Friday, December 26, 2014

MABASI 21 YAADHIBIWA KWA NAULI JUU KRISMASI

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamedi Mpinga (kulia) akizungumza na waandishi Dar es Salaam juzi kuhusu kupanda kwa nauli ya mabasi yaendayo mikoani, daladala zinazoishia Mnazi Mmoja, ajali za barabarani na mambo mbalimbali yanayohusu usalama wa abiria. Wengine kutoka kushoto ni Mkurugenzi Chama cha Kutetea Abiria Tanzania (CHAKUA) Kanda ya Mashariki, Thomas Haule na Mwenyekiti CHAKUA,Hassan Mchanjama. (Picha na Yusuf Badi).
Kamanda wa kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamedi Mpinga (kulia) akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam.
 
JESHI la Polisi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), limewaadhibu wamiliki wa magari zaidi ya 21.
Mawakala wao wa kukata tiketi, wamesombwa na kuburuzwa mahakamani, ambao baada ya kesi zao kusogeswa mbele, sasa wanasota mahabusu, watakakokuwa hadi baada ya shamrashamra za kuukaribisha Mwaka mpya 2015.
Wakati mabasi mengi yakinaswa Morogoro, mawakala wa tiketi ambao pia ni maarufu kama wapigadebe, wamekamatwa katika kikuo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo, Dar es Salaam.
Hayo yamethibitishwa na Ofisa Mfawidhi wa Sumatra Mkoawa Morogoro, Allen Mwanri aliyesema mabasi zaidi ya 21 yalikamatwa kwa makosa ya mbalimbali, likiwemo kubwa la kuzidisha nauli na kutoza nauli kubwa.
Hata hivyo, alisema kila mmiliki wa basi lililokamatwa kwa kuzidisha nauli na nauli kubwa, alitozwa adhabu ya kiasi cha Sh 250,000. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.
Alitaja wamiliki waliowajibishwa kwa kuzidisha nauli na namba za mabasi kwenye mabano ni Kheri Kidinilo (T 292 AZY), Ngailo Express (T 366 BQD), Idd A. Fundi (T 853 DBY), Mohammed Trans kwa mabasi yake mawili (T 738 AAP na T 647 AWD). Wengine na mabasi yao ni Omari Kilala Ally (T277 AJR), Ayoub Ntomola (T590 BHJ), Patrick K.Kimei (T 615 BRK) na Boadway Business Solution (T278 CLY).
Mabasi yaliyozidisha nauli kubwa ni Wegesa Iroga (T889 CNN) na Stanley Membo (T233 CVH). Kwa mujibu wa Mwanri, wengine ni Seif Omary ( T211 AJT), NBS CO LTD (T183 BVZ), Nyehunge mwenye mabasi mawili (T 508 CSX na T400 AEL), BM Coach (T542 CUW), Joseph Makanga (T166 BNC), Hassan Msofe (T819 CHY), Islam (T576 CVD), Abdallah Ally (T725 CXY) na Vicent Lusinde (T874 DAM).
Hata hivyo, wakizungumza kwa nyakati tofauti, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paul na Ofisa Mfawidhi wa Sumatra mkoa wa Morogoro, walisema ukaguzi huo umelenga kukomesha baadhi ya wamiliki wa mabasi ambao wanatumia kipindi cha sikukuu za mwisho wa mwaka, kukiuka masharti ya leseni za usafirishaji wa abiria.
Wengi wasombwa Ubungo Kikosi cha Polisi cha Usalama Barabarani kimeendelea kuwakamata watu waliokutwa wanauza tiketi kwa bei kubwa katika Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo Mikoani cha Ubungo, ambapo hadi jana watu 10 walikuwa wamekamatwa.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga alisema watu hao walipelekwa mahakamani na sasa wapo gereza la Segerea hadi Januari 5 mwaka kesho, kesi zao zitakapotajwa tena.
Alitaja waliokamatwa kuwa ni Victor Kombe ambaye ni wakala wa KVC, Mussa Msangi ambae ni karani wa tiketi za Happy Nation, Walter Nkya ni karani wa tiketi za Ibra Line na Fredrick Lema ambae ni Karani wa Mbazi Travel Coach.
Wengine ni Ramadhani Mbaga, Stephen Amos, Jane Gabriel, Kassim Azaria ambao walikuwa na usafiri wa Toyota Noah, Kelvin Charles ni wakala Islam, Mbaraka Tariba Kombo ambae nae ni wakala wa Islam. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na Habari Leo

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...