Monday, September 22, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATATU SEPTEMBA 22, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MATOKEO YA LIGI KUU SOKA NCHINI ENGLAND JANA HAYA HAPA

article-2764265-218D921900000578-139_964x386
ENGLAND: Premier League  
05:30 Finished Leicester 5 – 3 Manchester United       
05:30 Finished Tottenham 0 – 1 West Brom      
08:00 Finished Everton 2 – 3 Crystal Palace      
08:00 Finished  Manchester City 1 – 1 Chelsea       

MANCHESTER UNITED YAPIGWA 5-3 BILA HURUMA

1411308209470_wps_84_Esteban_Cambiasso_of_Leic

Cambiasso akishangilia goli alilofunga dhidi ya Manchester United katika uwanja wa The King Power 
MANCHESTER United wakicheza ugenini wametandikwa  mabao 5-3 dhidi ya Leicester.
Magoli ya wenyeji yalifungwa na Ulloa (2), Nugent, Cambiasso na Vardy.
United walijipatia magoli yao kupitia kwa Van Persie, Di Maria na Herrera 
Radamel Falcao shakes hands with Manchester United captain Wayne Rooney and Ander Herrera before kick-off ahead of his first start for the club

Katika mechi nyingine iliyomalizika jana jioni, Tottenham wakiwa nyumbani wamepigwa 1-0 na West Brom.

Muda huu mechi mbili zinaendelea ambapo Everton wapo nyumbani kuivaa Crystal Palace, wakati Man City wanachuana na Chelsea katika uwanja wa Etihad. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SIMBA YABANWA MBAVU NA WAGOSI WA KAYA, YATOKA 2-2…!!!

MESSI1

WEKUNDU wa Msimbazi, Simba wamelazimisha sare ya mabao 2-2- na Wagosi wa Kaya, Coastal Union katika mchezo wa ufunguzi wa ligi kuu soka Tanzania bara uliomalizika jana jioni uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
Simba chini ya kocha Patrick Phiri walianza mpira wakilishambulia mara kadhaa lango la Coastal na katika dakika ya 7 ya kipindi cha kwanza Mnyama aliandika bao la kuongoza kupitia mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na kiungo mkongwe, Shaaban Kisiga ‘Malone’.
Katika kipindi hicho cha kwanza, Simba waliendelea kucheza vizuri kuanzia safu ya kiungo ambapo Piere Kwizera na Kisiga walionekana kupiga pasi za uhakika, lakini haikuwa rahisi kupasua ngome ya Coastal.
Mara kadhaa Singano na Chanongo walipiga krosi kutoka pande zote za kulia na kushoto, lakini Amissi Tambwe na Okwi walishindwa kukaa maeneo sahihi.
Mnamo dakika ya 36, Tambwe aliandika bao la pili kwa njia ya kichwa akiunganisha krosi iliyochongwa na Okwi kutoka  winga ya kulia na kumuacha kipa wa Coastal Union Shaaban Kado akiokota manyoya.
Dakika ya 56, Uhuru aliingia akitoke benchi kuchukua nafasi ya Haruna Chanongo.
Phiri alifanya mabadiliko ambapo katika dakika ya 64 Tambwe alikwenda benchi na  nafasi yake ilichukuliwa na Paul Kiongera. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Thursday, September 18, 2014

SCOTLAND YAAMUA KUHUSU MUUNGANO

Wascochi wanapiga kura kuamua ikiwa wataendelea kuwa sehemu ya Uingereza au watajitawala
Wapiga kura wamekuwa wakielekea kwa vituo vya kupigia kura katika maeneo mbali mbali nchini Scotland, ambapo watu wanaamua leo ikiwa wataendela kuwa sehemu ya uingereza au wawe taifa huru kwa mara ya kwanza kabisa tangu zaidi ya miaka 300 iliyopita.
Mwandisi wa bbbc anasema kuwa siku ya leo inatarajiwa kuwa ya shughuli nyingi katika historia ya kupiga kura eneo la Scotland ikiwa asilimai 97 ya watu wamejisajili kupiga kura.
Kumekuwa na kampeni kali katika saa 24 zilizopita huku ikidhihirika matokeo yanaweza kwenda upande wowote.
Kiongozi wa chama cha Scotish National Party, Alex Salmond, ametaja kampeni ya kuitisha Uhuru wa Scotland kutoka kwa Uingereza kama tukio muhimu zaidi la kidemokrasia kuwahi kutendeka nchini humo.
Kadhalika amesema tayari limebadilisha mfumo wa maisha eneo la Scotland.
Idadi kubwa ya wapiga kura wamesajiliwa na kwa mara ya kwanza vijana wenye umri wa miaka 16 na 17 wataruhusiwa kupiga kura. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

POLISI WADAIWA KUTESA RAIA NIGERIA

Serikali ya Nigeria bado haijasema chochote kuhusu madai ya Amnesty International
Polisi nchini Nigeria wamedaiwa kuwatesa wanaume na wanawake pamoja na watoto. Taarifa hii ni kwa mujibu wa shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International.
Shirika hilo limechapisha ripoti yake ambayo inadai kwa watu huzuiliwa kinyume na sheria Kaskazini Mashariki mwa Nigeria ambako jeshi la serikali linapambana na wanamgambo wa Boko Haram.
Serikali ingali kujibu tuhuma hizo.
Shirika hilo linasema kuwa jeshi la Nigeria pamoja na polisi hutumia mbinu tofauti kuwatesa watu ikiwemo kuwapiga, kuwadunga misumari na kuwang'oa meno, ubakaji na dhuluma nyinginezo za kingono.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo wanajeshi huwatesa watu zaidi katika eneo la Mashariki ambako vita dhidi ya Boko Haram ni vikali zaidi.
Shirika hilo linasema kuwa kati ya watu efu tano na elfu 10 wamekamatwa tangu mwaka 2009 na kunyongwa katika kambi za wafungwa.
Ripoti hiyo yenye mada, "Welcome to hell fire", inatoa taswira mbaya sana kuhusu haki za binadamu kote nchini Nigeria, na inasema kuwa vituo vingi vya polisi vina afisaa wa polisi anayesimamia mateso na kutaka watu kulipa hongo ili kukwepa mateso hayo.
Licha ya kuharamisha mateso, shirika la Amnesty linasema kuwa wanasiasa nchini humo bado hawajapitisha sheria inayowachukulia hatua wale wanaohusika na mateso dhidi ya raia wasio na hatia. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, September 12, 2014

OSCAR HATIANI KWA KUMUUA MPENZI WAKE BILA KUKUSUDIA

Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius, amepatikana na hatia ya kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp kwa bahati mbaya
Akitoa uamuzi wake jaji Thokozile Masipaal alisema kuwa mwanariadha huyo alimuua Reeva kwa bahati mbaya alipofyatua risasi kupitia kwa mlango wake wa choo akiw akatika hali ua mshtuko akidhani kuwa jambazo alikuwa amevamia nyumba yake. Alisema kuwa upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha kuwa Pistorius alinuia kumuua Steenkamp nw akutekeleza mauaji hayo kwa kusudi. Pia alipatikana na hatia ya kosa la kutumia silaha yake visivyo alipokwenda mgahawani

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MTOTO ALIYEZAMIA NDEGE NA KUTUA ZANZIBAR UTATA MTUPU


Uwanja wa ndege wa Zanzibar  

Polisi Zanzibar wameanza uchunguzi kubaini mazingira ya safari tata ya mtoto Karine Godfrey aliyesafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar kwa ndege bila tiketi wala kugundulika.

Mtoto huyo, Karine au Jenipher Godfrey anayesoma darasa la tatu katika Shule ya Msingi Jitihada, Dar es Salaam alionekana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Septemba Mosi saa 11.30 jioni, akieleza kuwa aliingia Zanzibar kwa ndege ambayo hata hivyo, haikufahamika mara moja ni ya shirika gani.

Alikutwa uwanjani hapo akijiandaa kuondoka kwenda mahali asipopajua.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis alisema mbali ya kushangazwa na mazingira ya safari ya mtoto huyo, polisi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar wanalifanyia kazi suala hilo.

“Ni jambo la kushangaza. Tunajiuliza, huyu mtoto alifikaje katika ndege bila ya kuwa na tiketi wala taarifa zozote kuelezea safari yake na je, huko Dar es Salaam aliondokaje hadi kuingia katika ndege bila ya hivyo vitu, sielewi ilikuwaje. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

CHEYO AWAVAA UKAWA BUNGENI, ADAI HAWAKUKUBALIANA NA RAIS KULIVUNJA BUNGE...!!!


Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, John Cheyo akichangia mjadala kuhusu sura mbalimbali za kwenye Rasimu ya Katiba, mjini Dodoma jana.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Demokrasia Tanzania (TCD), John Cheyo amewavaa viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), akieleza kuwa walichokubaliana katika kikao chao na Rais Jakaya Kikwete ni kwamba Bunge liahirishwe Oktoba 4 na si kama wanavyodai wakiwa nje.
Akizungumza bungeni mjini Dodoma jana, Cheyo alisema hakuna makubaliano ya kutaka Bunge lisitishwe kabla ya kukamilisha kazi zake Oktoba 4, ikiwamo kutoa Katiba itakayopendekezwa kwa wananchi.
“Mojawapo tulilokubaliana ni Bunge hili lipate Katiba itayopendekezwa kwa wananchi,” alisema Cheyo huku akipigiwa makofi na kelele kutoka kwa baadhi ya wajumbe.
“Pia tulikubaliana kwa hali halisi ya muda tulionao, haiwezekani mchakato mzima ukamalizika na maana ya kumalizika mchakato ni kura ya maoni ya wananchi na ndiyo wenye Katiba.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 12, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.


.
.
.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SITTA ASHUKIWA KAMA MWEWE...!!!

Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta akizungumza bungeni. Picha na Maktaba 


Mpango wa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta wa kutaka ya wajumbe wake walioko nje ya nchi kupiga kura kupitisha Katiba inayopendekezwa, umepingwa na wasomi, ukielezwa ni kinyume na kanuni za Bunge na sheria za nchi.
Wasomi hao, wanaharakati na wanasiasa wamesema Tanzania haina utaratibu wa raia wake kupiga kura wakiwa nje ya nchi na kwamba hiyo ni mbinu ya kufanya udanganyifu.
Juzi, Sitta alisema wajumbe wa Bunge hilo watakaokuwa nje ya nchi kwa sababu zozote, ikiwamo ya matibabu na Hijja, watapiga kura hukohuko mara upigaji kura utakapoanza Septemba 26, mwaka huu na kuwataka wajumbe hao kuacha mawasiliano yao watakapokuwa nje na kwamba uongozi wa Bunge umeanza kufanya mawasiliano na balozi mbalimbali za Tanzania, ili wawepo watumishi wake watakaokula kiapo cha kisheria kusimamia kazi hiyo.
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alisema suala la Watanzania kupiga kura wakiwa nje ya nchi halimo kwenye kanuni zinazoongoza Bunge hilo na ni vizuri utaratibu huo ukaachwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

AAMRISHWA KUACHA KUSAMBAZA HIV...!!!

Takriban watu 50,000 nchini Marekani huambukizwa virusi vya HIV kila mwaka
Jaji nchini Marekani amemuamrisha mwanamume mmoja mwathiriwa wa virusi vya HIV kukoma kusambaza virusi hivyo na badala yake kupata matibabu.
Inaarifiwa mwanamume huyo amewaambukiza watu 8 virusi kwa kukusudia katika kipindi cha miaka minne
Mwanamume huyo, aliyetambuliwa tu kwa herufi...'AO' katika stakabadhi zake, ametakiwa na mahakama kupata ushauri nasaha ili aweze kuwakinga wapenzi wake katika siku za usoni.
Maafisa wanasisitiza kwamba sio lengo lao kuufanya uhusiano wa kimapeni kuwa uhalifu bali wanataka zaidi kulinda umma.
Mwanamume huyo huenda akatozwa faini au kufungwa jela ikiwa hatafuata sheria kama alivyotakiwa.
Takriban watu 50,000 nchini Marekani huambukizwa virusi vya HIV kila mwaka , kulingana na shirika la kupambana na maambukizi (CDC).
Asilimia 16% ya watu milioni 1.1 wanaishi na virusi vya HIV bila ya kujua kwamba wameambukizwa.
Mwanamume huyo, alipatikana na virusi vya HIV mwaka 2008 na kuanza kusambaza kwa watu wengine na hadi sasa watu 8 wamethiriwa baada ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi naye.
Alisambaza virusi hivyo licha ya kupokea ushauri nasaha ikiwemo kutumia kinga kila wakati anapojihusisha na tendo la ndoa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

Thursday, September 11, 2014

UKAWA WAPAZA SAUTI...!!!

 
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbroad Slaa akizungumza na wenyeviti wenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), James Mbatia (kulia) na Ibrahim Lipumba baada ya kumaliza kuzungumza na waandishi wahabari kuhusu mchakato wa Katiba na Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umemtaka Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba (BMK), Samuel Sitta kusitisha vikao vya Bunge sasa mpaka mwafaka utakapopatikana kwa kuwa kuendelea kwake kunahalalisha ulaji wa fedha za walipakodi.
Akisoma tamko la vyama hivyo mbele ya wanahabari jana, Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, James Mbatia, alisema: “Ukawa tunapaza sauti zetu, tukisema hapana! Hapana! Haikubaliki.”
Alisema kwa kuwa Rais Jakaya Kikwete na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), wameafikiana kuahirishwa kwa Bunge hilo kupisha maandalizi ya Bunge la Muungano wa Tanzania, kuendelea kwa BMK hadi Oktoba 4 ni ufujaji wa fedha za umma.
Mbatia alisema TCD walikubaliana kuwa mchakato wa Katiba hauwezi kufikia mwisho sasa kutokana na mambo kadhaa kutokwenda sawa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

'SARAFU YA SH 500 NI ISHARA MBAYA'




Huo ni uamuzi wa kawaida tu wa kuiongezea uimara wa kukaa muda mrefu kama BoT walivyosema. Kinach opunguza nguvu ya fedha siyo sarafu wala noti...hivyo uchumi tulionao na mfumuko wa bei hatujafikia kiwango cha kusema Shilingi imeshuka thamani,”  Dk Urassa  
Baada ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kutangaza matumizi ya sarafu mpya ya Sh500, baadhi ya wachumi na wadau wa sekta binafsi nchini wamesema hatua hiyo inaashiria kuporomoka kwa thamani ya shilingi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, wachumi hao walisema kuwapo kwa sarafu hiyo inaonyesha uwezo wa Shilingi kununua bidhaa unazidi kupungua.

Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA), Daniel Machemba alisema Serikali ingejikita zaidi kuzuia kushuka kwa thamani  badala ya kuongeza sarafu.

“Kadri unavyoongeza ukubwa wa fedha, ndivyo inavyozidi kushuka thamani. Hii inamaanisha tunakoelekea tunaweza tukawa kama Zimbabwe kuwa na noti hadi ya Sh100 milioni,” alisema Machemba.

Alisema kuna haja ya Serikali kuzuia matumizi makubwa ya fedha za kigeni nchini hususan Dola za Marekani katika taasisi mbalimbali. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS SEPTEMBA 11, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MBOWE AWAONYA WATAKAOCHAGULIWA KWA NJIA YA RUSHWA


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema chama hakitasita kumvua wadhifa yeyote atakayebainika kuchaguliwa kwa kutoa rushwa.

Mbowe alitoa kauli hiyo jana katika Mkutano Mkuu wa Baraza la Vijana wa Chama hicho, (Bavicha) kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa viongozi watakaoliongoza baraza hilo kwa miaka mitano.

“Hatutawavumilia watakaoshinda kwa rushwa, kinachotakiwa ni wanachama kuchagua viongozi watakaokipeleka mbele chama, chagueni vijana makini na watakaokipeleka chama kushinda chaguzi za vitongoji, serikali za mitaa, udiwani, ubunge na hatimaye uchaguzi mkuu,” alisema Mbowe.

Mbowe, ambaye ni Mbunge wa Hai na kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni aliwahadharisha viongozi watakaopatikana kuhakikisha wanakwenda kuendeleza mapambano. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

YONA AANZA KUJITETEA KISUTU



Waziri wa zamani wa Wizara ya Nishati na Madini, Daniel Yona. Picha na Maktaba 

Waziri wa zamani wa Wizara ya Nishati na Madini, Daniel Yona ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa mchakato wa kumpata mkaguzi wa madini ya dhahabu ulifuata utaratibu kwa kusimamiwa na Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BoT).

Aliyaeleza hayo jana alipojitetea dhidi ya mashtaka ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia Serikali hasara ya Sh11.7 bilioni yanayomkabili na wenzake wawili.

Akiongozwa na wakili wake, Eliasa Msuya kutoa ushahidi wa utetezi mbele ya jopo la mahakimu watatu wanaoisikiliza kesi hiyo, John Utamwa, Sam Rumanyika na Saul Kinemela, Yona alidai kuwa wakati wakiendelea na utaratibu wa kumtafuta mkaguzi wa dhahabu walipata ushauri kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

Alidai kuwa utaratibu wa kumtafuta mkaguzi huyo nchini ulitokana na malalamiko ya wananchi, Bunge, vyombo vya habari na mashirika yasiyo ya kiserikali mwaka 2002, kuhusu mapato ya madini hayo yaliyokuwa yakichimbwa na kampuni tano za kigeni. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RAIS JONATHAN AAMURU MABANGO YANG'OLEWE

Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan ameamuru mabango ya hekeheka za uchaguzi yenye nembo ya kauli mbiu ya 'Bring Back Jonathan 2015' yang'olewe mara moja.
Mabango hayo yamelaaniwa vikali kwenye mitandao ya kijamii kwani yanaonekana kuiga kauli mbiu iliyotumiwa katika kampeini ya kuitaka serikali kuwaokoa wasichana waliotekwa nyara na wanamgambo wa Boko Haram mwezi Aprili mwaka huu.
Kundi hilo la wapiganaji wa kiisilamu bado linawashikilia wasichana hao, Wakati ambapo mabango ya Bring Back Jonathan 2015 yaliowekwa kando ya barabara kuu mjini Abuja, yalilaaniwan vikali nchini Nigeria na kimataifa kupitia katika mitandao ya kijamii.
Watu walihisi kuwa ilikuwa ni kama kejeli kwa kampeini ya 'Bring Back Our Girls' ambayo ilienea kote duniani baada ya Boko Haram kuwateka nyara wasichana wa shule ya Chibok.
Wasichana hao 219, bado hawajulikani waliko miezi mitano baada ya kutekwa kwao.
Rais Jonathan, ameyataka mabango hayo kuondolewa kwenye barabara za mji haraka iwezekanavyo.
Katika taarifa yake alisema yeye pamoja na wanigeria wengi wanahisi kuwa kampeini hiyo ilikuwa na nia mbaya na kusisitiza kuwa juhudi bado zinafanywa kuwoakoa wasichana hao waliotekwa na Boko Haram. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

Wednesday, September 10, 2014

KIKWETE AWATIMUA MAKADA WA CCM WALIOKUSANYIKA KUMPOKEA...!!!

Rais Jakaya Kikwete jana aliwafukuza makada wa CCM waliokuwa wakimsubiri kwenye kituo cha dharura cha ebola alipokitembelea kwa kushtukiza katika Hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam.
Makada hao ambao baadhi yao walivalia sare za CCM, kinyume na matarajio yao, kiongozi huyo alipofika hospitalini hapo alionyesha kuwashangaa kabla ya kuwataka waondoke kwa kuwa hakuhitaji kuzungumza nao, bali wasimamizi wa kituo hicho.
“Hawa watu wote wanafanya nini hapa! Sijaja kuhutubia hapa mimi. Ndugu zangu hawa waliowaita wamewasumbua bure, nawashukuruni sana kwa kuja, endeleeni na shughuli zenu,” alisema Rais Kikwete ambaye aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki.
Hatua hiyo ilionekana kuwanyong’onyeza makada hao ambao hawakuwa na jinsi isipokuwa kuondoka taratibu kwenye eneo hilo na kumwacha Rais Kikwete na viongozi wa kituo hicho.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ZITTO "SIWEZI KUJIUNGA NA UKAWA"

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe. PICHA|MAKTABA 

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe amesema hawezi kujiunga na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwa sababu baadhi ya wajumbe wa umoja huo hawautaki Muungano na wamejificha nyuma ya pazia la kutaka muundo wa serikali tatu.
Amesema si kila mtu anayetaka serikali tatu anaupenda Muungano na kusisitiza kuwa ni aibu kuwa na marais watatu ndani ya nchi moja.
“Msimamo wangu wa serikali tatu si msimamo wa marais watatu kwa sababu najua msimamo wa marais watatu utavunja nchi. Msimamo wangu ni rais mmoja wa Jamhuri ya Muungano, Mkuu wa Serikali Zanzibar na Mkuu wa Serikali Bara,” alisema.
Zitto ambaye alivuliwa nyadhifa zake zote ndani ya Chadema, moja ya vyama vinavyounda Ukawa, alitoa ufafanuzi huo wiki iliyopita katika mahojiano maalumu na gazeti hili nyumbani kwake Masaki, Dar es Salaam. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 10, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MTOTO WA OBASANJO APIGWA RISASI NIGERIA

Wanamgambo wa Boko Haram
Mtoto wa aliyekuwa Rais wa Nigeria, Olesugun Obasanjo amejeruhiwa kwa risasi wakati wa mapambano na wanamgambo wa kiislamu Boko Haram.
Luteni Kanali Adeboye Obasanjo alijeruhiwa siku ya jumatatu wakati jeshi la Nigeria lilipokuwa likipambana kuudhibiti mji wa Michika karibu na mji wa Mubi mji uliokuwa ukidhibitiwa na wanamgambo katika jimbo la Adamawa.
Msemaji wa zamani wa Olusegun Obasanjo ameiambia BBC kuwa kanali Adeboye anaendela vizuri.
Wakazi wa eneo hilo wanasema kuwa maelfu ya watu wameyakimbia makazi yao, wanajeshi wameondoka kwenye kambi za kijeshi na chuo katika jimbo hilo kufungwa.
Wanamgambo wa Boko haram wamedhibiti miji mingi kaskazini mashariki na kutangaza kuwa himaya za kiislamu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

MLIPUKO WAUA VIONGOZI WA WAASI SYRIA

Waasi wakipambana nchini Syria
Wanachama 50 wa kundi moja la waasi wa Syria wameuawa au kujeruhiwa katika shambulio la kujitoa mhanga.
Vyombo vya habari vya serikali na wanaharakati wanasema mshambuliaji wa kujilipua aliilenga nyumba moja katika jimbo la Idlib, ambamo viongozi wa Ahrar al-Sham walikuwa wakikutana.
Kamanda wa kikundi hicho Hassan Abboud ni miongoni mwa watu waliouawa.
Kiongozi huyo ameuawa pamoja na makamanda wengine wa ngazi za juu wa kikundi hicho. Shambulio hilo limefanywa na mtu aliyejilipua katika mji wa Ram Hamdan kaskazini magharibi mwa Syria.
Ahrar al Sham ni sehemu ya kikundi cha Islamic State, muungano wa vikundi saba vya waasi wa kiislamu nchini Syria. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

YANGA HIYOOOO MPAKA FIFA

Kwa maana hiyo Okwi ni mchezaji huru, hivyo yuko huru kujiunga na timu yoyote.

Uongozi wa Yanga umepanga kuliandikia Shirikisho la Kimataifa la Soka (Fifa) kuishtaki TFF kwa kukiuka Kanuni ya 19 ya usajili katika kufanya uamuzi wa utata wa usajili wa mshambuliaji wa Uganda, Emmanuel Okwi.
Kikao cha Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF kilichofanyika jijini Dar es salaam juzi, kiliamua kumtangaza Okwi kuwa mchezaji huru baada ya kubaini kuwa Yanga ilivunja mkataba kwa kutomlipa stahiki zake za usajili na pia kuandika barua TFF kutaka mkataba wake na Mganda huyo uvunjwe, uamuzi ambao umeinufaisha Simba ambayo imemsajili.
Mkataba wa mchezaji huyo ulipitiwa na kamati hiyo ikiwamo kumsikiliza mchezaji mwenyewe pamoja na Yanga na kuridhika kuwa mkataba kati ya pande hizo umevunjika.
Kamati hiyo ilisema ukiwa ni mkataba wa pande mbili, Yanga ilikiuka kipengele namba nane kuhusu malipo ya ada ya usajili. Yanga ikiwa mwajiri, haikutekeleza kipengele hicho hadi kufikia Juni 27 mwaka huu, ilipoandika barua TFF kuomba mkataba huo uvunjwe. Kwa maana hiyo Okwi ni mchezaji huru, hivyo yuko huru kujiunga na timu yoyote.
Hata hivyo, uongozi wa Yanga jana ulisema haukubaliani na uamuzi huo na kwamba walikuwa wameshaandika barua kupinga baadhi ya wajumbe katika kamati ya sheria ya TFF wasisikilize kesi yao, akiwamo mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Pope ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo ya sheria.

Monday, September 08, 2014

"WAPAMBE WAMETUFITINISHA NA MBOWE" ZITTO KABWE


Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe akifafanua jambo. 


Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ameeleza tofauti yake na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, akisema imesababishwa na watu aliowaita wapambe.

Zitto (37), ambaye alikuwa naibu katibu mkuu wa Chadema, alisema kuwa hata kuvuliwa nyadhifa zake ndani ya chama kulisababishwa na wapambe hao, lakini akasisitiza kuwa hana kinyongo tena kwa kuwa alishamwomba Mungu na sasa amesamehe kabisa.

Tofauti za wawili hao hazijawahi kutolewa hadharani licha ya mitandao mbalimbali kuzungumzia kuharibika kwa uhusiano wao ikinukuu habari kutoka vikao vya ndani vya Chadema.

Hata hivyo, mapema mwaka huu, Zitto alirushiwa tuhuma nzito na Chadema kutokana na uhusiano wake na baadhi ya makada wa CCM, lakini mbunge huyo aliyahusisha maneno hayo na mwenyekiti wake na aliandika maneno makali dhidi ya Mbowe kwenye ukurasa wake wa facebook. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SARAFU YA SH. 500 KUANZA KUTUMIKA OCTOBA

Sarafu ya Shilingi mia tano inayotarajiwa kuanza kutumika mapema mwezi oktoba. Picha na Emmanuel Herman
Dar es Salaam. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imezindua rasmi sarafu mpya ya Sh500 itakayoanza kutumika Oktoba mwaka huu.
Akizungumza wakati wa kutambulisha sarafu hiyo, mkurugenzi wa huduma za kibenki wa BoT, Emmanuel Boaz alisema Serikali imefanya uamuzi huo ili kurahisisha upatikanaji wa chenji na kutunza ubora wa fedha.
“Noti ya Sh500 ndiyo inayopitia mikononi mwa wananchi wengi hivyo kuchakaa mapema. Lakini kutokana na gharama ya kuzichapisha ukilinganisha na sarafu ambazo hudumu kwa muda mrefu, tumeamua kuziondoa noti na kuleta sarafu yenye thamani ile ile.
Kuna taratibu tunaendelea kuzikamilisha kabla hatujaziingiza sarafu hizo katika mzunguko mwezi Oktoba. Zitakapoanza kutumika hakutakuwa na haja ya wananchi kwenda kubadilisha noti walizonazo kwani zitakuwa zinatumika pamoja hadi zitakapopotea katika mzunguko,”alisema.
Sarafu hiyo ina umbo la duara, lenye kipenyo cha milimita 27.5 na michirizi pembeni ikiwa na uzito wa gramu 9.5. Mbele ina picha ya Rais wa kwanza wa Zanzibar, Sheikh Abeid Aman Karume na nyuma ni nyati. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU SEPTEMBA 08, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WEZI WA GARI LA RAIS WAFIKISHWA MAHAKAMANI



Gari la msafara wa Rais Kenyatta lilipatikana mjini Kampala Uganda

Watu watano akiwemo raia mmoja wa Uganda pamoja na fundi mmoja wa magari wameshitakiwa kwa kosa la wizi wa gari la msafara wa ulinzi wa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta nchini Kenya.
Watano hao pia walishitakiwa kwa kumuibia gari inspekta wa polisi David Machui aliyekuwa akiendesha gari hilo aina ya BMW 735 tarehe 26 mwezi Agosti mjini Nairobi lilipoibwa.
Washukiwa hao wote walikanusha madai hayo kwamba walihusika katika wizi wa gari hilo.
Kila mshukiwa aliachiliwa kwa kima cha shilingi milioni 5 isipokuwa mwanamume mmoja aliyesemekana kuwa na kesi tofauti mahakamani.
Raia wa Uganda Robert Mande Ochan, aliamrishwa na mahakama kutoa dhamana ya shilingi milioni mbili ili aweze kuachiliwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TUHUMA ZA UBAKAJI DHIDI YA AU

Shirika la haki za binadamu la Human Rights Watch limetoa ripoti kuhusu udhalilishwaji kijinsia wanaofanyiwa wanawake nchini Somalia na askari wa kulinda amani nchini humo.Majeshi hayo yamo nchini Somalia yakiwakilisha Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa kupambana na wapiganaji wa kikundi cha Kiislam cha Al Shaabab.
Shirika hilo la kutetea haki za binadamula Human Rights Watch limesema liliwahoji wanawake 21, wakiwemo wasichana waliobakwa na wanajeshi hao mwaka 2013.
Visa vingi vimeripotiwa katika kambi zinazosimamiwa na wanajeshi wa Burundi na Uganda.
Walinda amani wa Muungano wa Afrika wamedaiwa katika ripoti hiyo, kutumia chakula cha misaada kushawishi wasichana na wanawake kufanya mapenzi nao.
Wanajeshi hao wanadaiwa pia kuwabaka ama kuwadhalilisha kingono wanawake waliofika katika kambi hizo kuomba msaada wa matibabu au maji. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

LIONEL MESSI AMGARAGAZA CRISTIANO RONALDO TUZO YA FIFA 15, LIGI KUU ENGLAND

1410107894477_wps_32_image001_png
Mcheza bora wa dunia: EA Sports wamemuweka nyota wa Barcelona, Lionel Messi kuwa namba moja katika michezo mipya ya FIFA 15
CRISTIANO Ronaldo alimgaragaza Lionel Messi katika tuzo ya  Ballon d’Or mapema mwaka huu,lakini nyota huyo wa Barcelona amelipa kisasi kwa mpinzani wake huyo mkubwa kwa kushinda tuzo nyingine.
Akiwa amepata pointi 93 kati ya 100, messi amekuwa namba moja katika tuzo ya michezo ya Video ya FIFA, (FIFA 15) ambayo itatangazwa rasmi septemba 26 mwaka huu huko UK.
Ili kuwapa nafasi mashabiki kupiga kura kabla, waendeshaji wa tuzo hiyo, EA Sports walitangaza majina ya wachezaji 50.
Wanted man: Barcelona are sure to prove popular on the new game given Messi's eye catching statistics

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...