Wednesday, December 31, 2014

ASKOFU MKUDE AASA VIONGOZI KUWA WAADILIFU

ASKOFU Telesphor Mkude wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro
 Askofu Telesphor Mkude wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro

WATUMISHI wa umma wa ngazi mbalimbali waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi wameombwa kuzisoma na kusikiliza kwa umakini hotuba mbalimbali za Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ili ziwaweke kwenye msingi wa kuwa na maadili mema, uadilifu na uwazi.
Changamoto hiyo imetolewa na Askofu Telesphor Mkude wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro, hivi karibuni wakati akizungumza na gazeti hili kwenye ofisi ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Patrice, mjini Morogoro.
Akijikita katika suala la maadili ya viongozi wa umma, Askofu Mkude, alisema suala la kufuata maadili, kuonesha uadilifu na uwazi katika uwajibikaji wa kuwatumikia wananchi ni sifa kuu ya kiongozi yoyote yule.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.
 
Askofu Mkude alisema ni muhimu kwa viongozi wetu wakazirejea hotuba mbalimbali za Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, ambaye wakati wa utawala sifa kuu ya kiongozi ilikuwa ni mwonekano wake katika maadili na uzingatiaji wa miiko ya uongozi.
“Nadhani kuna mahali tumeteleza ...viongozi wetu wengi hawatendi majukumu yao kwa kufuata maadili, uadilifu na uwazi na hili ndilo lililotufikisha hapa tulipo...ni budi tukaangalia wapi tulikotoka na tunaelekea wapi ili tujisahihishe,” alisema Askofu Mkude.
Hivyo alisema, Mwalimu Nyerere alilijenga taifa la watu wenye kuwa na uzalendo wa nchi yao na viongozi walioteuliwa ama kuajiriwa kuwa watumishi wa umma walifuata maadili ya utumishi wao tofauti na iliyo sasa.
“ Mwalimu Nyerere alikuwa mwadilifu katika matendo yake …hakujilimbikizia mali na hata watoto wake walikuwa ni sawa na watoto wa watu wa kawaida...na ndiyo maana alikuwa na uwezo wa kukemea maovu na wakosaji wakatii,“ alielezea:
“ ...Mwalimu Nyerere alijenga tabia ya kufuatilia nyendo za viongozi wake na pale alipoona ama kubaini kiongozi wake anakwenda kinyume na utaratibu hakusita kumuita ofisini na kumkanya sambamba na kumwongoza njia nzuri, “ alibainisha Askofu Mkude.
Hivyo alisema, kutokana na misimamo hiyo iliyotokana na uadilifu wake, hotuba zake alizokuwa akizitoa miaka mingi ya nyuma zinaporudiwa kwenye redio ama televisheni, zimekuwa na mvuto na mafunzo ndani yake kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Kwa mujibu wa Askofu huyo, hivyo ni vyema viongozi wa sasa pamoja na kuwa na majukumu mengine ya kikazi, ni jambo jema pia wakajikumbusha kwa kuzisikiliza kwa makini na zinaweza kuwarejesha kwenye mstari wa kuwa waadilifu, wanaofuata maadili mema ya utumishi wa umma na kujenga zana ya uwazi na uwajibikaji katika jamii.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na Habari Leo 

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...