Friday, December 26, 2014

KIJANA AKAMATWA KWA KUMTUKANA RAIS

Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki 
 
Polisi nchini Uturuki wamemkamata mwanafunzi wa sekondari mwenye umri wa miaka kumi na sita kwa tuhuma za kumtukana Rais Recep Tayyip Erdogan.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo, kijana huyo alipelekwa mahabusu baada ya kumtuhumu Bwana Erdogan na chama chake tawala cha AK kwa vitendo vya rushwa wakati wa mkutano wa hadhara katikati ya mji wa Anatolia.
Waziri Mkuu Ahmet Davutoglu ametetea kukamatwa kwa mwanafunzi huyo akisema ofisi ya rais lazima iheshimiwe.
Kumtukana mkuu wa nchi ni makosa kwa mujibu wa sheria za Uturuki na mwanafunzi huyo anakabiliwa na kifungo cha miaka minne jela endapo atapatikana na kosa. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...