Thursday, September 11, 2014

MBOWE AWAONYA WATAKAOCHAGULIWA KWA NJIA YA RUSHWA


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema chama hakitasita kumvua wadhifa yeyote atakayebainika kuchaguliwa kwa kutoa rushwa.

Mbowe alitoa kauli hiyo jana katika Mkutano Mkuu wa Baraza la Vijana wa Chama hicho, (Bavicha) kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa viongozi watakaoliongoza baraza hilo kwa miaka mitano.

“Hatutawavumilia watakaoshinda kwa rushwa, kinachotakiwa ni wanachama kuchagua viongozi watakaokipeleka mbele chama, chagueni vijana makini na watakaokipeleka chama kushinda chaguzi za vitongoji, serikali za mitaa, udiwani, ubunge na hatimaye uchaguzi mkuu,” alisema Mbowe.

Mbowe, ambaye ni Mbunge wa Hai na kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni aliwahadharisha viongozi watakaopatikana kuhakikisha wanakwenda kuendeleza mapambano. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

“Iwe ni marufuku kuruhusu nafasi yoyote eti kiongozi wa CCM anapita bila kupingwa, wa CCM akipita hivyo na wewe jiandae kuwajibika na sisi Ukawa hatutagombea nafasi tutaangalia jinsi gani tutaweza kushirikiana hadi kuiondoa CCM madarakani mwakani,” alisema Mbowe huku akishangiliwa na wajumbe wa mkutano huo.

Mbowe alivishauri vyama vya CUF na NCCR-Mageuzi kuendeleza harakati za kujijenga kila chama kwa namna yake ili utakapofika wakati wa kuunganisha nguvu iwe rahisi kushinda uchaguzi.

Naye Mwenyekiti aliyemaliza muda wake wa Bavicha, John Heche alisema chama hicho kwa sasa kimeimarika kuanzia ngazi ya misingi hadi mikoa na kufikia matawi 350.

“Ninyi vijana chagueni viongozi makini, watakaokitoa chama hapa kilipo kukipeleka mbele zaidi, wapo waliopoteza uhai, kujeruhiwa na kupoteza mali zao kwa ajili ya Chadema hivyo unapopata dhamana ya kuwa kiongozi ndani ya Chadema itumie vizuri,” alisema Heche.

Uchaguzi wa viongozi kuongoza baraza hilo, ulikuwa ukiendelea wakati gazeti hili likienda mitamboni. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na Mwananchi

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...