Tuesday, March 05, 2013

Uchaguzi wa rais nchini Kenya Uhuru Kenyatta aendelea kuongoza huku bado kura zikiwa bado zinaendelea kuhesabiwa.


Zoezi la kuhesabu kura linaendelea nchini Kenya kufuatia uchaguzi mkuu uliofanyika siku ya  Jumatatu.
Maafisa wa uchaguzi wamesema zaidi ya asilimia 70 ya watu milioni 14.3 waliojiandikisha kupiga kura walijitokeza katika uchaguzi huo.
Matokeo ya awali yanaonyesha kuwa mgombea urais kupitia muungano wa kisiasa wa Jubilee Bw.  Uhuru Kenyatta anaongoza kwa asilimia 55 dhidi ya mpinzani wake Waziri Mkuu Raila Odinga wa muungano wa kisiasa wa CORD akiwa na asilimia 40.
Hata hivyo, muungano wa CORD tayari umeelezea wasiwasi wake kuhusu matokeo hayo na kutilia shaka mfumo mzima wa utoaji wa matokeo hayo.
Hata hivyo Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya-IEBC Isaack Hassan amesisitiza kuwa matokeo hayo ni ya awali tu.
 Mshindi katika uchaguzi huo, anatakiwa kupata zaidi ya asilimia 50 ya kura la sivyo wagombea wawili wa juu watalazimika kuingia katika awamu pili ya uchaguzi mwezi Aprili mwaka huu.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...