Friday, December 26, 2014

ASKARI WATATU WA AU WAUAWA SOMALIA

Askari wa Somalia wakiangalia mabaki ya magari katika moja ya mashambulio ya kigaidi mjini Mogadishu, Somalia. 
 
Jeshi la kulinda amani la Umoja wa Afrika nchini Somalia limesema askari wake watatu na kandarasi raia wameuawa katika shambulio lililofanyika katika makao yake makuu mjini Mogadishu.
Taarifa ya Umoja wa Afrika imesema wapiganaji wa al-Shabab waliingia katika kambi wakivalia sare kama askari wa jeshi la serikali ya Somalia.
Taarifa hiyo imesema washambuliaji watano waliuawa na wengine kadha kukamatwa. Pamoja na kutoa eneo hilo kuwa makao makuu ya majeshi ya kulinda amani ya AU nchini Somalia, eneo hilo lililoimarishwa pia makao ya balozi za Uingereza na Italia. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC

LIGI KUU TANZANIA BARA KUANZA LEO

 Kikosi cha timu ya Azam ya Ligi Kuu ya Vodacom, Tanzania 
  
Ligi kuu ya Tanzania bara, maarufu kama Ligi Kuu ya Vodacom inaanza rasmi mzunguko wa pili leo, Ijumaa baada ya kusitishwa tangu Novemba 7, 2014.
Hadi ligi hiyo ilipositisha mzunguko wa kwanza, tayari timu 14 zinazoshiriki ligi hiyo zilikuwa zimecheza michezo saba kila moja.

Timu ya Simba ya ligi kuu ya Vodacom
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Shirikisho la Kandanda nchini Tanzania, TFF, Simba ambayo ni miongoni mwa timu kongwe za ligi hiyo na ambayo katika mzunguko wa kwanza haikuwa na matokeo mazuri baada ya kwenda sare mara sita na kushinda mchezo mmoja na kujikusanyia pointi tisa ikishika nafasi ya saba katika msimamo wa ligi hiyo, leo inaikaribisha Kagera Sugar inayoshikilia nafasi ya tano katika pambano litakalofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Michezo mingine itafanyika katika viwanja mbalimbali kuanzia Ijumaa, Jumamosi na Jumapili wiki hii.

Wachezaji wa timu ya Yanga
Mpaka sasa Mtibwa Sugar ndiyo inayoongoza ligi hiyo ya Vodacom baada ya kujikusanyia pointi 15, ikifuatiwa na Young Africans(Yanga) kwa kuwa na pointi 13 sawa na Azam mabingwa watetezi. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

WENGER AMUWINDA BEKI WA REAL MADRID

Sergio Ramos wa Real Madrid.Kocha wa Arsenal adaiwa kummezea mate 
 
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amewasiliana na ajenti wa beki wa Real Madrid Sergio Ramos kuhusu uwezekano wa mchezaji huyo kujiunga na kilabu hiyo ya uwanja wa Emirates.
Ramos mwenye umri wa miaka 28 amekuwa na kilabu hiyo ya Los Blancos kwa takriban muongo mmoja baada ya kuwasili kutoka sevilla kwa kitita cha pauni millioni 20 mwaka 2005.
Hatahivyo ripoti za hivi majuzi zimedai kwamba Ramos huenda akaondoka katika kilabu hiyo ya Santiago Bernabeu baada ya mazungumzo ya kandarasi yake mpya kugonga mwamba.
Na kulingana na mwandishi Esteban Manolete wa AS ,mkufunzi huyo wa The Gunners amewasiliana na wawakilishi wa Ramos ili kuona iwapo anaweza kumvuta mchezaji huyo katika eneo la London kazkazini.
''Wenger amewasiliana na Rene Ramos ajenti na ndugu ya Sergio Ramos'',mwandishi huyo alikimbia kipindi cha La Goleada.
Wenger juma hili alikiri kwamba safu ya ulinzi ya Arsenal haina uongozi baada ya kufungwa bao la dakika za mwisho na liverpool na hivyobasi kupata sare ya 2-2. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Thursday, December 25, 2014

JAMBO TZ BLOG INAWATAKIA WATU WOTE KHERI YA CHRISTMAS

 Heri ya X-mass kwa wadau wote wa blog hii. Tafadhari usisahau ku-like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

UKAWA WATAKA KICHWA CHA MUHONGO...!!!

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo. 

Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umelitaka Bunge kuiwajibisha Serikali ikiwa Rais Jakaya Kikwete atashindwa kutekeleza maazimio ya Bunge ikiwamo kumng’oa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Wakizungumza hapa jana, viongozi hao walisema endapo Rais atashindwa kumwajibisha Profesa Muhongo, basi wabunge wao watawasilisha hoja na kushawishi wengine kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu na umoja huo utaitisha maandamano nchi nzima.
Mwenyekiti mwenza wa umoja huo, Profesa Ibrahim Lipumba alihoji kwa nini Rais Kikwete anasita kumwondoa Profesa Muhongo wakati Bunge lilishatoa maazimio.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

UKAWA WATAKA SHERIA YA MAADILI INAYODHIBITI MAOVU

Viongozi wa Ukawa.

Viongozi wa UKAWA

VYAMA vya siasa vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), vimetaka sheria ya maadili itungwe upya ili kuweka uwazi wa watu wote kuona taarifa ya mali za viongozi.

Vyama hivyo vinaamini hatua hiyo, itasaidia wananchi wote kujua mali halisi za viongozi na pia itasaidia kupunguza ufisadi, kutokana na wananchi kutambua ukweli wa mali za viongozi wao.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa umoja huo, Profesa Ibrahim Lipumba wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu hatua zinazostahili kuchukuliwa, kutokana na suala la uchotwaji wa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

VIJIJI 45 KUPATA UMEME MARA

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesema vijiji 45 mkoani Mara vinatarajiwa kuunganishiwa na huduma ya umeme kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Alisema hayo katika ziara yake ya siku sita katika mkoa wa Mara, lengo likiwa ni kukagua na kuzindua miradi ya umeme vijijini inayosimamiwa na REA awamu ya pili kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Nchini (Tanesco).
Alisema ziara yake iliyohusisha wilaya za Musoma, Tarime, Rorya, Bunda na Serengeti, ililenga kubaini na kukagua mahitaji ya umeme katika wilaya hizo ili vijiji vilivyokosa umeme kwenye awamu ya pili, viingizwe katika awamu nyingine ya umeme vijijini. 
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

CHENGE, NGELEJA KUADHIBIWA NDANI YA SIKU 21 ZIJAZO

Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti bungeni, Andrew Chenge


Wenyeviti watatu wa Kamati za Bunge waliopendekezwa kuwajibishwa na Bunge hilo katika sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow wataondolewa katika nyadhifa zao ndani ya siku 21 zijazo, imeelezwa.

Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema jana kuwa utekelezaji wa maazimio ya Bunge kwa upande wa mhimili huo wa dola utafanyiwa kazi mapema mwakani.

“Hilo litatekelezwa wakati wa Kamati za Bunge ambazo zitaanza mwishoni mwa wiki ya pili ya Januari mwakani kwa kamati husika kuchagua wenyeviti wapya.”

Wenyeviti hao ni wa Kamati ya Nishati na Madini, Victor Mwambalaswa, William Ngeleja wa Katiba, Sheria na Utawala na Andrew Chenge wa Kamati ya Bajeti. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS DESEMBA 25, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC07568
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

KESI YA MH. NASSARI YAAHIRISHWA

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari  

Kesi ya kuchoma moto bendera ya CCM inayomkabili Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari jana iliahirishwa na Ofisa Mtendaji wa Kata ya Maji ya Chai, Ndikilo Mbise kutokana na Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo ya Maji ya Chai, David Mwita kuwa safarini.
Akiahirisha kesi hiyo, Mbise alisema itatajwa tena Januari 20 mwakani.Mbise alisema Hakimu Mwita amepata msiba, hivyo amekwenda nyumbani kwao mkoani Mara huku, hakimu mwingine wa mahakama hiyo akiwa likizo.
Mbise alisema ameahirisha kesi na kuipangia tarehe nyingine kwa kuwa ni mlinzi wa amani wa eneo hio.
Katika kesi hiyo, Nassari ambaye hakuhudhuria mahakamani hapo kutokana na kuwa safarini, anatuhumiwa kuchoma bendera ya CCM Desemba 15, saa 11 jioni katika eneo la Maji ya Chai. Bendera hiyo yenye thamani ya Sh250,000 ilikuwa mali ya Raphael Moses.
Ilielezwa mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa ataendelea kuwa nje kwa dhamana ya wadhamini watatu ya Sh1.5 milioni kila mmoja. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

FILAMU YENYE UTATA YAWEKWA MITANDAONI

Filamu ya the Interview iliozua utata 
 
Kampuni ya Sony Pictures imesema kuwa sinema yenye utata ya ucheshi kuhusu namna ya kumuuwa kiongozi wa Korea Kaskazini, imewekwa katika mitandao Nchini Marekani.
Kampuni hiyo inasema kuwa imechagua njia ya kusambaza sinema hiyo kupitia mitandao ya digitali, ili kuruhusu watu wengi zaidi kutizama sinema hiyo iitwayo, 'The Interview'.
Uzinduzi wa awali wa filamu hiyo ulizingirwa na utata wa mashambulizi ya kimitandao ambapo Marekani ililaumu Korea Kaskazini kwa hitilafu hiyo. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC

MAREKANI: IS HAIKUANGUSHA NDEGE YETU

 Wapiganaji wa IS wakibeba mabaki ya ndege waliodai kuidungua huko Syria 
 
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wamesema kuwa waliidungua ndege ya jeshi la muungano ,lakini Marekani inasema kuwa ushahidi uliopo unaonyesha kuwa hilo si kweli.
Jordan ni miongoni mwa mataifa manne ya kiarabu yaliopo katika muungano wa majeshi yanayoungwa mkono na Marekani ambayo yameanzisha mashambulizi dhidi ya wanamgambo wa IS.
Ndege hiyo aina ya F-16 ni ndege ya kwanza ya jeshi hilo la muungano kupotea katika maeneo yanayodhibitiwa na IS tangu mashambulizi yaanze mnamo mwezi Septemba.
Rubani wa ndege iliodaiwa kudunguliwa na wapiganaji wa IS akamatwa
Picha za IS zinamuonyesha rubani wa ndege hiyo akikamatwa. Wamemtaja rubani huyo kuwa Moaz Youssef al-Kasasbeh. Wakati huohuo Jordan imesema kuwa hasara iliyopata ya kupoteza ndege yake moja ya kivita, katika anga linalodhibitiwa na waasi wa Islamic State, haitayumbisha majeshi yake kuendelea kukabiliana na matendo ya kigaidi.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MARUFUKU YA EBOLA YATOLEWA SIERRA LEONE

Maafisa wa afya wakibeba miili ya watu waliofariki kutokana na Ebola nchini Sierra leone taifa hilo limetoa marufuku ya siku tatu kazkazini mwa taifa hilo ili kukabiliana na ebola. 
 
Serikali ya Sierra Leone imetangaza siku tatu za marufuku kaskazini mwa taifa hilo, ili kuruhusu jitihada za kukabiliana na kuenea zaidi kwa ugonjwa hatari wa Ebola.
Msemaji wa serikali amesema kuwa maduka na masoko yatafungwa na hakuna magari ya abiria au pikipiki zitakubaliwa kwenye barabara za eneo hilo.
Sherehe za makanisa kuadhimisha sherehe za siku ya Krismasi pia zimepigwa marufuku.
Sierra Leone ni mojawapo ya mataifa ya Afrika magharibi ambayo yalikumbwa pakubwa na ugonjwa huo wa ebola. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MWAMBUSI AISUKA UPYA MBEYA CITY

Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi.
 
Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi amesema tatizo kubwa kwa sasa katika kikosi chake ni safu ya ushambuliaji ambayo ameendelea kuisuka ili wafanye vyema Ligi Kuu Bara itakapoendelea.

Akizungumza na gazeti hili jana, Mwambusi alisema vijana wake wapo ‘fiti’ na wana ari mpya ya kurudisha heshima yao kwa mashabiki wao huku akisema kuteleza siyo kuanguka, kwani yalitokea hivi karibuni ndani ya klabu hiyo yamepita na sasa wanakuja kivingine.

“Ukiangalia mechi zilizopita tulipata mabao mawili tu, na raha ya mpira wa sasa ni kufunga mabao mengi, hivyo nimeona ushambuliaji ni tatizo kubwa, lakini tunaendelea na maboresho katika safu hii,” alisema Mwambusi. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAXIMO "MKAKATI WANGU UMENIONDOA YANGA"




Kocha Marcio Maximo 


Kocha Marcio Maximo amesema hana kinyongo na uamuzi wa uongozi wa Yanga kumuondoa, ingawa umefuta ghafla mkakati wa kutaka klabu hiyo iendeshwa kwa weledi.

Maximo na msaidizi wake Leonard Neiva walisitishiwa mikataba yao baada ya Yanga kufungwa na Simba 2-0 katika mchezo wa Nani Mtani Jembe mwezi huu, ikiwa ni takriban miezi mitano tangu aje nchini.

Akizungumza muda mfupi kabla ya kupanda ndege kurudi kwao Brazil jana, Maximo alisema hana kinyongo na uamuzi huo, lakini akaitaka klabu hiyo kongwe kuendeleza soka la vijana na kutengeneza mindombinu kama inataka kupata mafanikio makubwa katika soka.

Alisema katika muda mfupi aliokuwa klabu hiyo, alijenga misingi ya utendaji kazi wa kisasa ndani na nje ya uwanja kwa wachezaji ili waweze kujitambua katika kazi yao, lakini jambo hilo limeishia njiani. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

PLUIJM NA PHIRI WAJIGAMBA

Kocha wa Yanga, Hans van Pluijm




Kocha wa Yanga, Hans van Pluijm na mwenzake Patrick Phiri wa Simba wametamba kuibuka na ushindi dhidi ya Azam na Kagera Sugar wakati mechi za Ligi Kuu ya Vodacom zitakapoingia raundi ya nane kuanzia kesho.

Pluijm alisema kuwa anaiheshimu Azam FC kama moja ya timu bora kwenye ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, lakini hana hofu yoyote.

“Nawaandaa vyema vijana wangu waibuke na ushindi kwenye pambalo hilo kwa sababu litatuweka kwenye nafasi nzuri nje na ndani ya uwanja,” alisema Pluij
m. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Wednesday, December 24, 2014

PROF. TIBAIJUKA: BWANA ALITOA, BWANA AMETWAA


Aliekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka.
Siku moja baada ya kufukuzwa  uwaziri, Mbunge wa Muleba Kusini (CCM),  Profesa Anna Tibaijuka amewasili jimboni kwake na kusema, “Bwana alitoa na Bwana ametwaa.”
Profesa Tibaijuka alivuliwa uwaziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Rais Jakaya Kikwete juzi kutokana na kuhusika kupokea fedha katika akaunti binafsi.
Baada ya kuwasili na kupokewa kwa maandamano, Profesa Tibaijuka aliwaomba wananchi kukaa kimya kwa dakika moja ili kumkumbuka katibu wake wa jimbo aliyefariki dunia wakati sakata hilo likijadiliwa bungeni.
Profesa Tibaijuka aliyepokewa kwa msafara wa magari kutoka Uwanja wa Ndege wa Bukoba, aliwaeleza wananchi kuwa ilikuwa ni lazima kutafuta msaada kwa watu wengi ili aweze kuwasomesha watoto anaowasaidia kielimu.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MASWI ASIMAMISHWA KAZI KWA MUDA

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue.

 Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue.

SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kutengua uteuzi wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue naye ametangaza kumsimamisha kazi kwa muda Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliachim Maswi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Maswi amesimamishwa ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake, kama ilivyoelekezwa na Rais Kikwete juzi wakati anahutubia taifa kupitia wazee na wakazi wa Dar es Salaam kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

DAKTARI ALIYEKUTWA KALEWA GEITA AVULIWA CHEO


Wagonjwa wakimtia adabu Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya cha Nyakabale mkoani Geita, Josephat Msafiri baada ya kuwatelekeza juzi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Magreth Nakainga amemvua madaraka Mganga Mkuu wa Zahanati ya Nyakabale, Josephat Msafiri kwa kukiuka miiko ya kazi yake na kulewa wakati wa kazi.
Mkurugenzi huyo aliamua kuchukua uamuzi huo jana kutokana na tukio lililotokea Juzi hii la daktari huyo kufunga kituo cha afya na kuacha wagonjwa wakiwa wamezidiwa, kisha kwenda kunywa pombe jambo lililowalazima kumchapa viboko akiwa baa.
“Tumeshamchukulia hatua za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kumvua madaraka yake ili iwe fundisho kwa watumishi wengine wa Serikali,” alisema Nakainga.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO DESEMBA 24, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
DSC07535
DSC07530 
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

RAIS KIKWETE ATA WANAOKIUKA MAADILI KUWAJIBISHWA

Rais Jakaya Kikwete.

 RAIS Jakaya Kikwete 

RAIS Jakaya Kikwete amesema ni lazima watumishi wa umma wanaokiuka maadili ya utumishi wa umma wawajibishwe ili iwe fundisho kwao na kwa wengine.

Rais Kikwete aliyasema hayo Dar es Salaam juzi baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki kumkaribisha kuzungumza na wazee wa jiji hilo.
Awali kabla ya Rais kuzungumza, Sadiki katika hotuba yake alimwelezea Rais jinsi Uchaguzi Mkuu wa Serikali za Mitaa ulivyofanyika jijini mwake na kusema CCM imefanya vizuri kwa kuibuka na ushindi wa jumla ya asilimia 75.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

GEORGE BUSH ALAZWA BAADA YA KUPATA TATIZO LA KUPUMUA

 George H.W Bush.
 
Aliyekuwa rais wa Marekani George H.W Bush amekimbizwa katika hospitali moja ya Houston nchini Marekani baada ya kupatikana na tatizo la kupumua.
Kulingana na madaktari,Bush mwenye umri wa miaka 90 anachunguzwa katika hospitali ya Methodist.
Alipelekwa katika hospitali hiyo na ambalensi jumanne usiku.
Wawakilishi wa Bush wanasema kuwa hatua hiyo ya kupelekwa hospitali ni kama tahadhari.
Rais huyo wa 41 ndio mzee kuwahi kuiongoza Marekani akimshinda Jimmy Carter kwa miezi michache.
Alihudumu kwa muhula mmoja baada ya kushindwa na Rais Bill Clinton.
Bush ambaye hawezi kutumia miguu yake,hivi majuzi alionekana amekaa katika kiti cha magurudumo katika hafla iliofanyika mwezi November katika chuo kikuu cha Texas na mwanawe aliyekuwa rais George W Bush. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...