Friday, September 26, 2014

BAWACHA YAPANGA KUMUONA RAIS KIKWETE KWA MAANDAMANO...!!!


Mwenyekiti wa Baraza la wanawake Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha), Halima Mdee akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu mandamano ya kupinga kuendelea kwa vikao vya Bunge la katiba. Kulia ni Makamu Mwenyekiti Bara, Hawa Mwaifunga.

Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) limetangaza maandamano kwenda Ikulu kumuomba Rais Jakaya Kikwete asikubali kutia saini Rasimu ya Katiba inayopendekezwa iwapo itapitishwa na Bunge.

Mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee alisema jana kwamba maandamano hayo yatafanyika mwishoni mwa wiki ijayo, baada ya maandalizi yatakayofanyika kwa siku saba kuanzia jana kukamilika.

Mdee ambaye pia ni mbunge wa Kawe, alisema baraza hilo limeamua kuitisha maandamano hayo ili kuwakilisha kilio cha wanawake ambao ndiyo waathirika wa kwanza pale nchi inapokuwa katika mfumo usio wa haki.

Alivitaka vyombo vya dola hasa polisi kujitokeza kuwasindikiza na kuandamana nao kwa kuwa nao ni miongoni mwa Watanzania ambao wataathiriwa na uamuzi usiolenga kujenga umoja wa kitaifa.

Hata hivyo, Polisi imetahadharisha kuwa itaendelea kuwachukulia hatua za kisheria wanachama wa Chadema watakaojiingiza katika maandamano yaliyopigwa marufuku nchini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA WATISHIWA MAISHA


Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, wakiwa katika vikao vya Bunge hilo Dodoma jana. Picha ya Maktaba

Siku tatu kabla ya Bunge la Katiba kuanza kupigia kura Rasimu ya Katiba inayopendekezwa, watu wasiojulikana wameanza kusambaza vitisho vya kuwatia hofu wajumbe wa Bunge hilo.

Watu hao wamesambaza vipeperushi katika maeneo mbalimbali ya mji wa Dodoma usiku wa kuamkia jana, wakiwataka wajumbe kutoingia bungeni vinginevyo yatakayowapata watajuta, huku wajumbe kutoka Zanzibar wakitishiwa kwa ujumbe wa simu kupitia mtandao wa WhatsApp.

Tayari, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd ametoa kauli kuhusu vitisho hivyo akisema Serikali itachukua kila hatua kuhakikisha wajumbe kutoka visiwani humo ambao wamekuwa wakipokea vitisho wanakuwa salama.

Mbali na kusambazwa kwa karatasi hizo, maandishi mekundu yamechorwa katika kuta za jengo la Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma yakisomeka, “No Katiba. No ufisadi.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ZAIDI YA RAIA 3, 000 WA ULAYA NI WAFUASI WA I.S


Inakisiwa kuwa zaidi ya raia 3000 kutoka Ulaya ni wafuasi wa Islamic State
Idadi ya raiya kutoka Uropa wanaojiunga na kundi la wapiganaji wa Kiislamu nchini Syria na Iraqi imeongezeka hadi zaidi ya 3,000 kulingana na mkuu wa kitengo cha kupambana na ugaidi bara la ulaya.
Gilles de Kerchove ameonya kuwa mashambulizi ya hewa yanayofanywa na nchi za Magharibi yataongezea hatari ya mashambulizi ya kulipiza kisasi katika bara la Ulaya.
Vikosi vikiongozwa na Marekani vimetekeleza mashambulizi ya hewa mia mbili dhidi ya wanamgambo wa Islamic state wa Iraqi tangu Agosti na Jumatatu iliyopita wakaanza kulenga wale walioko Syria.
Bunge la Uingereza litapiga kura kwa mashambulizi ya hewa dhidi ya Iraqi siku ya Ijumaa.
Kundi la IS wameteka sehemu kubwa za Syria na Iraqi katika miezi ya hivi karibuni.
CIA inakisia kuwa kundi la IS linaweza kuwa na wapiganaji mpaka 31,000 huko Iraq na Syria, mara tatu zaidi ya wale waliohofiwa.
Mashambulizi haya yaliotekelezwa siku ya Alhamisi na ndege za Marekani, Saudi na UAE zilikuwa zinalenga mitambo 12 ya kusafisha mafuta nchini Syria .
Msemaji wa Pentagon Rear Admiral John Kirby alisema kuwa kusudi la mashambulizi haya ya hewa halikuwa kuwaua wanamgambo hao lakini ilikuwa kuharibu maeneo ambayo yalikuwa yakiletea kundi hilo fedha kupitia soko nyeusi.
Baadaye, siku ya Ijumaa, wabunge wa Uiungereza wataulizwa kuunga mkono mashabulizi dhidi ya wanamgambo wa IS Iraqi lakini sio Syria. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TALIBAN YATEKA MJI WA GHAZNI AFGHANISTAN


Afisa wa usalama akishika doria katika mji wa Ghazni
Maafisa huko mashariki mwa Afghanistan wanasema kuwa wapiganaji wa Taliban wamechukua udhibiti wa baadhi ya Wilaya katika jimbo la Ghazni.
Watu zaidi ya 70 wanahofiwa kufariki katika Wilaya ya Ajrestan katika mapambano hayo ya kuteka vijiji vyao hapo jana jioni.
Ripoti zinasema Kuna makabiliano makali ya risasi huku walinda usalama wakifanya kila wawezalo kujaribu kutwaa tena wilaya hizo zilizotekwa.
Ghazni ni mji muhimu umnaochukuliwa kama mlango unaounganisha mji mkuu Kabul na eneo la kusini mashariki mwa nchi hiyo.
Wadadisi wa hali ya usalama nchini humo wanasema kuwa kutekwa kwa mji huo ni ilani kwa miji iliyoko karibu na
Ghazni huenda pia zikatekwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

AZAM YAZIPIGA BAO SIMBA NA YANGA


Klabu ya Azam FC ndiyo inayoongoza kwa kulipa posho kubwa wachezaji wake kati ya timu zote 14 zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa wachezaji wa Azam ndiyo vinara wa kupata posho zilizoshiba wakizizidi Yanga na Simba ambao kwa kauli yao wamekubali matokeo.

Mgawanyo huo unaonyesha kwamba Azam kila inaposhinda mechi moja ya ligi inavuna kiasi cha Sh 4milioni, ambapo kila mchezaji anapewa Sh130,000 kiwango ambacho ni kikubwa kwa Simba na Yanga

Kitu kibaya kwa Azam ni pale inapotoa sare au kufungwa, ambapo hakuna chochote watakaochopata ingawa Simba na Yanga huambulia kitu zikitoka sare.

Hata hivyo, kiutaratibu unaonekana utaratibu unaotumiwa na Simba ndiyo mzuri kwani wachezaji wake hupata 40 % ya pato la mlangoni endapo timu hiyo inaibuka na ushindi huku ikiambulia 20% inapopata sare katika michezo yao.

Yanga, ambayo hivi karibuni wachezaji wake waliwasilisha maombi maalumu juu ya kutaka kubadilishiwa viwango vya posho, mpaka sasa wanaambulia kiasi cha Sh70,000 kila mchezaji kwa mechi wanayoshinda na hupata Sh 30,000 wanapopata sare.

“Hatuwezi kushindana na Azam, unajua Azam hata kama haupo katika orodha ya wachezaji wanaocheza mechi, Sh130,000 ipo palepale, lakini Simba na Yanga haipo hivyo, mchezaji anayecheza mechi anapata zaidi ya yule aliyekosa mechi,” alisema mmoja wa mabosi wa Simba ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TFF YAZIKINGIA KIFUA SIMBA NA YANGA


Wachezaji wa kimataifa wa Yanga, Gelinson Santos ‘Jaja’ (kushoto) na Andrey Coutinho. Picha na maktaba.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limezikingia ‘kifua’  Simba na Yanga na kueleza kuwa haliwezi kwa sasa kuzinyang’anya pointi kwa kuchezesha wachezaji wasio na vibali vya kufanya kazi  nchini.

Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwisigwa alisema jana  kuwa suala hilo lipo kisheria zaidi.

“Kama kweli Simba, Yanga wamechezesha wachezaji wasio na vibali vya kufanya kazi nchini ni kosa na Serikali, inaweza kuwachukulia hatua klabu na wachezaji wao,” alisema Mwesigwa.

Hata hivyo, alisema kuwa adhabu ya kunyang’anywa pointi haielezi moja kwa moja na hadi sasa hakuna timu iliyokwenda TFF kulalamikia suala hilo.

“Hatuwezi sisi kuzinyang’anya pointi kama hakuna timu iliyokuja kwetu kulalamika, isitoshe Simba nimezungumza nao leo (jana) baada ya gazeti  kuripoti habari hiyo wakasema tayari wamewaombea vibali wachezaji na kocha wao, hivyo siwezi kujua nani mkweli, Simba na Uhamiaji,” alisema .

Juzi, Idara ya Uhamiaji ilitoa tamko kuhusu baadhi ya wachezaji na makocha wa kigeni wa timu hizo kutokuwa na vibali  vya  kufanya kazi nchini na kueleza kuwa tayari imeanza msako wa kuwakamata watakapoonekana wakijihusisha na mazoezi au mechi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, September 24, 2014

ESTER BULAYA ATANGAZA VITA NA WASIRA...!!!




Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Mkoa  wa Mara, Ester Bulaya akizungumza  katika mahojiano maalumu na waandishi wa gazeti hili, Dar es Salaam jana.

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya ametangaza rasmi nia ya kugombea ubunge katika Jimbo la Bunda ambalo linashikiliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wasira.

Kwa nia hiyo, Bulaya anaweza kuwa ametangaza vita dhidi ya Wasira ambaye hivi karibuni akiwa Bunda, alitangaza kukitetea kiti chake hicho katika Uchaguzi Mkuu 2015.

Julai 8, mwaka huu Wasira akiwa kwenye kikao cha kawaida cha Halmashauri Kuu ya CCM wilayani Bunda, alitangaza kuwa atatetea nafasi hiyo katika Uchaguzi Mkuu ujao, huku akijigamba kuwa yeye ni “mwarobaini wa matatizo” yanayowakabili wakazi wa jimbo hilo.

Kabla ya kutangaza nia hiyo, mara kadhaa Wasira amekuwa akihusishwa na suala la urais na ni mmoja wa makada sita wa CCM ambao walipewa adhabu na chama hicho Februari 18 mwaka huu, baada ya kukutwa na makosa ya kuanza mapema kampeni za urais mwaka 2015.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili jana, Bulaya alisema atagombea ubunge katika Jimbo la Bunda na anamtakia kila heri mpinzani wake huyo (Wasira) katika nafasi ya juu ya urais anayotaka kuwania. Alisema ameamua kufanya hivyo baada ya kuombwa na watu kadhaa kutoka jimboni humo wakiwamo vijana, wazee na kinamama. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BUNGE LA KATIBA KUTUMA OFISA SAUDIA KUSIMAMIA KURA




Mwenyekiti wa Kamati ya Uandishi ya Bunge Maalumu la Katiba, Andrew Chenge akionyesha Rasimu ya Katiba inayopendekezwa kabla ya kumkabidhi Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta kwenye kikao cha Kamati ya Uongozi ya Bunge hilo, mjini Dodoma jana. Rasimu hiyo inatarajiwa kuwasilishwa bungeni leo. 


Ofisi ya Bunge la Katiba itamtuma ofisa wake kwenda Makka, Saudi Arabia kusimamia upigaji kura kupitisha Katiba inayopendekezwa kwa wajumbe wa Bunge hilo wanaokwenda Hijja.

Hayo yalielezwa jana na Katibu wa Bunge hilo, Yahya Khamis Hamad alipotakiwa kueleza idadi kamili ya wajumbe wa Bunge hilo wanaotarajiwa kuwa nje ya nchi na jinsi watakavyopiga kura.

Juzi, Bunge hilo lilizifanyia marekebisho kanuni zake ili kuwaruhusu wajumbe watakaokuwa nje ya Ukumbi wa Bunge wakiwamo wanaokwenda Hijja kuipigia kura Katiba inayopendekezwa, iliyokabidhiwa kwa Kamati ya Uongozi jana.

Chini ya marekebisho hayo, mjumbe aliye nje ya Bunge, ataruhusiwa kupiga kura ya wazi au ya siri kwa njia ya fax au mtandao kama itakavyoelekezwa na katibu kwa kushauriana na mwenyekiti.

Hamad alisema hadi kufikia jana mchana walikuwa wamewatambua wajumbe wanane ambao watakwenda Hijja huko Uarabuni lakini orodha ya watakaokuwa nchi nyingine bado haijajulikana.

Hamadi alisema ofisa wake huyo atasimamia kura za wajumbe wanaokwenda Hijja katika upigaji kura unaotarajiwa kuanza Septemba 29 hadi Oktoba 2 mwaka huu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KINANA, NAPE WAKERWA NA MASHINE ZA EFD NA BVR




Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimiana na wazee wa Kijiji cha Kwenjugo, Handeni jana, akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Tanga.

Chama Cha Mapinduzi kimeonyesha wasiwasi kuhusu matumizi ya teknolojia ya kielektroniki katika uandikishaji wa wapigakura na mashine za ukusanyaji wa kodi (EFD).

Wasiwasi huo umeelezewa kwa nyakati tofauti na Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakati wakihutubia mkutano wa hadhara katika Mji Mdogo wa Chalinze, wilayani Bagamoyo juzi.

Kinana alihoji utaratibu aliouita mbovu katika matumizi ya mashine za kielektroniki za kutunza hesabu za wafanyabiashara (EFD) na Nnauye alieleza wasiwasi wake kuhusu uamuzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kutumia teknolojia ya Biometric Voter Registration (BVR) katika kuandikisha upya wapigakura.

Nnauye aliishauri Nec kuangalia upya uamuzi wake huo akisema hauna mantiki kwa kuwa utaliingizia Taifa gharama ambazo zinaweza kuepukwa kwa urahisi.

Teknolojia hiyo iliwahi kulalamikiwa bungeni na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe katika hotuba yake ya bajeti mwaka jana, akisema NEC imeanzisha utaratibu huo bila kuwashirikisha wadau.

Akitoa mifano, Nnauye alisema matumizi ya teknolojia hiyo yalizua mtafaruku katika chaguzi za nchi za Kenya, Malawi na Ghana na haitakuwa busara Tanzania nayo kujiingiza kwenye matatizo kama hayo wakati ina uwezo wa kuyaepuka. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 24, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MMILIKI WA ALIBABA ATARAJIRIKA ZAIDI

Mwanzilishi wa Alibaba ndiye tajiri zaidi nchini Uchina 

Mwanzilishi wa mtandao wa Alibaba ndiye tajiri mkubwa zaidi nchini Uchina kulingana na rekodi za kampuni yake.
Hili imethibitishwa na ripoti rasmi ya kifedha ya Hurun.
Bw.Ma ameongoza orodha ya watu tajiri zaidi nchini Uchina kwa mali ya takriban dola bilioni 25 akifuatwa na mwenyekiti wa Wanda Group Wang Jianlin.
Matajiri watano katika ya kumi walio katika orodha hiyo, wanamiliki kampuni za mitandaoni huku wakiwabwaga wale wanaomiliki mali isiyohamishika ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiongoza orodha hiyo.

Orodha hiyo inahusisha pia kiongozi wa Tencent Pony Ma.
Mabwenyenye wengine walio katika orodha hiyo ni mwanzilishi mwenza wa mtandao wa intanet marufu sana nchini China Baidu, Robin Li na pia mwanzilishi wa soko la mtandao la JD.com, Richard Liu Qiangdong.
Bw Liu ambaye kampuni yake ilihusika katika ubadilishanaji wa hisa huko New York hapo Agosti mwaka huu, aliorodheshwa katika nafasi ya kumi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

JESHI LABADILI KAULI KUHUSU WANAFUNZI WALIOTEKWA

Wazazi wa wanafunzi waliotekwa nyara na Boko Haram nchini Nigeria wakiishi kwa kilio 

Jeshi la Nigeria limekanusha taarifa ya awali kuwa baadhi ya wanafunzi wa shule waliotekwa nyara kutoka Chibok na wapiganaji wa Boko Haram, wameachiliwa.
Msemaji wa jeshi nchini Nigeria, Meja Generali Chris Olukolade, ameambia BBC kuwa wanawahifadhi wasichana kadhaa lakini akakana kuwa wasichana hao ni baadhi ya wale waliotekwa nyara na wapiganaji wa Boko Haram kutoka Chibok.
Zaidi ya wasichana 200 walitekwa nyara na Boko Haram kutoka shule ya mabweni Kaskazini Mashariki mwa jimbo la Borno.
Utekaji nyara huo ulisababisha ghadhabu kote nchini Nigeria na duniani kote kiasi cha kusababisha kampeini ya kutaka kuokolewa kwa wasichana hao kwenye mitandao ya kijamii. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MHUBIRI ABU QATADA AACHIWA HURU

Abnu Qatada alikabiliwa na tuhuma za kupanga njama ya mashambulizi ya kigaidi nchini Jordan
Mhubiri muisilamu mwenye utata ambaye alihamishwa kutoka Uingereza mwaka 2013, Abu Qatada, ameachiliwa huru nchini Jordan baada ya mahakama kutompata na hatia.
Alikuwa ametuhumiwa na kosa la kuhusika katika njama ya kupanga mashambulizi ya kigaidi ambayo ilitibuliwa mwaka 2000.
Jopo la majaji waliokuwa katika mahakama hiyo, hawakumpata na hatia yoyote bwana Qatada kutokana na madai kuwa alihusika na njama hiyo ya ugaidi.
Uamuzi huo umetolewa baada ya Abu Qatada kutopatikana na hatia mwezi Juni katika kosa lengine la kupanga njama ya mashambulizi mwaka 1998 nchini Jordan.
Abu Qatada alitimuliwa kutoka Uingereza mwezi Julai mwaka 2013 kwa madai ya kueneza itikadi kali Uingereza ikitaka afunguliwe mashitaka nchini Jordan. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

JAJA AFUTA KESI YA OKWI FIFA

 

Mhaiti huyo alisema katika timu mbalimbali alizowahi kucheza, amekutana na Wabrazili kadhaa walioonekana kuwa moto wakati wa maandalizi ya ligi, lakini walipotea baada ya mechi tatu hadi nne ligi husika zilipoanza.


Kiwango cha juu kilichoonyeshwa na mshambuliaji Genilson Santos ‘Jaja’ kimefanya uongozi wa Yanga, kutupilia mbali wazo la kumshitaki Emmanuel Okwi kwa Shirikisho la Soka la Kimataifa( Fifa).

Tangu aliposajiliwa na Yanga, Jaja ameonyesha kiwango cha juu cha ufungaji mabao akiwa amefunga mabao manne katika mechi sita alizocheza hadi sasa katika michuano mbalimbali.

Jaja aliwasahaulisha Wanayanga kabisa habari za Okwi wakati alipofunga mabao mawili ya ufundi wa hali ya juu katika mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Azam walioshinda 3-0.

Kwa mujibu wa taarifa ilizolifikia gazeti hili, zinasema kikao kilichofanyika wiki iliyopita kati ya wanasheria na baadhi ya wanachama wa Yanga wamemshauri mwenyekiti wao Yusuf Manji kuachana na jambo hilo kwa sasa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...