Wednesday, March 06, 2013

RAIA WA UGANDA WAFUNGA NDOA YA JINSIA MOJA

Lawrence na jimmy raia wa uganda ila wanaishi Sweden wamefunga ndoa ya jinsia moja daaaah!! aibu tupu je ungekuwepo we ungefanya nini hapo... watu wanasheherekea kabisaaa.

LIVEEE DOGO AAMBIWA NYIE NDIYO MNAOTULETEA ZIRO TWENDE SHULE HII MBEYA VIJIJINI

MWANAFUNZI EMMANUEL ZAWADI WA SHULE YA MSINGI RUANDA KATA YA ILEMBO WILAYA YA MBEYA VIJIJINI AKIKAMATWA NA WANAFUNZI KUMPELEKA SHULE SABABU YA UTORO DOGO HUYO HUWA HAENDI SHULE HUSHINDA VICHAKANI LEO KAPATIKANA
NYIE UTORO WENU NDIYO UNASABABISHA SHULE ZETU ZIPATE ZIRO NYINGI WALISIKIKA WANAFUNZI HAO WAKISEMA 


Picha na Ezekiel Kamanga  Mbeya

SAFARICOM YADAIWA KUCHAKACHUA MATOKEO KENYA



Kampuni ya simu ya mkononi ya safaricom yashutumiwa Uchaguzi Kenya Nairobi,Kenya
KAMPUNI ya Simu ya Mkononi ya Safaricom inatuhumiwa kula njama ya kumuingiza madarakari mgombea wa Jubilee Uhuru Kenyatta,Safaricom inadaiwa kuchakachua
matokeo hayo kabla ya kuyarusha kwenda tume ya Uchaguzi. Kwa muujibu wa taarifa
zilizolifikia Habarimpya.com hivi punde inadai kwamba tume ya Uchaguzi nchini humo imekesha usiku kucha kujadili suala hilo huku ikitafuta namna ya kuzuia machafuko
yanayohofiwa kutoka nchini humo.
"SIRI KUBWA YAFICHUKA KUHUSU UCHAKACHUAJI WA MATOKEO YA KURA KATIKA UCHAGUZI MKUU 2013 NCHINI KENYA NA KUSABABISHA MIKUTANO KIBAO KUTAFUTA KUOKOA HALI KUSITOKEE MACHAFUKO"kilisema chanzo hicho. Siri kubwa yabainika nchini Kenya muda si
mrefu kuhusu utitiri wamatokeo kutoka mashinani na jinsi gani yalivyokua yakichakachuliwa na Injinia wa kampuni ya Simu Safaricom kabla ya kukabidhi matokeo hayo kwa tume ya uchaguzi na vyombo vya habari nchini humo. Safaricom ni kampuni ya simu iliojitolea kusaidia
tume ya uchaguzi kutoka mashinani na kutarajiwa kuzikabidhi kwa wahusika bila ya kuvurugwa kwa namna yoyote ile lakini uhalisia wa mambo haukua hivo.Hali hiyo ilionekana
kumkera sana meneja mkuu wa kampuni hiyo ya simu mara baada ya kubaini kwamba hadi hivi sasa sehemu kubwa ya matokeo yanayorushwa hewani kamwena yale yaliopokelewa na kampuni yake tangu awali kiasi cha kumfanya kuchapisha katika rundo la makaratasi 'matokeo halisi' anayodai kuwa ni tofauti kabisa na yale yanayoendelea kuzungushwa kote katika vyombo vya habari nchini humo. Kwa msingi wa hali hiyo ya sintofahamu katika


uchaguzi wa Kenya kuna madai kwamba kuna misururu ya mikutano inayoendelea hadi hivi
sasa nyuma ya pazia kutafuta namna gani ya kudhibiti taarifa hizi zisiwafikie wananchi wa
nchi hiyo kwa ujumla wao na pengine kusababisha hasira na michafuko.source jamii foram

MBATIA AJITOA TUME YA KUCHUNGUZA KUSHUKA ELIMU

                                     
Na: Patricia Kimelemeta na Fidelis Butahe, Mwananchi
Mwenyekiti  wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia amejitoa kwenye Tume ya serikali kuchunguza chanzo cha kushuka kwa kiwango cha kustisha cha matokeo ya kidato cha nne, iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Mbatia ambaye ametajwa kuwa mmoja wa wajumbe wa tume hiyo yenye wajumbe 15, alisema kamwe hatoweza  kufanya kazi yake kwa uhuru kwa sababu  ni Mbunge wa kuteuliwa, kamati hiyo
imeundwa na serikali hivyo lazima kutakuwa na mgongano wa maslahi.
Hatua hiyo imekuja siku tatu baada ya chama hicho kumwandikia barua Rais Jakaya Kikwete, kikimuomba aunde tume ya kudumu ya elimu nchini.
Tume hiyo iliundwa kutokana na matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne,  watahiniwa 240,903 kati ya 480,036  waliofanya mtihani walipata alama sifuri, huku 23,520 sawa na asilimia 5.16 wakifaulu na wengine 103,327 sawa na asilimia 26.02 wakipata daraja la nne.

Januari 31, mwaka huu katika kikao cha bunge, Mbatia aliwasilisha hoja binafsi kuhusu udhaifu katika sekta ya elimu akielezea kwa kina, sera ya elimu iliyopitwa na wakati, kukosekana kwa mitalaa, kuwapo kwa mihtasari mibovu ya masomo na vitabu kuwa na viwango duni.
Hata hivyo, wabunge wa CCM wakishirikiana na Serikali walimaliza hoja hiyo   bila kutolewa majibu ya msingi.
Mbatia alisema jana kuwa hawezi kufanya kazi yake kwa ufanisi ndani ya tume hiyo, kwa sababu ndiye aliwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusu udhaifu sekta ya elimu,  hoja ambayo ilizimwa bila kutolewa majibu ya msingi.
“Kamati ya Waziri mkuu haina jipya la kufanya kwa sababu ipo Kamati iliyoundwa mwaka 2011 kuchunguza matokeo mabaya ya kidato cha nne,  imeeleza kila kitu na ripoti ipo ofisi ya waziri mkuu, sasa hii ya sasa inakwenda kuchunguza nini?” alihoji Mbatia.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AMTEMBELEA MAMA MARIA NYERERE BUTIAMA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza jambo na Mama Maria Nyerere, wakati alipomtembelea nyumbani kwake Butiama Machi 4, 2013.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza jambo na Mama Maria Nyerere, wakati alipomtembelea nyumbani kwake Butiama Machi 4, 2013. Kushoto ni Mke wa Makamu, Mama Asha Bilal.

Rais Hugo Chavezi wa Venezuela afariki dunia baada ya kuugua saratani kwa muda mrefu.


Rais Hugo Chavez enzi za uhai wake.
Rais Hugo Chavez wa Venezuela amefariki dunia baada ya kuugua kwa miaka miwili ugonjwa wa saratani na hivyo kufikisha ukingoni uongozi wake wa miaka kumi na nne katika taifa hilo la Amerika ya kusini lenye utajiri mkubwa wa mafuta.
Makamu wa Rais wa Venezuela Nicolas Maduro, ametangaza kupitia kituo cha televisheni ya nchi hiyo kuwa Chavez mwenye umri wa miaka 58 ameaga dunia na kusema kifo chake kimewaacha na uchungu mwingi.
Chavez amefariki katika hospitali ya kijeshi huko Caracass baada ya kuugua kwa muda na kufanyiwa upasuaji mara nne uliosababisha afya yake kuzorota.
Serikali ya Venezuela imetangaza siku saba za maombolezo ya kitaifa na kwamba Rais huyo atazikwa Ijumaa wiki hii.
Mwezi Oktoba mwaka jana Chavez alishinda uchaguzi lakini hali yake ya afya haikuwa nzuri hivyo kushindikana kumuapisha.

TAKUKURU MBEYA YANASA WALIMU WAKITOZA RUSHWA WANAFUNZI

Na: Godfrey Kahango, Mbeya 


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), mkoani Mbeya imewanasa walimu wawili wa Shule ya Sekondari ya Forest kwa tuhuma za kushawishi na kupokea rushwa ya kati ya Sh500 na Sh1,000 kwa wanafunzi wanaochelewa asubuhi. Imeelezwa kwamba kutokana na mtindo huo, walimu hao wamekuwa wakijikusanyia wastani wa Sh150,000 kwa siku. Walimu hao walikamatwa saa 8.30 mchana jana shuleni hapo baada ya baadhi ya wanafunzi kutoa taarifa Takukuru za kuwapo kwa tabia hiyo ya kulazimishwa kutoa fedha wanapokuwa wamechelewa kufika shuleni asubuhi. Kamanda wa Takukuru wa Mkoa wa Mbeya, Daniel Mtuka, aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake kwamba walimu hao
(majina tunayo), walitiwa mbaroni wakati wakiwatoza wanafunzi hao fedha hizo.
Hadi wanakamatwa, walimu hao walikutwa na kiasi cha Sh64,000 walizokuwa wamezikusanya kutoka kwa wanafunzi hao, huku pembeni kukiwa na rundo la fimbo lililokuwa likitumika kuwachapa.
Mtuka alisema waligundua kuwa walimu hao walikuwa wanatengeneza kiasi cha 150,000 kwa siku kutokana na wastani wa wanafunzi 300 waliokuwa wanawachapa. Shule hiyo ina wanafunzi 900.
“Walimu hao wamekuwa na mradi huo wa kuwalipisha wanafunzi na wanaoshindwa kulipa walikuwa wanachapwa viboko visivyokuwa na idadi,” alisema na kuongeza:
“Kwanza walimu hao walikuwa wanachukua majina ya wanafunzi waliochelewa kutoka kwa walimu walioko zamu na kuanza kuwaita kwenye chumba walichokuwa wanakiita ‘Gwantanamo’ na kutoza fedha hizo.”
Walimu hao walichukua jina hilo kutoka Kambi ya Guantanamo Bay iliyoko karibu na Kisiwa cha Cuba, ambako Marekani imeweka kambi ya kijeshi.
Kambi hiyo ilianzishwa Januari, 2002 wakati Marekani ikiwa chini ya George Bush kwa ajili ya kuhifadhi mateka wa kivita kutoka Afghanistan na Iraq.
Kwa nyakati tofauti, wanafunzi walisimulia vituko vya walimu hao.

Mwanafunzi wa kidato cha kwanza, (jina tunalihifadhi), alisema kuwa mwanafunzi ambaye alikuwa hana fedha za kuwapatia, alikuwa anaambiwa kuweka kichwa chini, miguu na miguu juu kisha mwalimu huyo anamchapa kwenye makalio hadi sehemu unapopita uti wa mgongo.
“Baada ya kuona vitendo hivyo vinaendelea, huku uongozi wa shule ukiwa umekaa kimya, tukaamua kuwaambia viongozi wa serikali ya wanafunzi na ndiyo waliokwenda Takukuru,” alisema.

ZIARA YA RAIS WA ZANZIBAR DK.SHEIN MJINI MAGHARIBI

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein, akionesha zawadi aliyopewa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Abdalla Mwinyi Khamis,(katikati) alipofika Ofisini kwake akiwa katika ziara ya Mkoa huo iliyoanza leo,(kushoto) Mkuu wa Wilaya Mjini, Abdi Mahmoud Mzee.
 Meneja Mkuu wa Shirika la Umeme, Hassan Ali Mbarouk,(kulia) akitoa maelezo kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,wakati alipotembelea kituo kipya cha Umeme huko Welezo alipokuwa katika ziara ya Mkoa wa Mjini Magharibi iliyoanza leo.
 Msoma Utenzi, Shadat Juma,akiwaburudisha wananchi katika hafla ya uzinduzi wa kituo cha Mafunzo ya Kazi za Amali,Chumbuni Wilaya ya Mjini Mkoa Mjini Magharibi,  mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,alipokuwa katika ziara Mkoa huo.
 Rais wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akipata maelezo ya Ujenzi kutoka kwa Mhandisi wa Ujenzi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Iddi Khatib,alipotembelea kukagua Ujenzi wa Skuli ya Sekondari ya Wilaya huko Mpendae Mjini Zanzibar,akiwa katika ziara ya mkoa Mjini Magharibui iliyoanza leo. 

Rais wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akibadilishana mawazo na Meneja Mkuu wa Shirika la Umeme, Hassan Ali Mbarouk,(wa pili kushoto) wakati alipotembelea kituo kipya cha Umeme huko Welezo alipokuwa katika ziara ya Mkoa wa Mjini Magharibi iliyoanza leo. Picha na Ramadhan Othman,Ikulu

Waziri Mkuu wa Denmark Awasili Tanzania, alakiwa kwa shangwe

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Waziri mkuu wa Denmark Mhe.Helle Thorning-Schmidt muda mfupi baaday kuwasili katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jioni hii
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Waziri mkuu wa Denmark Mhe.Helle Thorning-Schmidt wakipokea heshima za nyimbo za Taifa pamoja na saluti ya mizinga 21  katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam

 Waziri mkuu wa Denmark Mhe.Helle Thorning-Schmidt akikagua gwaride lililoandaliwa kwa heshima yake
 Waziri mkuu wa Denmark Mhe.Helle Thorning-Schmidt na mwenyeji wake wakifurahia burudani mbalimbali
 Waziri mkuu wa Denmark Mhe.Helle Thorning-Schmidt akipkea shada l maua
Waziri mkuu wa Denmark Mhe.Helle Thorning-Schmidt akisalimiana na kinamama waliofurika uwanjani kumlaki. Picha na Freddy Maro

Tuesday, March 05, 2013

NICKI MINAJ AWATIMUA WAFANYAKAZI WAKE

Kutokana na kuwepo kwa uvumi wa kufanyiwa upasuaji wa kurekebisha sura yake Nicki Minaj awatimuwa kazi watengeneza nywele pamoja na wapambaji wake muda mfupi kabla ya kupanda jukwaani

Nicki amewatimuwa wafanyakazi wake hao siku moja baada ya rapa huyo kusema kwamba hajafanyiwa upasuaji wowote wa kurekebisha sura yake

Chanzo cha habari kinasema kuwa "Nicki anajaribu kutengeneza hali ambayo watu wanamuheshimu kama msanii amemfukuza kazi mtengeneza nywele wake wa muda mrefu"

"Nicki anaamini kwamba sasa amemalizana na masuala ya American Idol hivyo watu wataanz kumuangalia kwa jicho la tatu kipindi hiki ambacho anapanga kutoa albamu yake mpya ya Hip Hop

Uchaguzi wa rais nchini Kenya Uhuru Kenyatta aendelea kuongoza huku bado kura zikiwa bado zinaendelea kuhesabiwa.


Zoezi la kuhesabu kura linaendelea nchini Kenya kufuatia uchaguzi mkuu uliofanyika siku ya  Jumatatu.
Maafisa wa uchaguzi wamesema zaidi ya asilimia 70 ya watu milioni 14.3 waliojiandikisha kupiga kura walijitokeza katika uchaguzi huo.
Matokeo ya awali yanaonyesha kuwa mgombea urais kupitia muungano wa kisiasa wa Jubilee Bw.  Uhuru Kenyatta anaongoza kwa asilimia 55 dhidi ya mpinzani wake Waziri Mkuu Raila Odinga wa muungano wa kisiasa wa CORD akiwa na asilimia 40.
Hata hivyo, muungano wa CORD tayari umeelezea wasiwasi wake kuhusu matokeo hayo na kutilia shaka mfumo mzima wa utoaji wa matokeo hayo.
Hata hivyo Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya-IEBC Isaack Hassan amesisitiza kuwa matokeo hayo ni ya awali tu.
 Mshindi katika uchaguzi huo, anatakiwa kupata zaidi ya asilimia 50 ya kura la sivyo wagombea wawili wa juu watalazimika kuingia katika awamu pili ya uchaguzi mwezi Aprili mwaka huu.

SAKATA LA DIAMOND PLATNUM KUMDHURUMU MENEJA WAKE

                                  Raque akiwa na Diamond kwenye interview
Meneja wa Diamond Platnumz, Raqey Mohamed amelazimika kutumia mtandao wa Facebook kukanusha habari iliyoandikwa na gazeti la udaku la ‘Jumatatu’ kuwa ametapeliwa na Diamond. Amesema Diamond ni mchapakazi na mwaminifu na mkataba wao hauhusiani na mtu yeyote.

Raqey ameandika, “this is coming from me Raqey known as Diamond Platnumz Manager, hakuna ukweli wowote juu ya habari hii, Diamond is a hard working kind and loyal. Our contract has nothing to do with anybody. If you want to write a story at least pay a visit to my studio or call me before you write a story.”

Bongo imempigia simu Raqey ambaye ameendelea kusisitiza kuwa habari hiyo ni ya uzushi na ya upuuzi mtupu.

JOHN MNYIKA APANGA KUITISHA MAANDAMANO MAKUBWA MACHI 26


Mbunge wa Jimbo la Ubungo JOHN MNYIKA amesema Ofisi yake imepanga kuitisha Maandamano makubwa Machi 16 Mwaka huu kuelekea Ofisi za Wizara ya Maji, kutokana na Wizara hiyo kushindwa kulipatia ufumbuzi suala la upatikanaji wa Majisafi pamoja na uondoaji wa Majitaka katika maeneo mbalimbali ya Jimbo hilo.
 
Akizungumza na CLOUDS FM, MNYIKA amesema kuwa tayari Ofisi yake imekamilisha hatua za msingi za uratibu wa maandano hayo, ikiwa ni pamoja na kulishirikisha Jeshi la Polisi pamoja na Uongozi wa Manispaa ya Kinondoni.Endelea kupiti audifacejackson blog ..Amebainisha kuwa licha ya ofisi yake kulifikisha suala la tatizo la Maji katika baadhi ya maeneo ya Jimbo hilo Wizarani sambamba na kuwasilisha hoja Binafsi bungeni, hakuna hatua zozote za awali zilizochukuliwa huku Wakazi wa maeneo hayo wakitaabika kwa kukosa maji.

SHULE INA WALIMU 8 WA KIKE,6 KATI YAO NI WAJAWAZITO WAOMBA MSAADA

SERIKALI imeombwa iwapatie walimu wa kiume Shule ya Msingi Orbili, kutokana na walimu wote wanawake wa shule hiyo kupata ujauzito na hawafundishi hivi sasa.

Ombi hilo limetolewa na wakazi wa Kijiji cha Orbili Kata ya 
Shambarai wilayani Simanjiro mkoani Manyara.

Wakazi hao ambao hawakutaka kutaja majina yao wakati wakiongea na waandishi wa habari, walisema kuwa shule hiyo ina walimu nane, ambapo wanaume ni wawili na wanawake ni sita, akiwemo Mwalimu Mkuu, wote wana ujauzito.
Walisema walimu wawili wanaume, hawawezi kuwafundisha wanafunzi wote wa shule hiyo kuanzia darasa la kwanza hadi la saba, hasa ukizingatia kuwa darasa la nne na la saba, watafanya mtihani wa Taifa mwaka huu.

Walisema kuwa hivi karibuni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, alijifungua mtoto na walimu wengine watano waliobaki, wanatarajiwa kujifungua wakati wowote.Endelea kupiti audifacejackson blog

Nadhani shule hii ifungwe ili Serikali ilete walimu wengine kwani hawa walimu wenye mimba hawafundishi wanafunzi wetu, wenyewe wamebaki kula udongo na malimao,” alisisitiza mkazi mmoja.

SOURCE::HABARI LEO:

President Kikwete Meets With MCC Officials In Dar Es Salaam.

President Jakaya Mrisho Kikwete greets Mr Steve Kaufman, the Millenium Challenge Corporation’s Chief of Staff, who paid him a visit at the State House in Dar es salaam March 4, 2013. Centre is the US Ambassador to Tanzania, Mr Alfonso Lenhardt.
President Jakaya Mrisho Kikwete holds talks with (from left)  Mr Steve Kaufman, the Millenium Challenge Corporation’s Chief of Staff, MCC’s Vice President for East and Southern Africa, Mr Andrew Mayock,the US Ambassador to Tanzania, Mr Alfonso Lenhardt. and Mr Matt KAvanagh, MCC Resident Country Director ,  who paid him a visit at the State House in Dar es salaam March 4, 2013. Centre is the US Chief of Staff, Ambassador to Tanzania, Mr Alfonso Lenhardt.
President Jakaya Mrisho Kikwete in a group photos with (from left)  Mr Steve Kaufman, the Millenium Challenge Corporation’s Chief of Staff (right) MCC’s Vice President for East and Southern Africa, Mr Andrew Mayock (second row right),the US Ambassador to Tanzania, Mr Alfonso Lenhardt (front row left) Mr Matt KAvanagh, MCC Resident Country Director (second row left) and the Minister for Finance Dr Willim Mgimwa and Mr Bernard Mchomvu, the CEO of the Millenium Challenge Account (MCA) -Tanzania,  at the State House in Dar es salaam  March 4, 2013. Centre is the US Chief of Staff, Ambassador to Tanzania, Mr Alfonso Lenhardt.(STATE HOUSE PHOTO)

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...