Wednesday, December 24, 2014

VILABU VYA ULAYA NA TETESI ZA USAJILI

 Gareth Balle akiwa kazini.
 
Uongozi wa Timu ya Manchester United umesema upo tayari kutoa paundi milioni 120 kwaajili ya kumsajili winga Gareth Balle mwenye umri wa miaka 25 kwa mwezi januari kutoka klabu ya Real Madrid , winga ambaye ni miongoni mwa wachezaji ghali zaidi ulimwenguni.
Gareth Bale alijiunga na Real Madrid kwa kuweka rekodi kubwa duniani kwa usajili wa rekodi ya paundi milioni 85.3 mwaka 2013.
Wakati huo huo kocha Laurent Blanc wa Timu ya Paris St Germain anafikiria kumsajili mshambuliaji Edinson Cavani( 27), kwa gharama ya pauni milioni 50 ikiwa ndio hitaji la Timu ya Arsenal katika katika usajili wa mwezi Januari 2015.
Nayo klabu ya Manchester City inandaa pauni milioni 25 katika jitihada za kutaka kumsajili msahambuliaji wa Atletico Madrid Mario Mandzukic (28). Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...