Saturday, December 14, 2013
Friday, December 13, 2013
AZIMIO LA KUWANG'OA MAWAZIRI LAPITISHWA RASMI NA BUNGE...!!!
********
Bunge limepitisha azimio la kuwataka mawaziri katika Ofisi ya
Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), kujipima
iwapo wanatosha kuendelea kuongoza wizara hiyo nyeti.
Azimio hilo lilipitishwa jana na wabunge kwa kura
ya ndiyo bila kupingwa, baada ya kuhojiwa na Spika wa Bunge Anne Makinda
iwapo wanaipokea taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali
(Laac) iliyowasilishwa na Mwenyekiti wake Rajabu Mbaruku.
Moja ya mapendekezo yake ni Waziri wa Tamisemi,
Hawa Ghasia na manaibu wake, Aggrey Mwanri na Kassim Majaliwa kujipima
kama wanatosha kuendelea kuongoza wizara hiyo kutokana na kugubikwa na
vitendo vya ufisadi.
Kwa mujibu wa taratibu za Bunge, taarifa ya kamati
inapowasilishwa na kupitishwa pamoja na mapendekezo yake, huwa ni
azimio kamili ambapo Serikali hutakiwa kutoa maelezo ya utekelezaji
wake.
Kabla ya azimio hilo kupitishwa, Mwenyekiti wa
Laac, Rajabu Mbaruku alijibu michango ya wabunge waliochangia katika
taarifa ya kamati yake iliyowasilishwa Ijumaa iliyopita, akiwemo Waziri
Ghasia.
KUMBE GRACA MACHEL NA WINNIE MANDELA NI MTU NA 'DADA YAKE'
Winnie Madikizela-Mandela, (77) aliinama kumbusu Graca Machel
(68), kabla ya kukaa katika kiti cha tatu kutoka kile alichokalia
mwanamke huyo. Graca Machel alimwambia maneno machache ‘dada yake’
Winnie wakati akimbusu.
Wanawake hao wote wakiwa wamevalia majaketi meusi
na vilemba, walikumbatiana kwa sekunde kadhaa huku Winnie akitabasamu na
Graca akitazama mbele.
Wote wawili wanaheshimika nchini Afrika Kusini
kutokana na sababu mbalimbali. Winnie anaheshimika kwa mchango wake
mkubwa wa kupigania ubaguzi wa rangi; Graca kwa moyo wake wa kujitolea
kumtunza kiongozi wao mpaka anafariki dunia.
Hata hivyo Winnie amekuwa akikosolewa kutokana na
sababu mbalimbali ikiwamo ile ya kuruhusu wapinzani wake wauawe kwa
kuchomwa moto wakitumia mafuta ya petroli na matairi ya magari.
ZITTO AWASHA MOTO MPYA CHADEMA...!!!
Siku moja baada ya kuwasilisha maelezo yake ya utetezi baada ya
kuvuliwa nyadhifa zake ndani ya Chadema, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa
chama hicho, Zitto Kabwe amekata rufaa Baraza Kuu kupinga hatua hiyo.
Zitto pamoja na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema
Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba na Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk Kitila
Mkumbo walivuliwa nyadhifa zao na Kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika
Novemba 20 na 21 jijini Dar es Salaam.
Akizungumza jana, Mwanasheria wa Zitto, Albert
Msando alitaja sababu mbili za kukata rufaa kuwa ni kukiukwa kwa
taratibu za kuchukua hatua za nidhamu na sababu zilizotolewa kutokuwa
sahihi.
Hata hivyo, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa
Chadema, John Mnyika alisema mambo hayo yalishatolewa ufafanuzi na chama
na kwamba kukata rufaa ni haki ya kikatiba kwa mwanachama yeyote.
“Kukata rufaa ni haki ya kikatiba ya wanachama
yeyote. Rufaa ikatwe tu, itashughulikiwa kwa mujibu wa katiba, kanuni,
maadili na itifaki ya chama. Hata hivyo, ieleweke, rufani inahusu
kuvuliwa nafasi za uongozi, kusudio hilo haliwaondolei wajibu wa
kujieleza kwa maandishi mbele ya Kamati Kuu kwa nini wasifukuzwe
uanachama,” alisema Mnyika.
Thursday, December 12, 2013
DR. ASHA ROSE MIGIRO ALA KIAPO BUNGENI DODOMA LEO
Mbunge
wa Kuteuliwa , Dr. Asha Rose Migiro akiongozwa na Mpambe wa wa Bunge
na kusindindikizwa na badhi ya wabunge wa CCM kuingia Bungeni ili
kuapishwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda, Mjini Dodoma Desemba 12,
2013.
Mbune
wa Kuteuliwa , Dr. Asha Rose Migiro akiongozwa na Mpambe wa wa Bunge
na kusindindikizwa na badhi ya wabunge wa CCM kuingia Bungeni ili
kuapishwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda, Mjini Dodoma Desemba 12,
2013.
OPRAH WINFREY AELEZEA KWA NINI HANA WATOTO...!!!
Kwenye
taarifa za hivi karibuni za Waandishi wa Hollywood, Oprah amefunguka
juu ya kwa nini hana watoto na ukweli wa juu ya hali hiyo kutohusani na
wanachohisi wengi kwamba hana uwezo wa kushika ujauzito huku akielezea
kwa sababu kuu ni yeye kutaka kuwa mwanamke mwenye nguvu.
"Kama
ningekuwa na watoto, watoto wangu wangenichukia. "Wangeishia kwenye
hali ya kuniongelea kama ilivyo kwenye Oprah show; sababu kuna kitu
katika maisha yangu kingeishia kuteseka na inawezekana kabisa wangekuwa
wao.
Gayle [King, rafiki wa karibu Winfrey ambaye ni mama wa watoto
wawili] alikuwa ni aina ya mtoto ambaye, kwenye daraja la saba la
darasa, alikuwa anaandika jina lake chini na majina ya watoto wake.
Wakati alipokuwa na ndoto hizo za mchana, nilikuwa na ndoto za mchana
juu vipi naweza kuwa Martin Luther King.
BASI LA BURUDANI LAPATA AJALI LEO HII MKOANI TANGA, WATU 12 WAPOTEZA MAISHA NA WENGINE KUJERUHIWA
Basi la Burudani baada ya ajali leo Wilaya ya Handeni, Tanga.
Basi la Burudani leo limepata ajali kijiji cha Kwaluguru Kata ya Kwedizinga wilayani Handeni,
Imeripotiwa mpaka sasa watu zaidi ya 12 wamefariki na majeruhi zaidi ya
55. Watu 4 wamepelekwa MOI na KCMC. Tuwaombee majeruhi.
Hospitali ya wilaya ya Korogwe.
Wednesday, December 11, 2013
Tuesday, December 10, 2013
'BABU SEYA, PAPII LAZIMA WATAACHIWA HURU TU'
NGUZA Mbangu,
mtoto mkubwa wa mwanamuziki mahiri wa muziki wa dansi anayetumikia
kifungo cha maisha jela, Nguza Viking maarufu kama Babu Seya, amesema
mzazi wake pamoja na mdogo wake, Papii, ni lazima wataachiwa huru hivi
karibuni.
Mbangu,
ambaye pia hufahamika kisanii kama Mashine, ambaye hivi sasa ni
mwinjilisti, alitoa kauli hiyo hivi karibuni alipozungumza na gazeti la Uwazi, akisema kuwa kutolewa jela kwa ndugu zake hao, kutawafanya
Watanzania kumsujudia Mungu kupitia tukio hilo.
“Amini
nakuambia, Mungu amenipa maono, Babu Seya na Papii wako huru, watatoka
tu, kinachosubiriwa ni muda tu ambao hauko mbali, ni lazima watatoka kwa
sababu hawana hatia,” alisema Mbangu, ambaye pia alihukumiwa kifungo
cha maisha jela kama mzazi wake, lakini akaachiwa wakati walipokata
rufaa kwa mara ya kwanza mahakamani.
JIONEE PICHA ZAIDI YA 200 ZA IBADA YA KUMUOMBEA MANDELA INAVYOENDELEA IKIWAMO NA MARAIS NA VIONGOZI WALIOWASILI
Sombre occasion: Members of Nelson Mandela's
family take their seats amid heavy rain ahead of his memorial service
at the FNB Stadium in Soweto, near Johannesburg
Respect: Nelson Mandela is shown on a giant
screen inside the stadium as thousands of South Africans and global
dignitaries file into the ground
NORA AFUNGUKA KUHUSU RAY ADAI ALIMTONGOZA. MSIKILIZE HAPA..!!!
Muigizaji wa kike aliyefanya vizuri kupitia kundi la Kaole Sanaa
Group, Nuru Nassoro aka Nora amedai kuwa amekuwa akifanyiwa fitina na
muigizaji mwenzake Vicent Kigosi aka Ray kwa kuwa aliwahi kumtaka
kimapenzi akamkataa.
Nora amefunguka kupitia kipindi cha Filamonata cha 100.5 Times Fm na
kudai kuwa Ray amekuwa akimbania hata kwenye baadhi ya makampuni ambayo
anapeleka kazi zake.
“Mpaka kwenye kampuni ambayo nimepeleka kazi nimeshawahi kusikia
wanasema, wakaniahidi sana mpaka nikawakubalia walichokuwa wanataka wao.
Lakini yeye (Ray) alitanguliza movies zake, akasema ana movie zake
sijui kitu gani..” amelalamika Nora.
Ameeleza kuwa Ray amewahi kumbania kufanya kazi na marehemu Kanumba, na hata Mtitu sababu ikiwa ile ile kumkataa kimapenzi.
WINNIE MANDELA NA GRACA MACHEL WAKUTANA MSIBANI, MARAIS ZAIDI YA 90 KUHUDHURIA MAZISHI.... R.I.P MANDELA
Marais
zaidi ya 90 wa nchi mbalimbali duniani akiwemo Barack Obama wa Marekani
ni miongoni mwa maelfu ya waliojitokeza Johannesburg South Africa
kwenye uwanja wa soka wa FNB leo kumuaga Mzee Mandela anaetarajiwa kuzikwa Jumapili ijayo December 15 2013.
Serikali
ya Afrika Kusini imeimarisha ulinzi kwa kutumia vikosi vyake vya jeshi
vyenye ulinzi wa hali ya juu ambapo sniper team ni miongoni mwa
wanaohusika na ulinzi kwenye eneo lote la kiwanja anakoagiwa Mzee
Mandela huku helicopter pamoja na ndege za kijeshi zikipita angani mara
kwa mara.
ANGALIA PICHA ZA BIRTHDAY PARTY YA NICK MINAJ, BONGE LA KEKI...!!!
First
lady wa label ya YMCMB Nicki Minaj amesherehekea birthday yake ya
kutimiza miaka 31 na mafanikio ya kujivunia kwenye kazi yake ya muziki
ambapo party ilifanyika huko L.A na Restaurant nzima ilibadilika rangi
yake na kuwa ya pink maalum kwa ajili ya party ya Minaj ambayo
ilihudhuriwa na Lil Twist, Safaree boyfriend wa Nicki Minaj na watu
wengine.
YAFAHAMU MAAJABU 10 YA MSIBA WA MANDELA...!!!
RAIS
wa zamani wa Afrika Kusini, Mzee Nelson Mandela, mweusi wa kwanza
kushika wadhifa huo katika taifa lenye uwezo mkubwa kiuchumi na kijeshi
barani Afrika, alifariki dunia Alhamisi iliyopita akiwa nyumbani kwake
jijini Johannesburg.
AIR FORCE ONE KUBEBA MARAIS WATANO WA MAREKANI
AIR Force One ni ndege inayombeba Rais wa Marekani aliye madarakani na kumpeleka popote duniani. Lakini katika hali ya kushangaza, Idara ya Usalama ya Marekani imetoa ruhusa kwa marais wastaafu wakiwa na wake zao, kuandamana na Rais Barak Obama kuhudhuria mazishi ya shujaa huyo wa dunia.
Kifo chake kimeushtua ulimwengu na kwa mara ya kwanza katika
historia, dunia nzima imesimama nyuma ya jemedari huyo, kila mmoja
akionesha masikitiko yake.
Wakati dunia ikisubiri mazishi yake ambayo pia yatavunja rekodi ya
mazishi yote yaliyowahi kufanywa tokea kuumbwa kwa uso wa dunia hapo
Desemba 15 mwaka huu, Uwazi limebaini maajabu kumi yanayoambatana na
msiba huo.
AIR FORCE ONE KUBEBA MARAIS WATANO WA MAREKANI
AIR Force One ni ndege inayombeba Rais wa Marekani aliye madarakani na kumpeleka popote duniani. Lakini katika hali ya kushangaza, Idara ya Usalama ya Marekani imetoa ruhusa kwa marais wastaafu wakiwa na wake zao, kuandamana na Rais Barak Obama kuhudhuria mazishi ya shujaa huyo wa dunia.
Monday, December 09, 2013
JE, UNAJUA KUWA WOGA, AIBU HUPUNGUZA KUJIAMINI KATIKA MAPENZI...??!
KARIBU mpendwa wa blog yetu ya Jambo Tz inayopendwa na wengi na kuwashukuru wote wanaotumia muda wao kutupongeza wengine kutukosoa ili kuiboresha blog yetu.
Vilevile
wapo walio na matatizo wanaoomba msaada ambao nashukuru umewasaidia wengi.
Kama ilivyo ada, umekaa mkao wa kula kutaka
kujua leo nimekuja na mpya gani. Nasema hakuna jipya chini ya jua kwa sababu
kitu mapenzi kilikuwapo tangu enzi ya mababu na hata hao waliyakuta tokea enzi
ya Adamu na Eva.
Tumepata malalamiko mengi kutoka kwa wasomaji wetu waliolalamika juu ya matatizo wanayokumbana nayo katika kula chakula cha roho, wengi wanalalamika kuwa hawali chakula kilichokamilika.
Kwa mfano mtu anauliza; Mbona mpenzi wangu si mtaalam wa mambo flani?, wengine hudiriki kusema tangu waanze mapenzi na waume zao au wake zao hawajafurahia mapenzi na kushangaa kusikia mapenzi yakikukolea hukufanya upandishe mashetani na kumaliza maneno yote mdomoni au kumfanya mwanaume atoe ahadi ambazo hana hata uwezo nazo kwa kusema atakununulia ndege wakati hata baiskeli hana.
Tumepata malalamiko mengi kutoka kwa wasomaji wetu waliolalamika juu ya matatizo wanayokumbana nayo katika kula chakula cha roho, wengi wanalalamika kuwa hawali chakula kilichokamilika.
Kwa mfano mtu anauliza; Mbona mpenzi wangu si mtaalam wa mambo flani?, wengine hudiriki kusema tangu waanze mapenzi na waume zao au wake zao hawajafurahia mapenzi na kushangaa kusikia mapenzi yakikukolea hukufanya upandishe mashetani na kumaliza maneno yote mdomoni au kumfanya mwanaume atoe ahadi ambazo hana hata uwezo nazo kwa kusema atakununulia ndege wakati hata baiskeli hana.
Yote hayo ni
mtu kuguswa pale panapomfanya ajione yupo dunia nyingine na kujiona juu hayupo
wala chini hayupo. Wao hujiuliza kulikoni wenzao wafaidi wao wasifaidi kwani
wamekosa nini.
Swadakta
swali zuri sana,
kumekuwa na utamaduni wa watu wengi kuona aibu kuuliza jambo walisilolijua hasa
katika mapenzi hii imepelekea watu kuwa wavivu kujifunza kwa kuona aibu kuuliza
kitu wasichokijua kwa kuogopa kuitwa washamba.
Nani alikuambia wote wamezaliwa wanajua, usichokijua uliza usisubiri aibu ikukute kwa mpenzio, kuuliza nje au kutoa nje udhaifu wako. Siku zote wasiojua huwa wajanja sana ili kuficha udhaifu wao lakini unauficha udhaifu wako wakati lazima uingie kwenye gemu.
Nani alikuambia wote wamezaliwa wanajua, usichokijua uliza usisubiri aibu ikukute kwa mpenzio, kuuliza nje au kutoa nje udhaifu wako. Siku zote wasiojua huwa wajanja sana ili kuficha udhaifu wao lakini unauficha udhaifu wako wakati lazima uingie kwenye gemu.
MARAIS KUINGIA KWA KADI MAZISHI YA MANDELA...!!!
Sunday, December 08, 2013
Saturday, December 07, 2013
PICHA ZAIDI ZA MUONEKANO WA NDANI NA WA NJE WA BASI LIENDALO KASI
Subscribe to:
Posts (Atom)