Wednesday, March 06, 2013

SAFARICOM YADAIWA KUCHAKACHUA MATOKEO KENYA



Kampuni ya simu ya mkononi ya safaricom yashutumiwa Uchaguzi Kenya Nairobi,Kenya
KAMPUNI ya Simu ya Mkononi ya Safaricom inatuhumiwa kula njama ya kumuingiza madarakari mgombea wa Jubilee Uhuru Kenyatta,Safaricom inadaiwa kuchakachua
matokeo hayo kabla ya kuyarusha kwenda tume ya Uchaguzi. Kwa muujibu wa taarifa
zilizolifikia Habarimpya.com hivi punde inadai kwamba tume ya Uchaguzi nchini humo imekesha usiku kucha kujadili suala hilo huku ikitafuta namna ya kuzuia machafuko
yanayohofiwa kutoka nchini humo.
"SIRI KUBWA YAFICHUKA KUHUSU UCHAKACHUAJI WA MATOKEO YA KURA KATIKA UCHAGUZI MKUU 2013 NCHINI KENYA NA KUSABABISHA MIKUTANO KIBAO KUTAFUTA KUOKOA HALI KUSITOKEE MACHAFUKO"kilisema chanzo hicho. Siri kubwa yabainika nchini Kenya muda si
mrefu kuhusu utitiri wamatokeo kutoka mashinani na jinsi gani yalivyokua yakichakachuliwa na Injinia wa kampuni ya Simu Safaricom kabla ya kukabidhi matokeo hayo kwa tume ya uchaguzi na vyombo vya habari nchini humo. Safaricom ni kampuni ya simu iliojitolea kusaidia
tume ya uchaguzi kutoka mashinani na kutarajiwa kuzikabidhi kwa wahusika bila ya kuvurugwa kwa namna yoyote ile lakini uhalisia wa mambo haukua hivo.Hali hiyo ilionekana
kumkera sana meneja mkuu wa kampuni hiyo ya simu mara baada ya kubaini kwamba hadi hivi sasa sehemu kubwa ya matokeo yanayorushwa hewani kamwena yale yaliopokelewa na kampuni yake tangu awali kiasi cha kumfanya kuchapisha katika rundo la makaratasi 'matokeo halisi' anayodai kuwa ni tofauti kabisa na yale yanayoendelea kuzungushwa kote katika vyombo vya habari nchini humo. Kwa msingi wa hali hiyo ya sintofahamu katika


uchaguzi wa Kenya kuna madai kwamba kuna misururu ya mikutano inayoendelea hadi hivi
sasa nyuma ya pazia kutafuta namna gani ya kudhibiti taarifa hizi zisiwafikie wananchi wa
nchi hiyo kwa ujumla wao na pengine kusababisha hasira na michafuko.source jamii foram

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...