Monday, September 08, 2014

LIONEL MESSI AMGARAGAZA CRISTIANO RONALDO TUZO YA FIFA 15, LIGI KUU ENGLAND

1410107894477_wps_32_image001_png
Mcheza bora wa dunia: EA Sports wamemuweka nyota wa Barcelona, Lionel Messi kuwa namba moja katika michezo mipya ya FIFA 15
CRISTIANO Ronaldo alimgaragaza Lionel Messi katika tuzo ya  Ballon d’Or mapema mwaka huu,lakini nyota huyo wa Barcelona amelipa kisasi kwa mpinzani wake huyo mkubwa kwa kushinda tuzo nyingine.
Akiwa amepata pointi 93 kati ya 100, messi amekuwa namba moja katika tuzo ya michezo ya Video ya FIFA, (FIFA 15) ambayo itatangazwa rasmi septemba 26 mwaka huu huko UK.
Ili kuwapa nafasi mashabiki kupiga kura kabla, waendeshaji wa tuzo hiyo, EA Sports walitangaza majina ya wachezaji 50.
Wanted man: Barcelona are sure to prove popular on the new game given Messi's eye catching statistics
Second best: Real Madrid's Cristiano Ronaldo has been given a rating of 92 on FIFA 15
Dangerous: EA Sports rate Ronaldo's shooting ability and pace at 93 out of 100
FIFA 15 TOP 10 PLAYERS 
1. Lionel Messi 93
2. Cristiano Ronaldo 92
3. Arjen Robben 90
4. Zlatan Ibrahimovic 90
5. Manuel Neuer 90
6. Andres Iniesta 89
7. Luis Suarez 89
8. Bastian Schweinsteiger 88
9. Franck Ribery 88
10. Eden Hazard 88 

Messi amemshinda Ronaldo kwa tofauti ya pointi moja nyota wa Real Madrid aliyepata alama 92 hasa katika uwezo wa kufunga mabao.
Nyota wa Bayern Munich na Uholanzi Arjen Robben ameshika namba tatu kwa pointi zake 90.
Takwimu hizo zinazozingatia zaidi kiwango cha mchezaji katika mechi za ligi na makombe katika siku 365 zilizopita, zinaonesga uwezo wa kila mchezaji kila anapotumika katika mechi.
Mshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Zlatan Ibrahimovic na kipa wa Bayern Munich,  Manuel Neuer wameshika nafasi ya nne na tano, licha ya kupata pointi sawa na Robben.
Nyota wawili wa Barca, Andres Iniesta naLuis Suarez – ambao wote wamepewa alama 89 wanakalia nafasi ya sita na saba, wakati nyota wawili wa Bayern Munich, Bastian Schweinsteiger na Franck Ribery (wote pointi 88) wanashika nafasi ya nane na tisa.
Winga wa Chelsea,  Eden Hazard, waliyepata pointi 88 mwaka jana, ni mchezaji pekee wa ligi kuu England aliyeingia 10 bora, akiwazidi kete nyota wa Manchester United  Robin van Persie na Radamel Falcao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...