Mwenyekiti wa Chadema,
Freeman Mbowe amefanya mkutano mkubwa Urambo Mashariki na kumshutumu
Mbunge wa jimbo hilo, Samuel Sitta kwa kuchakachua maoni ya wananchi
katika mchakato wa Katiba Mpya.
Katika mkutano huo ulifanyika katika Uwanja wa
Extended mjini hapa takriban mita 100 kutoka nyumbani kwa Sitta
aliyeongoza Bunge la Katiba, Mbowe alisema historia ya nchi hii
itamhukumu mbunge huyo kwa maovu hayo.
Alisema kutokana na uovu huo wa Sitta ambaye
amekuwa akiisifia Katiba Inayopendekezwa kuwa itakuwa nzuri Afrika
Mashariki na Kati, vyama vya upinzani vitaendelea kuidai katiba ya
wananchi hata kwa miaka 100 ijayo. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz