Wednesday, December 24, 2014

IVORY COAST WAGOMEA BAJETI YA SERIKALI - AFCON

 Timu ya Ivory Coast 
 
Shirikisho la soka Ivory Coast (FIF) limegomea bajeti waliyopewa na Serikali ya nchi hiyo kwa ajili ushiriki wa timu ya taifa, The Elephants kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika kwa sababu ni ndogo.
Serikali imekubali kutoa dola za Kimarekani 575 805 kwa Tembo wa Ivory Coast kwenye Fainali za AFCON zitakazofanyika Equatorial Guinea kuanzia Januari 17 hadi Februari 8.
Pamoja na hayo, Makamu wa rais wa FIF, Sory Diabate amewaambia Waandishi wa Habari kwamba Hawawezi kwenda CAN (Mataifa ya Afrika) na faranga (za Ivory Coast, CFA Francs) Milioni 310. Kwa kuwa wamewasilisha bajeti yao kwa ufafanuzi mzuri.
Waziri wa Michezo wa nchi hiyo alikuwa tayari kutoa fungu kamili waliloombwa katika bajeti ya awali faranga bilioni 3.5, pamoja na hayo Ivory Coast ilikwenda michuano hiyo mwaka 2013 Afrika Kusini na jumla ya Faranga bilioni 3.9, huku Serikali ikichangia Bilioni 2.7 wakati Tembo walitolewa na Nigeria katika Robo Fainali.
Kikois cha Herve Renard, kitaanza maandalizi yake kwa kuweka kambi Abu Dhabi, Falme za Kiarabu Januari 5, mwakani. Ivory Coast imepangwa Kund D pamoja na Mali, Cameroon na Guinea. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...