Thursday, January 01, 2015

PAPA AKEMEA UFISADI MWAKA MPYA

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis 
 
Papa Francis ametumia sherehe za kuupokea mwaka wa 2015 kuzungumzia tatizo la rushwa katika mji wa nyumbani wa Rome nchini Italia.
Akizungumza katika Kanisa kuu la St. Peter Basilica, papa amesema rushwa ni shumbulizi dhidi ya maskini na wasiokuwa na uwezo ambapo ametaka mabadiliko ya kiroho na kimaadili katika mji huo.
Papa ambaye ndiye Askofu wa Rome amefanya utetezi dhidi ya maskini kama nguzo muhimu katika uongozi wake wa upapa.
Maafisa wa polisi kwa sasa wanawachunguza maafisa wa Roma wanaotuhumiwa kujihusisha na kundi la Mafia na ufisadi dhidi ya fedha za umma zikiwemo zilizotengwa kwa ajili ya kituo wahamiaji. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MWAKA MPYA MAAAFA CHINA WATU 35 WAFARIKI

Umati wa watu waliokanyagana na wengine kufa nchini China wakati wakiupokea mwaka mpya 2015 
 
Sherehe za kuupokea mwaka mpya 2015 zimeguka kuwa majonzi baada ya watu thelathini na watano kufa kwenye taharuki ya kukanyagana kwenye msongamano wakati wakiiupokea mwaka mpya.
Maafa hayo yametokea katika mji Shanghai ambapo maelfu ya watu walikuwa wamekusanyika ili kuupokea mwaka mpya.
Chanzo cha taharuki hiyo bado haijafamika lakini vyombo vya habari vya nchi hiyo vimenukuliwa vikisema imetokana na maelfu ya watu kuzuiwa kugombea fedha bandia zilizotupwa eneo hilo kutoka katika jengo moja. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KANO WAPOKEA MWAKA MPYA MARA YA KWANZA

 
Mwaka mpya 2015 ulivyopokelewa Hong Kong
 
Mwaka mpya wa 2015 umepokewa kwa kishindo katika maeneo mbali mbali duniani na barani Afrika.
Nchini Nigeria kumekuwa shamra shamra ambapo kwa mara ya kwanza mafataki yalirushwa katika eneo la kaskazini mwa nchi hiyo lenye waislamu wengi.
Shamra shamra hizo zimefanyika katika kituo cha michezo katika mji wa Kano ambapo waliohudhuria ni wale waliopata mwaliko pekee.
Habari zinasema kumekuwa na mwitikio mkubwa ambapo umati wa watu ulihudhuria shamra shamra hizo jambo lililowapa wakati mgumu maafisa usalama kuudhibiti umati huo.
Waandaji wa shamra shamra hizo za maonyesho ya kulipua mafataki hayo wanasema wanataka jimbo la Kano kuungana na miji mingine mikubwa duniani kusherehekea siku kuu ya Mwaka Mpya.
Ulinzi mkali uliimarishwa kwa tahadhari ya shambulio lolote kutoka kundi la wapiganaji wa kiislamu la Boko Haram.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Na BBC

RATIBA YA LIGI KUU ENGLAND LEO, MAN U, ARSENAL, CHELSEA MZIGONI

Chelsea+v+Manchester+United+Premier+League+SSB1R4Q96Y8l
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
EnglandPremier League
15:45 Stoke City ? – ? Manchester United
18:00 Aston Villa ? – ? Crystal Palace
18:00 Hull City ? – ? Everton
18:00 Liverpool ? – ? Leicester City
18:00 Manchester City ? – ? Sunderland
18:00 Newcastle United ? – ? Burnley
18:00 Queens Park Rangers ? – ? Swansea City
18:00 Southampton ? – ? Arsenal
18:00 West Ham United ? – ? West Bromwich Albion
20:30 Tottenham Hotspur ? – ? Chelsea 

KOMBE LA MAPINDUZI KUANZA KUTIMUA VUMBI LEO

MICHUANO ya Kombe la Mapinduzi inaanza kutimua vumbi leo Visiwani Zanzibar ambapo Simba itacheza na Mtibwa Sugar, na mabingwa watetezi, Azam watacheza na KCCA ya Uganda Ijumaa kwenye Uwanja wa Amaan.
Mashindano hayo ni maalumu kwa ajili ya kuadhimisha siku ya Mapinduzi ya Zanzibar yanashirikisha timu mbalimbali kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na Kati ambazo ni KCCA, Sports Club Villa zote kutoka Uganda, El Merreikh ya Sudan, Ulinzi ya Kenya, Azam, Simba na Yanga zote kutoka Tanzania Bara na Shaba, JKU, Mtendeni, Mafunzo na KMKM kutoka Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa waandaaji wa mashindano hayo ambao ni Chama cha Soka cha Zanzibar (ZFA) zilisema kwamba baadhi ya timu zimeshawasili kwa ajili ya mashindano hayo.
Michuano ya mwaka huu inatarajia kuwa na ushindani mkali kutokana na kushirikisha timu nyingi kubwa na zinazofahamiana kutoka ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WILFIED BONY AWINDWA NA MAN CITY

24457D2A00000578-0-image-a-54_1420058218252
Wilfried Bony anawindwa na Manchester City 
 
Manchester City wameanza mazungumzo ya kumsajili mshambuliaji wa Swansea City, Wilfried Bony kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 25.
Mwenyekiti wa Swansea,  Huw Jenkins  alisema jana kuwa klabu yake haijapokea ofa yoyote mpaka sasa, lakini City wameshafungua mazungumzo ili kumnasa Muivory Coast huyo ambaye pia anawaniwa na Real Madrid.
Mazungumzo yalifanyika na washauri wa Bony jana usiku.
Wiki ijayo Bony ataenda Abu Dhabi ambapo Ivory Coast imeweka kambi ya kujiandaa na michuano ya mataifa ya Afrika mwaka huu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Wednesday, December 31, 2014

CCM KUTUMIA PANGA LA 2005

 
Vigezo 13 vilivyowekwa na CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2005 kumpima mwanachama anayefaa kugombea urais, ndivyo vitakavyotumika kuwaengua makada wanaoendelea kujitokeza kuwania nafasi hiyo mwakani, imefahamika.
Vigezo hivyo vinaonekana kuwa kizingiti kwa baadhi ya makada wa chama hicho ambao tayari wametangaza na wengine wanaotajwa kutaka nafasi hiyo ya juu nchini, ukiachilia mbali mnyukano unaotarajiwa kutoka vyama vya upinzani vinavyoonekana kupata nguvu.
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula amelithibitishia gazeti hili kwamba, “Sifa hizo 13 zilizotumika mwaka 2005 na 2010 ndizo zitakazotumika pia mwaka 2015 na wala hakutakuwa na maboresho wala nyongeza ya aina yoyote.”
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

ASKOFU MKUDE AASA VIONGOZI KUWA WAADILIFU

ASKOFU Telesphor Mkude wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro
 Askofu Telesphor Mkude wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro

WATUMISHI wa umma wa ngazi mbalimbali waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi wameombwa kuzisoma na kusikiliza kwa umakini hotuba mbalimbali za Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ili ziwaweke kwenye msingi wa kuwa na maadili mema, uadilifu na uwazi.
Changamoto hiyo imetolewa na Askofu Telesphor Mkude wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro, hivi karibuni wakati akizungumza na gazeti hili kwenye ofisi ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Patrice, mjini Morogoro.
Akijikita katika suala la maadili ya viongozi wa umma, Askofu Mkude, alisema suala la kufuata maadili, kuonesha uadilifu na uwazi katika uwajibikaji wa kuwatumikia wananchi ni sifa kuu ya kiongozi yoyote yule.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO DESEMBA 31, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

RAIS JAMMEH "BADO NIPO MADALAKANI"

Rais wa Gambia Yahya Jammeh 
 
Rais wa Gambia amesema kuwa bado analiongoza taifa hilo la Afrika magharibi baada ya vikosi vyake vya usalama kutibua jaribio la mapinduzi.
Yahya Jammeh amesema kuwa kamanda mmoja wa jeshi wa zamani alijaribu kuchukua udhibiti wa taifa hilo alipokuwa ziarani Ufaransa.
Hatahivyo hajulikani aliko.Milio mikali ya riasi ilizuka karibu na makao ya rais katika mji mkuu.
Bwana Jammeh alichukua mamlaka kupitia mapinduzi mwaka 1994 na wapinzani wake wamekuwa wakimkosoa kwa uongozi wake wa kiimla.
Duru za kidiplomasia na zile za kijeshi zinasema kuwa wanajeshi kutoka kwa jeshi la ulinzi wa rais wanadaiwa kufanya shambulizi hilo katika makao ya rais mjini Banjul mapema siku ya jummane.
Serikali imekana kwamba kulikuwa na jaribio la mapinduzi katika taarifa iliotangazwa katika radio ya taifa.
Hatahivyo,bwana Jammeh baadaye alikiri kuhusu shambulizi hilo na kusema kuwa wanajeshi waaminifu wa Lamin Sanneh aliyemtaja kama mwenye aibu walivamia mji mkuu wa Gambia kutoka Senegal katika jaribio la kutaka kuipindua serikali yake.
Amesema kuwa wavamizi hao hatahivyo walikabiliwa na vikosi vya usalama na kuwaua wanne kati yao huku wengine wanne zaidi wakikamatwa. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

RAIS MPYA WA TUNISIA KUAPISHWA

Rais mteule Beji Caid Essebsi kuapishwa kama rais mpya wa Tunisia baada ya kuibuka mshindi katika uchaguzi wa urais nchini Tunisia 
 
Rais mteule wa Tunisia Beji Caid Essebsi anatarajiwa kuapishwa baada ya kushinda uchaguzi wa kwanza uliokuwa huru nchini humo. Alimshinda rais aliyekuwa mamlakani Moncef Marzouk. Ushindi wake unaaminisha kwamba Tunisia ndilo taifa ambalo limejinasua kutoka utawala wa kiimla hadi ule wa kidemokrasia.
Siku ya jumatatu,tume ya uchaguzi ilithibitisha kuwa bwana Essebsi alishinda kura ya raundi ya pili dhidi ya Marzouk. Rais huye mteule ataapishwa katika bunge la wawakilishi wapwa ambapo chama chake Nidaa Tounes kimepata wabunge wengi.
Raia wa Tunisia wakisherehekea ushindi wa Caid Essebsi
Tayari maandalizi ya kumuapisha yamekamilika mjini Tunis.
Hatua hiyo hiyo itafikisha tamati mvutano wa demokrasia wa miaka minne ya ghasia zilizoghubika taifa hilo zilizopeleekea kung'olewa kwa utawala wa Rais Zine el-Abedine Ben Ali.
Bwana Essebsi alihudumu katika utawala wa Ben Ali, pamoja na uongozi wa rais wa zamani Habib Bourguiba. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

BOKO HARAM WAVAMIA KIJIJI NA KUUA WATU 15

Wapiganaji wanaodhaniwa kuwa ni Boko Haram wamevamia kijiji Kaskazini mashariki mwa Nigeria na kuua watu takriban 15.
Shambulizi hilo lilitokea katika kijiji cha Kautikari katika jimbo la Borno, pale washukiwa wa Boko Haram walipowasili kijijini humo kwa magari yenye silaha, wakilenga askari wa ulinzi wa jadi wa mji huo.
Kijiji hicho kipo karibu na Chibok mahali ambapo kundi la Boko Haram, liliwateka nyara wasichana wa shule zaidi ya mia mbili mwezi Aprili mwaka huu.
Zaidi ya watu elfu kumi wameuwawa Nchini Nigeria na Boko Haram mwaka huu pekee. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

YANGA, SIMBA, AZAM KUUMANA KOMBE LA MAPINDUZI

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeahirisha mechi za raundi ya tisa na kumi za timu nne zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara na kuziruhusu kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi inayotarajiwa kuanza kesho hadi Januari 13, 2015 Zanzibar.

Timu za Tanzania bara zitakazoshiriki ni mabingwa watetezi Azam FC, Simba, Yanga na Mtibwa Sugar.
Awali, kabla ya TFF kushindwa kuthibitishiwa uwepo wa mashindano hayo kutokana na viongozi wa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) kupelekana mahakamani, timu zilikuwa zikiendelea na mazoezi kwa ajili ya mechi za raundi ya tisa zilizokuwa zifanyike Jumamosi ijayo.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MZUNGU WA SIMBA AMETUA ASUBUHI HII KUMRITHI PHIRI


IMG-20141231-WA0000
KOCHA mpya wa Simba sc, Mserbia Goran Kapunovic amewasili asubuhi ya leo majira ya saa 1:00 katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
Goran ametua kwa ndege ya Shirika la Qatar Airways na baada ya kuwasili amesema amekuja kufanya kazi na sivinginevyo.
Hata hivyo kocha huyo anayerithi mikoba ya Patrick Phiri amesema atazungumza mengi baada ya kumalizana na viongozi na kuanza kazi yake.
Goran anatarajia kuiongoza Simba kwa mara ya kwanza katika mechi za kombe la Mapinduzi linaloanza kutimua vumbi kesho januari mosi mwakani. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

BOSI UEFA AISHAURI FIFA KURUHUSU KADI NYEUPE UWANJANI

Soccer - Michel Platini File Photo

Rais wa UEFA Michel Platini amesisitiza mpango wake wa kuanza matumizi ya ‘Kadi Nyeupe’ itakayowafanya wachezaji watolewe nje kwa muda kisha kurejeshwa baadaye. Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 59 alitoa wazo hilo kwa mara ya kwanza Oktoba lakini likapingwa na Rais wa FIFA Sepp Blatter.
Hata hivyo, Platini ameshikilia msimamo wake katika mkutano wa tisa wa kimataifa wa michezo unaofanyika Dubai.
“Kadi nyeupe ni kitu kipya. Inahusiana na tabia ya wachezaji wa soka. Kujiangusha na kujifanya kuumia, kupinga maamuzi ndani ya uwanja, haya hayakubaliki kwa watu wanaopenda mchezo. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...