Monday, April 22, 2013

WANAWAKE WATANO WANASWA WAKIGAWA URODA KWA WANAUME WAWILI NDANI YA CHUMBA KIMOJA HUKO MWANANYAMALA

Kwa tukio hili, vijana wa mjini wanasema; kimenuka! Hivi karibuni wanawake watano ambao majina yao hayakuweza kufahamika mara moja walinaswa usiku mnene wakifanya mapenzi na wanaume wawili kwenye chumba kimoja kilichopo Mwananyamala jijini Dar.

Watu hao walinaswa katika oparesheni kabambe iliyoongozwa na Kamanda Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kinondoni, OCD Wilbroad Mtafungwa pamoja na Ofisa wa Oparesheni, Inspekta Jacob Swai.


Katika zoezi hilo, polisi walivamia kambi kuu inayotajwa kusheheni wanawake wanaojiuza iliyopo Mwananyamala A ambapo ‘wauza sukari’ hao hutumia vyumba vyao kufanya ufuska huo.
Polisi hao walipofika kwenye chumba kimoja kilichopo eneo hilo, walikumbana na upinzani mkubwa wa watu waliokuwa ndani na baada ya kufanikiwa kuufungua mlango, waliwakuta wanawake watano na wanaume wawili wakiwa kimahaba.
Mbali na hao, polisi walifanikiwa kuwanasa wanawake wengine kwenye vyumba vyao na baadhi mtaani wakijiuza ambapo walipewa kibano cha hali ya juu.
Imeelezwa kuwa, wanawake hao wamekuwa na tabia ya kujiuza na wakati mwingine hukubali kufanya mapenzi na wanaume zaidi ya mmoja, hali ambayo ni hatari sana.
Mkazi mmoja wa eneo hilo, Husein Juma alisema: “Kwanza tunampongeza Kamanda Mtafungwa kwa operesheni hii, wanawake hawa wamekuwa ni tatizo kwani wamekuwa wakijiuza waziwazi na kutupa ovyo kondomu.
 Naye Inspekta Swai alisema wamekuwa wakipokea malalamiko kutoka kwa wananchi wa eneo hilo wakaona ni vyema kuyafanyia kazi ambapo waliwakamata zaidi ya watu 35, wanawake kwa wanaume wanaohusika.

BI KIDUDE UMEKWENDA, UMEACHA MAJANGA YA WASANII WA KIKE BONGO!, WAJUE BAADHI YAO HAPA

Kishindo cha kuondoka kwako kwenye uso wa dunia tunayoishi kinaweza kuwa kikubwa ama kidogo au hakuna kabisa kutokana na mazingira au heshima uliyojijengea katika jamii.
Fatma Binti Baraka maarufu kwa jina la Bi Kidude aliaga dunia wiki iliyopita akiwa na zaidi ya miaka 100. Bado jina lake linatamkwa kwenye vinywa vya wengi na linaweza kuendelea kutamkwa kwa miaka mingi zaidi.
Bi Kidude, mwanamke shujaa mzaliwa wa Visiwani Zanzibar alileta mapinduzi katika muziki asilia wa mwambao. Aliitangaza Zanzibar, Tanzania na Bara la Afrika sehemu mbalimbali duniani alipokwenda kwa ziara za kimuziki. Inaaminika alifanya kazi hiyo ya muziki, mafunzo ya unyago na biashara ya hina na wanja kwa zaidi ya miaka 90. Katika kipindi chote, Bi Kidude hakushuka kimuziki hadi pale mdomo ulipoanza kuwa mzito kutokana na uzee miaka 10 kabla ya kifo chake Aprili 17, mwaka huu baada ya kuugua maradhi ya kisukari na kongosho kwa muda mrefu.
Pia inaaminika kuwa ndiye msanii mkongwe zaidi aliyekuwa akipanda jukwaani na umri mkubwa ukilinganisha na wengine unaowajua.

Mpango wa bunge kuidhinisha Sheria ya ndoa za jinsia moja Ufaransa wazua kizazaa mjini Paris.

Siku mbili kabla ya bunge la Ufaransa kuidhinisha sheria inayohalalisha ndoa za jinsia moja kumetokea maandamano ya dakika za mwisho mwisho mjini Paris.
Watu wanaopinga sheria hiyo wamekusanyika katika eneo la Montparnasse la mji mkuu katika juhudi za mwisho za kuizuia sheria hiyo, huku maandamano mengine ya kundi hasimu pia yaliandaliwa kuiunga mkono sheria hiyo.
 Zaidi ya watu 100 wamekamatwa katika kipindi cha wiki moja iliyopita katika maandamano mengine ya kupinga ndoa za jinsia moja.
Makundi ya kutetea haki za binadamu pia yameripoti ongezeko la matusi na mashambulizi ya kimwili dhidi ya jamii ya mashoga na wasagaji nchini Ufaransa.
Ufaransa inatarajiwa kuwa nchi ya 14 kuhalalisha ndoa za jinsia moja, kufuatia kuidhinishwa sheria hiyo nchini New Zealand wiki iliyopita.

Liewig akabidhi majina ya anaowabakiza Simba.

WAKATI Ligi Kuu Tanzania Bara ikielekea ukingoni, Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Liewig, tayari ametoa mapendekezo ya wachezaji watakaobaki Msimbazi.
Kocha huyo alijiunga na klabu hiyo katikati ya msimu huu akichukua mikoba ya Mserbia, Milovan Cirkovic, aliyetimuliwa.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Ofisa Habari wa timu hiyo, Ezekiel Kamwaga, alisema wachezaji wengi waliopendekezwa na Liewig ni vijana.
 
“Ni mapema kuzungumzia usajili katika kipindi hiki, lakini kikubwa ni kwamba kocha tayari amekabidhi orodha ya wachezaji anaowahitaji watakaoendelea kuichezea Simba katika msimu ujao.
“Wachezaji hao aliowapendekeza wengi wao ni vijana tuliowapandisha msimu huu na wachache wa timu ya wakubwa ambao amepanga kuwaandaa zaidi,” alisema Kamwaga.

TAPELI ANAYETUMIA JINA LA WAZIRI LUKUVI AMTAPELI LOWASSA IRINGA

maofisa  wa  polisi mkoa wa  Iringa
wakiweka mtego katika nje ya
 ukumbi wa St Dominic  ili kumnasa
  tapeli  huyo anayejiita ni mtoto  wa
  waziri Lukuvi  na kutapeli  watu
Tapeli  anayetapeli  watu maeneo
 mbali mbali ya Tanzania  kupitia jina
 la  waziri Lukuvi akiingizwa ktk  gari maalum leo
Tapeli  Jonathan Wiliam Lukuvi
feki akitiwa matatani askari kanzu  Iringa
Mkuu  wa  mkoa  wa Iringa Dkt
 Christina  Ishengoma ,askofu Dkt
Boaz Sollo na Waziri mkuu wa
  zamani Edward  Lowassa akimsikiliza
 tapeli huyo akimpa maneno ya kitapeli  Lowassa
Kijana  huyo Tapeli akimsomesha
waziri Lowassa ukumbini kwa
kuahidi kuchangia 100,000 huku
akimwomba  kumsaidia misaada  zaidi
Hapa akipelekwa  katika gari
 maalum Hapa akiingizwa katika
Taxi tayari  kwenda  polisi

MAGAZETI YA LEO APRILI 22, 2013

11 6fa4e
13 d676614 a60d6

LADY JAYDEE AWACHANA TENA CLOUDS..... ANADAI KWAMBA MUNGU SI "RUGE" WALA "KUSAGA"

Baada ya kipindi kirefu cha kuongea kwa mafumbo dhidi ya wamiliki wa Clouds FM kuwanyonya wanamuziki akianzia na wimbo wake waJoto Hasira, mwanamuziki Judith Wambura ameendelea kuishambulia redio hiyo na leo Jumapili ameamua kufunguka kwa kuwachana live wamiliki wa redio hiyo.

Hii ni post yake aliyoipost twitter:

Lady JayDee ‏@JideJaydee 1h Naamini kabisa kuwa Mungu sio Ruge wala Kusaga. Atanisimamia kwenye hili #Confidence
\

BABY MADAHA: NTAWACHANGANYA WANAUME KAMA DIAMOND

STAA wa muziki na filamu Bongo, Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’ amesema mwaka huu atawachanganya wanaume kama afanyavyo Nasibu Abdul ‘Diamond’ ili kwenda sawa.
Akifafanua kauli yake kwa paparazi wa Stori 3, Baby Madaha aliweka bayana kuwa haoni tatizo kunaswa na Mwisho Mwampamba kama ilivyoripotiwa hivi karibuni wakati huohuo anatoka kisela na mkali wa Bongo Fleva, Juma Kassim ‘Nature’.
“Watakoma mwaka huu, lazima niwachanganye sana, mbona wao wanatuchanganya sana kama Diamond vile anavyofanya!” alisema Baby.

Sunday, April 21, 2013

WASOMI:::SPIKA ANAVURUGA BUNGE

Baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kutoa mwongozo na kuunga mkono uamuzi wa Naibu wake, Job Ndugai kuwasimamisha wabunge sita wa Chadema, wasomi, wanasiasa na wanaharakati wamesema Kiti cha Spika ndiyo chanzo cha mvutano bungeni kwa kuwa kinapendelea wabunge wa chama tawala (CCM).
Wamesema licha ya Bunge kuongozwa na kanuni, wakati mwingine viongozi hao wa Bunge wanatumia kanuni hizo kuwapendelea wabunge wa CCM, huku wakieleza kuwa licha ya wabunge wa chama hicho kutukana, hawakupewa adhabu yoyote.
Jumatano ya wiki hii, Ndugai aliwasimamisha Tundu Lissu (Singida Mashariki), Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Ezekiah Wenje (Nyamagana) na Godbless Lema wa Arusha Mjini kutohudhuria Bunge kwa siku tano kutokana na alichokiita kufanya vurugu ndani ya Bunge.
Uamuzi huo wa Spika Makinda ulikuja baada ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kumtaka Ndugai aeleze alitumia kanuni gani kuwasimamisha wabunge hao.

DAWA ZA KUONGEZA AKILI ZATUA NCHINI

Mtindo wa maisha, ulaji na msongo wa mawazo, vimewasababishia Watanzani wengi maradhi lukuki hata vifo.Hata hivyo, wataalamu wa afya kutoka Afrika Kusini wamekuja na dawa maalumu, zilizo na uwezo wa kurudisha kumbukumbu, kuongeza upeo darasani, kuondoa sumu mwilini na kumfanya mzee kuonekana kijana.

 Dawa hizo zinazotumia vitamini zilizomo kwenye vyakula vya kila siku, zina uwezo wa kuongeza kiwango cha uelewa kwa mwanafunzi au mfanyakazi.
Kiwango hicho cha uelewa kitaalamu unatambulika kama ‘IQ’.
Mratibu wa dawa hizo hapa nchini, John Haule anasema kuwa dawa hizo zina uwezo wa kufanya kazi kwa haraka.
“Virutubisho hivi ni vizuri kwa wale wanaokwenda katika
mitihani au wanataka kufanya kazi inayohitaji umakini wa hali ya juu,” anasema Haule na kuongeza: “Zimetengenezwa kwa vyakula tunavyotumia na siyo kemikali.”
Haule ambaye ni mtaalamu wa tiba asili na mimea anasema kwamba mtindo wa maisha na vyakula vinavyoliwa na watu mara kwa mara kwa sasa huufanya mwili kuhifadhi sumu nyingi mwilini.

MUME WA MTU ATIWA MBARONI KWA KOSA LA KUFANYA MAPENZI NA MBUZI MWENYE MIMBA NA KUHARIBU MIMBA YA MBUZI HUYO

Marcel ambaye ni mume wa mtu, alifunguliwa kesi namba 29/2013 katika Mahakama ya Mwanzo ya Bashneti mkoani Babati kwa kosa la kuiingilia kimwili mifugo, kinyume na kifungu cha 325 kanuni ya adhabu, sura ya 16 na kesi hiyo ilisomwa hivi karibuni.
Mshitakiwa aliwekewa dhamana lakini siku chache baadaye kesi ilipotakiwa kuendelea, hakuonekana na imebainika mahakamani hapo kuwa ametoroka.

Kesi hiyo ipo mbele ya Hakimu Julius Dagharo wa mahakama hiyo na aliyethibitisha mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa ametoroka ni Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Bashneti, Omari Mwanditi.
Akizungumza mwishoni mwa wiki iliyopita, mmiliki wa mbuzi anayedaiwa kuingiliwa,  Clementina Masay alidai kuwa mtuhumiwa huyo amemsababishia hasara kwani mbuzi wake alikuwa na mimba lakini baada ya kitendo hicho, imeharibika.
Jamii ya wafugaji wa Kiiraq wa eneo hilo wamesikitishwa na kitendo cha mtuhumiwa kudaiwa kuiingilia mifugo yao kimwili mara kwa mara na wameahidi kumsaka hadi wamkamate.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Babati, ACP Akili Mpwapwa amekiri kutokea kwa tukio hilo na ametoa wito kwa wananchi kutoa taarifa wakimuona mtuhumiwa huyo ili afikishwe mahakamani.

AMA kweli dunia imekwisha kwani mtu mmoja, Daniel Marcel (27), mkazi wa Kijiji cha Madunga, wilayani Babati, Manyara, amekamatwa na kufikishwa mahakamani kwa madai ya kufanya mapenzi.

WAREMBO WA XTRA BONGO WAZITWANGA NGUMI, KISA BUZI LA KIZUNGU.


Otilia Boniface kulia na Janeth Tingisha

Wanenguaji wa Bendi ya Extra Bongo, Otilia Boniface na Janeth Tingisha mwishoni mwa wiki iliyopita walitoa kali ya mwaka baada ya kutaka kutwangana makonde wakigombea kutoa namba zao za simu kwa buzi la Kizungu.

Tukio hilo lilitokea ndani ya Ukumbi wa Meeda uliopo Sinza jijini Dar ambapo awali Mzungu huyo alivutiwa na wadada hao hivyo kuwafuata na kuomba namba ya simu ya mmoja wao.

Kufuatia ombi la Mtasha huyo, kila mmoja alitaka apate nafasi hiyo ndipo wanenguaji hao waliposukumana na kufikia hatua ya Janeth kuchukua simu ya Otilia na kuipiga chini ila kwa busara za Mzungu huyo alichukua namba za wote.

JUMA NATURE ATIMULIWA EATV BAADA YA KUINGIA AKIWA AMEVAA KANDAMBILI.....

Msanii mkongwe na maarufu nchini, Juma Kassin Kiroboto, aka Nature, ameonyesha kukerwa na kitendo  cha  kutimuliwa  jana usiku katika kipindi cha burudani cha televishen inayotizamwa africa ya mashariki alipokuwa akifanya nao interview. 
Nature alionekana akiwa amevaa kawosh na ndala na mara baada ya mahojiano mafupi ya mwanzo  mtangazaji alisema watarejea baada ya mapumziko mafupi  na ndipo Nature hakuonekana tena.
  Kilichotokea kwa mujibu wa Nature mwenyewe, ni wakati wa mapumziko hayo, mtangazaji wa kipindi hicho alimfuata na kumuambia kuwa hataendelea na interview tena kwasababu ya mavazi aliyokuwa kavaa ambayo ni ndala na kawosh. kuonyesha kukerwa kwake na ishu hiyo Nature aliamua kuandika yafuatayo  kupitia ukurasa wake wa facebook....

"hivi kwa mfano angekuwepo mzungu pale na kavaa ndala wangesitisha mahojiano na kuvaa kaoshi ni tatizo....

kunywa nimekunywa bt kuna baya nimeliongea na hivi kama kweri we nimuandishi wa habari unaruhusiwa kuvaa vile kisheria kama yule mtangazaji nimeboreka kinoma na ikiwezekana nasitisha kuanzia ssa kupeleka ngoma zangu pale siitaji interview"

WABUNGE WATAKA JUMBA LA MCHUNGAJI LWAKATARE LIVUNJWE.........!!!

'Hekalu' linalomilikiwa na Mchungaji Getrude Lwakatare.
Wabunge wamemtaka Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira Terezya Huvisa kuzivunja nyumba mbili zilizopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam zilizojengwa katika fukwe ya bahari ya Hindi ikiwemo ya mbunge licha ya kwamba kuna zuio la mahakama.

Bila kutaja majina ya wamiliki hao, wabunge hao walitaka hatua hizo zichukuliwe kwa haraka kwa nyumba hizo zilizojengwa kwenye fukwe kinyume cha sheria zivunjwe kwa maelezo kuwa hazina ofa wala hati.
 
Sambamba na hilo wametaka watendaji wa serikali waliohusika kutoa vibali kuruhusu ujenzi huo kwa maelezo kuwa walichukua rushwa wachukuliwe hatua.

SHY- ROSE BHANJI APATA AIBU YA KARNE TOKA KWA ANNA KIBIRA

Aliyekuwa mjumbe baadae katibu mkuu wa CHANETA Anna Kibira amechaguliwa tena kuwa mwenyekiti wa chama cha mpira wa pete chaneta Katika uchaguzi uliofanyika jioni ya leo hii Mkoani Dodoma , huku msimazi wa uchaguzi huo akiwa mkuu wa wilaya ya bahi na aliyekuwa Mtangazaji wa zamani wa itv Betty Mkwasa .
Anna Kibira amemshinda mpinzani wake Shy-Rose Bhanji kwa tofauti ya la kura arobaini katika nafasi ya uenyekiti Anna Kibira amepata kura 61 dhidi ya mpinzani wake Shy-Rose Bhanji ambaye amepata kura arobaini na moja .
Aidha kulikuwa na nafasi mbalimbali ambazo zilikuwa zikigombewa katika chama hicho cha mpira wa pete ambapo kulikuwa na wajumbe wa kamati ya utendaji ambao walikuwa wagombea tisa lakini wamepataikana wagombea sita tu.

Grace Khatib ambaye alikuwa hana mpinzani katika nafasi ya mweka hazina alipata kura za ndio 66 na kura za hapana 16 kati ya kura 82 zilizopigwa.
Katika nafasi ya makamu mwenyekiti kulikuwa na wagombea wawili Zainab Mbiro na Agnes Madasila katika nafasi hiyo Zainabu Mbiro alipata kura hamsini saba wakati mpinzani wake amepata kura 27
Kwa maana hii CHANETA imepata safu mpya kabisa ya uongozi baada ya ile ya mwanzo ile kuamua kuachia ngazi na wagombea wengine kuamua kutokugombea kabisa uongozi katika chama hicho cha mchezo wa pete kwani safu mpya inatakiwa kufanya kazi ya ziada kufikia malengo ya kuinua mchezo wa mpira wa pete kwani uongozi uliopita uliiwezesha CHANETA kuifikisha timu ya taifa ya mchezo huo katika mashindano ya dunia.
Chama kiliweza kuaandaa michuano ya mataifa ya afrika ni wazi kabisa wanachangamoto kubwa ya kufanya japokuwa mara baada ya ushindi kibira amesema kuwa anataka kuupeleka mchezo huo mikoani na kwenda kuuimarisha zaidi vijijini .

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...