Friday, September 12, 2014

CHEYO AWAVAA UKAWA BUNGENI, ADAI HAWAKUKUBALIANA NA RAIS KULIVUNJA BUNGE...!!!


Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, John Cheyo akichangia mjadala kuhusu sura mbalimbali za kwenye Rasimu ya Katiba, mjini Dodoma jana.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Demokrasia Tanzania (TCD), John Cheyo amewavaa viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), akieleza kuwa walichokubaliana katika kikao chao na Rais Jakaya Kikwete ni kwamba Bunge liahirishwe Oktoba 4 na si kama wanavyodai wakiwa nje.
Akizungumza bungeni mjini Dodoma jana, Cheyo alisema hakuna makubaliano ya kutaka Bunge lisitishwe kabla ya kukamilisha kazi zake Oktoba 4, ikiwamo kutoa Katiba itakayopendekezwa kwa wananchi.
“Mojawapo tulilokubaliana ni Bunge hili lipate Katiba itayopendekezwa kwa wananchi,” alisema Cheyo huku akipigiwa makofi na kelele kutoka kwa baadhi ya wajumbe.
“Pia tulikubaliana kwa hali halisi ya muda tulionao, haiwezekani mchakato mzima ukamalizika na maana ya kumalizika mchakato ni kura ya maoni ya wananchi na ndiyo wenye Katiba.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
“Tukasema kama inabidi tufike mpaka kule (kura ya maoni) inatubidi tuahirishe uchaguzi wa 2015 jambo ambalo sisi wote hatuliafiki na mheshimiwa Rais alisema msinitwishe mzigo huu,” alisisitiza Cheyo.
Cheyo alisema Rais katika mazungumzo hayo alitaka utaratibu wa kufanya uchaguzi kila Oktoba ya mwisho wa kipindi cha miaka mitano uendelee ili wananchi wenyewe watoe ridhaa kupitia uchaguzi wa viongozi.
“Bunge hili haliendeshwi kwa amri ya mtu ambaye yuko barabarani. Bunge hili linaendeshwa kwa mujibu wa Sheria na sheria tuliyokuwa nayo kwa sasa ni GN 254 (tangazo la Serikali) ambayo inasema uhai wa Bunge ni mpaka Oktoba 4,”alisema Cheyo.
Cheyo alisema haiwezekani Rais akasimama mara baada ya makubaliano na kutangaza kuwa siku inayofuata Bunge lisitishe shughuli zake.
“Watu tumekubaliana na kuna video ambayo kila mmoja aliyekuwa akizungumza alirekodiwa. Kweli mnataka tumuombe sasa mheshimiwa Rais tutengenezewe kipindi maalumu kila mmoja aonekane anasema nini?” alihoji.
“Tuwe waungwana. Itoshe mimi kusema yale niliyotangaza hayo ndiyo makubaliano. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na Mwananchi

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...