Thursday, November 06, 2014

MAKONDA: "VURUGU ZILIZIMA NDOTO ZANGU"



Katibu wa Uhamasishaji Umoja wa Vijana wa CCM, Paul Makonda akizungumza na waandishi wa gazeti la Mwananchi alipotembelea makao makuu ya Mwananchi Communications Limited, Tabata jijini Dar es Salaam jana. 

Katibu wa Hamasa wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Paul Makonda amesema alitamani kuzungumza siku ya mdahalo ulioandaliwa na Kigoda cha Mwalimu Nyerere Foundation lakini vurugu zikazima ndoto yake.

Makonda ambaye anatuhumiwa kuwa ndiye aliyepanga vurugu hizo zilizosababisha aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji mstaafu Joseph Warioba kushambuliwa, alikana na kudai kuwa hata yeye alitamani kukisikia kile kilichopangwa kuzungumzwa na wasemaji wakuu wa mdahalo huo ili ajibu hoja zao katika mkutano huo.

Akizungumza jana katika ofisi za gazeti hili, Makonda alisema aliingia ukumbini akiwa na nakala ya Katiba Inayopendekezwa kwa madai kuwa ingeweza kumsaidia kuainisha yale ambayo yangejadiliwa na ikibidi achangie hoja kwa kutetea au kutoa ufafanuzi wa kile kilichoandikwa ndani ya Katiba hiyo.

“Nasikitika kwa sababu malengo yangu hayakutimia kutokana na vurugu zile. Lengo langu lilikuwa; nipate nafasi ya kuzungumza ili nitoe hoja zangu na kufafanua uzuri wa Katiba Inayopendekezwa,” alisema.

Hata hivyo, alisema yaliyosemwa na Jaji Warioba kabla ya mdahalo kuvunjika, yalimpa fursa ya kujua ni vifungu vipi vina kasoro na vipi viko sahihi. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

“Kwa maelezo ya Jaji Warioba, asilimia 90 ya maoni yaliyokuwamo katika Rasimu waliyoipendekeza ndiyo yaliyomo katika Katiba hii Inayopendekezwa,” alisema Makonda.

Tuhuma zinazomwandama

Kada huyo wa CCM, akizungumzia tuhuma kuwa alishiriki kumpiga Jaji Warioba, alisema kamwe hawezi kufanya kitu kama hicho na hakuna mtu yeyote anayeweza kuthubutu kumpiga mzee huyo.

Alisema tuhuma zinazozidi kumwandama sasa ni mwendelezo wa zile zilizokuwa zikiwatuhumu awali, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Bara ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba.

“Mimi ni kama napokea kijiti kutoka kwa hawa watangulizi wangu, walishatuhumiwa sana kuwa walikuwa wakitumwa kuanzisha vurugu na mambo mengine mengi, lakini hakuna hata mtu mmoja aliyethibitisha hili, binafsi naona huu ni mchezo tu wa kisiasa wa watu kutaka kutafuta huruma kutoka kwa watu wengine,” alisema Makonda.

Alisema hata malumbano yanayoendelea hivi sasa kuhusiana na Katiba hiyo mpya, hayaihusu Tume ya Warioba bali ni baina ya vyama vya siasa vinavyotaka kujitafutia umaarufu kila kimoja kwa mtindo wake.

Alipoulizwa ni kwa nini UVCCM iliamua kutoa tamko linaloashiria kuanza kwa mapambano ya kuhakikisha Katiba hiyo inapita kwa kupigiwa kura ya ndiyo na Watanzania wote, Makonda alisema: “Mimi kama msemaji wa UVCCM, hatukuwahi kutoa tamko kama hilo, hii ni propaganda tu ya wapinzani wetu.” Makonda alisema daima huwa anaamini katika ukweli na siku zote hupenda kusimamia kile anachokiona kina masilahi kwa umma wa Watanzania.
Alisema kutokana na msimamo huo, ndio unaomfanya apakaziwe mabaya ili aonekana hafai mbele ya jamii. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
“Tanzania hii ya leo kuna watu wako kwa ajili ya kutengeneza matukio halafu wao wanakaa kando... Binafsi sikumpiga Jaji Warioba na sitathubutu kufanya hivyo.
“Mimi ninahusika kujenga hoja zenye masilahi kwa umma na siko kwa ajili ya kujenga hoja za kubomoa, ninajenga hoja za kulinda na kutetea amani ya nchi na si kuivuruga,” alisema Makonda.
Alisema msimamo huo ndiyo uliosukuma pia kwenda kuhudhuria mdahalo ule kwa lengo la kusikiliza kile ambacho kingejadiliwa na kama usingevunjika, alipenda kuchangia hoja ambazo alikuwa ameziainisha wakati Jaji Warioba alipokuwa akizungumza na kile alichokizungumza Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku.
“Nilitaka kufanya hivyo kwasababu pia mimi ni mwanasiasa na ni miongoni mwa wajumbe tulioandika hii Katiba Inayopendekezwa,” alisema Makonda.
Alisema hajisikii vizuri kubambikiziwa kosa ambalo hakulifanya na hatarajii kulifanya.
“Kama Jaji Warioba amekana kuwa hakupigwa katika vurugu hizo zinazodaiwa kuwa mimi na vijana wangu 23 tulizianzisha, sasa ni Warioba yupi aliyepigwa na Makonda?” alihoji kada huyo wa Chama cha Mapinduzi. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...