Mutharika, ambaye ni mwanasheria, aliyasema hayo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika juzi Mkoa wa Kati.
Akikaririwa na gazeti la Nyasa Times, Mutharika alisema Tanzania haina cha kuambulia kwa Ziwa Malawi.
Kiongozi huyo ambaye hakuwapo katika
mkutano wa Rais Joyce Banda na wapinzani kuzungumzia mustakabali wa
ziwa, aliwahakikishia Wamalawi kuwa wasiwe na wasiwasi wa mvutano huo.
Thursday, August 08, 2013
HII NDIO HOTEL ILIYOKUWA INAUZA NYAMA ZA WATU ILIYOBOMOLEWA NA WANANCHI WENYE HASIRA KALI...!!!
HAPA WANANCHI WAKIIVUNJA HOTELI HIYO
Polisi walifanikiwa kuvikamata vichwa hivyo baada ya
kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema wanaoishi karibu na hoteli hiyo ambapo
mbali na vichwa hivyo viwili lakini pia walikamata bunduki mbili aina ya AK47,kofia mbili za jeshi pamoja na simu
nyingi. |
Watu saba wanashikiliwa na jeshi la polisi nchini Nigeria
katika hoteli moja iliyopo karibu na soko moja maarufu sana nchini humo
linalofahamika kwa jina la Ose-Okwodu katika mji wa Anambra baada ya kukamatwa
kwa vichwa viwili vya binadamu vikiwa bado vibichi lakini jina la hoteli hiyo
linahifadhiwakutokana na sababu za kiusalama
"MAUAJI YA SOWETO YALIPANGWA NA KUTEKELEZWA NA POLISI" LEMA
Lema alitoa madai hayo juzi alipohutubia mkutano wahadhara Viwanja vya Shule ya Msingi Ngarenaro.
Alidai Rais Jakaya Kikwete amegoma kuunda tume huru ya kimahakama kuchunguza tukio hilo, ili kunusuru polisi na aibu ya kushiriki uhalifu na mauaji ya raia wasio na hatia.
“Mauaji ya Soweto yalipangwa na kutekelezwa na polisi, RPC (Kamanda wa Polisi) wa Arusha anajua mpango mzima ndiyo maana Rais hataki kuunda tume kama Chadema tulivyomuomba, ili tuwasilishe ushahidi wa video kuonyesha jinsi walivyohusika,” alisema Lema
MTUHUMIWA WA WIZI WA FEDHA KWENYE ATM ANASWA JANA JIJINI DAR
Dar es Salaam. Msako wa wezi wa kwenye Mashine za Kutolea Fedha (ATM), umeanza kuzaa matunda baada ya raia wa Bulgaria kukamatwa akiiba kwenye ATM ya Bank of Africa (BOA), Tawi la Afrikana, Kinondoni, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa za benki, mtuhumiwa huyo ambaye
hakutajwa jina lake alikamatwa baada ya kamera maalumu zilizowekwa kwenye ATM za BOA, kumtambua kuwa ni mwizi sugu wa benki hiyo anayetafutwa.
Mmoja
wa wafanyakazi wa benki hiyo ambaye hakupenda kutajwa jina kwa kuwa si
msemaji, alisema tukio hilo lilitokea jana saa 12 asubuhi baada ya
mtuhumiwa huyo kuwekewa mitambo maalumu ya kumnasa.
Alisema benki hiyo ilipelekewa malalamiko na baadhi ya wateja kwamba wakienda kutoa fedha kwenye ATM wanakuta akaunti zao hazina salio wakati wanaamini zilikuwa na fedha.
Wednesday, August 07, 2013
MFANYABIASHARA MKUBWA WA MADINI JIJINI ARUSHA AUWAWA KWA KUPIGWA RISASI NA WATU WASIOJULIKANA.
Pichani juu askari wakikagua mwili wa Erasto Msuya, mmoja wa Wafanyabiasha wakubwa wa Madini jijini Arusha aliyejulikana ambaye pia ni mmiliki wa SG HOTEL mkoani humo, baada ya kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi na kufa papo hapo.
Kwa mujibu wa baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa mfanya biashara huyo alifariki dunia mara baada ya majibishano ya risasi baina ya majambazi hayo na mfanya biashara huyo ambapo alizidiwa nguvu na kupigwa risasi na kufariki dunia
Habari zinaeleza na kubainisha zaidi kuwa Marehemu alikuwa akitokea KIA kwenda BOMA ambako alikuwa ameitwa na watu (ambao hawakujulikana mara moja) ili wakafanye biashara.Habari zaidi tuvute subra kidoogo, tutazidi kufahamishana kadiri ya taarifa zitakapokuwa zikiingia. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi-Amen.
CHADEMA WATOA TAMKO KALI JUU YA KUNG'ATUKA KWA JOHN TENDWA .....!!!
John Tendwa alipaswa kuwa
ameondoka kwenye Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, tangu mwaka 2008,
alipofikisha umri wa kustaafu kwa mujibu wa sheria. Aliendelea kufanya kazi
zake hata baada ya muda wa mkataba wake
alioongezewa kuwa umefikia mwisho, hivyo alikuwa anakalia ofisi hiyo ya umma,
kinyume cha sheria.Ametumia muda huo wa miezi kadhaa, aliokuwa
anakalia ofisi ya umma kinyume cha sheria, kuropoka na kuharibu demokrasia, kwa
manufaa ya mamlaka iliyomteua na CCM. Kutokana na mwenendo (maneno na matendo)
wake mbovu, CHADEMA ilitangaza kutokumpatia ushirikiano wowote, yeye kama
Tendwa. Ikamtangaza kuwa adui wa demokrasia nchini.
Kwa muda wote huo, CHADEMA ilikuwa ikitoa ushirikiano kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa. Badala ya kuifuta CHADEMA na kufanikisha dhamira ovu ya kuharibu amani ya nchi, ameondoka yeye.
Kuondoka kwa Tendwa hakuzuii kutekelezwa kwa mapendekezo ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, iliyomkuta na hatia ya kuvunja Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Sensa, hivyo akasababisha kutokea kwa mauaji ya Mwandishi wa Habari, Daudi Mwangosi, Nyololo, Iringa.
Kwa muda wote huo, CHADEMA ilikuwa ikitoa ushirikiano kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa. Badala ya kuifuta CHADEMA na kufanikisha dhamira ovu ya kuharibu amani ya nchi, ameondoka yeye.
Kuondoka kwa Tendwa hakuzuii kutekelezwa kwa mapendekezo ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, iliyomkuta na hatia ya kuvunja Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Sensa, hivyo akasababisha kutokea kwa mauaji ya Mwandishi wa Habari, Daudi Mwangosi, Nyololo, Iringa.
MADAM RITA ATAJA SABABU ZILIZOMFANYA AIHAMISHIE BONGO STAR SEARCH TBC1
Epiq Bongo Star Search ya mwaka 2013 haitaoneshwa tena kupitia ITV.
Mwaka huu shindano hilo la kusaka vipaji vya kuimba litakuwa likioneshwa
kupitia TBC1.
Kupitia Facebook, Rita Paulsen aka Madam Rita ambaye ni mwanzilishi na jaji mkuu wa shindano hilo ametoa sababu mbili za kuhamisha matangazo hayo kutoka ITV hadi TBC1.
“Baada ya kusoma maoni yenu, ningependa kufafanua sababu mbili za kurusha Epiq Bongo Star Search 2013 kupitia kituo cha Televisheni cha TBC1.
Kwanza kabisa ni sababu za kibiashara ndio zimepelekea kipindi cha EBSS kurushwa kupitia TBC1 na sababu ya pili ni kwamba baada ya kwenda kidigitali, TBC1 sasa inapatikana kwenye ving’amuzi karibia vyote vikiwemo Star Times, DSTV na Zuku.”
Kupitia Facebook, Rita Paulsen aka Madam Rita ambaye ni mwanzilishi na jaji mkuu wa shindano hilo ametoa sababu mbili za kuhamisha matangazo hayo kutoka ITV hadi TBC1.
“Baada ya kusoma maoni yenu, ningependa kufafanua sababu mbili za kurusha Epiq Bongo Star Search 2013 kupitia kituo cha Televisheni cha TBC1.
Kwanza kabisa ni sababu za kibiashara ndio zimepelekea kipindi cha EBSS kurushwa kupitia TBC1 na sababu ya pili ni kwamba baada ya kwenda kidigitali, TBC1 sasa inapatikana kwenye ving’amuzi karibia vyote vikiwemo Star Times, DSTV na Zuku.”
PETER WA P-SQUARE AOMBA KUMUOA MSICHANA KWA KUMZAWADIA RANGER ROVER SPOT MPYAAAA...!!!
WEMA, KAJALA... WATINGA GEREZANI, WAMLIZA PAPII KOCHA....!!!
Kajala Masanja na Wema Isaac Sepetu.
MASTAA wawili wanaotamba katika filamu za Kibongo, Kajala
Masanja na Wema Isaac Sepetu hivi karibuni walifunga safari hadi Gereza
la Ukonga jijini Dar kwa ajili ya kumuona Johnson Nguza ‘Papii Kocha’
anayetumikia kifungo cha maisha gerezani humo.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, mara baada ya mastaa hao kufika na
kuonana na Papii Kocha ambaye anatumikia kifungo cha maisha sambamba na
baba yake Nguza Viking ‘Babu Seya’ inadaiwa kuwa Papii aliangua kilio
cha nguvu.“Nimewaona Kajala na Wema Gerezani Ukonga,wameenda kumuona Papii Kocha. Sasa nimeamini kuwa Kajala amejifunza mengi kutokana na kuwekwa mahabusu kipindi kile,” kilisema chanzo chetu kwa sharti la kutotajwa jina lake gazetini.
Baada ya kupata taarifa hizo Risasi Mchanganyiko liliwatafuta mastaa hao ili kutaka kujua undani wa safari yao hiyo.
Gazeti hili liliwapigia simu na kuzungumza na Kajala baada ya namba ya Wema kutokuwa hewani.
“Kweli mimi na Wema tulienda gerezani kumuona Papii ilikuwa ni safari ya majonzi sana, Papii aliangua kilio sana alipotuona,” alisema kwa kifupi Kajala na kukataa kusema kilichojiri zaidi.
SELLY AMUOMBA MSAMAHA MPENZI WAKE KWA KUFANYA MAPENZI NA NANDO NDANI YA BIG BROTHER
Hatimaye mshiriki wa Ghana katika reality show ya Big Brother ‘The Chase’ Selorm Galley maarufu kama Selly aliyetoka wiki moja iliyopita, amemuomba msamaha boy friend wake (wa Ghana) kwa yale aliyoyafanya mbele ya Camera za nyumba ya Big Brother.
Kupitia kipindi cha live ‘Celebrity Show’ cha ETV ya Ghana Selly ambaye pia ni muigizaji alianza kwa kumshukuru mpenzi wake Praye Tietia, na kutokana na kwamba kuna uwezekano yaliyomkwaza mpenzi wake ni mengi, Selly alimuomba msamaha kwa yale yote yaliyojiri mjengoni (ikiwemo kufanya mapenzi na Nando) alipokuwa anaiwakilisha nchi yake kuzifukuzia $300,000.
Selly mwenye miak 25 alisema “I am very thankful for the opportunity given me. I want to thank my boyfriend, Praye Tietia and also use this opportunity to say I am very sorry (for all that happened)”, na akasisitiza “I am very sorry”.
Selly amekuwa akiandamwa na maneno mengi toka camera za Big Brother zimnase akifanya mapenzi na aliyekuwa mwandani wake katika The chase Nando, kitendo kilichowaudhi zaidi mashabiki wa nchini kwake Ghana ambao wamekuwa wakimuandama kupitia mitandao ya kijamii.
POLISI AMWANDIKIA BARUA NZITO MAKAMU WA RAIS...!!!
Na
Bryceson Mathias
ASKARI
Polisi (pichani) mwenye namba D5788D Koplo Patrice Masiko wa Upelelezi Wilaya ya
Dodoma, amemwandikia Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akipinga
kufukuzwa kwa aibu Juni 24, 2011.
Katika
barua yake ya Agosti 2, mwaka huu, Masiko anamuomba Makamu wa Rais Dk. Bilal,
amsaidie kumhimiza Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Said Mwema, ampe Majibu ya
rufaa ya Mashitaka ya Kijeshi yaliyosikilizwa tangu Novemba 30, 2010 hadi Juni
24, 2011.
Katika
barua hiyo kwa Dk. Bilal, Masiko anasema, anamuombi amsaidie kumhimiza IGP
ampatie majibu ya rufaa ya Mashitaka na Hukumu ya Kijeshi dhidi yake,
yaliyosikilizwa na ZM Majunja na SSP-OCD Mpwapwa toka Novemba 30, 2010 hadi Juni
24, 2011.
“Julai 19,
nilimwandikia IGP rufaa ya kupinga mwenendo mzima wa Mashitaka na Hukumu
iliyotolewa lakini sikupata majibu. Agosti 16, 2011 nilimwandikia tena
kukumbushia, lakini sijapata majibu.
MOTO MKUBWA WAZUKA UWANJA WA NDEGE WA JOMO KENYATTA...!!!
NAIROBI, Kenya Aug 7 – Operations were grounded at Kenya's main airport, JKIA on Wednesday following a major fire that broke out at dawn, authorities said, adding flights were being diverted to other airports."There is a serious fire at JKIA, but we are doing everything possible to avert a crisis," Interior and Coordination of National Government Principal Secretary Mutea Iringo said.
His office also posted on twitter "A serious fire at JKIA kindly take caution."
Fire fighters were battling the inferno.
Witnesses said they had seen a huge smoke billowing from the international arrivals and departure areas, but there were no immediate reports of casualties.
MKENYA WA DR. ULIMBOKA AFUTIWA KESI.....!!!
MKURUGENZI wa Mashitaka nchini (DPP), Dk. Eliezer Feleshi, amefuta kesi ya kuteka na kujaribu kumuua Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka, iliyokuwa ikimkabili raia wa Kenya, Joshua Mulundi, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Hatua hiyo imeelezwa kuwa ni baada ya DPP kuona hana haja ya kuendelea kumshitaki kwa makosa hayo ambayo yalikuwa hayana dhamana.
Hati hiyo ya DPP iliwasilishwa chini ya kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002 kwa niaba yake na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Tumaini Kweka, jana mbele ya Hakimu Mkazi Waliarwande Lema.
Kweka aliiambia mahakama kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa lakini upande wa Jamhuri hauna nia tena ya kuendelea kumshitaki Mulundi kwa kesi hiyo.
Hakimu Lema alikubaliana na hoja hiyo na akamfutia kesi hiyo Mulundi ambaye yupo gerezani tangu Julai 13, mwaka jana.
Tuesday, August 06, 2013
NI AIBU TANZANIA KUWA KITOVU CHA DAWA ZA KULEVYA....!!!
Dk. Harrison Mwakyembe.
Sifa hiyo sasa imegeuka na kuonekana sisi ni mabingwa wa kusafirisha dawa za kulevya. Hakika hili la kubobea katika biashara ya dawa za kulevya siyo sifa ya kujivunia hata kidogo mbele ya mataifa.
Hakuna siri wala kificho kwamba Tanzania sasa imejizolea medani za aibu kimataifa kwani katika miaka ya hivi karibuni, imekuwa na sifa ya kuwa moja ya vinara wa biashara ya dawa za kulevya duniani.
Ni aibu na ni sifa inayochafua taswira ya nchi yetu, kwani hivi sasa Watanzania wanaosafiri nje ya nchi wanaficha nyuso zao kwa aibu kutokana na upekuzi wa aina yake wanaofanyiwa na mamlaka za forodha na uhamiaji katika nchi wanazopitia.
TENDWA ASTAAFU, JAJI FRANCIS MUTUNGI ACHUKUA NAFASI YAKE
Ban Ki Moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alipata kusema; “ Tatizo kubwa kwa nchi za Afrika si nakisi kwenye bajeti zao, bali, nakisi ya IMANI”.
Na Profesa Gaudence Mpangala naye amepata kusema; “ Msingi wa matatizo yetu mengi ni uwepo wa mfumo wa Chama Dola.”
Na kwangu mimi, changamoto kubwa kwa Katiba yetu ijayo ni kuona kama itatoa nafuu ya hayo mawili hapo juu.
Maana, haiyumkini tukafanikiwa kujenga taifa la kisasa kama
Jakaya Kikwete ameonyesha kuwa mfano wa kiongozi mwenye ujasiri wa kuzipa mgongo kanuni na taratibu za kijima. Swali, ni wangapi wengine kwenye mfumo anaoutumikia wenye mitazamo kama ya kwake? Maana, maamuzi mengine ya kimageuzi anayoyafanya Kikwete yasingeweza kufikiriwa miaka kumi iliyopita.
Jana Jakaya Kikwete amefanya uteuzi wa Jaji Francis Mutungi kushika nafasi ya John Tendwa kama Msajili wa Vyama. Ukweli unabaki, kuwa kwenye utendaji wake, Tendwa kama mlezi hakuaminika na baadhi ya aliowalea. Hilo ni pungufu kubwa na linakwaza juhudi za kukuza demokrasia ya nchi. Msajili wa vyama vya siasa anapaswa aonekane kuwa ni mlezi wa vyama vya siasa na wala si mwonezi wa vyama vya siasa. Na kazi ya ulezi inatakiwa ionekane.
MGOMBEA ALITUMIA ZIWA NYASA KUJIPIGIA DEBE MALAWI
Mgombea Urais wa Democratic Progressive Party (DPP) nchini Malawi, Peter Mutharika, amesema hakuna sababu za kufanya majadiliano kuhusu Ziwa Malawi ambalo Tanzania wanaliita Ziwa Nyasa. (HM)
TAARIFA YA SIKU KUU YA EID KUTOKA JESHI LA POLISI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
Anuani ya Simu “ MKUUPOLISI” Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi,
Simu : (022) 2110734 Makao Makuu ya Polisi,
Fax Na. (022) 2135556 S.L.P. 9141,
Unapojibu tafadhali taja: DAR ES SALAAM.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Dar Es Salaam Agosti 06, 2013.
Ndugu Wanahabari,
Jeshi la Polisi Nchini linatoa shukrani kwa wananchi wote wakiwemo waandishi wa habari, viongozi wa dini, wanasiasa, makampuni binafsi ya ulinzi kwa ushirikiano mkubwa wanaoutoa kwa njia mbalimbali katika kuhakikisha kwamba nchi yetu ya Tanzania inakuwa salama na raia wote wanaishi kwa amani na utulivu bila hofu ya uhalifu na wahalifu.
Katika kipindi hiki cha kuelekea sikukuu ya Eid-El-Fitr, Jeshi la Polisi linatoa tahadhari kwa wananchi wote kuwa makini na kuchukua hatua stahiki na za haraka kwa kutoa taarifa pindi wanapoona viashiria vyovyote vya uhalifu katika maeneo wanamoishi na sehemu mbalimbali zikiwemo maeneo ya biashara.
Ikumbukwe kuwa, wananchi wenye imani ya kiislam na hata madhehebu mengine hutumia muda huo kwenda kuabudu pamoja na muendelezo wa sherehe hizo kwenye maeneo mbalimbali ya starehe. Uzoefu unaonyesha kuwa baadhi ya watu hutumia kipindi hicho cha sikukuu kama mwanya wa kufanya matukio ya uhalifu kutokana na mikusanyiko hiyo ya watu. Jeshi la Polisi limejipanga vizuri kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha kwamba, wananchi wote wanasherekea sikukuu hiyo kwa amani na utulivu, pasipo vitendo ama viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani.
Monday, August 05, 2013
KESI YA UGAIDI TABORA YAFUTWA, MUME WA JOYCE KIRIA NA WENZAKE WABAKI NA SHITAKA MOJA...!!!
Katibu
Wa Chadema mkoa wa kinondoni na Kanda maalum ya Dar es salaam, mjumbe
wa mkutano mkuu Henry Kilewo(Kulia) na Wenzake Wanne Wameachiwa. Wamefutiwa mashitaka yote ya Ugaidi, sasa wamebakia na shitaka moja la
kudhuru mwili, dhamana itatolewa na mahakama ya wilaya Igunga. Habari zaidi Baadae
WEMA SEPETU NA IRENE UWOYA WAPIMANA UWEZO, ALIANZA WEMA, UWOYA AJIBU MASHAMBULIZI
“Mashabiki wa Clouds TV watapata kuona vita ya kibiashara, Uwoya atakuwa akionekana katika kipindi hicho ambacho kitakuwa kinahusu upakaji rangi katika nyumba za watu mbalimbali huku Wema naye akikimbiza katika In My Shoes,” alisema Ruge.
ARSENAL 1 VS 2 GALATASARAY: DROGBA AKUMBUKIA ENZI ZAKE, AWAFUMUA ARSENAL MAWILI NA KUTWAA KOMBE LA EMIRATES
Kama kawaida rafiki wa nyavu: Drogba alifumania nyavu mara mbili na kutwaa taji la kombe la Emirates
Drogba akimpeleka sokoni kipa wa Arsenal, Wojciech Szczesny
Mnanikumbuka? Drogba akishangilia baada ya kipenga cha mwisho cha mwamuzi
Ufunguzi wa karamu ya mabao: Walcott akiandika bao la kuongoza kwa klabu yake ya Arsenal
DR. SLAA AWAUNGA MKONO WAASI WA KONGO NA KUMKINGIA KIFUA KAGAME...!!!
Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, amemkosoa Rais Jakaya Kikwete, kuhusu kauli yake ya kumshauri Rais wa Rwanda, Paul Kagame, kuzungumza na waasi wa serikali yake ...
Dk. Slaa amesema haoni busara kwa Rais Kikwete kuwaambia viongozi wa Rwanda, akiwamo Rais Kagame, kuzungumza na wafuasi wa chama cha FDRL walioko Congo.
Slaa aliyasema hayo wakati akizungumza katika kongamano la vijana wa Chadema (BAVICHA) la uchumi na ajira lililofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
“Rais Kikwete hapa nyumbani hawezi kuzungumza na wapinzani na hajachukua hatua dhidi ya wauaji wa mwandishi Daudi Mwangosi...
"Alishauriwa amuwajibishe Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda na badala yake amempandisha cheo,” alisema Slaa.
MTOTO MDOGO WA KIKE AUAWA KINYAMA MKOANI MBEYA...!!!
MTOTO mmoja
wa kike ameuawa kinyama kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kisha kunyofolewa
macho na ubongo wake.
Tukio hilo
la kikatili, limetokea mwishoni mwa wiki eneo la Idiwili kata ya Isuto wilaya
ya Mbeya vijijini mkoani hapa.
Mtoto huyo
wa kike, asiye na hatia, mwenye umri wa miaka miwili, aliyejulikana kwa jina la
Lilian Nex Kasonso, alikatishwa uhai wake kwa makusudi kisha mwili wake
kutelekezwa chini ya mti.
Baadhi ya
wananchi wa eneo hilo waliozungumza mwandishi wa habari hii wamesema kuwa, Mama wa mtoto huyo, alimwacha
mwanae akiwa salama mikononi mwa bibi yake kisha yeye kwenda kutafuta kuni.
Punde, Bibi
yake Lilian, naye alienda kuchota maji mtoni huku akimwacha mjukuu wake akiwa
na furaha tele, ndipo majitu hayo makatili, kwa makusudi walimteka mtoto huyo
kisha kutokomea naye pasipo mtu kuwaona ama kuwashitukia.
PEPSI WAIPA YANGA KIBURI...!!!
Habari za uhakika ambazo Mwananchi limezipata zinadai kuwa, Yanga wamepata kiburi cha kugomea udhamini wa Azam baada ya kuwa na ofa mbili mkononi ya Pepsi na ile ya Zuku.
“Pepsi wanatoa kinywaji chao kipya Pepsi Cola na wametupa ofa ya Sh600 milioni, Azam walifuatwa na kuelezwa juu ya ofa hiyo wakakataa Pepsi wasiingie kwa vile ni wapinzani wao kwa Azam Cola,” kilisema chanzo cha habari.
Chanzo hicho kilisema kuwa, Yanga waliwapa sharti Azam la kuongeza dau kutoka Sh100 milioni na kama isingewezekana basi waingie mkataba na Kampuni ya Pepsi.
Sunday, August 04, 2013
TAMBUA SABABU ZA WATOTO WACHANGA KULIA, HIZI NDIZO SABABU ZAKE !!!!.
Sababu za Watoto Wachanga Kulia Mara kwa Mara na Namna ya Kuwabembeleza
Kwa nini watoto wachanga wanalia .?
Ni
kawaida kwa watoto kulia. Hata watoto wanaozaliwa na afya njema kabisa
wanaweza kulia kwa jumla ya wastani wa kati ya saa moja mpaka matatu kwa
siku. Kwa vile watoto hawawezi kujifanyia chochote wao wenyewe zaidi ya
kutegemea wazazi, walezi ama watu wengine wanaowazunguka katika
kuwapatia chakula, joto, na faraja, kilio ni njia ya mtoto ya
kuwasilisha moja ya mahitaji hayo.
Kama
mzazi mpya, wakati mwingine inakuwa vigumu kutambua mtoto wako
anahitaji nini anapolia. Mzazi anaweza kuwa na maswali kadhaa kichwani
mwake, je, mtoto ana njaa, anasikia baridi, ana kiu, anaumwa ama
amechoka ? Katika siku za mwanzo, hali ya namna hii inawawia vigumu
wazazi wengi, wasijue nini la kufanya.
Hata hivyo, kwa kadiri siku
zinavyopita mzazi mpya ataweza kutambua kuwa kilio cha mtoto wake
kinamaanisha anahitaji nini kutokana na mfumo wake wa kulia.
SERIKALI: WALIOOANA NA WAHAMIAJI HARAMU WAVUNJE NDOA HIZO.....!!!
Mkuu wa mkoa wa Geita, Said Magalula
******
Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa mkoa wa Geita, Said Magalula, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na hali ya ulinzi na usalama wa mkoa huo.
Agizo hilo limekuja siku chache, tangu Rais Jakaya Kikwete kutoa siku 14 kwa wahamiaji wote haramu kutokana nje ya nchi kuondoka kwa hiari yao kabla ya kuwasaka na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.
JK AKUTANA NA BINGWA WA DUNIA WA KURUKA KAMBA HAMISI MOHAMED NA WENZAKE
Rais
Jakaya Kikwete akimpongeza kijana wa Kitanzania Hamisi Mohamed mwenye
umri wa miaka 14 aliyeipatia sifa Tanzania kwa kunyakua ubingwa wa
Dunia wa mchezo wa kuruka kamba kwenye michuano iliyofanyika huko
Orlando, Marekani, mwezi uliopita. Kijana huyo, ambaye awali
alilelewa katika kituo cha watoto yatima cha Dogo Dogo Dar es Salaam,
alianza kupata mafunzo ya mchezo huo ambapo alishiriki mashindano ya
Afrika Mashiriki yaliyofanyika Mombasa na kunyakua Medali ya Dhahabu.
Kulia ni mfadhili wa kijana huyo, Amy Canady, na kushoto kwa Rais
Kikwete ni Sister Jean Pruitt, mwanzilishi wa kituo cha kule yatima cha
Dogodogo Centre |
Rais
Kikwete akiwa na bingwa wa dunia Hamisi Mohamed pamoja na wachezaji
wenzie na viongozi wa timu ya Tanzania iliyoshiriki katika mashindano ya
dunia
RAIS MSTAAFU WA MAREKANI BILL CLINTON ATUA BONGO KIAINA.....!!!
Rais Jakaya Kikwete akimpokea mgeni wake Rais mtaafu wa Marekeni Bill Clinton anayepanda gari (HM)
Clinton alitembelea eneo hilo akitokea moja kwa moja Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam (JNIA), alipowasili akiwa katika ziara ya nchi mbalimbali za Afrika kukagua miradi inayoendeshwa na mfuko wake.
Katika eneo hilo rais huyo mstaafu alipokewa kwa shamrashamra mbalimbali ikiwamo ngoma za kiasili huku baadhi ya wananchi wakipigwa butwaa na kutoamini macho yao kwa kiongozi huyo kutembelea makazi yao.
AUA MKE WAKIBISHANA KIPI KITANGULIE KUPIKWA KATI YA MAINI NA NYAMA ....!!!
Mkazi wa kijiji cha Minyughe, wilayani Ikungi, Bonphace Misanga (70) anashikiliwa na polisi mkoani Singida, kwa tuhuma za kumpiga mkewe Amina Kunyonga (67) hadi kufariki dunia baada ya kuzuka mabishano ya nini kianze kupikwa kati ya nyama na maini.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela, aliwaeleza waandishi wa habari kuwa tukio hilo lilitokea Jumanne wiki hii.
Alisema siku hiyo wanandoa hao walikwenda kwenye mnada kijijini hapo na baada ya kunywa kiasi kingi cha pombe ya kienyeji walikubaliana wanunue nusu kilo ya maini na nusu ingine ya nyama mchanganyiko ya ng'ombe, huku wakiwa tayari wamekwisha lewa.
TANESCO WAANZA KUTUMIA TRANSFORMA ZISIZOTUMIA MAFUTA KUDHIBITI WIZI
Dar es Salaam. Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limelazimika kufunga transfoma zisizotumia mafuta kutokana na tatizo kubwa la wizi wa mafuta ya transfoma kwa maeneo mengi nchini.
Meneja mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud amesema, shirika hilo limelazimika kufunga transfoma zijulikanazo kama ‘Dry type Transfoma’ambazo hazitumii mafuta ili kupambana na changamoto za wizi wa mafuta unasababisha baadhi ya maeneo kukosa umeme.
“Tatizo la wizi wa mafuta ya Transfoma ni kubwa, limesababisha shirika kununua transfoma zisizotumia mafuta ambazo zinapatikana kwa gharama kubwa ukilinganisha na transfoma zitumiazo mafuta ili kuepusha kutokukatika kwa umeme kwa maeneo husika,” alisema Badra
Aliyataja baadhi ya maeneo ambayo yamefungwa transfoma zisizotumia mafuta kutokana na kukithiri kwa tatizo la wizi huo kuwa ni pamoja na Mbezi Beach na maeneo mengi katika Wilaya ya Temeke.
Subscribe to:
Posts (Atom)