Friday, September 12, 2014

SITTA ASHUKIWA KAMA MWEWE...!!!

Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta akizungumza bungeni. Picha na Maktaba 


Mpango wa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta wa kutaka ya wajumbe wake walioko nje ya nchi kupiga kura kupitisha Katiba inayopendekezwa, umepingwa na wasomi, ukielezwa ni kinyume na kanuni za Bunge na sheria za nchi.
Wasomi hao, wanaharakati na wanasiasa wamesema Tanzania haina utaratibu wa raia wake kupiga kura wakiwa nje ya nchi na kwamba hiyo ni mbinu ya kufanya udanganyifu.
Juzi, Sitta alisema wajumbe wa Bunge hilo watakaokuwa nje ya nchi kwa sababu zozote, ikiwamo ya matibabu na Hijja, watapiga kura hukohuko mara upigaji kura utakapoanza Septemba 26, mwaka huu na kuwataka wajumbe hao kuacha mawasiliano yao watakapokuwa nje na kwamba uongozi wa Bunge umeanza kufanya mawasiliano na balozi mbalimbali za Tanzania, ili wawepo watumishi wake watakaokula kiapo cha kisheria kusimamia kazi hiyo.
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alisema suala la Watanzania kupiga kura wakiwa nje ya nchi halimo kwenye kanuni zinazoongoza Bunge hilo na ni vizuri utaratibu huo ukaachwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Alisema anachokiona sasa ni Bunge kuendelea kupoteza fedha za wananchi wakati hakuna maridhiano huku uamuzi ukiwa umefikiwa kwamba Katiba Mpya itapatikana baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema: “Hata kanuni za mabunge ya Jumuiya za Madola ambazo sisi tunazifuata ikitokea mjumbe anaumwa anapelekwa kwenye ukumbi wa Bunge kupiga kura, kura haipigwi sehemu yoyote.
“Hata katika Bunge la Uingereza ikionekana mjumbe anatakiwa kupiga kura lakini anaumwa atapelekwa ukumbini kwa msaada wa uongozi wa Bunge, ili aweze kutimiza haki yake ya kidemokrasia lakini haki hiyo haiwezi kumfuata huko aliko.
“Sitta analichukulia suala la Katiba kama lake binafsi, utaratibu wa kupiga kura za kificho haukubaliki kwa sababu utasababisha uchakachuaji,” alisema.
Mkurugenzi Mkuu wa Utetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Onesmo Olengurumwa alisema Tanzania haina utaratibu wa raia wake kupiga kura wakiwa nje ya nchi.
Mwanasheria huyo alisema kinachofanywa na Sitta kinaonyesha namna Bunge la Katiba linavyolazimisha mchakato huo.
“Kituo pekee cha wajumbe wa Bunge Maalumu kupiga kura ni ndani ya Ukumbi wa Bunge na si vinginevyo. Kinachofanywa na Sitta ni kuwahadaa Watanzania, mtu anaumwa atapigaje kura wakati hata kwenye majadiliano hakuwapo? Unalipigia kura jambo ambalo umeshiriki kwenye majadiliano,” alisema.
Alisema Tanzania haina utaratibu wa raia wake kupiga kura wakiwa nje ya nchi na kwamba endapo Serikali inataka kuuruhusu basi ifanye hivyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Rais wa zamani wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Felix Kibodya alisema kama kuna idadi kubwa ya wajumbe wa Bunge Maalumu ambao wamesafiri kwenda nje ya nchi katika kipindi hiki, basi Bunge liahirishwe kama ambavyo wadau wamekuwa wakishauri.
“Nani atatuhakikishia usalama wa kura hizo, kama ni upigaji wa kura za siri nani atatunza siri hizo, tunajiuliza maswali mengi je, kutakuwa na msimamizi wa upigaji huo wa kura,” alisema.
Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Hebron Mwakagenda alisema ingawa kuna nchi zenye utaratibu wa raia wake kupiga kura wakiwa nje ya nchi, Tanzania haina utaratibu huo.
“Sitta anafanya mambo ya ajabu kuanzisha utaratibu huo, hii inaonyesha mambo yameshakuwa magumu na sasa wanaokoteza kura popote zilipo,” alisema.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Ruaha, Iringa, Profesa Gaudence Mpangala alisema Sitta anataka kuokoteza kura na kwamba Katiba ni suala la maridhiano na si wingi wa kura... “Ndiyo maana nimekuwa nikipendekeza Bunge Maalumu lisitishwe kwa sababu linapoteza fedha za wananchi,” alisema.
Wakili Peter Shayo wa Arusha alisema utaratibu wa kuwaruhusu wajumbe walioko nje ya nchi kupigia kura Rasimu ya Katiba inayopendekezwa ni kukiuka kanuni za Bunge hilo.
“Ukisoma vizuri kanuni za hilo Bunge, kura za siri zinataka kuwapo kwa mawakala, nje ya nchi watapatikanaje? Maana ama anapiga kura ya ndiyo au hapana lazima kuwe na wakala anayemwamini, huko nje wanawapataje?” alihoji.
Hata hivyo, Mjumbe wa Bunge hilo, Charles Mwijage alisema haoni tatizo kwa wajumbe watakaokuwa nje ya nchi kupiga wakiwa huko... “Naamini Mwenyekiti (Sitta) na timu yake ya wataalamu wamezipitia hizo kanuni na kujiridhisha lakini usisahau kanuni pia zinaweza kufanyiwa marekebisho kama ni lazima.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Na Mwananchi

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...