Tuesday, November 11, 2014

USALAMA MDOGO, BENI DRC

Kikosi cha UN, DRC kinashutumiwa kwa kutolinda usalama vya kutosha
Baada ya miezi kadhaa ya utulivu katika eneo la mashariki mwa DRC, ghasia zimerejea tena.
Zaidi ya watu 120 wakiwemo wanawake na watoto waliuawa kwa mapanga na mashoka mwezi uliopita katika eneo la mpakani na Uganda.
Inadhaniwa kuwa kundi la waasi kutoka nchini Uganda la ADF ndilo linalohusika na mashambulizi hayo.
Vikosi cha Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo MONUSCO kimekuwa kikilalamikiwa katika mji huo wa Beni kwa kushindwa kuzuia mauaji, licha mamia ya wanajeshi wake kuweka kambi katika eneo hilo.
Lakini hata hivyo wenyewe wanasema ni vigumu kuweza wakuwalinda raia wote, licha ya kuchukua hatua kadhaa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...