Wednesday, December 31, 2014

YANGA, SIMBA, AZAM KUUMANA KOMBE LA MAPINDUZI

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeahirisha mechi za raundi ya tisa na kumi za timu nne zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara na kuziruhusu kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi inayotarajiwa kuanza kesho hadi Januari 13, 2015 Zanzibar.

Timu za Tanzania bara zitakazoshiriki ni mabingwa watetezi Azam FC, Simba, Yanga na Mtibwa Sugar.
Awali, kabla ya TFF kushindwa kuthibitishiwa uwepo wa mashindano hayo kutokana na viongozi wa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) kupelekana mahakamani, timu zilikuwa zikiendelea na mazoezi kwa ajili ya mechi za raundi ya tisa zilizokuwa zifanyike Jumamosi ijayo.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.
Akizungumza jana Katibu Mkuu wa ZFA, Kassim Salum alisema kesi iliyokuwa ikiwakabili imekwishaondolewa mahakamani na mashindano yataendelea kama yalivyopangwa.
“Maandalizi yanakwenda vizuri na timu zitaanza kwenda Zanzibar kuanzia kesho (leo) ambapo ni Simba na KCCA za Uganda itafika kesho asubuhi(leo asubuhi),” alisema.
Timu nyingine zinazotarajiwa kushiriki kwenye michuano hiyo mabingwa wa Zanzibar KMKM, Police FC, JKU, Mtende Rangers na Shaba FC wakati za kigeni ni El Merreikh ya Sudan, Ulinzi Kenya na mabingwa wa kombe hilo KCCA.
Alisema wamekuwa wakichagua timu ambazo ni kubwa na zenye mashabiki wengi Zanzibar ili mchezo kuwa na msisimko na wenye kuvutia. Alitaja zawadi kuwa mshindi wa kwanza ataondoka na Sh milioni 10 na wa pili Sh milioni tano.
Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, Boniface Wambura alisema kutokana na michuano hiyo ya Mapinduzi, timu hizo za Tanzania zitalazimika kucheza mechi za Ligi katikati ya wiki baada ya kumaliza michuano hiyo.
Hii itakuwa ni mara ya tisa kufanyika kwa michuano hiyo tangu ianzishwe kuenzi Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofanyika Januari 12, 1964. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...