Sunday, December 28, 2014

WANAWAKE WANAOCHELEWA KUBEBA UJAUZITO WAONYWA

Dk Ali Mzige
 Dk. Ali Mzige

WANAWAKE wanaochelewa kubeba ujauzito, wameonywa kuwa kuchelewa huko kunawaweka hatarini kuja kupata watoto wenye mtindio wa ubongo.
Mbali na hilo, pia wanaume wanaotafuta watoto wakiwa katika umri mkubwa wa zaidi ya miaka 60, nao wametajwa kuwa hatarini kupata watoto wa aina hiyo na wakiepuka hilo, watakosa uwezo mzuri wa akili darasani.
Taarifa ya daktari mkongwe nchini, Dk Ali Mzige aliyotoa wiki hii, amebainisha kuwa hali ya umri mkubwa wa wazazi wa kike na kiume, ndio chanzo kikubwa cha kuzaliwa kwa watoto wa aina hiyo, na siyo uchawi wala mazingaombwe.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

DK. SLAA AZIDI KUMBANA KIKWETE ACHUKUE HATUA DHIDI YA PROF. MUHONGO

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa amesema Rais Jakaya Kikwete asitumie kivuli cha mapumziko ya sikukuu kuchukua uamuzi dhidi ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo anayehusika katika kashfa ya fedha za Akaunti ya Tegeta Escrow ya Sh306 bilioni.
Pia, amemtaka Rais Kikwete kuwaeleza ukweli Watanzania kuhusu kigogo wa Ikulu aliyenufaika na mgawo wa fedha, Sh800 milioni za akaunti hiyo zilivyotumika na mnufaikaji alikuwa nani.
Dk Slaa aliyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru wananchi wa Somangila-Kigamboni Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam kwa kuwachagua wenyeviti sita kati ya 13 wa Ukawa wa kata hiyo yenye mitaa sita.
“Tunamtaka haraka Rais Kikwete amfukuze kazi Profesa Muhongo, asiseme anakula ‘bata’ Msoga (Kijijini kwake Bagamoyo mkoani Pwani) eti sikukuu...Tumemchagua atusimamie na kutuongoza kwa saa 24 kwenda kula Krismasi huku wagonjwa wanakufa hospitalini ni dharau kwa Watanzania,” alidai.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

UGONJWA WA TB HATARI WINGIA NCHINI


 
Moja ya Chumba cha maabara kwa ajili ya vipimo na utafiti wa ugonjwa wa Kifua Kikuu katika Hospitali ya Taifa ya Kifua Kikuu Kibong'oto.

Wakati Taifa likikabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa dawa hospitalini, aina mpya na hatari zaidi ya ugonjwa wa kifua kikuu sugu imegundulika na kuathiri mtu mmoja nchini.
Mgonjwa huyo alibainika kuwa na kifua kikuu sugu kisicho na tiba, aina ya ‘Xtreme Drug Resistant’ au XDR-TB ambayo hapo awali haikuwa ikiwaathiri Watanzania.
Huyu ni mgonjwa wa pili kubainika kuwa na aina hii hatari ya TB baada ya kesi ya kwanza kuripotiwa mwaka 2011.
Shirika la Afya Duniani (WHO) linaeleza kuwa XDR-TB ni nadra sana ambapo ni nchi 77 tu duniani ikiwamo Tanzania zimeripoti tatizo moja moja, mwishoni mwa mwaka 2011.
Taarifa zilizokusanywa na WHO kutoka katika mataifa mbalimbali duniani zinahakiki kuwa kuna asilimia tisa tu ya kesi za XDR-TB. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI DESEMBA 28, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MWENYEKITI WA CHADEMA AREJESHWA KWAO RWANDA


MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wilayani Mbogwe mkoani Geita Omari Atanas, amekamatwa na maofisa Uhamiaji wilayani hapa kurudishwa kwao nchini Rwanda baada ya kubainika sio raia wa Tanzania.
Akizungumzia tukio hilo, Kaimu Mkuu wa wilaya hiyo, Aman Mwenegoha, alisema Mwenyekiti huyo alikamatwa Desemba 22, mwaka huu na maofisa Uhamiaji na kuhojiwa kwa muda na kugundulika sio raia wa Tanzania bali ni raia wa Rwanda.
Mwenegoha alisema , awali tetesi za uraia wa Atanas, zilianza wakati wa kampeni za Uchaguzi wa Serikali wa Mitaa uliofanyika hivi karibuni nchini, baada ya Mwenyekiti huyo kufika kijiji cha Luganga. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

RUSHWA, NGONO TATIZO MISS TANZANIA


“Kwa sasa hana uamuzi wowote mpaka pale atakapokuwa amepewa barua rasmi.” Lundenga 

Serikali imesema imeyafungia mashindano ya Miss Tanzania baada ya waandaaji kukiuka taratibu na kanuni huku pia yakitajwa kukithiri kwa rushwa ya ngono na upendeleo.
Mashindano hayo yalifunguliwa mwaka 1994, yamefungiwa kwa miaka miwili baada ya kuwapo kwa malalamiko kutoka kwa wananchi na washiriki.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Bazara la Sanaa Tanzania (Basata), Godfrey Mngereza alisema jana kuwa Kamati ya Miss Tanzania kupitia kampuni yake ya Lino Agency, imekiuka kanuni na taratibu zinazoongoza mashindano hayo.
“Ni kweli kwamba tumeifungia Miss Tanzania kwa miaka miwili, lakini haya si maazimio ya tathmini iliyofanyika mapema mwezi huu, bali kulikuwa na vikao mbalimbali vilivyofanyika na si kimoja, ni uamuzi mgumu ambao umekuja kutokana na sababu maalumu,” alisema Mngereza.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

YANGA, AZAM MWISHO WA UBISHI LEO

Sehemu ya uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambako kutafanyika mchezo kati ya Azam na Yanga
Sehemu ya uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam

YANGA leo itakuwa mwenyeji wa Azam FC katika mechi ya raundi ya nane ya Ligi Kuu bara itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Timu zote zinashuka dimbani zikiwa na pointi 13 kila moja zikitofautiana kwa uwiano wa mabao.
Mechi ya leo ni ya pili kukutana kwa timu hizo msimu huu, baada ya ile ya Ngao ya Jamii iliyofanyika mapema Septemba na Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 yaliyofungwa na aliyekuwa mchezaji wao Geilson Santos ‘Jaja’ na Simon Msuva.
Katika historia ya kukutana kwao kwenye mechi ya Ngao ya Jamii, Yanga wanaonekana kuwazidi Azam baada ya msimu wa mwaka 2012/2013 kuwafunga bao 1-0. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

FIFA YAMPA BEJI MWAMUZI WA SIMBA NA YANGA

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara akijiandaa kuusaini mpira ulioshikiliwa na mwamuzi wa mchezo huo, Jonesia Rukyaa (kulia)

MWAMUZI aliyechezesha mechi ya Nani Mtani Jembe2
Jonesia Rukyaa ni miongoni mwa waamuzi wa kike sita waliopata beji ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).

Jonesia alimudu vyema kuchezesha mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Taifa Desemba 13, mwaka huu na Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Yanga.
Wengine waliopata beji hiyo ni Florentina Zablon wa Dodoma na Sophia Ismail wa Mara (Waamuzi wa kati) na Hellen Mduma wa Dar es Salaam, Kudra Omary wa Tanga, Grace Wamala kutoka Kagera na Dalila Jaffary wa Zanzibar (Waamuzi Wasaidizi).
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

KIONGOZI WA AL-SHABAAB AKAMATWA

 Kundi la wapiganaji wa Al shabaab
 
Maafisa nchini Somali wanasema kuwa kiongozi mkuu wa kundi la wapiganaji wa Alshabaab amekamatwa karibu na mji mmoja karibu na mpaka wa Kenya na Somali.
Kamishna wa Wilaya ya El Wak mjini Gedo ameiambia BBC Somalia kwamba vikosi vya usalama vilimkamata Zakariya Ismail Ahmed Hersi katika maficho yake ndani ya nyumba moja baada ya kupashwa habari.
Mwaka 2012 Marekani ilitoa zawadi ya dola millioni 3 kwa yeyote yule ambaye angeweza kutoa habari za Hersi. Kundi la Al Shabaab limejiondoa kutoka miji kadhaa nchini Somalia tangu uzinduzi wa mashambulizi makali dhidi ya kundi hilo yanayotekelezwa na vikosi vya AMISOM vikishirikiana na wanajeshi wa serikali ya Somalia.
Bwana Hersi alikuwa kiongozi wa kundi la Alshabaab upande wa Amniyat. Mapema mwaka huu alikosana na kiongozi wa kundi hilo Ahmed Abdi Godane ambaye aliuawa katika mashambulizi ya Marekani mnamo mwezi Septemba.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC 

WANAUME WALIOOANA WAPUNGUZIWA HUKUMU

 Wanaume waliooana Misri wapunguziwa hukumu jela
 
Mahakama moja ya Misri imepunguza hukumu ya watu wanane waliodaiwa kushiriki katika ndoa ya watu wa jinsia moja kutoka miaka mitatu hadi mwaka mmoja.
Mwezi Uliopita ,wanane hao walipatikana na hatia ya kuchochea uasherati.
Walishtakiwa baada ya kanda moja ya video kusambaa katika mitandao ikiwaonyesha wakisherehekea katika boti moja lililokuwa mto Nile huku wanaume wawili wakionekana wakivalishana pete na kukumbatiana.
Watu hao baadaye walikataa kwamba ilikuwa harusi ya watu wa jinsia moja. Ushoga ni kinyume na utamaduni wa Misri ,ijapokuwa si kinyume na sheria. Wanaharakati wa kupigania haki za kibinaadamu wanasema kuwa kampeni dhidi ya mashoga imeimarishwa katika kipindi cha miezi ya hivi karibuni nchini Misri. 
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Friday, December 26, 2014

MAASKOFU WATAKA JK AENDELEZE FAGIO LAKE

Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Zanzibar, Michael Hafidh (kulia) akifurahi jambo na Fred Msongole aliyebeba mtoto wake, Jonathan Msongole (miezi 8) baada ya kukamilisha ibada ya Sikukuu ya Krismasi iliyofanyika kitaifa katika Kanisa la Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) Chuo Kikuu cha Dar es Salaam jana. (Picha na Fadhili Akida).
Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Zanzibar, Michael Hafidh (kulia) akifurahia jambo na Fred Msongole.

MAASKOFU wa madhehebu mbalimbali ya Kikristo nchini, wamepongeza uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete kuwajibisha watendaji wake, huku wakimtaka asiishie kuchukua hatua kwa waliotajwa kuhusika na sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow pekee, bali pia wazembe na wote wanaokutwa na tuhuma mbalimbali katika utawala wake.
Aidha, wamesisitiza kamwe asicheke nao, kwani kitendo cha kuwavumilia kinaweza kugeuka shubiri katika utawala wake kwa kuwa watamharibia kazi. Walisema hayo kwa nyakati tofauti katika salamu zao za maadhimisho ya Sikukuu ya Krismasi, jana.
Weka pembeni Akiongoza mahubiri katika Ibada Kuu ya Krismasi katika Kanisa la Champlesy la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Askofu Michael Hafidh wa Zanzibar, alishauri Rais Kikwete aendeleze utaratibu wa kuwawajibisha viongozi wazembe na wasio waadilifu katika kazi zao.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MABASI 21 YAADHIBIWA KWA NAULI JUU KRISMASI

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamedi Mpinga (kulia) akizungumza na waandishi Dar es Salaam juzi kuhusu kupanda kwa nauli ya mabasi yaendayo mikoani, daladala zinazoishia Mnazi Mmoja, ajali za barabarani na mambo mbalimbali yanayohusu usalama wa abiria. Wengine kutoka kushoto ni Mkurugenzi Chama cha Kutetea Abiria Tanzania (CHAKUA) Kanda ya Mashariki, Thomas Haule na Mwenyekiti CHAKUA,Hassan Mchanjama. (Picha na Yusuf Badi).
Kamanda wa kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamedi Mpinga (kulia) akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam.
 
JESHI la Polisi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), limewaadhibu wamiliki wa magari zaidi ya 21.
Mawakala wao wa kukata tiketi, wamesombwa na kuburuzwa mahakamani, ambao baada ya kesi zao kusogeswa mbele, sasa wanasota mahabusu, watakakokuwa hadi baada ya shamrashamra za kuukaribisha Mwaka mpya 2015.
Wakati mabasi mengi yakinaswa Morogoro, mawakala wa tiketi ambao pia ni maarufu kama wapigadebe, wamekamatwa katika kikuo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo, Dar es Salaam.
Hayo yamethibitishwa na Ofisa Mfawidhi wa Sumatra Mkoawa Morogoro, Allen Mwanri aliyesema mabasi zaidi ya 21 yalikamatwa kwa makosa ya mbalimbali, likiwemo kubwa la kuzidisha nauli na kutoza nauli kubwa.
Hata hivyo, alisema kila mmiliki wa basi lililokamatwa kwa kuzidisha nauli na nauli kubwa, alitozwa adhabu ya kiasi cha Sh 250,000. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MALASUSA: UFISADI NI ZAO LA KUTOKUWA NA HOFU YA MUNGU




Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Alex Malasusa akihubiri katika ibada ya Krisimasi ya kuadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo katika Kanisa la Azania Front jijini Dar es Salaam 
 

Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Alex Malasusa amesema watanzania wengi hivi sasa wamekosa kitu muhimu na cha thamani katika maisha yao, ambacho ni kutokuwa na hofu ya Mungu.

Amesema kufuatia hali hiyo Tanzania imejikuta ikiingia kwenye vitendo vya rushwa na ufisadi, huku viongozi waliopewa dhamana na wananchi wakiweka mbele maslahi yao binafsi badala ya Taifa.

Askofu Malasusa ameyasema haya leo katika Kanisa la Azania Front jijini Dar es Salaam wakati akitoa salamu na akihubiri katika ibada ya Krisimasi ya kuadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA DESEMBA 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


DSC07606
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

KIJANA AKAMATWA KWA KUMTUKANA RAIS

Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki 
 
Polisi nchini Uturuki wamemkamata mwanafunzi wa sekondari mwenye umri wa miaka kumi na sita kwa tuhuma za kumtukana Rais Recep Tayyip Erdogan.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo, kijana huyo alipelekwa mahabusu baada ya kumtuhumu Bwana Erdogan na chama chake tawala cha AK kwa vitendo vya rushwa wakati wa mkutano wa hadhara katikati ya mji wa Anatolia.
Waziri Mkuu Ahmet Davutoglu ametetea kukamatwa kwa mwanafunzi huyo akisema ofisi ya rais lazima iheshimiwe.
Kumtukana mkuu wa nchi ni makosa kwa mujibu wa sheria za Uturuki na mwanafunzi huyo anakabiliwa na kifungo cha miaka minne jela endapo atapatikana na kosa. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC

INDONESIA WAKUMBUKA TSUNAMI

Wanawake eneo la Aceh wakifanya sala ya kukumbuka maafa makubwa yaliyosababishwa na tsunami miaka kumi iliyopita nchini Indonesia 
 
Wananchi wa Indonesia wameanza kuadhimisha mwaka wa kumi tangu kutokea kwa tetemeko la ardhi lililosababisha mawimbi makubwa katika bahari ya Hindi, tsunami na kusababisha vifo vya watu zaidi ya watu laki mbili na elfu ishirini katika eneo kubwa.
Umati wa watu umekusanyika karibu na jengo la makumbusho la tsunami katika eneo la Banda Aceh katika kisiwa cha Sumatra.
Mji huo ulisambaratishwa kabisa na tetemeko kubwa la ardhi na mawimbi ya tsunami. Makamu wa Rais wa Indonesia(Jusuf Kalla) anaongoza maadhimisho hayo na atawashukuru wafanyakazi wa kujitolea katika eneo hilo na duniani kote kwa kulisaidia eneo la Aceh kurejea katika hali ya kawaida baada ya mkasa huo. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

ASKARI WATATU WA AU WAUAWA SOMALIA

Askari wa Somalia wakiangalia mabaki ya magari katika moja ya mashambulio ya kigaidi mjini Mogadishu, Somalia. 
 
Jeshi la kulinda amani la Umoja wa Afrika nchini Somalia limesema askari wake watatu na kandarasi raia wameuawa katika shambulio lililofanyika katika makao yake makuu mjini Mogadishu.
Taarifa ya Umoja wa Afrika imesema wapiganaji wa al-Shabab waliingia katika kambi wakivalia sare kama askari wa jeshi la serikali ya Somalia.
Taarifa hiyo imesema washambuliaji watano waliuawa na wengine kadha kukamatwa. Pamoja na kutoa eneo hilo kuwa makao makuu ya majeshi ya kulinda amani ya AU nchini Somalia, eneo hilo lililoimarishwa pia makao ya balozi za Uingereza na Italia. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC

LIGI KUU TANZANIA BARA KUANZA LEO

 Kikosi cha timu ya Azam ya Ligi Kuu ya Vodacom, Tanzania 
  
Ligi kuu ya Tanzania bara, maarufu kama Ligi Kuu ya Vodacom inaanza rasmi mzunguko wa pili leo, Ijumaa baada ya kusitishwa tangu Novemba 7, 2014.
Hadi ligi hiyo ilipositisha mzunguko wa kwanza, tayari timu 14 zinazoshiriki ligi hiyo zilikuwa zimecheza michezo saba kila moja.

Timu ya Simba ya ligi kuu ya Vodacom
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Shirikisho la Kandanda nchini Tanzania, TFF, Simba ambayo ni miongoni mwa timu kongwe za ligi hiyo na ambayo katika mzunguko wa kwanza haikuwa na matokeo mazuri baada ya kwenda sare mara sita na kushinda mchezo mmoja na kujikusanyia pointi tisa ikishika nafasi ya saba katika msimamo wa ligi hiyo, leo inaikaribisha Kagera Sugar inayoshikilia nafasi ya tano katika pambano litakalofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Michezo mingine itafanyika katika viwanja mbalimbali kuanzia Ijumaa, Jumamosi na Jumapili wiki hii.

Wachezaji wa timu ya Yanga
Mpaka sasa Mtibwa Sugar ndiyo inayoongoza ligi hiyo ya Vodacom baada ya kujikusanyia pointi 15, ikifuatiwa na Young Africans(Yanga) kwa kuwa na pointi 13 sawa na Azam mabingwa watetezi. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

WENGER AMUWINDA BEKI WA REAL MADRID

Sergio Ramos wa Real Madrid.Kocha wa Arsenal adaiwa kummezea mate 
 
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amewasiliana na ajenti wa beki wa Real Madrid Sergio Ramos kuhusu uwezekano wa mchezaji huyo kujiunga na kilabu hiyo ya uwanja wa Emirates.
Ramos mwenye umri wa miaka 28 amekuwa na kilabu hiyo ya Los Blancos kwa takriban muongo mmoja baada ya kuwasili kutoka sevilla kwa kitita cha pauni millioni 20 mwaka 2005.
Hatahivyo ripoti za hivi majuzi zimedai kwamba Ramos huenda akaondoka katika kilabu hiyo ya Santiago Bernabeu baada ya mazungumzo ya kandarasi yake mpya kugonga mwamba.
Na kulingana na mwandishi Esteban Manolete wa AS ,mkufunzi huyo wa The Gunners amewasiliana na wawakilishi wa Ramos ili kuona iwapo anaweza kumvuta mchezaji huyo katika eneo la London kazkazini.
''Wenger amewasiliana na Rene Ramos ajenti na ndugu ya Sergio Ramos'',mwandishi huyo alikimbia kipindi cha La Goleada.
Wenger juma hili alikiri kwamba safu ya ulinzi ya Arsenal haina uongozi baada ya kufungwa bao la dakika za mwisho na liverpool na hivyobasi kupata sare ya 2-2. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Thursday, December 25, 2014

JAMBO TZ BLOG INAWATAKIA WATU WOTE KHERI YA CHRISTMAS

 Heri ya X-mass kwa wadau wote wa blog hii. Tafadhari usisahau ku-like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

UKAWA WATAKA KICHWA CHA MUHONGO...!!!

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo. 

Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umelitaka Bunge kuiwajibisha Serikali ikiwa Rais Jakaya Kikwete atashindwa kutekeleza maazimio ya Bunge ikiwamo kumng’oa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Wakizungumza hapa jana, viongozi hao walisema endapo Rais atashindwa kumwajibisha Profesa Muhongo, basi wabunge wao watawasilisha hoja na kushawishi wengine kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu na umoja huo utaitisha maandamano nchi nzima.
Mwenyekiti mwenza wa umoja huo, Profesa Ibrahim Lipumba alihoji kwa nini Rais Kikwete anasita kumwondoa Profesa Muhongo wakati Bunge lilishatoa maazimio.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

UKAWA WATAKA SHERIA YA MAADILI INAYODHIBITI MAOVU

Viongozi wa Ukawa.

Viongozi wa UKAWA

VYAMA vya siasa vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), vimetaka sheria ya maadili itungwe upya ili kuweka uwazi wa watu wote kuona taarifa ya mali za viongozi.

Vyama hivyo vinaamini hatua hiyo, itasaidia wananchi wote kujua mali halisi za viongozi na pia itasaidia kupunguza ufisadi, kutokana na wananchi kutambua ukweli wa mali za viongozi wao.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa umoja huo, Profesa Ibrahim Lipumba wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu hatua zinazostahili kuchukuliwa, kutokana na suala la uchotwaji wa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

VIJIJI 45 KUPATA UMEME MARA

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesema vijiji 45 mkoani Mara vinatarajiwa kuunganishiwa na huduma ya umeme kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Alisema hayo katika ziara yake ya siku sita katika mkoa wa Mara, lengo likiwa ni kukagua na kuzindua miradi ya umeme vijijini inayosimamiwa na REA awamu ya pili kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Nchini (Tanesco).
Alisema ziara yake iliyohusisha wilaya za Musoma, Tarime, Rorya, Bunda na Serengeti, ililenga kubaini na kukagua mahitaji ya umeme katika wilaya hizo ili vijiji vilivyokosa umeme kwenye awamu ya pili, viingizwe katika awamu nyingine ya umeme vijijini. 
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

CHENGE, NGELEJA KUADHIBIWA NDANI YA SIKU 21 ZIJAZO

Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti bungeni, Andrew Chenge


Wenyeviti watatu wa Kamati za Bunge waliopendekezwa kuwajibishwa na Bunge hilo katika sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow wataondolewa katika nyadhifa zao ndani ya siku 21 zijazo, imeelezwa.

Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema jana kuwa utekelezaji wa maazimio ya Bunge kwa upande wa mhimili huo wa dola utafanyiwa kazi mapema mwakani.

“Hilo litatekelezwa wakati wa Kamati za Bunge ambazo zitaanza mwishoni mwa wiki ya pili ya Januari mwakani kwa kamati husika kuchagua wenyeviti wapya.”

Wenyeviti hao ni wa Kamati ya Nishati na Madini, Victor Mwambalaswa, William Ngeleja wa Katiba, Sheria na Utawala na Andrew Chenge wa Kamati ya Bajeti. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS DESEMBA 25, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC07568
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

KESI YA MH. NASSARI YAAHIRISHWA

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari  

Kesi ya kuchoma moto bendera ya CCM inayomkabili Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari jana iliahirishwa na Ofisa Mtendaji wa Kata ya Maji ya Chai, Ndikilo Mbise kutokana na Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo ya Maji ya Chai, David Mwita kuwa safarini.
Akiahirisha kesi hiyo, Mbise alisema itatajwa tena Januari 20 mwakani.Mbise alisema Hakimu Mwita amepata msiba, hivyo amekwenda nyumbani kwao mkoani Mara huku, hakimu mwingine wa mahakama hiyo akiwa likizo.
Mbise alisema ameahirisha kesi na kuipangia tarehe nyingine kwa kuwa ni mlinzi wa amani wa eneo hio.
Katika kesi hiyo, Nassari ambaye hakuhudhuria mahakamani hapo kutokana na kuwa safarini, anatuhumiwa kuchoma bendera ya CCM Desemba 15, saa 11 jioni katika eneo la Maji ya Chai. Bendera hiyo yenye thamani ya Sh250,000 ilikuwa mali ya Raphael Moses.
Ilielezwa mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa ataendelea kuwa nje kwa dhamana ya wadhamini watatu ya Sh1.5 milioni kila mmoja. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

FILAMU YENYE UTATA YAWEKWA MITANDAONI

Filamu ya the Interview iliozua utata 
 
Kampuni ya Sony Pictures imesema kuwa sinema yenye utata ya ucheshi kuhusu namna ya kumuuwa kiongozi wa Korea Kaskazini, imewekwa katika mitandao Nchini Marekani.
Kampuni hiyo inasema kuwa imechagua njia ya kusambaza sinema hiyo kupitia mitandao ya digitali, ili kuruhusu watu wengi zaidi kutizama sinema hiyo iitwayo, 'The Interview'.
Uzinduzi wa awali wa filamu hiyo ulizingirwa na utata wa mashambulizi ya kimitandao ambapo Marekani ililaumu Korea Kaskazini kwa hitilafu hiyo. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC

MAREKANI: IS HAIKUANGUSHA NDEGE YETU

 Wapiganaji wa IS wakibeba mabaki ya ndege waliodai kuidungua huko Syria 
 
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wamesema kuwa waliidungua ndege ya jeshi la muungano ,lakini Marekani inasema kuwa ushahidi uliopo unaonyesha kuwa hilo si kweli.
Jordan ni miongoni mwa mataifa manne ya kiarabu yaliopo katika muungano wa majeshi yanayoungwa mkono na Marekani ambayo yameanzisha mashambulizi dhidi ya wanamgambo wa IS.
Ndege hiyo aina ya F-16 ni ndege ya kwanza ya jeshi hilo la muungano kupotea katika maeneo yanayodhibitiwa na IS tangu mashambulizi yaanze mnamo mwezi Septemba.
Rubani wa ndege iliodaiwa kudunguliwa na wapiganaji wa IS akamatwa
Picha za IS zinamuonyesha rubani wa ndege hiyo akikamatwa. Wamemtaja rubani huyo kuwa Moaz Youssef al-Kasasbeh. Wakati huohuo Jordan imesema kuwa hasara iliyopata ya kupoteza ndege yake moja ya kivita, katika anga linalodhibitiwa na waasi wa Islamic State, haitayumbisha majeshi yake kuendelea kukabiliana na matendo ya kigaidi.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MARUFUKU YA EBOLA YATOLEWA SIERRA LEONE

Maafisa wa afya wakibeba miili ya watu waliofariki kutokana na Ebola nchini Sierra leone taifa hilo limetoa marufuku ya siku tatu kazkazini mwa taifa hilo ili kukabiliana na ebola. 
 
Serikali ya Sierra Leone imetangaza siku tatu za marufuku kaskazini mwa taifa hilo, ili kuruhusu jitihada za kukabiliana na kuenea zaidi kwa ugonjwa hatari wa Ebola.
Msemaji wa serikali amesema kuwa maduka na masoko yatafungwa na hakuna magari ya abiria au pikipiki zitakubaliwa kwenye barabara za eneo hilo.
Sherehe za makanisa kuadhimisha sherehe za siku ya Krismasi pia zimepigwa marufuku.
Sierra Leone ni mojawapo ya mataifa ya Afrika magharibi ambayo yalikumbwa pakubwa na ugonjwa huo wa ebola. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MWAMBUSI AISUKA UPYA MBEYA CITY

Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi.
 
Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi amesema tatizo kubwa kwa sasa katika kikosi chake ni safu ya ushambuliaji ambayo ameendelea kuisuka ili wafanye vyema Ligi Kuu Bara itakapoendelea.

Akizungumza na gazeti hili jana, Mwambusi alisema vijana wake wapo ‘fiti’ na wana ari mpya ya kurudisha heshima yao kwa mashabiki wao huku akisema kuteleza siyo kuanguka, kwani yalitokea hivi karibuni ndani ya klabu hiyo yamepita na sasa wanakuja kivingine.

“Ukiangalia mechi zilizopita tulipata mabao mawili tu, na raha ya mpira wa sasa ni kufunga mabao mengi, hivyo nimeona ushambuliaji ni tatizo kubwa, lakini tunaendelea na maboresho katika safu hii,” alisema Mwambusi. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAXIMO "MKAKATI WANGU UMENIONDOA YANGA"




Kocha Marcio Maximo 


Kocha Marcio Maximo amesema hana kinyongo na uamuzi wa uongozi wa Yanga kumuondoa, ingawa umefuta ghafla mkakati wa kutaka klabu hiyo iendeshwa kwa weledi.

Maximo na msaidizi wake Leonard Neiva walisitishiwa mikataba yao baada ya Yanga kufungwa na Simba 2-0 katika mchezo wa Nani Mtani Jembe mwezi huu, ikiwa ni takriban miezi mitano tangu aje nchini.

Akizungumza muda mfupi kabla ya kupanda ndege kurudi kwao Brazil jana, Maximo alisema hana kinyongo na uamuzi huo, lakini akaitaka klabu hiyo kongwe kuendeleza soka la vijana na kutengeneza mindombinu kama inataka kupata mafanikio makubwa katika soka.

Alisema katika muda mfupi aliokuwa klabu hiyo, alijenga misingi ya utendaji kazi wa kisasa ndani na nje ya uwanja kwa wachezaji ili waweze kujitambua katika kazi yao, lakini jambo hilo limeishia njiani. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...