Wednesday, December 24, 2014

EBOLA BADO TISHIO

 Peter Piot 
 
Shirika la Afya Duniani limesema ugonjwa wa Ebola hautaweza kudhibitiwa kikamilifu katika kipindi cha mwaka mmoja unaokuja.
Mwenyekiti kutoka kitengo maalumu kinachoshughulikia ugonjwa huo, kutoka katika Shirika la Afya Duniani Profesa Peter Piot anasema hali halisi kwa sasa ya ugonjwa huo ni kama ugonjwa utakaodumu muda mrefu.
Profesa Peter Piot ambaye amerejea kutoka nchini Sierra Leone, nchi ambayo imeathiriwa zaidi na ugonjwa huo, ameiambia BBC kwamba amehamasishwa na ahadi za kupatikana kwa kinga mpya ambayo inaaminika itakuwa tayari katika kipindi cha miezi mitatu.
Hata hivyo Profesa Piot ambaye aligundua virusi vya ugonjwa wa Ebola mwaka 1976, ameonya pia kwamba janga lililopo sasa halitakuwa la mwishon na chanjo kudhibiti kirusi hicho itachukua muda kufanya kazi. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC Swahili

VILABU VYA ULAYA NA TETESI ZA USAJILI

 Gareth Balle akiwa kazini.
 
Uongozi wa Timu ya Manchester United umesema upo tayari kutoa paundi milioni 120 kwaajili ya kumsajili winga Gareth Balle mwenye umri wa miaka 25 kwa mwezi januari kutoka klabu ya Real Madrid , winga ambaye ni miongoni mwa wachezaji ghali zaidi ulimwenguni.
Gareth Bale alijiunga na Real Madrid kwa kuweka rekodi kubwa duniani kwa usajili wa rekodi ya paundi milioni 85.3 mwaka 2013.
Wakati huo huo kocha Laurent Blanc wa Timu ya Paris St Germain anafikiria kumsajili mshambuliaji Edinson Cavani( 27), kwa gharama ya pauni milioni 50 ikiwa ndio hitaji la Timu ya Arsenal katika katika usajili wa mwezi Januari 2015.
Nayo klabu ya Manchester City inandaa pauni milioni 25 katika jitihada za kutaka kumsajili msahambuliaji wa Atletico Madrid Mario Mandzukic (28). Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

EBOSSE: ALGERIA YAPINGA RIPOTI YA MAUAJI

Marehemu Albert Ebosse aliyeaga dunia.Algeria imepinga ripoti ya mauaji yake kwamba mchezaji huyo aliuawa baada ya kuvamiwa. 
 
Waziri wa habari nchini Algeria Mohammed Tahmi amesisiiza kwamba kifo cha mchezaji wa Cameroon Albert Ebosse kilisababishwa na mashabiki waliokuwa wakirushi vitu.
Tahmi ambaye alikuwa akizungumza na radio ya Algeria alikuwa akijibu ripoti ya wiki jana ya daktari wa kuchunguza mauaji kwamba majereha ya Ebosse yalisababishwa na mashambulizi.
Ebosse mwenye umri wa miaka 25 aliaga dunia tarehe 23 mwezi Agosti baada ya kilabu yake JS Kabylie kupoteza 2-1 nyumbani. ''Tumefanya uchunguzi wetu unaoonyesha kwamba mchezaji huyo aliuawa kutokana na kitu kilichorushwa kutoka kwa mashabiki.'',alisema
Mchezaji Ebose aliyekuwa akiichezea timu yake JC kabylie kutoka Algeria
''Mimi si mtaalamu wa sheria lakini nitasema kuwa kifo hicho ni cha bahati mbaya''.,aliongezea ''Vitu vilirushwa kutoka pande zote mbili na wachezaji wote walilengwa na kwa bahati mbaya kisa hicho kikatokea'',alisema.
Swala hilo kwa sasa liko mahakamani ambapo uamuzi utatolewa. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

IVORY COAST WAGOMEA BAJETI YA SERIKALI - AFCON

 Timu ya Ivory Coast 
 
Shirikisho la soka Ivory Coast (FIF) limegomea bajeti waliyopewa na Serikali ya nchi hiyo kwa ajili ushiriki wa timu ya taifa, The Elephants kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika kwa sababu ni ndogo.
Serikali imekubali kutoa dola za Kimarekani 575 805 kwa Tembo wa Ivory Coast kwenye Fainali za AFCON zitakazofanyika Equatorial Guinea kuanzia Januari 17 hadi Februari 8.
Pamoja na hayo, Makamu wa rais wa FIF, Sory Diabate amewaambia Waandishi wa Habari kwamba Hawawezi kwenda CAN (Mataifa ya Afrika) na faranga (za Ivory Coast, CFA Francs) Milioni 310. Kwa kuwa wamewasilisha bajeti yao kwa ufafanuzi mzuri.
Waziri wa Michezo wa nchi hiyo alikuwa tayari kutoa fungu kamili waliloombwa katika bajeti ya awali faranga bilioni 3.5, pamoja na hayo Ivory Coast ilikwenda michuano hiyo mwaka 2013 Afrika Kusini na jumla ya Faranga bilioni 3.9, huku Serikali ikichangia Bilioni 2.7 wakati Tembo walitolewa na Nigeria katika Robo Fainali.
Kikois cha Herve Renard, kitaanza maandalizi yake kwa kuweka kambi Abu Dhabi, Falme za Kiarabu Januari 5, mwakani. Ivory Coast imepangwa Kund D pamoja na Mali, Cameroon na Guinea. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Tuesday, December 23, 2014

RAIS KIKWETE ATENGUA UTEUZI WA PROFESA TIBAIJUKA

Rais Jakaya Kikwete
RAIS Jakaya Kikwete

RAIS Jakaya Kikwete, ametengua uteuzi wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, huku pia akitengua kitendawili cha nani mmiliki wa fedha za akaunti ya Escrow na kusema sio za umma bali ni za IPTL.
Aidha, Serikali kupitia Kamati ya Maadili inaendelea kumfanyia uchunguzi kwani kuna upungufu wa kimaadili umeonekana kutendeka.
Rais Kikwete aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana alipokuwa anahutubia taifa kupitia wazee na wakazi wa Dar es Salaam kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, lengo likiwa kuzungumzia mambo mbalimbali ya kitaifa, yakiwemo yale yaliyokuwa yakisubiri uamuzi wake, kubwa likitajwa la sakata la Akaunti ya Escrow.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

RAIS KIKWETE: FEDHA ZA TEGETA ESCROW NI ZA EPTL

Rais Jakaya Kikwete akihutubira wazee wa mkoa wa Dar es Salaam kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini hapa.

Rais Jakaya Kikwete amesema fedha zilizochotwa katika Akaunti ya Tegeta Escrow hazikuwa zinafikia Sh306 bilioni, bali ni Sh202 bilioni na zilikuwa mali ya Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL.
Akijibu swali alilojiuliza mwenyewe katika hotuba yake ya zaidi ya saa mbili kuwa: “Fedha hizi mwenyewe nani, umma au IPTL?” Rais Kikwete alisema kumekuwapo na maneno mengi, kila mtu anasema yake na wenzangu Wakwere tunasema ‘tunazoza sana’ akimaanisha waongea sana.
Alisema, “Kimsingi fedha hizi ni za IPTL, katika swali pesa za nani, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alipoulizwa na Kamati ya Bunge alisema humu yawezekana zipo za umma pia zipo za IPTL.
“Nilipomuuliza maana, akasema zamani walikuwa wanalipa moja kwa moja kwa Tanesco lakini baada ya mzozo walikubaliana kwanza waziweke Benki Kuu ya Tanzania (BoT).”
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE DESEMBA 23, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAALIM SEIF AITABIRIA CUF USHINDI MKUBWA


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad 


Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amesema upepo wa kisiasa unakivumia vizuri chama chake na ana matumaini Uchaguzi Mkuu ujao kitapata viti 18 vya uwakilishi katika ngome ya CCM Unguja.

Hivi sasa CUF inashikilia majimbo manne ya Unguja kati ya 32 na kwa muda wote ngome yake imekuwa ni Pemba kinakoshikilia majimbo yote 18.

Akihutubia mkutano wa hadhara baada ya kuzindua miradi ya maendeleo katika Jimbo la Magogoni, Wilaya ya Magharibi Unguja, Maalim Seif alisema suala la Katiba Mpya na ufisadi uliokithiri vitaipa wakati mgumu CCM, hasa upande wa Zanzibar.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

KITISHO CHA USALAMA: POLISI AUAWA NCHINI KENYA

Polisi nchini Kenya katika doria.
 
Askari mmoja ameuawa na mwingine akiwa mahututi baada ya kushambuliwa kwa kupigwa risasi kaskazini mwa Kenya.
Askari hao wa Kenya wanadaiwa kushambuliwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa kundi la Al Shabaab.
Askari hao wa jeshi la polisi kikosi cha ziada walikutwa na kisa hicho mjini Wajir kaskazini mwa Kenya usiku wa kuamkia leo. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

RAIS WA UFARANSA AWATULIZA RAIA WAKE

Rais wa Ufaransa  

Rais wa Ufaransa amewataka raia wake wasishtushwe na visa vya kushambuliwa kwa polisi na raia katika kipindi cha siku kadhaa.
Rais Francois Hollande ameyasema hayo baada ya mtu mmoja kuendesha gari na kulivurumisha katika soko la Krismasi lililosheheni watu, magharibi mwa mji wa Nantes na kujeruhi watu kumi.
Waendesha mashtaka wamesema, shambulizi hilo linafanana na lile lililotokea katika mji wa Dijon siku ya Jumapili ambapo dereva wa gari aliyekuwa akisema kwa sauti maneno ya kiislamu mfululizo alipowagonga wapita kwa miguu katikati mwa mji.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

PLUIJM AWALILIA KASEJA NA KIIZA

Kocha wa Yanga, Hans Van Pluijm akiteta jambo na wachezaji wake, siku za hizi karibuni. Picha na maktaba 

Kocha wa Yanga, Hans Van Pluijm amesikitishwa na kitendo cha kuondoka kwa nyota wake Juma Kaseja, Hamisi Kiiza na Didier Kavumbagu, lakini akawataka wachezaji wake wasahau yaliyopita na waangalie yajayo.
Pluijm amechukua mikoba ya Marcio Maximo aliyetupiwa virago baada ya Yanga kufungwa na Simba 2-0 katika mchezo wa Nani Mtani Jembe kama ilivyokuwa mwaka jana alipoinoa timu hiyo kwa mara ya kwanza baada ya Ernie Brandts kutimuliwa kutokana na timu hiyo kunyukwa 3-1 na Simba.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Pluijm alisema Kaseja alikuwa nahodha, lakini sasa hayupo kutokana na tofauti zake na viongozi.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

PHIRI AOMBA MIAKA MIWILI


Kocha wa Simba, Mzambia Patrick Phiri amesema iwapo klabu yake itamvumilia kwa miaka miwili atatengeneza wachezaji bora kama ilivyo kwa nyota wa TP Mazembe ya DR Congo (DRC), Mbwana Samatta.

Phiri alisema: “Najivunia mafanikio ya Samatta (Mbwana). Kwanza yanatokana na uvumilivu wake na kujituma kwake pamoja na kupewa nafasi. Naamini makocha wanapopewa muda na timu wanaweza kutengeneza wachezaji wapya na hata kuinufaisha klabu kwa kuuza wachezaji hao kwa bei nzuri huku ikiendelea kutengeneza wengine.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

YANGA KWA WANAJESHI, AZAM SUDAN

Mabingwa wa Tanzania, Azam wataanza harakati zake za Ligi ya Mabingwa Afrika, kwa kuivaa El Merreikh ya Sudan, wakati Yanga wenyewe watakuwa na kibarua kwa BDF ya Botswana katika Kombe la Shirikisho.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa jana na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) inaonyesha wawakilishi wa Tanzania wataanzia nyumbani katika michezo yao itakayopigwa Februari 13, 14, 15 na mechi za marudiano zitakuwa kati ya Februari 27, 28 na Machi Mosi 2015.

Azam itawakaribisha El Merreikh na kurudiana wiki mbili baadayezijazo nchini Sudan na endapo itafanikiwa kushinda mechi hiyo katika hatua ya 16 bora itacheza na mshindi kati ya Lydia Ludic B.A (Burundi) au Kabuscord do Palanca (Angola).
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Monday, December 22, 2014

"WATANZANIA KUNUFAIKA NA AJIRA QATAR" PINDA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema Watanzania watanufaika na kipato na maarifa ya teknolojia ya kisasa kutokana na ajira, ambazo watapata katika nchi ya Qatar baada ya mkataba kusainiwa hivi karibuni.

Alitoa kauli hiyo jana jijini Doha, Qatar wakati akizumgumza na waandishi wa habari ili kuwapa taarifa fupi juu ya mambo yaliyojiri kwenye mazungumzo yake na Waziri Mkuu wa Qatar, Sheikh Abdulla Nasser Al Thani.
Katika mazungumzo hayo ambayo yalifanyika ofisini kwa Sheikh Abdulla, Pinda alisema wamekubaliana kutoa ajira kwa Watanzania kwa sababu nchi hii inahitaji wafanyakazi wengi kwenye sekta mbalimbali na raia wake ni wachache.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU DESEMBA 22, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

WAHITIMU 344 WA DARASA LA SABA HAWJUI KUSOMA NA KUANDIKA...!!!


Wanafunzi 344 waliomaliza darasa la saba mwaka huu mkoani hapa wamebainika kuwa hawajui kusoma, kuandika na kuhesabu. Ofisa elimu wa mkoa, Nestory Mloka alitoa taarifa hiyo juzi katika kikao cha elimu kilichoitishwa kwa ajili ya kuchambua matokeo ya mtihani wa darasa la saba na kuwapangia shule wahitimu waliofaulu.

Mloka alisema kati ya walihitimu hao ambao hawajui kusoma na kuandika, wavulana ni 163 na wasichana 181. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

KIKWETE "HATUWEZI KUENDELEA KWA KUTEGEMEA RAMLI"

Sehemu ya Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela iliyoko Tengeru, Arusha

Sehemu ya Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela iliyoko Tengeru Arusha.

RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa kamwe Tanzania, kama ilivyo nchi nyingine yoyote duniani, haiwezi kuendelea kwa kutegemea mazingaombwe ama ramli bila kuwekeza kwenye maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Aidha, ametaka Watanzania kuacha mwenendo wa kutumia ubishi wa kisiasa kutafuta majawabu ya changamoto za maendeleo akisisitiza kuwa majawabu ya maendeleo yatapatikana katika maendeleo ya sayansi na teknolojia.
Amewataka Watanzania kuongeza kasi yao ya matumizi ya intaneti akisema kuwa mfumo huo wa habari na mawasiliano ni chimbuko kubwa la elimu ikiwemo elimu ya sayansi kuliko kutegemea kupata elimu hiyo katika magazeti.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MUME AMJERUHI MKEWE KWA SHOKA KISA WIVU WA MAPENZI

Muonekano wa Malaysia.

Mama mwenye watoto watatu anapata matibabu hospitalini nchini Malaysia baada ya mumewe kuvamia mikono yake na miguu nakumcharanga kwa shoka la kucharangia nyama,na baadaye mwanamume huyo kujinyonga .
Mama huyo anatajwa kama K Menaga,amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya Kluang upande wa kusini mwa jimbo la Johor baada ya shambulio hilo hatari lililotokea mapema mwezi huu.
Ingawa taarifa kutoka hospitalini hapo zinaarifu kuwa mama huyo ameshatolewa katika chumba cha wagonjwa mahututi baada ya hali yake kuendelea vyema,na amelazwa katika wodi ya wagonjwa wa kawaida.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

WAAMUZI 11 WA KITANZANIA KWENYE ORODHA YA FIFA

Nembo ya shirikisho hilo,iliyo nakshiwa vyema.
 
Shirikisho la soka ulimwenguni FIFA limetoa orodha mpya ya waamuzi linaowatambua ,Kwenye orodha hiyo kuna jumla ya waamuzi 18 kutoka Tanzania,miongoni mwa waamuzi hao waamuzi 11 wapya na 7 wa zamani.
Waamuzi wapya wa kati kutoka Tanzania ni Mfaume Ali Nassor kutoka visiwani Zanzibar pamoja na Martin Saanya kutoka Morogoro, pia wamo waamuzi watatu wa kike ambao ni Florentina Zabron ,Jonesia Rukyaa pamoja na Sofia Ismail.
Kwa upande wa waamuzi wasaidizi wanaume ni Frank John Komba na Soud Idd Lila , kwa upande wa wanawake ni Kudura Omary Maurice,Hellen Joseph Mduma,Dalila Jafari Mtwana na Grace Mawala.
Waamuzi wa zamani wa Tanzania kwenye orodha ya FIFA ,kwa upande wa wanaume ni Israel Mujuni Nkongo na Waziri Sheha Waziri,kwa upande wa waamuzi wasaidizi ni Josephat Bulali,Fernand Chacha,John Longino Kanyenye ,Ali Kinduli na Samuel Hudson Mpenzu .
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

STERLING MWANASOKA BORA CHIPUKIZI

Raheem Sterling.
 
Mshambuliaji kinda wa Liverpool, Raheem Sterling amekabidhiwa Tuzo ya Mwanasoka bora chipukizi mwaka 2014 na Chama cha soka cha England FA.
Sterling alikabidhiwa tuzo hiyo kabla ya Mechi wa ligi kuu ya England kati ya Liverpool dhidi ya Arsenal wakiwa uwanja wa nyumbani Anfield, ambapo mechi hiyo imemalizika kwa sare ya goli 2-2.
FA imekuwa na utaratibu wa kutoa tuzo ya Mwanasoka bora wa mwaka kwa wachezaji chipukizi wanaofanya vizuri katika mchezo wa soka.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Sunday, December 21, 2014

BIBI AMUUA MJUKUU WAKE KWA KUMTUPA NJE YA BASI

 
Mmoja wa abiria waliokuwamo kwenye basi hilo, Ebenezer Hans alilieleza gazeti hili kwamba mama huyo akiwa miongoni mwa abiria, alikuwa na mtoto wake mwenye umri unaokadiriwa miaka 14 na wajukuu wawili, ambao alikuwa akisafiri pamoja nao. PICHA|MAKTABA  

Jeshi la Polisi mkoani Singida, linamshikilia Nawaridi Saidi (45), mkazi wa Dar es Salaam kwa tuhuma za kumtupa mjukuu wake Mayasa Meshack (6) kutoka ndani ya gari wakati akisafiri kwenda Kigoma akitokea Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Thobias Sedoyeka alisema kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 18, saa 2 usiku katika Kijiji cha Igugumo, wilayani Iramba ambapo mama huyo akiwa kwenye basi aina ya Scania, alifungua dirisha kutoka katika kiti alichokaa na kumtupa Mayasa wakati basi likiwa katika mwendo.

“Mama alikuwa anaenda mkoani Kigoma kwa ajili ya Sikukuu za Krisimasi na Mwaka Mpya, aliambatana na mtoto wake mwingine ambaye jina bado halijafahamika,” alisema Kamanda Sedoyeka. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

SERIKALI YAONYA DAFTARI LA WAPIGAKURA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Mh. Willium Lukuvi akifafanua jambo kwa waandishi wa habari.

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) William Lukuvi, ameonesha kutoridhishwa na utaratibu mbovu unaotumika kuandikisha wananchi katika daftari la kudumu la wapiga kura, kutokana na kuwa na mianya inayoweza kuingiza wasio raia wa Tanzania.
Lukuvi aliyasema hayo jana, wakati alipotembelea kituo cha Bunju A kuangalia uandikishwaji wa wananchi kwa kutumia teknolojia mpya ya Biometric Voter Registration (BVR).
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MITAA 89 KURUDIA UCHAGUZI LEO DAR



Jumla ya mitaa 89 kutoka wilaya tatu za Mkoa wa Dar es Salaam, leo zinatarajiwa kufanya uchaguzi wa marudio wa Serikali za Mitaa kutokana na kasoro kadhaa zilizojitokeza katika uchaguzi uliofanyika Desemba 14 mwaka huu.

Moja ya kasoro hizo ni kuchanganywa kwa majina ya wagombea wa uenyekiti na wajumbe.

Manispaa ya Temeke ina mitaa 10, Kinondoni 16 na Ilala 63 .

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni, Mhandisi Mussa Natty, ameingia kwenye mvutano mkubwa na Chama cha Wananchi (CUF), kuhusu uamuzi wake wa kutaka uchaguzi urudiwe katika Mtaa wa Mwinyimkuu huku ikidaiwa chama hicho kilishinda.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI DESEMBA 21, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

AFUNGULIWA MASHTAKA KWA KUSABABISHA KIFO CHA PUNDA...!!!

pua 
Mwanaume mmoja nchini Hispania amefunguliwa mashtaka ya kutesa wanyama baada ya kusababisha kifo cha punda aliyemuua wakati akimkalia kwa lengo la kupiga nae picha.
Sabu ya kifo cha punda aliejulikana kwa jila na Platero inasemekana ni uzito uliopitiliza wa mwanaume huyo na kusababisha kumpa maumivu makali mnyama huyo hadi alipopoteza maisha baada ya siku tatu.
dd
Picha hiyo iliwekwa katika mitandao ya kijamii ikimuonyesha mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 38 akitabasamu huku akipiga picha na mnyama huyo.
Baada ya siku mbili Punda huyo aliyekua akiugulia maumivu alishindwa kusimama na baada ya uchunguzi wa Polisi aligundulika kuvunjika baadhi ya viungo vyake kutokana na kubeba kitu kizito. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

POLISI WAWILI WAUAWA MAREKANI

Eneo la mauaji ya polisi wawili mjini New York nchini Marekani.
 
Maafisa wawili wa polisi mjini New York Marekani wameuawa kwa kupigwa risasi walipokuwa ndani ya gari lao eneo la Brooklyn.
Kamishna wa idara ya polisi mjini New York Bill Bratton amesema kuwa maafisa hao walilengwa na kuuawa kutokana na sare walizokuwa wamevaa.
Alisema kuwa awali mwanamume huyo alikuwa ameandika ujumbe wa kuwashutumu polisi kwenye mtandao wa kijamii baada ya kumfyatulia risasi na kumjeruhi vibaya mpenzi wake wa zamani .
Mauaji hayo ya polisi yanajiri wakati kunashuhudiwa ghadhabu kali kufuatia uamuzi wa hivi majuzi wa kutowafungulia mashtaka polisi wazungu waliohusika kwemye mauaji ya waamerika weusi.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

PLUIJM ATOA SIKU SABA (7) KUIBADILI YANGA


Kocha Hans Van Der Pluijm akiwa na Boniface Mkwasa katika moja ya mechi za Yanga Uwanja wa Taifa.

BAADA ya kupewa mkataba wa mwaka moja na nusu kukinoa kikosi cha Yanga kocha Hans van der Pluijm ameomba siku saba kuibadili timu hiyo.

Pluijm alisema atahakikisha anatoa mbinu zake zote alizokuwa nazo za ukocha ili aweze kuipa mafanikio timu hiyo msimu huu ikiwemo kutwaa ubingwa wa Tanzania bara.
Pluijm aliyetua Yanga kwa mara ya pili akichukua nafasi ya Mbrazil Marcio Maximo alisema kwa kuanza atatumia siku saba kwa ajili ya kubadilisha mfumo na kasi ya wachezaji ili waweze kushinda mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya mabingwa watetezi Azam FC utakaopigwa Uwanja wa Taifa Desemba 28.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

U.S.A YAITAKA KOREA KASKAZINI KUILIPA SONY

Wakuu wa kampuni ya filamu ya Sony Pictures.Marekani imeitaka Korea Kazkazini kuilipa kampuni hiyo kwa hasara iliopata baada ya madai ya kuhusika na uhalifu wa mtandao dhidi yake.
 
Marekani imezitaka China na nchi zingine kuthibitisha kuwa Korea Kaskazini ilihusika na uhalifu wa mtandao dhidi ya kampuni ya Sony Pictures.
Marekani inasema kuwa Korea Kaskazini ni lazima ikiri kuwa ilihusika na iilipe Kampuni ya Sony kutokana na hasara ambayo imepata
Korea Kaskazini imeyataja madai hayo ya Marekani kuwa ya uongo.
Wataalamu wanasema kuwa kuna ushahidi wa kutosha kuwa Korea Kaskazini ilihusika.
Lakini mwandishi wa BBC nchini Korea Kusini anasema kuwa kampuni ya Sony Pictures nchini Marekani na wakuu wake nchini Japan watahitajika kuamua iwapo wataonyesha filamu ya uchesi yenye utata ya rais wa Korea Kazkazini Kim Jong-un. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC

WAPIGA KURA WAHOFIA EBOLA LIBERIA


Uchaguzi wa kuwachagua maseneta nchini Liberia.

Idadi ndogo ya wapiga kura imeripotiwa kwenye kura ya kuwachagua maseneta nchini Liberia.
Kura hiyo ilikuwa imeahirishwa mara mbili kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa ebola na huenda hofu ya ugojwa huo iliosababisha watu kukosa kufika kwa vituo vya kupigia kura.
Wapiga kura walishauriwa kusimama umbali wa mita moja kutoka kwa mtu mmoja hadi kwa mwingine walipokuwa wakipanga milolongo kupiga kura baada ya viwango vyao vya joto kuchukuliwa na maafisa wa afya.

Uchaguzi wafanyika nchini liberia licha ya idadi ndogo iliojitokeza kwa hofu ya kuambukizwa Ebola.
Kwenye taifa jirani la Guinea waandamanaji waliwazuia wafanyikazi wa shirika la madaktari wasio na mipaka MSF kuweka kituo cha ebola kusini mwa nchi hiyo.
Polisi wanasema kuwa mahema yalichomwa na wafanyikazi wakafukuzwa na megenge ya vijana.
Jamii kwenye sehemu zingine za magharibi mwa afrika zilipinga jitihada za kukabiliana na ugonjwa huo zikihofia kuwa huenda zikapata maambukizi kutoka kwa wafanyikazi wa kutoa huduma za afya. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC

MOHAMMED ALI ALAZWA HOSPITALINI

 Aliyekuwa bingwa wa ndondi duniani Mohammed Ali na Mwanawe leila Ali.Bondia huyo mkongwe amelazwa hospitalini akiugua maambukizi ya mapafu. 
 
Aliyekuwa bingwa wa ndondi ulimwenguni Mohammed Ali amelazwa hospitalini baada ya kuugua maambukizi ya mapafu.
Ali ambaye ana umri wa miaka 72 na ambaye ana ugua ugonjwa wa Parkinson anadaiwa kuwa katika hali imara .
Msemaji wake amesema kuwa ugonjwa huo uligunduliwa mapema.
Mohammed Ali wakati wake alipokuwa bingwa wa ndoni duniani.
Hatahivyo hakutoa maelezo zaidi na kutaka haki ya faragha ya familia ya bondia huyo mkwongwe kuheshimiwa.
Ali alipataikana na ugonjwa wa Parkinson mwaka 1984,miaka mitatu baada ya kuustafu katika masumbwi.
Alionekana hadharani katika sherehe moja mnamo mwezi Septemba nyumbani kwake Louisville Marekani wakati wa kutoa tuzo za kibinaadamu za bondia huyo. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

REAL MADRID NDIO CLUB BINGWA DUNIANI

Real Madrid washerehekea ushindi wao wa kombe la kilabu bingwa duniani baada ya kuinyuka kilabu ya marekani kusini San Lorenzo 2-0 katika fainali iliochezwa nchini Morrocco. 
 
Kilabu ya Real Madrid imeshinda taji lao la nne mwaka 2014 baada ya kuwashinda mabingwa wa Marekani Kusini kutoka Argentina San Lorenzo katika fainali la za kilabu bingwa duniani zilizochezwa nchini Morrocco.
Mabingwa hao wa kombe la kilabu bingwa barani ulaya,Copa Del Rey na mabingwa wa Super Cup barani Ulaya walianza kufunga kupitia kichwa cha Sergio Ramos.
Makosa ya mlinda lango wa Lorenzo yaliihakikisha ushindi Real madrid baada ya Gareth Bale kuongeza bao la pili.
Real madrid hawakutatizwa na mabingwa hao wa Marekani kusini na hivyobasi kuongeza rekodi yao ya ushindi katika mecho zote kufikia 22.
Ushindi huo pia ni wa kwanza wa kilabu hiyo Bernabeu. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Saturday, December 20, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI DESEMBA 20, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MBUNGE ADAI KUVULIWA NGUO BUNGENI

Muheshimiwa Millie Odhiambo ni mbunge wa eneo bunge la Mbita nchini kenya aliyedaiwa kuwa wabunge wenzake walijaribu kumvua nguo wakati walipokuwa wakipinga mswada wa usalama uliopitishwa katika bunge hilo siku ya alhamisi. 

Kufuatia vurugu na purukushani zilizoonekana katika bunge la Kenya wakati wa kupitishwa kwa mswada wa usalama ,mbunge mmoja mwanamke sasa amejitokeza na kudai kwamba wabunge wenzake watatu wanaume walijaribu kumvua nguo.
Mbunge huyo Millie Odhiambo aliandika katika mtandao wake wa facebook kwamba wabunge wengi walipigwa huku yeye akidai kupigwa ngumi machoni na mbunge mmoja kabla ya wabunge wawili kujaribu kumvua nguo.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MSAKO MKALI KWENYE MTANDAO WA INSTAGRAM

 Justin Bieber anasema amepoteza wafuasi zaidi ya milioni moja. 

Mtandao wa kijamii wa Instagram umefuta mamilioni ya akaunti za watumiaji wa mtandao huo katika msako wake wa kufuta akaunti bandia zilizokuwa zikituma ujumbe ovyo ovyo kwa watumiaji wengine wa mtandao huo.
Watu waliokuwa wanatumia mtandao huo na kuwa na wafuasi wengi, walilalamika sana kufuatia hatua hio na kuitaja kama "Instagram Rapture".
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...