Thursday, November 06, 2014

BADO HAKIJAELEWEKA SIMBA


 
Wachezaji wa Simba wakifanya mazoezi kwenye Ufukwe wa Coco kujiandaa na mchezo dhidi ya Ruvu Shooting juzi jijini Dar es Salaam.

Ni presha kila kona Simba. Ndivyo unavyoweza kusema wakati kamati ya utendaji ya klabu hiyo ikikutana leo, kocha Patrick Phiri ameanza upya kuwanoa wachezaji kwa kuwapeleka ufukweni ili kujenga stamina.
Dharura hiyo ya kikao cha kamati ya utendaji inaonyesha hali si shwari ndani ya Simba, jambo linalowafanya viongozi wahangaike ili kuhakikisha timu inapata matokeo mazuri.
Kwa upande wao, viongozi wanawatuhumu baadhi ya wachezaji kucheza chini ya kiwango, utovu wa nidhamu huku kocha Patrick Phiri akipewa mtihani wa mechi ili akishindwa, iwe sababu ya kutimuliwa.
Mashabiki wengi wa klabu hiyo wanaamini kuwa kocha anaonewa, tatizo lipo kwa uongozi unaotakiwa kujichunguza ili kuona wapi umekosea na kuondoa kasoro zilizopo na si kukimbilia kumlaumu kocha. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Rais wa Simba ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya utendaji, Evance Aveva alisema jana kuwa kamati yake inakutana leo kujadili mwenendo mbovu wa timu pamoja na suala la kocha na wachezaji waliosimamishwa.
Wachezaji waliosimamishwa, Amri Kiemba, Shaaban Kisiga na Haroun Chanongo, wanadaiwa pia kuhusika na utovu wa nidhamu.
“Kamati ya Utendaji itakutana Jumatano (leo) ili kuamua hatima ya wachezaji na kesho tutatoa majibu, waendelee na adhabu au la,” alisema Aveva.
Kuhusu mwenendo wa sare za timu hiyo msimu huu, Aveva alisema hiyo ni sehemu ya mchezo na klabu yake siyo ya kwanza kupata matokeo hayo, ijapokuwa si mazuri, wala si mabaya.
Pamoja na Aveva kukubali matokeo, uongozi wake umempa Phiri mechi mbili akiwa amebakiza moja dhidi ya Ruvu Shooting Jumamosi ili kunusuru kibarua chake.
Baada ya sare na Mtibwa Sugar, Jumamosi iliyopita, Phiri ameamua kuwarudisha mazoeni wachezaji wake, safari hii ufukweni ili kuwaongezea stamina.
Alisema kikosi chake kinacheza vizuri kwa muda mfupi, kadri muda unavyokwenda, kipindi cha pili wachezaji huchoka, kuwaruhusu wapinzani kutawala na kusawazisha mabao.
“Nimeona kuna tatizo la kukosa stamina, jambo ambalo limekuwa likitugharimu, kipindi cha pili, kwani mara nyingi sisi huanza kufunga, lakini mabao yanarudi, hicho si kitu kizuri.
“Ndiyo maana nimeamua kuwapeleka wachezaji ufukweni kuwajengea stamina na kuwaongezea nguvu ili wacheze kwa ufanisi, najua mashabiki wanaumia kwa matokeo mabaya tunayopata, ninawaomba waendelee kutuunga mkono kwani bado hatujafanya vibaya, wasichoke, tunawahitaji kwa kiasi kikubwa ili kuwapa morali wachezaji wafanye vizuri,” alisema Phiri.
Aliyekuwa kocha wa Simba, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ameibuka na kusema, tatizo siyo kocha ni uongozi.
“Phiri ni kocha mzuri ndiyo maana wanamwajiri mara kwa mara, si mara ya kwanza kuifundisha Simba, angekuwa mbovu wasingemwomba mara kwa mara awafundishie.
“Kiwango cha wachezaji kidogo, pia umri bado, Phiri siyo anayefunga, kazi yake kufundisha, kama wachezaji hawafungi yeye afanyaje?
“Tatizo lipo kwao (viongozi), Aveva na wenzake wanayajua, wajitathimini kwanza kabla ya kumfukuza Phiri, huo siyo mwarobaini wa kufanya vizuri wakati viongozi ni wale wale.” Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...