Wednesday, January 21, 2015

ARSENAL YAMSAJILI KRYSTIAN BIELIK

Krystian Bielik aliyesajiliwa na Arsenal
Arsenal imekamilisha usajili wa kiungo wa kati Krystian Bielik mwenye umri wa miaka 17 kutoka kilabu ya Legia warsaw kwa kitita kisichojulikana.
Bielik aliichezea timu kubwa ya kilabu hiyo ya Poland mnamo mwezi Agosti akiwa na umri wa miaka 16.
Pia alishiriki katika mechi tano ya kilabu hiyo na mara moja katika ligi ya yuropa.Mchezaji huyo anayesifiwa na wengi anaweza kucheza katika safu ya kati na ile ya Ulinzi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Sunday, January 18, 2015

MATOKEO YA MECHI ZA EPL LEO JUMAPILI HAYA HAPA


article-2915617-24D1DC2000000578-487_964x390 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
 
EnglandPremier LeagueJanuary 18
FT West Ham United 3 – 0 Hull City
FT Manchester City 0 – 2 Arsenal

UPINZANI DRC: KATIBA IMEPINDULIWA

 
Wabunge wa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo wamekubali mswada ambao wadadisi wanasema unakusudiwa kumpa Rais Joseph Kabila idhini ya kubaki madarakani, baada muhula wake wa pili kumalizika.
Mswada huo unapendekeza kufanywe sensa ya taifa kabla ya uchaguzi ambayo serikali inasema inaweza kuchukua miaka kadha kukamilisha.
Rais Kabila anamaliza muhula wa pili mwaka ujao.
Katiba ya nchi haimruhusu kugombea muhula wa tatu.
Mwandishi wa BBC mjini Kinshasa anasema wabunge wengi wa upinzani walisusia kura hiyo ya bunge, na kuielezea kuwa mapinduzi ya katiba. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

BOKO HARAM WAFANYA UVAMIZI CAMEROON

Askari jeshi wanaodhaniwa kuwa wapiganaji wa kundi haramu Boko Haram wameteka watu zaidi ya 60 katika nchi jirani ya Cameroon imethibitika.
Inasemekana miongoni mwa mateka wengi wao ni watoto waliokamtwa mpakani mwa nchi mbili hizo.Na inaarifiwa kuwa watu kadhaa waliuawa wakati wa utekelezaji wa tukio hilo.
Boko Haram siku za hivi karibuni zimekamata udhibiti wa miji kadhaa na vijiji upande wa kaskazini Mashariki mwa Nigeria, na sasa wameanza kuwa tishio kwa nchi jirani wanazopakana na Nigeria .Katika shambulio hilo la siku ya Jumapili askari hao walivamia vijiji viwili vilivyoko eneo la Tourou .
Katika uvamizi huo nyumba kadhaa zilichomwa moto na idadi ya mateka ni themanini kati yao watu wazima ni thelathini,na watoto wapatao hamsini na walielekea upande wa Kaskazini mwa Cameroon .
Kundi hilo limepigana vita takribani miaka sita sasa, wakijaribu kuusimika utawala wa dola ya kiislam nchini humo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ARSENAL YAWASHANGAZA MABINGWA WA EPL

 Santi Carzola alifunga bao moja na kutengeza jengine na kuisadia Arsenal kuicharaza Mancity mabao 2-0 nyumbani Manchester.
Ushindi huo wa Arsenal pia ulisitisha msururu wa kutofungwa wa Mancity wa mechi 12.
Mchezaji wa Uhispania Santi Carzola aliyekuwa moto wa kuotea mbali dhidi ya Mancity alifunga mkwaju wa penalty baada ya beki wa Arsenal Nacho Monreal kuangushwa katika eneo la hatari na beki Vincent Kompany.
 
Arsenal iliongeza bao la pili katika kipindi cha pili baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na Santi Carzola kuwekwa wavuni na Olivier Giroud.
Matokeo hayo yameiwacha City ikiwa na alama 5 chini ya viongozi wa ligi Chelsea.
City na Arsenal walitoka sare ya 2-2 wakati walipokutana kwa mara ya kwanza katika uga wa Emirates mnamo mwezi Septemba. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

VIWANJANI MWISHONI MWA WIKI

Ligi kuu ya England imeendelea kwa mechi mbili ambapo..Arsenal imeibamiza Man City ,Huku Westham Ikiibamiza Hull City bao 3-0
Nayo Michuano ya Kombe la Mataifa barani Afrika ikiwa imeng'oa nanga hapo jana kwa Gabon Kuilaza Burkina faso bao 2-0 Huku Pierre Emerick Aubemeyang aking'ara vilivyo.Nao wenyeji Equitorial Guinea wakishikwa shati na Congo Brazaville kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1.
Ligi kuu ya England ambapo Jumapili zimechezwa mechi mbili ,Katika mechi ya awali Westham United iliibamiza Hull City bao 3-0 mabao yaliyotiwa kambani na Andy Carrol katika dakika ya 49,Amalfitano katika dakika ya 69 na Stewart Downing aliyehitiisha ushindi huo mnono wa Westham katika ya 72 akimalizia pasi murua ya kiungo Mcameroun aliyeko kwenye Fomu Alexandre Song.
Kwa matokeo hayo Westham imefikisha Point 36 wakiwa nafasi ya 7,wakiwa pointi moja mbele ya Liverpool wenye pointi 35 walioko nafasi ya 8,huku timu hizo zikitaraji kukutana katika mechi ijayo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Wednesday, January 14, 2015

'HATUFUKUZI MGOMBEA URAIS CCM'

 
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akifungua kikao cha Kamati Kuu ya CCM , mjini Unguja , Zanzibar jana.  Kushoto ni Makamu wake (Zanzibar), Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed Shein .

Wakati Kamati Kuu ya chama tawala, CCM ikimaliza vikao vyake mjini hapa, Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana amesema mambo mengi yanayozungumzwa kuhusu baadhi ya wanachama wanaotajwa kuwania urais hayana ukweli, wala hakuna atakayefukuzwa uanachama.
Kinana aliyasema hayo jana mjini hapa kuhusu mambo yaliyojitokeza kwa wagombea wa nafasi za urais kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu, Oktoba.
Kamati Kuu ya CCM hadi jana jioni ilikuwa ikiendelea na kikao chake kwenye ofisi kuu ya chama, Kisiwandui, Zanzibar.
Kauli ya Kinana imekuja baada ya kuwapo kwa minong’ono kuwa baadhi ya makada waliojitokeza kutangaza ama kuonyesha nia kuutaka urais watachukuliwa hatua, zikiwamo kutimuliwa. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

NGELEJA, CHENGE WAPELEKWA KWENYE KAMATI YA MAADILI

 
Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za mitaa (LAAC) za Mitaa, Kangi Lugola akizungumza wakati wa kikao cha kamati hiyo kilichofanyika Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mjumbe mwenzake, Omari Nundu.

Licha ya Bunge kuazimia kuwa wenyeviti wa kamati zake waliotajwa kuhusika kwenye kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow wavuliwe nyadhifa zao, hali imekuwa tofauti katika vikao vya kamati hizo vilivyoanza jana baada ya baadhi yao kuongoza vikao hivyo. Jana, Kamati Kuu ya CCM imeamua viongozi hao, Andrew Chenge, William Ngeleja Na Profesa Anna Tibaijuka wafikishwe Kamati ya Maadili ya chama.
Awali, walitakiwa kuachia ngazi na kamati zao katika mabano ni Ngeleja (Katiba, Sheria na Utawala), Chenge (Bajeti) na Victor Mwambalaswa (Nishati na Madini).
Kikao cha 16 na 17 cha Bunge kiliazimia kuwa kamati husika za kudumu za Bunge zichukue hatua za haraka na kwa vyovyote vile kabla ya Mkutano wa 18 wa Bunge unaoanza Januari 27, kuwavua nyadhifa zao wenyeviti tajwa wa kamati husika.
Hata hivyo, jana, Ngeleja alisema anaendelea na madaraka yake, kwa kuwa hatua iliyopo sasa ni ya uchunguzi.  Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JANUARI 14, 2015


.


.
.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

GAZETI LENYE KIBONZO CHA MTUME LAUZWA TENA...!!!

Gazeti la Charlie Hebdo leo limeanza kusambaza toleo la gazeti lake ambalo limechapishwa kibonzo cha Mtume Mohammad kwenye ukurasa wake wa mbele.
Nakala Milioni za gazeti hilo zimeanza kusambazwa na nyingine zitafuata iwapo wanunuzi wataongezeka.
Picha ya kibonzo hicho iliyopo ukurasa mbele wa gazeti hilo inamwonyesha Mtume Mohammad akilia.
Wandishi wa jarida la Charlie Hebdo wamechapisha tena picha ya kibonzo cha mtume Muhammad
Wachambuzi wa mambo wanaona kuwa picha hiyo itachochea chuki.
Hata hivyo waandishi wa habari wa gazeti hilo wanasema ukurasa wa mbele unamaanisha Waandishi wa habari wamewasamehe waliotekeleza shambulizi la kigaidi lilolofanyika jumatano wiki iliyopita.
Naibu Mhariri wa Gazeti la Liberalation Alexandra Schwatzbrod anasema ulikuwa uamuzi mwepesi kwa gazeti lake kuchapisha picha ya kibonzo hicho. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ONGWEN AKABIDHIWA KWA WANAJESHI WA UGANDA

Kamanda Ongwen sasa yuko mikononi mwa wanajeshi wa Uganda 
 
Kamanda mkuu wa kundi la waasi la LRA nchini Uganda, aliyejisalimisha wiki jana, Dominic Ongwen , amekabidhiwa kwa wanajeshi wa Uganda walio katika Jamuhuri ya Afrika ya kati.
Muasi huyo, Dominic Ongwen, anasemekana kuwa naibu kiongozi wa kundi hilo Joseph Kony na alikamatwa na wanajeshi wa Marekani wiki jana ingawa waasi wa Seleka wanasema wao ndio waliomkamata.
Waasi hao walisema kwamba walimkatama Ongwen baada ya makabiliano ya muda ingawa jeshi la Marekani lilisitiza kuwa alijisalimisha na tangu hao wamekuwa wakimzuilia.
Uganda imesema kwamba itamkabidhi kwa mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC, ambako anatakikana kwa kutenda uhalifu dhidi ya binadamu.
Kundi la LRA liliwateka nyara wasichana na wavulana huku wavulana wakilazimishwa kuwa wapiganaji na wasichana wakifanywa watumwa wa ngono.
Ongwen pamoja na Joseph Kony wanatakikana na mahakama ya ICC kujibu tuhuma za kutenda uhalifu dhidi ya binadamu.
Je Ongwen ni nani?
-Inaarifiwa alitekwa nyara na waasi wa LRA akiwa na umri wa miaka 10 wakati alipokuwa anaelekea shuleni Kaskazini mwa Uganda.
-Miaka iliyofuata, alipanda ngazi na kuwa kamanda
-Anatuhumiwa kutenda uhalifu dhidi ya binadamu ikiwemo, kuwatumia watoto kama watumwa.
-ICC ilitoa kibali cha kumkamata mnamo mwaka 2005.
-Kuliwa na madai kwamba aliuawa katika mwaka 2013 ambapo Marekani ilitangaza ahadi ya zawadi kwa yeyeote mwenye taarifa kumhusu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

AVULIWA NGUO KUTHIBITISHA JINSIA YAKE

Genoveva Anonma
 
Genoveva Anonma alidhalilishwa,kwa takriban miaka minne,amekuwa akihisiwa kuwa si mwanamke naye amekuwa akizidharau tuhuma hizo mara kwa mara.
Lakini kuna kitu ambacho hakukitegemea kilichokuwa kinamuandama kufuatia uwezo wake michezoni alipokuwa Equatorial Guinea mwaka 2008 katika michuano ya soka la wanawake wa mataifa ya Afrika.
Goli lake la ushindi katika ardhi ya nyumbani,na timu yake kuwa ya kwanza wakiifuatia Nigeria ,ambayo iliibuka kuwa washindi wa jumla,Anonma badala ya kuhesabika kuwa mkombozi na mwenye kuitimiza ndoto yake michezoni, badala yake amebaki njia panda.
Anonma awapo uwanjani huwa ana haha uwanjani huku na kule na nguvu alo nayo,timu pinzani humbeza kuwa hawezi kuwa mwanamke bali wanacheza na janadume,na ndipo sasa kituko kikaja kutokana na tuhuma hizo shirikisho la soka barani Africa walichagua njia ya kuhakiki jinsia ya Anonma. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KOCHA NOOIJ KUTAJA STARS MABORESHO

IMG_0316
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij anatarajia kutaja kikosi cha Maboresho kitakachoingia kambini Januari 18 mwaka huu kujiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Rwanda itakayofanyika Januari 22 mwaka huu jijini Mwanza.

Nooij atataja kikosi hicho kwenye mkutano na waandishi wa habari utakaofanyika kesho (Januari 15 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Uwanja wa Karume. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TANZANIA KUIKABILI KENYA BEACH SOCCER

Soka la ufukweni 
 
Timu ya Taifa ya Tanzania ya mpira wa ufukweni (beach soccer) imepangiwa kucheza na Kenya katika raundi ya kwanza ya michuano ya Afrika kwa ajili ya fainali za Afrika ambapo michuano hiyo itafanyika Aprili mwaka huu nchini Shelisheli.
Mwenyekiti wa Kamati ya Beach Soccer, Ahmed Idd Mgoyi amesema jijini Dar es Salaam, kuwa Tanzania itaanzia ugenini ambapo mechi ya kwanza itachezwa kati ya Februari 13 na 15 mwaka huu nchini Kenya.
Mechi ya marudiano itafanyikaa Tanzania kati ya Februari 20 na 22 mwaka huu. Iwapo timu ya Tanzania itasonga mbele, katika raundi ya pili itacheza na Misri ikianzia nyumbani kati ya Machi 13 na 15 mwaka huu.
Mgoyi alisema maandalizi ya Tanzania kushiriki kwenye mashindano hayo yameanza ambapo timu ya Tanzania Bara itacheza na Zanzibar ikiwa ni sehemu ya mchakato wa kupata kikosi kimoja kitakachoingia kwenye michuano hiyo ya Afrika.
Benchi za ufundi la timu ya Tanzania litaongozwa na John Mwansasu wakati Msaidizi wake ni Ali Shariff 'Adolf' kutoka Zanzibar, na Meneja wa timu hiyo ni George Lucas. Wote hao walishiriki kwenye kozi ya ukocha wa beach soccer iliyoendeshwa mwaka jana nchini na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).
Kocha Mwansasu atatangaza timu ya Tanzania Bara, Januari 19 mwaka huu, na mazoezi ya pamoja na timu ya Zanzibar yatafanyika Januari 24 na 25 mwaka huu.
Wachezaji wa timu ya Tanzania Bara watatokana na michuano ya beach soccer iliyofanyika mwaka jana ikishirikisha timu za vyuo vya elimu ya juu vya Mkoa wa Dar es Salaam. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Tuesday, January 13, 2015

"WALIOJITOKEZA KUWANIA URAIS CCM HAWANA SIFA" KINGUNGE


Mwanasiasa mkongwe nchini Mzee Kingunge Ngombare Mwiru akizungumza na wanahabari. Picha na Maktaba 

Harakati za kuwania urais ndani ya CCM zimeingia katika hatua mpya baada ya mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale - Mwiru kuibuka na kudai kuwa wote waliojitokeza kuwania nafasi hiyo hawana sifa kwa kuwa wanatumia fedha kutaka kuingia Ikulu.
Kauli ya mwanasiasa huyo ambayo imekuja siku moja kabla ya Kamati Kuu ya CCM kukutana leo mjini Unguja na moja ya ajenda ikitajwa kuwa suala la maadili, inaweza kuwa mwiba mchungu kwa wanasiasa hao ambao wanaongezeka kila kukicha.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Kingunge alisema: “Kuna suala la kukosa uadilifu, kuna suala la matumizi ya pesa na nikwambie ukweli, hao wanaotangaza urais wote wanatumia pesa, wanatumia faulo mbalimbali na wananchi wanajua.” Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

AFRIKA YAJIFUNGULIA MTANDAO WAKE WA AFRILEAKS

Afrileaks utakuwa kamna mtandao wa Wikileaks ambao kazi yake ni kufichua ufisadi 
 
Mtandao mpya mfano ule wa Wiki Leaks , unaolenga kutangaza visa vya ufisadi umezinduliwa barani Afrika. Mtandao huo kwa jina 'Afri Leaks' unanuiwa kutumiwa kulinganisha na kutangaza wazi visa vya ufisadi katika bara nzima.
Kile Afrileaks inaahidi ni mfumo wa hali yajuu wa kama posta mtandaoni ambapo mtu anaweza kuutumia kufichua habari za siri lakini muhimu kwa jamii bila wao wenyewe kujulikana.
Mwenye habari nyeti ataweza kuzipeleka kwa vyombo vya habari kote barani Afrika ambavyo wamejiridhisha navyo kwamba viko huru na wana uhariri wa hali ya juu unaotambulika kimataifa.
Mojawapo ya Maswala yanayowakera wengi ambayo huenda yakapata kuchipuliwa kwa wingi iwapo mfumo huo wa Afrileaks utafana , ni kashfa za ufisadi.
Licha ya kuwa na viwango vya kuridhisha vya ukuaji wa uchumi,Mataifa mengi ya Afrika hata yale yaliyo na utulivu wa kisiasa hupoteza mabillioni ya fedha kila mwaka kutokana na ufisadi uiokithiri, huku taasisi hafifu zikibuniwa bila kuwa na nia ya dhati ya kukabiliana na rushwa. .
Ufisadi ni jinamizi kubwa barani Afrika
Lakini Je Afrileaks wataweza kupata umaarufu kama ule wa wikileaks?
Shirika hilo la Afrileaks linasisitiza kuwa halitachapisha habari zozote za kibanfsi za mfichua siri.
Na kwamba lengo lao ni kuwaunganisha wenye taarifa muhimu na waandishi habari wanaoandika makala zilizopelelezwa na kuchunguzwa kwa kina. Pia wameahidi kutoa mafunzo zaidi kwa waandishi habari waliobobea ili kufahamu vyema vipi kuzishughulikia taarifa kama hizo.
Mashirika kadhaa ya habari barani Afrika tayari yameshajisajili na Afrileaks -ikiwemo kutoka nchini Zimbabwe, Mozambique, Angola na Botswana.
Hivyo wenye habari nyeti ambazo alikuwa anatafuta kwa kuzipeleka bila kutambuliwa anahimizwa kuziwasilisha kwa tovuti hiyo ya Afrileaks lakini wanapaswa kufuata utaratibu uliowekwa na wala wasitumie computer za ofisini mwao ili kutotambulika na kujiweka katika hatari.
Je nani atakuwa wa kwanza kujitosa na habari moto moto katika Afrileaks! Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC Swahili

KAMANDA WA LRA KUFIKISHWA ICC

Muasi Ongwen
Kamanda wa kundi la waasi la LRA nchini Uganda ambaye alijisalimisha katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati, Dominic Ongwen atakabidhiwa kwa mahakama ya kimataifa ya ICC, yasema serikali ya Uganda.
Kamanda huyo ni miongoni mwa watu wa kundi la LRA wanaosakwa na viongozi wa mashitaka katika mahakama ya kimataifa ya ICC kwa kutenda uhalifu dhidi ya binadamu.
Waasi wa Seleka walioko katik Jamhuri ya Afrika ya Kati, ambako Ongwen alikamatwa walisema kuwa muasi huyo alikamtwa ingawa wanajeshi wa Marekani wanasema kuwa alijisalimisha.
Msemaji wa jeshi la Uganda, ameambia shirika la habari la Reuters kwamba Ongwen atakabidhiwa ICC na serikali ya Jamhuri ya Afrika ya Kati ambako alijisalimisha.
Ongwen alikabidhiwa wanajeshi wa Marekani wiki jana na bado anazuiliwa na wanajeshi hao.
Marekani ilikuwa imeahidi kutoa kitita cha dola miliono 5 kama zawadi kwa atakayetoa taarifa zitakazopelekea kukamatwa kwa kamanda huyo, kuhamishwa kwake na hatimaye kufunguliwa mashitaka.
Maafisa wakuu nchini Uganda wanasema kwamba Ongwen atapelekwa nchini Uganda katika siku chache zijazo.
Anajaulikana kwa jina "White Ant", jina lake la msituni na yeye ndiye naibu kamanda wa kundi la LRA Joseph Kony ambaye pia anasakwa na mahakama ya kimataifa ya ICC.
Kundi la LRA liliwateka nyara maelfu ya watoto na kuwalazimisha kupigana huku wasichana wakifanywa watumwa wa ngono. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Thursday, January 08, 2015

NAIBU WAZIRI AZOMEWA MCHANA KWEUPEEE...!!!

 
Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk Makongoro Mahanga akisindikizwa na Polisi kutoka katika Ukumbi wa Arnautoglu Dar es Salaam jana, baada ya mafuasi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi kumzonga alipokwenda kuhudhuria hafla ya kuapishwa wenyeviti wa Serikali za Mtaa wa Halmashauri ya Wilaya ya Ilala.

Wakati utata ukizidi kujitokeza katika uapishaji wa viongozi wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam kutokana na waliodaiwa kushinda kuwekwa kando na kuapishwa walioshindwa, Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk Makongoro Mahanga jana alikumbana na zomeazomea hadi kulazimika kuondoka kwenye Ofisi za Manispaa ya Ilala, Arnatouglou ambako shughuli hiyo ilikuwa ikifanyika.
Dk Mahanga ambaye pia ni Mbunge wa Segerea (CCM), alizomewa akitakiwa kuondoka katika eneo hilo, akidaiwa kwamba angebadilisha matokeo na kuwapa ushindi wagombea wa chama chake.
Eneo hilo lilijaa wafuasi wa Chadema, CUF na CCM huku kila kundi likiwa limesindikiza wenyeviti wake kuapishwa katika shughuli ambayo ilifanyika kwa awamu tatu kwa kila jimbo; Segerea, Ilala na Ukonga kupewa saa mbili.
Waziri Mahanga aliwasili wakati wa zamu ya Segerea saa saba mchana, ndipo kundi la mashabiki wa upinzani lilipoanza kumzomea na kuimba nyimbo za kumkashifu na kutaka atoke katika ukumbi ulioandaliwa kwa ajili ya kuwaapisha wenyeviti. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ESCROW YAWANG'OA WAFANYAKAZI 7 TRA

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba (kulia), akimjulia hali aliyejifungua watoto pacha katika Hospitali ya Mwananyamala, Mwamvita Kilasi wakati waziri huyo alipokwenda hospitalini hapo kutoa misaada mbalimbali katika wodi ya watoto. Waziri huyo alikuwa akisheherekea siku yake ya kuzaliwa.

Sakata la ufisadi wa Sh306 bilioni katika Akaunti ya Tegeta Escrow limewang’oa wafanyakazi saba wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Wafanyakazi hao wamesimamishwa kazi ikiwa ni mwendelezo wa utekelezaji wa maazimio manane ya Bunge kuhusu ripoti ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), kuhusu kashfa hiyo.
Wengine ambao tayari wameshawajibika katika kashfa hiyo ni aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema aliyejiuzulu, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka aliyefukuzwa kazi na Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi aliyesimamishwa kupisha uchunguzi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JANUARI 08, 2015

.
.
. 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

POLISI UFARANSA WATOA PICHA ZA WASHUKIWA

Picha za washukiwa waliotajwa na polisi wa Ufaransa 

Polisi wa Ufaransa wametoa majina na picha ya washukiwa wawili waliohusika na shambulio katika ofisi za jarida la vibonzo nchini humo.
Polisi wamemtaja Said Kouachi na kaka yake Cherif wanaweza kuwa watu hatari na wenye silaha.
Cherif Kouachi aliwahi pia na kuhusika na kupeleka wapiganaji wenye msimamo mkali wa kidini nchini Iraq.
Vyombo vya Habari vya Ufaransa vimesema mtu wa tatu ambaye amegunduliwa pia kama ni mshukiwa Hamyd Mourad mwenye umri wa miaka 18 alijisalimisha polisi baada ya kuona jila lake katika mitandao ya kijamii.
Baadhi ya rafiki zake walisema katika mitandao hiyo kwamba alikuwa shule wakati shambulio hilo katika ofisi za jarida la vibonzo la Charlie Hebdo likitokea, ambako watu 12 waliuawa.
Uchunguzi mkali bado unaendelea kuwasaka watu hao wenye silaha.
Awali jarida hilo lilipandisha hasira kwa waislamu baada ya kuchapisha kibonzo walichodai kuwa ni Mtume Muhamad SAW. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

UN KUSHIRIKIANA NA DRC KUWAONDOA FDLR

Wanamgambo wa FDLR  
 
Umoja wa Mataifa umesema Rais Joseph Kabila ameahidi kuwa jeshi lake litaungana na la UN katika operesheni dhidi ya waasi wa FDLR.
kikosi cha wanajeshi elfu 20 wa umoja huo watashirikiana na wale wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo katika kampeni zilizopangwa kuanza karibuni dhidi ya waasi wa Kihutu wa Rwanda.
Wanamgambo wa Kihutu, wanaojulikana kama FDLR, wamekuwa wakilitumia eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kama kambi yao ya kufanya mnashambulizi dhidi ya serikali ya nchi jirani ya Rwanda.
Waasi hao wameshindwa kufikia muda wa mwisho wa kimataifa uliowekwa wiki hii wa kuweka silaha chini na kuondoka katika eneo hilo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAREKANI KUPAMBANA NA UKIMWI AFRIKA

Baadhi ya dawa za kupunguza makali ya virusu vya ukimwi.  
 
Marekani itatoa madawa ya kupambana na ugonjwa wa ukimwi kwa zaidi ya watoto laki tatu wanaoishi na virusi vya ugonjwa huo.
Nchi hiyo imetangaza kwamba madawa hayo yatatolewa katika nchi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara, barani Afrika, katika kipindi cha miaka miwili ijayo.
Hatua hiyo ni sehemu ya mpango wake wa dola milioni mia mbili zilizoandaliwa kwa ajili ya kupambana na virusi vya ukimwi na ukimwi.
Balozi wa Marekani, Deborah Birth amesema mpango huo utalenga pia kuzuia maambukizo ya virusi vya ukimwi toka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Umoja wa Mataifa umesema asilimia 95 ya watoto walioambukizwa virusi vya ugonjwa wa ukimwi wanaishi katika nchi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

MATOKEO YA KOMBE LA MFALME JANA HISPANIA... REAL MADRID YA RONALDO YAPIGWA 2-0

article-2901036-247E14AF00000578-297_964x390
 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
SpainCopa del Rey January 7
FT Villarreal 1 – 0 Real Sociedad
FT Atletico Madrid 2 – 0 Real Madrid

SIMBA YATINGA NUSU FAINALI YA MAPINDUZI

Vijana wa timu ya Simba yenye makao yake makuu Msimbazi jijini Dar es Salaam  
 
katika michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani Zanzibar, timu ya Simba imetinga hatua ya nusu fainali baada ya kuichakaza Taifa Jang'ombe mabao 4-0 katika mchezo wa robo fainali uliochezwa jana usiku mjini Zanzibar. Michezo mingine ya robo fainali inaendelea leo kwa timu za KCC ya Uganda kumenyana na Polisi Zanzibar, Azam ya Tanzania itakwaruzana na Mtibwa Sugar pia ya Tanzania, huku Yanga ikikamilisha michezo ya hatua hiyo kwa kupambana na JKU ya Zanzibar saa mbili usiku mjini Zanzibar. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

FERNANDO TORRES AREJEA KWA KISHINDO

Fernando Torres  
 
Fernando Torres arejesha ushindi katika klabu yake ya Atletico Madrid kwa kuwabamiza Real Madrid 2-0 katika michuano ya Kombe la Mfalme, Copa del Rey.
Mbele ya umati wa mashabiki 46,800 waliokuwa wakiishuhudia mechi hiyo ya aliyekuwa mchezaji mahiri wa timu za Liverpool na Chelsea, amerejea katika timu yake iliyomkuza na kumtambulisha kipaji chake, Atletico Madrid.
Raul Garcia,aliipatia timu yake bao la kuongoza katika dakika ya 58 akifunga kwa njia ya penalti, huku Jose Maria Gimenez akikamilisha ushindi wa Atletico kwa kufunga bao kwa njia ya kichwa katika dakika ya 76 ya mchezo.
Torres mwenye miaka 30 alibadilishwa katika dakika ya 59. Mchezaji aliyechukuliwa kwa mkopo kutoka katika timu ya Italia ya AC Milan wiki iliyopita, ndiye aliyeongoza kwa ufungaji katika timu ya Atletico kwa misimu mitano kabla hajatia mguu Liverpool mwaka 2007.
Mashabiki wapatao 45,000 waliishuhudia mechi iliyopigwa katika uwanja wa Vicente Calderon mnamo siku ya Jumapili wakati ambapo utambulisho wa Torres ulipofanyika na papo hapo jezi zenye jina lake zikaanza kuuzwa ambapo ndani ya saa 24, ziliuzwa jezi 2,000. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

STEVEN GERRARD AKARIBISHWA LA

Kobe Brayan  
 
Mchezaji maarufu wa mpira wa kikapu nchini Marekani, Kobe Brayant katika kuonyesha umoja michezoni amemtumia ujumbe nahodha wa timu ya Liverpool Steven Gerrard, baada ya uthibitisho kutoka timu ya LA Galaxy kwamba kiungo huyo mkabaji ataungana na timu hiyo mwaka huu.
Katika ujumbe wake wa video kwa Steven, Brayant anamwambia mchezaji huyo wa zamani wa timu ya England kuwa yeye ni shabiki wake wa muda mrefu na kwa hilo Brayant anaamini ushindi mwingine unakuja kwa timu ya Galaxy, na anathibitisha ushindi upo, maana ana imani na Steven Gerrard.
Gerrard atakipiga katika ligi kubwa za vilabu baada ya mkataba wake wa awali na Anfield kumalizika. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Wednesday, January 07, 2015

CCM, CUF WALIANZISHA


 
Utata mpya umeibuka kuhusu matokeo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa baada ya wagombea watatu waliotangazwa washindi kuwekwa kando ikidaiwa kuwa badala yake walioshindwa waliapishwa kuchukua nafasi zao, hali iliyozua vurugu kubwa zilizotulizwa na polisi kwa mabomu ya machozi Ubungo jana.
Kutokana na hali hiyo, wafuasi wa CUF wanaodai wagombea wa chama chao ndiyo walioshinda, waliibuka na kutanda nje ya Hoteli ya Landmark kupinga kuapishwa kwa baadhi ya wenyeviti wa Serikali za Mitaa wa CCM katika Wilaya ya Kinondoni, hatua iliyosababisha baadhi ya wagombea na mashabiki kushushiwa kipigo hadi polisi walipoingilia kati kwa kurusha mabomu ya machozi na risasi za moto kuwatawanya.
Vurugu hizo zilizodumu kuanzia saa tatu hadi saa tano asubuhi, zililenga kuzuia wateule watatu wa mitaa ya Ukwamani, Pakacha na King’ong’o kuapishwa kwa madai kuwa siyo walioshinda.
Kwa upande mwingine, aliyekuwa mgombea wa Mtaa wa Msisiri, Juma Mbena alivamia eneo hilo akidai kuwa Gasper Chambembe (CUF), ambaye alishinda katika mtaa huo hakustahili kuapishwa, kitendo kilichosababisha ashushiwe kipigo na wafuasi wa CUF. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAFUTA YAZIDI KUSHUKA BEI NCHINI




Bei ya mafuta ya petroli, dizeli na ya taa nchini inazidi kushuka kutokana na kuporomoka kwa bei ya mafuta ghafi katika soko la dunia tangu Juni mwaka jana.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), Felix Ngamlagosi alisema jana kuwa bei ya rejareja ya petroli kuanzia leo imeshuka kwa Sh74, dizeli kwa Sh62 na mafuta ya taa kwa Sh54.

Bei hizo zinashuka wakati kukiwa na mjadala mkali kuwa bei zilizopo sasa hazisadifu hali halisi ya kuporomoka kwa mafuta ghafi yanayouzwa kwa Dola 50 za Marekani kwa pipa. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JANUARI 07, 2015

.
.
.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ZIARA YA MH. RIDHWANI KIKWETE JIMBONI KWAKE CHALINZE


 Ridhiwani akihutubia wananchi katika Kitongoji cha Chalinze Mzee wakati wa ziara ya kuwashukuru wananchi na kusikiliza kero zao pamoja na kuwashuru kwa kumchagua, pia alisema atatumia unasheria wake kuwasaidia baadhi ya wakazi wa jimbo hilo wanaonyimwa haki zao za msingi ikiwemo kuporwa ardhi.
 Mkazi wa Chalinze, Bibi akitoa malalamiko yake mbele ya Mbunge Ridhiwani Kikwete ya kudhulumiwa shamba lake na watu wasiojulikana.
 Mkazi wa Chalinze Methodius Kaijage, akiuliza swali kuhusu alama za x zilizowekwa kwenye nyumba zao kwa ajili ya upanuzi wa barabara ambazo alidai ni takribani miaka kumi imepita bila kupewa fidia hivyo kusababisha kukosa maendeleo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

UTATA WAJITOKEZA KIFO CHA MESHACK YEBEI

William Ruto 

hali tata imezidi kujitokeza juu ya kifo cha Meshack Yebei, anayetajwa kuwa shahidi katika kesi inayomkabili Naibu Rais wa Kenya William Ruto.
Shahidi huyo alitarajiwa kutoa ushahidi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu-ICC dhidi ya naibu Rais wa Kenya.
Lakini mwishoni mwa wiki mwili wa Yebei ambao ulionekana kuunguzwa kiasi ,ulikutwa umetupwa kando ya mto huko Eldoret Magharibi mwa nchi hiyo.
Familia ya Yebei wanashuku kwamba chanzo cha mauaji hayo ilikuwa ni kumzuia ndugu yao asiweze kutoa ushahidi wake katika mahakama ya ICC huko The Hague. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SHELL YAKUBALI KULIPA FIDIA NIGERIA

Kampuni ya Shell nchini Nigeria 
 
Kampuni kubwa ya mafuta ya Shell imekubali kulipa dola milioni 80 kama fidia.
Kampuni hiyo ya Uholanzi imewapa fidia wakazi wa jamii ya Bodo katika eneo la Niger Delta walioathiriwa na uvujaji wa mafuta.
Mawakili wa wavuvi 15,600 wa Nigeria wamesema wateja wao watapokea dola za Kimarekani 3,300 kila mmoja kutokana na hasara iliyosababishwa na uvujaji wa mafuta hayo.
"Kiasi kilichobaki cha dola milioni 30 zitatumika kwa ajili ya shughuli za jamii ya Bodo ambayo iliathirika vibaya kutokana na matukio mawili ya kuvuja mafuta mwaka 2008 na 2009".
Mawakili hao wamesema mafuta hayo yaliharibu maelfu ya hekta za mikoko kusini mwa Nigeria.
Fidia hiyo imesemekana kuwa kuwa kubwa kuwahi kuliko zote zilizowahi kulipwa nchini Nigeria, na hivyo kumaliza mvutano wa kisheria uliodumu kwa miaka mitatu. Wanaharakati wanasema kampuni ya Shell ililazimika kukiri kosa hilo mapema zaidi.
Matukio yote mawili ya kuvuja kwa mafuta yametokea katika bomba hilo hilo la Trans Niger Pipeline, linaloendeshwa na kampuni ya Shell, ambalo linachukua mafuta kutoka visima vyake(Shell) kwenda kituo cha mwisho cha kusafirisha mafuta hayo nje kilichopo pwani ya Bonny. Bomba hilo linasafirisha mapipa 180,000 ya mafuta kwa siku. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...