miji mingi ya Brazil ikiwemo mji mkuu wa nchi hiyo Brasilia.
Maandamano makubwa kabisa yamefanyika katika mji wa Sao Paulo ambalo ni eneo la upinzani waliokuwa wakipita mitaani.
Mmoja wa waandamanaji Francisco Pestana alilalama akisema"Dilma hana uwezo wa kuongoza nchi yetu. Tunachokabiliwa nacho ni bahati mbaya sana, namna mamabo yanavyokwenda, yanaweza kuelekea kubaya zaidi, tutakuwa Venezuela nyingine."
Naye mwandamanaji mwingine mwanamke Janaina Lima anasema "leo ni maandamano ya watu. Watu wamejitokeza mtaani kusema hakuna ghasia zaidi, hakuna rushwa, hakuna uvivu zaidi, hakuna uzembe zaidi, hakuna utawala mbaya. Na kuunga mkono Brazil mpya." Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

YANGA YAIADHIBU PLATNUM YA ZIMBABWE 5-1

Kikosi cha Yanga kilichoisambaratisha Platnum ya Zimbabwe kwa mabao 5-1
Timu pekee iliyobakia kwenye mashindano ya shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika kutoka Tanzania, Yanga, imeendelea kuweka matumaini hai ya kusonga mbele baada ya kuiangushia kipigo kikali timu ya Platnum ya Zimbabwe kwa mabao 5-1.
Mchezo huo wa raundi ya kwanza ya vilabu vinavyoshiriki Kombe la Shirikisho la CAF, ulifanyika Jumapili jijini Dar es Salaam.
Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa kufungana mabao 2-1.
Kipindi cha Pili ndicho kilichokuwa kiama chya Platnum baada ya kuruhusu mabao matatu zaidi.
Wafungaji wa timu ya Yanga ni Mrisho Ngasa aliyefunga magoli mawili, Haruna Niyonzima, Salum Telela, na Amisi Tambwe walifunga bao moja kila mmoja. Kwa matokeo hayo Yanga imejenga mazingira ya kusonga mbele. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Sunday, March 15, 2015

ZITTO: IPO SIKU NITASHIKA NAFASI KUBWA TANZANIA

Wananchi wa Kijiji cha Nyalubanda wakiwa wamembeba Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alipowasili katika kijiji hicho jana katika hafla ya kukabidhi gari la wagonjwa alilotoa ahadi katika kampeni za Uchaguzi wa mwaka 2010.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amesema kutimuliwa uanachama na Chadema ni dhoruba inayomkumba mwanasiasa yeyote anayefanikiwa na kwamba iko siku atashika “nafasi kubwa ya uongozi ya kuwatumikia Watanzania”.
Zitto aliwasili mjini hapa juzi, ikiwa ni siku chache baada ya Chadema kutangaza kumtimua uanachama kwa kosa la kupeleka mgogoro wa ndani ya chama kwenye mahakama.
Alifungua kesi Mahakama Kuu akitaka imuamuru katibu mkuu wa Chadema kumpa nyaraka za mwenendo wa vikao vya Kamati Kuu vilivyomvua madaraka yote na baadaye kukizuia chama hicho kumjadili. Hata hivyo mahakama ilitupilia mbali shauri lake na Chadema ikatangaza mara moja kumtimua. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

PENGO ATOFAUTIANA NA MAASKOFU....!!!

 
Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo akibariki matoleo yakiotolewa na Umoja wa Wanawake wa katoriki(WAWATA), wakati wa Ibada iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, Dar es Salaam jana.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amesema waumini hawana budi kusoma vizuri na kuelewa Katiba Inayopendekezwa ili wakati ukifika, wafanbye uamuzi kwa hiari na utashi wao wakati wa kupiga Kura ya Maoni.
Ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku mbili baada ya Jukwaa la Wakristo kutoa tamko linalowataka waumini kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye Daftari la Wapigakura, kushiriki kikamilifu kwenye shughuli zote za elimu ya Katiba Inayopendekezwa na kupiga kura ya “hapana” kuikataa Katiba Inayopendekezwa.
Lakini jana, Kardinali Pengo alisema kuisoma na kuielewa katiba hiyo ndiyo wajibu wa msingi ambao Wakristo wanao kwa sasa ili kupiga kura inayostahili wakati ukifika. Kuhusu maaskofu kuagiza waumini waikatae Katiba Inayopendekezwa, Kardinali Pengo alisema wao wakiwa viongozi wa watu, hawana mamlaka wala uwezo huo, bali wenye uwezo ni wananchi wenyewe. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

LIPUMBA AKUBALI TAMKO LA MAASKOFU

Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba  

Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba ameunga mkono tamko la Jukwaa la Wakristo Tanzania kupinga Katiba Inayopendekezwa, akisema hoja zao ni za msingi kwa kuwa kuna mambo mengi yanayopingwa na wananchi.
Kauli ya Profesa Lipumba ni mwendelezo wa kauli tofauti zilizotolewa na watu mbalimbali kuhusu tamko la jukwaa hilo, wakiwamo wasomi, viongozi wa dini, wanaharakati na wanasiasa kuhusu hatima ya Kura ya Maoni na muswada wa Makahama ya Kadhi.
Alhamisi iliyopita, jukwaa hilo linaloundwa na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT) liliwataka waumini wake kujitokeza kwa wingi kujiandikisha, kushiriki kikamilifu katika elimu ya Kura ya Maoni, na kisha kuipigia kura ya “hapana” Katiba Inayopendekezwa. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO MARCHI 15, 2015

.

.

.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MILIPUKO YALENGA MAKANISA...!!!

Wasichana walia kufuatia mashambulizi mawili yaliolenga makanisa Pakistan
Mabomu mawili yamelipuka yakilenga makanisa mawili yaliyokuwa yamejaa watu kwenye mji wa Lahore chini Pakistan wakati watu walipokuwa wakihudhuria misa ya jumapili.
Polisi wanasema kuwa takriban watu 6 wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Mashambulizi hayo yanaoyoaminika kuwa ya kujitoa mhanga yalifanyika eneo lenye waumini wengi wa kikristo la Youhanabad
Sehemu ya kundi la Taliban linalofahamika kama Jamatul Ahra limesema kuwa ndilo lililoendesha shambulizi hilo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMO KUHUSU UBAKAJI KUFUNZWA UINGEREZA




Wanafunzi nchini Uingereza
Wanafunzi kuanzia miaka 11 nchini Uingereza watafundishwa kuhusu tofauti kati ya ubakaji na tendo la ngono ambalo limetekelezwa kutokana na idhini ya wapenzi wawili kama mojawapo ya mipango ya kuwawapa ujuzi kuhusu maisha ya sasa nchini humo
Somo hilo ambalo litaanzishwa mara moja baada ya siku kuu ya Easter litaongezwa katika mtaala wa Uingereza baada ya wasiwasi kutolewa kwamba vijana walikuwa wakishinikizwa kushiriki katika ngono.
Nick Morgan ambaye ni katibu wa elimu alitoa tangazo hilo siku ya kimataifa ya wanawake.
''Lazima swala hili tulikabili kwamba mambo ambayo wasichana wetu wanapitia hayakuwepo wakati wa ujana weyu,kwa hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha kuwa wasichana wetu wanamaliza shule wakiwa na uwezo wa kukabiliana na changaomoto watakazokumbana nazo wakiwa watu wazima'', aliandika. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

VATICAN: NGUVU ZITUMIWE DHIDI YA IS

Askofu mkuu wa Vatican Silvano Tomasi
Makao makuu ya kanisa katoliki duniani Vatican yanasema kuwa nguvu inaweza kutumiwa kusitisha mashambulizi yanayoendeshwa na wanamgambo wa Islamic State dhidi ya wakristo na makundi mengine madogo .
Askofu mkuu Silvano Tomasi ambaye ni mwakilishi mkuu wa Vatican kwenye umoja wa mataifa mjini Geneva ameyashutumu makundi ya jihad kwa kuendesha mauaji ya halaiki.
Akizungumza kupitia mtandao wa Vatican amesema kuwa hatua za kijeshi zitaanzishwa ikiwa suluhu ya kisiasa haitapatikana.
Lakini amesema kuwa muungano wowote dhidi ya Islamic State ni lazima ujumuishe nchi za kiislamu kutoka mashariki ya kati. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAN UNITED KUMKOSA DI MARIA

Manchester United kumkosa nyota wake Angel Di Maria
Kilabu ya Manchester United itamkosa Angel Di Maria,ambaye anahudumia mafuruku ya mechi moja baada ya kupewa kadi nyekundi dhidi ya Arsenal,naye Jonny Evans akiwa anahudumia marufuku.
Mshambuliaji nyota Robbin Van Persie bado anauguza jeraha huku Marcos Rojo akiwa hajulikani iwapo atachezeshwa kutokana na jeraha la paja.
Hatahivyo Ashley Young atacheza licha ya kujiumiza mguu siku ya jumatatu.
Kocha wa kilabu ya Tottenham Mauricio Pochettino ana kikosi chake kizima.
Danny Rose huenda akacheza mechi ya leo katika safu ya ulinzi wa kushoto huku Mousa Dembele pia akitarajiwa kuanza. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...