Tuesday, November 11, 2014

MADEREVA WA KAMPUNI YA MWANANCHI (MCL) WAKAMATWA NA MIRUNGI

  Polisi mkoani Iringa wanawashikilia watu watatu wakiwamo madereva wawili wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi alisema tukio hilo lilitokea jana saa 11 alfajiri katika kituo cha ukaguzi cha Igumbilo mkoani hapa nabaada ya ukaguzi polisi walibaini magunia mawili ya mirungi ndani ya gari la kusafirishia magazeti ya kampuni hiyo.
Mungi alisema mirungi hiyo ilipakiwakatika eneo la Chalinze mkoani Pwani na taarifa za awali zinaeleza kuwa ilikuwa ikisafirishwa kwenda Zambia. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
“Taarifa zinaonyesha kuwa gari hilo liliondoka Dar es Salaam jana saa 5:00 usiku likiwa limepakia magazeti ya Mwananchi,The Citizen na Mwanaspoti, yote yakiwa yanachapishwa na Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd, na ilipofika eneo la Chalinze mkoani Pwani watuhumiwa walipakia magunia hayo ya mirungi.
“Ndani ya gunia hizo kulikuwa na mabunda 302 yenye uzito wa kilo 121 ambayo gharama zake kwa sasa hazijajulikana kwa kuwa bidhaa hiyo ilikuwa inakwenda kuuzwa nje na sisi hatujajua soko lake huko likoje,”alisema.
Mungi aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Ayubu Gwabugano (33), mkazi wa Forest jijini Mbeya,  Mohamed Rwamo (27), mkazi wa Kiluvya, Dar es  Salaam ambaye alikuwa anaendesha gari hilo na mwenzake Adamu Komba (33 ),mkazi wa Mabibo, Dar es Salaam.
Kamanda Mungi alisema usafirishaji wa mirungi kupitia Mkoa wa Iringa umeongezeka kulinganisha na mwaka jana.
Alisemakuwa katika kipindi cha Januari hadi Novemba mwaka huu jeshi hilo limekwishakamata kilo 201 za mirungi wakati katika kipindi kama hicho mwaka jana walikamata kilo 75 pekee.
Akizungumzia tukio hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa MCL, Francis Nanai alisema, “Jambo hili limetushtua na kutusikitisha sana, mimi binafsi na wafanyakazi wenzangu wa MCL. Tukio hili limefanywa na madreva wetu wakijua wazi kwamba (1) sheria ya kampuni inazuia magari ya magazeti kubeba abiria wa aina yoyote (2) hairuhusiwi kubeba mzigo wa aina yoyote isipokuwa magazeti ya MCL pekee. Na katika hili MCL haihusiki kwa hali yoyote ile kwani hatujawahi, hatufanyi na hatuna mpango wa kujihusisha katika biashara yoyote haramu.
Kwa vile kosa ni la jinai, basi sheria itachukua mkondo wake na tunaomba vyombo vya usalama vichukue hatua kali kabisa kwa wote waliohusika. Sisi MCL tutashirikiana na yeyote mwenye mapenzi mema katika juhudi za kukomesha biashara haramu ya aina yoyote hapa nchini.
Ninanchukua fursa hii kuwapa pole wasomaji wetu kwa usumbufu walioupata kutokana na tukio hili la kufedhehesha na ninawahakikishia kwamba jambo hili halivumiliki hapa MCL na hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya wahusika.” Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...