Wednesday, March 28, 2018

VIWANJA VYA NDEGE 10 BORA HIVI HAPA

Tovuti ya utafiti wa anga ya Skytrax ya nchini Uingereza imetoa orodha ya viwanja vya ndege bora duniani ambapo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Singapore Changi umeshika nafasi ya kwanza.



Orodha ya viwanja 10 vinavyoongoza kwa ubora ni;
1. Singapore Changi Airport
2. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Incheon (Seoul, Korea Kusini)
3. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Tokyo Haneda)
4. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hong Kong
5. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hamad (Doha, Qatar)
6. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Munich (Ujerumani)
7. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Chubu Centrair Nagoya (Japan)
8. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa London Heathrow
9. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zurich (Switzerland)
10. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Frankfurt (Ujerumani)

JESUS AWAFUTA MACHOZI BRAZIL

Timu ya taifa ya Ujerumani walishindwa kwa mara ya kwanza katika mechi 23 baada ya mshambuliaji wa Manchester City Gabriel Jesus kuwafungia Brazil bao moja na kuwapa ushindi wa 1-0 jijini Berlin.

Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa mataifa hayo mawili kukutana uwanjani tangu Ujerumani walipowaaibisha Brazil 7-1 katika nusu fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2014 mjini Belo Horizonte.
Jesus aliwaweka Brazil mbele kwa mpira wa kichwa dakika za mwishi mwisho kipindi cha kwanza, dakika ya 37.

ARGENTINA WACHEZEA KICHAPO KITAKATIFU TOKA KWA UHISPANIA

Katika mchezo uliochezwa jana Mjini Madrid, Isco alifunga mabao matatu na kuwasaidia Uhispania kupata ushindi mnono wa 6-1 dhidi ya Argentina ambao walifika fainali Kombe la Dunia 2014.

Uhispania waliongoza 2-0 baada ya Diego Costa kumbwaga Sergio Romero kisha Isco akafunga bao lake la kwanza.

Tuesday, March 27, 2018

MAAJABU: JENEZA LAKUTWA NJE YA GETI LA NYUMBA

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Nelson Edson mkazi wa eneo la Nsalaga Uyole Jiji la Mbeya amestaajabu baada ya kuamka na kukuta jeneza nje ya geti la nyumba yake lililowekwa na watu wasiojulikana.

Kwa mjibu wa mwenyekiti wa mtaa huo Paulo Ngonde amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia siku ya leo March 27, 2018 ambapo alipigiwa simu na mjumbe wa mtaa huo juu ya uwepo wa tukio la jeneza kukutwa nje ya nyumba ya Nelson Edson.
Aidha Mwenyekiti Ngonde ameongeza kuwa katika mtaa wake kumekuwa na matukio mbalimbali ikiwa ni pamoja na matukio ya utupaji watoto lakini hili la kukutwa kwa jeneza nyumbani kwa mtu ni la kwanza.

WATU WANNE WAKAMATWA WAKIHUJUMU MIUNDOBINU YA TANESCO MKOANI MBEYA

Meneja wa TANESCO Mbeya akiongea na waandishi wa habari pembeni ni Kamanda wa polisi mkoani Mbeya DCP Mohammed Mpinga.

 Polisi Mkoani Mbeya wamefanikiwa kuwakamata watu wanne kwa tuhuma za kuingilia miundombinu ya shirika la umeme nchini (TANESCO).

Akiongea na waandishi wa habari leo kamanda wa polisi mkoani humo DCP Mohammed Mpinga amesema jeshi hilo kwa kushirikiana na maafisa wa Tanesco march 23, mwaka huu walifanya Oparesheni katika maeneo ya vijiji vya Isebe na Isajilo vilivyopo Wilaya ya Rungwe kufuatia taarifa za siri kutoka kwa raia wema kuwa kuna watu wanaingilia miundombinu ya Tanesco katika vijiji vyao pamoja na kufanya wizi wa nguzo za umeme na kuwaunganishia umeme wakazi wa maeneo hayo kinyume cha sheria. 
Watuhumiwa wa uhujumu miundombinu ya TANESCO wakiwa chini ya ulinzi wa jeshi la polisi.


Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Idd Hamis Mwambusye Mkazi wa Bagamoyo, Benard Kibondi Mkazi wa Kikota, Thobias Wilfred, Mkazi wa Iponjola, Eng. Geofrey Msunga Mkazi wa Mbeya.

Kamanda Mpinga amesema miongoni mwa watuhumiwa hao baada ya kukamatwa na kupekuliwa majumbani kwao walikutwa na vifaa mbalimbali vya umeme ikiwa ni pamoja na Mita za umeme 27, nyanya za umeme mkubwa na ndogo, nguzo 57 za umeme ambazo walikuwa zikitumika kuwaunganishia umeme wananchi pamoja na vifaa vingine.

Watuhumiwa watafikishwa Mahakamani mara tu baada ya upelelezi kukamilika. Pia ameelez kuwa jeshi hilo litaendelea na msako mkali kuwasaka watuhumiwa wengine wanaojihusisha na uhujumu wa miundombinu ya Shirika la Umeme  TANESCO katika maeneo mbalimbali.

MKUU WA MKOA APIGA MARUFUKU KUPIGA YOWE

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima, amepiga marufuku utaratibu wa wananchi wa vijiji vitatu vya Remng’orori, Mikomarilo na Sirorisimba vilivyoko katika wilaya za Bunda, Serengeti na Butiama vinavyogambania mipaka ya wilaya zao, kupiga yowe pale inapotokea kuwapo na jambo la hatari.
Marufuku hiyo imekwenda sambamba na katazo la kuzuia shughuli zozote zikiwamo za kilimo eneo linalogombaniwa, kutotumiwa na pande zote hadi hapo Serikali itakapoamua vinginevyo, ikiwa ni njia pekee ya kuzuia athari zitakazoweza kutokea.
Malima amewataka wananchi wa vijiji hivyo kutoa taarifa Jeshi la Polisi pale linapotokea jambo la kiuhalifu au linalohatarisha usalama wao, kuliko kujichukulia sheria mkononi na kusababisha uvunjifu wa amani.

MBOWE NA VIGOGO WENGINE WA CHADEMA WASWEKWA RUMANDE

Viongozi sita wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), akiwamo Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe wamefutiwa dhamana na kuwekwa mahabusu katika Kituo Kikuu cha Polisi (Central), jijini Dar es Salaam.
Pamoja na Mbowe, viongozi wengien ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Vincent Mashinji, Naibu Katibu Mkuu Bara, John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko.
Viongozi hao wameripoti kituoni hapo leo Jumanne Machi 27, saa tatu asubuhi ikiwa ni mwendelezo wa kuitikia wito wa polisi ambao wamekuwa wakiwahoji kwa madai ya kufanya mkusanyiko usio halali Februari 16, mwaka huu.
Wakili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Fredrick Kihwelo wamefutiwa dhamana kwa sababu baadhi ya viongozi walikuwa wanakaidi kuripoti polisi kila wanapotakiwa kufanya hivyo huku Msigwa akiongezwa katika orodha ya viongozi hao baada ya kuhojiwa jana na kupewa dhamana ambayo pia leo imefutwa.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE MARCH 27, 2018 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


      
Tunapenda kuwataarifu wadau wetu kuwa hivi karibuni tutapatikana kwa website ya jambotz.co.tz

MABALOZI WA URUSI WAFUKUZWA KATIKA NCHI MBALIMBALI

Australia imekuwa nchi ya karibuni kufukuza wanadiplomasia wa Urusi kutoka nchini kwake kutokana na shambulio la jasusi wa zamani wa urusi nchini Uingereza Sergei Skripal na binti yake ambao wako katika hali mbaya kiafya.
Waziri mkuu Malcolm Turnbull amesema uamuzi huo unatokana na shambulio hatari la kutumia kemikali za neva zinazotengezwa na Urusi na zilitomiwa mara mwisho vita vya pili vya dunia.
Idadi ya wanadiplomasia wa Urusi wanaofukuzwa inazidi kuongezeka, na hii ndio idadi kubwa kuwahi kutokea katika historia. Zaidi ya nchi 20 zimeungana na umoja wa Ulaya kuwafukuza zaidi ya wanadiplomasia 100.

URENO YA CRISTIANO RONALDO WAPIGWA 3-0 NA UHOLANZI

Cristiano Ronaldo
Haki miliki ya ja

Mabingwa wa Ulaya Ureno walipokezwa kichapo cha kushangaza na Uholanzi katika mechi ya kimataifa ya kirafiki iliyochezewa mjini Geneva, Uswizi.
Winga wa zamani wa Manchester United Memphis Depay na mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Ryan Babel waliwaweka Waholanzi 2-0 mbele.

Beki wa Uholanzi Virgil van Dijk, ambaye majuzi alitawazwa nahodha mpya wa timu hiyo, alifunga la tatu.

BRAZIL KULIPIZA KICHAPO CHA 7-1 AU KUAIBISHWA TENA?!

Brazil full-back MarceloHaki miliki ya pichaJambo tz
Mkufunzi wa Brazil Tite amesema timu yake bado inatatizwa na "mizimu" ya kipigo cha 7-1 ambacho walipokezwa na Ujerumani katika nusu fainali ya Kombe la Dunia miaka minne iliyopita.
Mataifa hayo mawili yatakutana tena mara ya kwanza Jumanne mjini Berlin tangu Brazil walipoaibishwa kwao nyumbani wakati wa michuano hiyo ya Kombe la Dunia.
"Hii ina maana kubwa sana kisaikolojia hakuna anayehitaji kujidanganya kuhusu hilo," Titea aliambia jarida la Kicker.

Monday, March 26, 2018

MAGUFULI AZINDUA MAGARI 181 YA BOHARI KUU YA DAWA (MSD)

Rais Magufuli akiwasili Bohari kuu ya Madawa (MSD) Jijini Dar es salaam kabla ya kuzindua magari  181, Pamoja naye ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu,Mwakilishi wa Taasisi ya Global Fund Bw. Linden Morrison na viongozi wengine.Machi 26,2018.
  

SIMBA NA YANGA KUKUTANA TAREHE HII HAPA

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kupitia Mtendaji Mkuu, Boniface Wambura leo imetangaza rasmi tarehe ambayo Watani wa Jadi (Simba SC na Yanga SC) watakutana kucheza mechi yao ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

  Wambura amesema timu hizo sasa zitacheza tarehe 29 Aprili 2018 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mechi ambayo Simba atakuwa mwenyeji wa pambano hilo. Awali Bodi ya Ligi ilikuwa haijaweka tarehe hiyo wazi kutokana na mambo mbalimbali kuingiliana na kufanya ratiba ya mchezo huo kutopangwa kwa wakati.

Timu hizi zenye wafuasi wengi nchini, zilikutana Oktoba 28 2017 kwenye mzunguko wa kwanza wa ligi na kwenda sare ya bao 1-1, huku wafungaji wa mabao hayo wakiwa ni Shiza Kichuya upande wa Simba na Obrey Chirwa kwa Yanga.

Pamoja na michezo mingine mbalimbali ambayo leo imetolewa ratiba yake rasmi, klabu ya Simba imepangwa kucheza;

Njombe Mji FC Vs Simba April 3
Mtibwa vs Simba Aprili 9
Lipuli FC vs Simba Aprili 20
Simba vs Yanga Aprili 29

NONDO AACHIWA HURU KWA DHAMANA

Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa leo Jumatatu, Machi 26, imemuachia Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania(TSNP), Abdul Nondo kwa dhamana ya Sh. 5 milioni na mali isiyohamishika.

Nondo amepewa dhamana hiyo mbele ya Hakimu mkazi mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa, John Mpitanjia anayeendesha kesi hiyo baada ya mtuhumiwa kukamilisha taratibu zote za dhamana.

Wiki iliyopita, Nondo alinyimwa dhamana baada ya upande wa Jamhuri kudai kuwa ni kwa sababu za usalama wake.

Sunday, March 25, 2018

HUU HAPA WARAKA WA MAASKOFU WA KKKT

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia waumini huku akisikilizwa na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex Malasusa na Mchungaji Chalres Mzinga baada ya Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam Machi 27, 2016 (Picha na maktaba)

"Fumbua Kinywa chako kwa ajili yake aliye bubu; Uwatetee watu wote walioachwa peke yao; Fumbua kinywa chako, uhukumu kwa haki; uwapatie maskini na wahitaji haki yao" (Mithali 31: 8-9)

Tunapoadhimisha sikukuu ya kukumbuka kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo, tunatambua kuwa utume wa Kanisa letu katika taifa letu, unafanyika katikati ya changamoto kadhaa. Kwa kuwa Kanisa ni sehemu ya jamii, linaguswa na changamoto hizo.

Katika kukaa pamoja na kuliombea taifa letu, sisi maaskofu wa KKKT, tumetafakari na kubaini changamoto hizo. Kwa njia ya salaam za Pasaka, tunaleta kwenu changamoto tatu ili ziongeze mzigo wa kuliombea taifa letu na viongozi wake.

1. Jamii na Uchumi:

Kiini cha Utume wetu katika jamii kinatuingiza kwa nia njema katika maisha ya uchumi na mshikamano wa kijamii. Neno la Mungu linatufundisha kuwa "Mwanadamu hawezi kuishi kwa mkate peke yake" (Luka 4:4).

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...