Wednesday, December 24, 2014

EBOSSE: ALGERIA YAPINGA RIPOTI YA MAUAJI

Marehemu Albert Ebosse aliyeaga dunia.Algeria imepinga ripoti ya mauaji yake kwamba mchezaji huyo aliuawa baada ya kuvamiwa. 
 
Waziri wa habari nchini Algeria Mohammed Tahmi amesisiiza kwamba kifo cha mchezaji wa Cameroon Albert Ebosse kilisababishwa na mashabiki waliokuwa wakirushi vitu.
Tahmi ambaye alikuwa akizungumza na radio ya Algeria alikuwa akijibu ripoti ya wiki jana ya daktari wa kuchunguza mauaji kwamba majereha ya Ebosse yalisababishwa na mashambulizi.
Ebosse mwenye umri wa miaka 25 aliaga dunia tarehe 23 mwezi Agosti baada ya kilabu yake JS Kabylie kupoteza 2-1 nyumbani. ''Tumefanya uchunguzi wetu unaoonyesha kwamba mchezaji huyo aliuawa kutokana na kitu kilichorushwa kutoka kwa mashabiki.'',alisema
Mchezaji Ebose aliyekuwa akiichezea timu yake JC kabylie kutoka Algeria
''Mimi si mtaalamu wa sheria lakini nitasema kuwa kifo hicho ni cha bahati mbaya''.,aliongezea ''Vitu vilirushwa kutoka pande zote mbili na wachezaji wote walilengwa na kwa bahati mbaya kisa hicho kikatokea'',alisema.
Swala hilo kwa sasa liko mahakamani ambapo uamuzi utatolewa. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...