Wednesday, November 26, 2014
MKOSAMALI APANDISHWA KIZIMBANI
Mbunge wa Jimbo la
Muhambwe mkoani Kigoma, Felix Mkosamali amefikishwa katika Mahakama ya
Wilaya ya Kibondo akikabiliwa na shtaka la kumzuia karani mwandikishaji
kufanya kazi yake.
Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Peter Makala alidai
jana mahakamani hapo kuwa mbunge huyo alitenda kosa hilo juzi, baada ya
kufika Kituo cha Kitongoji cha Nduta, Kijiji cha Kumhasha, Kata ya
Murungu, wilayani Kibondo na kumzuia karani kuendelea kuandikisha wakazi
kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Makala alidai kuwa kitendo cha kumzuia karani huyo
kuendelea kufanya kazi yake ni kinyume na ukiukwaji wa Sheria ya
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Pia, alidai kuwa kitendo cha kuwazuia wakazi hao
kujiandikisha ni kuwanyima haki yao ya msingi, kwani baada ya kuzuiwa
waliendelea kudai kutaka kujiandikisha lakini mshtakiwa hakusikiliza
kilio chao.
Mshtakiwa alikana shtaka na Hakimu Erick Marley
alisema dhamana iko wazi kwa mdhamini kusaini bondi ya Sh4 milioni.
Mbunge huyo alitimiza masharti na kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba
29.
Mkosamali alikamatwa juzi jioni baada ya kudaiwa
kumnyang’nya karani vitabu na madodoso na kuyapeleka ofisi ya Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
BOKO HARAM WAFANYA MAUAJI TENA
Watu 78 wameuawa katika mashambulio mawili ya kujitoa mhanga yaliyofanywa sokoni, katika mji wa Maiduguri kaskazini mwa Nigeria.
Watu
walioshuhudia tukio hilo wamesema mlipuko wa kwanza ulitokea wakati
washambuliaji hao walipomuwekea mlipuko mwanamke mmoja mwenye matatizo
ya akili.Wakati umati wa watu wakienda kutoa msaada, mwanamke mwingine alijitoa mhanga.
Kundi la kiislamu la wapiganaji la Boko Haram ambalo linadhibiti maeneo mengine ya miji ya kaskazini mwa nchi hiyo na vijiji, linadhaniwa kuhusika na shambulio hilo.
Mwandishi wa BBC anasema Wanaigeria wamekosa Imani na jaribio la serikali ya nchi yao kufanya mazungumzo na Boko Haram, kutokana an kuongezeka kwa ghasia hizo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
ZAIDI YA WATU 60 WAUAWA SYRIA
Zaidi ya watu 60 wameuwawa, katika mashambulio kadhaa ya angani yaliyofanywa na Jeshi la serikali ya Syria.
Raia wengi waliuwawa katika mashambulio tisa yaliyolenga ngome kuu za kundi la wapiganaji wa Islamic State.Wakereketwa wameiambia BBC kuwa Hospitali kuu ya Raqqa imesalia bila huduma kwani HAKUNA chakula na umeme. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
KLABU BINGWA BARANI ULAYA
Usiku
wa kuamkia leo kindumbwe ndumbwe cha michuano ya Klabu Bigwa barani
Ulaya kiliendelea na kushuhudia Chelsea ikitoa kipigo cha mbwa mwizi
mbele ya mashabiki wa Schalke 04 ya Ujuremani pale ilipoishindilia
magoli 5 bila majibu.
Manchester City ya England nao wakawabamiza
wababe wengine wa Ujerumani Bayern Munich kwa kwa kuwafunga magoli 3 - 2
na kufufua matumaini ya kusonga mbele katika michuano hiyo huku magoli
yote matatu ya Man City yakitiwa kimiani Sergio Aguero.Katika mechi nyingine Paris St. Germain ya Ufaransa waliwashikisha adabu Ajax ya Uholanzi kwa kuifunga magoli 3 - 1 huku Becelona kwa upande mwingine wakiisasambua Apoel Nicosia ya Syprus kwa kuishushia kichapo cha magoli 4 kwa yai.
CSKA Moscow ya Urusi na AC Roma zikatoka suluhu ya goli moja 1 - 1
Burudani hiyo itaendelea leo ambapo Liverpool ya England baada ya kufanya vibaya katika mechi zilizotangulia leo wanajaribu bahati yao wakiwa ugenini dhidi Ludogorets ya Bulgaria.
Arsenal nao watawakaribisha Borusia Dortmud ya Ujerumani huku vita vingine vikiwa ni kati ya FC Basel ya Uswis watakaopopepetana na Real Madrid. Malmo FF ya Sweden watakuwa wenyeji wa Juventus ya Italia. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Tuesday, November 25, 2014
MKONO ASIMULIA ALIVOLISHWA SUMU LONDON
Mbunge wa Musoma
Vijijini (CCM), Nimrod Mkono ambaye hivi karibuni alinusurika kifo
akidaiwa kulishwa sumu akiwa London, Uingereza amesimulia jinsi tukio
hilo lilivyomkuta.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkono
alisema endapo uchunguzi wa suala hilo utakamilika na kuthibitisha
kwamba alilishwa sumu, atapambana na wahusika kwa kuwa wamehatarisha
maisha yake.
Mkono ambaye pia ni wakili maarufu nchini, alitoa
kauli hizo jijini hapa jana, alipokuwa akizungumza na waandishi wa
habari kuelezea mwenendo wa afya yake.
Alidai kwamba, lengo la kumlisha sumu ni kuharibu figo zake ndani ya saa 72 wakati alipokuwa katika ziara ya nchini humo. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
ULINZI MKALI MDAHARO WA JAJI WARIOBA LEO
Kamanda wa
Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova amesema
ulinzi utaimarishwa kabla, wakati na baada ya mdahalo maalumu wa Katiba
ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), kwenye Ukumbi wa
Mlimani City, Dar es Salaam mzungumzaji mkuu akiwa Mwenyekiti wa
iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Hatua ya Kova imekuja baada ya kuibuka kwa vurugu
zilizosababisha kuvunjika mdahalo wa kwanza uliofanyika Novemba 2,
kwenye Hoteli ya Blue Pearl Ubungo, Dar es Salaam. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
RAIS KIKWETE KUREJEA JUMAMOSI
Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kurejea nchini
Jumamosi, Novemba 29 baada ya taratibu za matibabu yake nchini Marekani
kukamilika.
Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu
ilisema jana kuwa taratibu hizo zilikamilika saa 12 asubuhi jana, baada
ya madaktari bingwa katika Hospitali ya Johns Hopkins kumfanyia hatua
ya mwisho ya tiba.
Hata hivyo, Rais Kikwete ataendelea kupumzika na
kuangaliwa kwenye Hoteli Maalumu inayohusiana na Hospitali ya Johns
Hopkins kwa siku mbili hadi tatu kabla ya kuanza safari ya kurejea
nyumbani.
Rais Kikwete aliondoka nchini Alhamisi ya Novemba
6, 2014, kwenda kufanyiwa uchunguzi wa afya yake lakini madaktari katika
Hospitali ya Johns Hopkins waliamua kumfanyia upasuaji wa tezi dume
Jumamosi ya Novemba 8, 2014.
Taarifa hiyo ilisema Rais Kikwete anaendelea
kuwashukuru Watanzania kwa sala na maombi yao ya kumtakia heri ya kupona
haraka na kurejesha afya njema katika kipindi chote cha ugonjwa wake. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
JENGO LAANGUKA, KUMI WAFA
Watu kumi wamepoteza maisha baada ya jengo la ghorofa kuanguka mjini Cairo nchini Misri, maafisa wameeleza.
Watu saba wamejeruhiwa baada ya jengo la ghorofa nane kuanguka usiku.Mkuu wa Idara ya dharula Jenerali Mamdouh Abdul Qader amesema vikosi vya uaokoaji vinawasaka Watu 15 wanaokisiwa kunasa kwenye kifusi.
Mara kadhaa majengo yameanguka nchini humo, sababu kubwa ikiwa ujenzi usiofuata kanuni na Sheria pia usimamizi mbovu wa taratibu za ujenzi.
Jenerali Qader ameliambia shirika la Habari la Ufaransa kuwa hawajui chanzo cha ajali hiyo,lakini walipatiwa taarifa kuwa ghorofa mbili za juu zilijengwa kinyume cha sheria.
Wakazi wa majengo ya karibu na lilipoanguka jengo hilo wameondoka katika makazi yao kwa nia ya kujihadhari.
Mwezi Januari Mwaka jana,Watu 28 walipoteza maisha baada ya jengo la ghorofa nane kuanguka mjini Alexandria. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
WAANDAMANAJI WAFANYA VURUGU ST. LUIS
Mji
wa St Louis limeshuhudia maandamano na vitendo vya uporaji baada ya
jaji kupitisha uamuzi wa kumshtaki aliyemuua kijana mweusi Michael
Brown.
Polisi mjini humo wamesema vurugu zimeleta madhara makubwa zaidi kuliko ya mwezi Agosti baada ya kuuawa kwa kijana huyo.Kamanda wa Polisi wa St Louis, Jon Belmar amesema alisikia milio ya risasi takriban 150 kutoka kwenye makundi ya watu.
Brown alifyatuliwa risasi na Polisi tarehe 9 Mwezi Agosti, hali iliyoibua ghadhabu na maandamano.
Watu wengi wa jamii ya Afrika na Marekani walitoa wito wakitaka Afisa Polisi Darren Wilson ashtakiwe kwa mauaji.
Rais wa Marekani Barack Obama alitoa wito kwa wamarekani kuwa watulivu na kukubali maamuzi ya Jaji kuhusu kesi hiyo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Monday, November 24, 2014
MDAHALO WA JAJI WARIOBA KESHO DAR
Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.PICHA|MAKTABA
Taasisi ya
Mwalimu Nyerere (MNF), imeandaa mdahalo maalumu wa Katiba utakaofanyika
kesho kwenye Ukumbi wa Mlimani City ambao mzungumzaji mkuu atakuwa
Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph
Warioba.
Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Joseph Butiku alisema
jana kwamba mdahalo huo wa amani ni kwa ajili ya Watanzania wenye
mapenzi mema na utakuwa wa wazi, ikiwa ni sehemu ya kuziba pengo la
mdahalo wa Katiba uliovunjika Novemba 2 ambao ulifanyika kwenye Hoteli
ya Blue Pearl.
Ulivunjika baada ya kutokea vurugu zinazodaiwa
kuanzishwa na kikundi cha watu kwa lengo la kuvuruga uwasilishwaji wa
ujumbe wa Katiba, huku Katibu wa Uhamasishaji wa UVCCM, Paul Makonda
akitajwa kinara wa vurugu hizo. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
BUNDUKI BANDI YAMLETEA MAAFA
Wakili
anayewakilisha familia ya kijana mweusi mwenye umri wa miaka kumi na
mbili aliyepigwa risasi na polisi katika mji wa Cleveland nchini
Marekani, amesema familia yake itafanya uchunguzi wake sambamba na ule
unaofanywa na Polisi kubaini kilichotokea.
Kijana huyo kwa jina
Tamir Rice mwenye umri wa miaka 12 alikuwa amebeba kile kilichoonekana
kuwa bunduki bandia. Polisi wanadai kuwa kijana huyo alikataa kutii amri
alipoambaiwa asalimu amri.Kifaa walichokuwa nacho polisi ndicho kilibaini kuwa bunduki hiyo ilikuwa bandia.
Inaarifiwa kijana huyo alipigwa risasi mara mbili baada ya kuitoa bunduki yake kiunoni mwake lakini hakujaribu hata wakati mmoja kuielekeza kwa poliso wala kujribu kuifyatua.
Wakili wa familia hiyo amesema kuwa ikiwa watapata kuwa haki za kijana huyo zilikiukwa, familia yake itachukua hatua za kisheria dhidi ya polisi.
Mwanasiasa mmoja anapendekeza sheria ambayo itahakikisha kuwa bunduki bandia zinakuwa na rangi unayong'aa zaidi ili ziweze kutambulika haraka. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
MFANYAKAZI KATILI MATATANI UGANDA
Polisi
wamebadilisha mashtaka ya mfanyikazi wa nyumbani aliyenaswa kwa kamera
akimpiga na kumtendea unyama mtoto wa mwaka mmoja na nusu, kutoka kwa
kosa la kutesa na sasa anakabiliwa na kosa la jaribio la mauaji.
Video
hiyo iliwaudhi watu wengi sana kwenye mitandao ya kijamii ila babake
mtoto huyo alisema walisambaza video hiyo ili kuwatahadharisha wazazi
wenegine. Mfanyakazi huyo wa nyumbani Jolly Tumuhirwe, alikuwa amezuiliwa katika gereza la Luzira na mahakama ya Nakawa kwa kosa la kutesa chini ya kifungo cha 41 kwenye katiba kinachoongelea dhidi ya mateso.
Mwanamke huyo sasa anatarajiwa kufikishwa mahakamani tarehe 8 Disemba.
Hata hivyo, msemaji wa polisi Bwana Fred Enanga, amesema "shtaka dhidi ya mwanamke huyo lilibadilishwa baada ya kupitiwa mwendesha mkuu wa mashitaka. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
ROGDERS AKUBALI LAWAMA KIPIGO CHA LIVERPOOL
Kocha
wa Liverpool Brendan Rodgers amesema anapokea lawama zote kufuatia
kipigo cha timu yake ya Liverpool ilichokipata kutoka kwa Cyristal
Palace.
Liverpool ambayo msimu uliopita ilishika nafasi ya pili
katika msimamo wa ligi ya England jana ilipata kipigo cha mbwa mwizi cha
mabao 3 -1 kutoka kwa Crystal Palace.Rodger amesema amekubali kwamba ulikuwa ni wakati mgumu na analazimika kufanya juhudi kubwa ili kutafuta ufumbuzi wa tatizo ndani ya Liverpool.
Amesema wamesikitishwa na kiwango cha timu pamoja na matokeo mabovu na kwamba kama meneja wa ni lazima achukue lawama. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
SHABIKI WA MPIRA AMNG'ATA MWENZIE KENYA
Mwanamume
mmoja mjini Kisumu Magharibi mwa Kenya, alimng'ata sikio jirani yake
baada ya mechi ya soka ya ligi ya uingereza iliyokuwa na matokeo yasiyo
ya kuridhisha kwa mmoja wao.
Mwanamume huyo ambaye ni shabiki sugu
wa klabu ya soka ya Arsenal aliamua kujiondolea hasira ya klabu yake
kushindwa na Manchester United kwa kumng'ata hasimu wake wa Man U sikio
lake Jumamosi usiku.Walioshuhudia tukio hilo wanasema kuwa shabiki huyo sugu wa Arsenal hangeweza kustahimili kukejeliwa na jirani yake shabiki wa Man United baada ya klabu yake kushindwa mabao mawili kwa moja
Mwanamume huyo alifungiwa katika chumba kimoja na wakazi wa mtaa wa Railways mjini humo, ambao walitaka kumuua kwa kitendo chake. Inadaiwa hii ni mara ya pili kwa mwanamume huyo kumng'ata mwenziwe sikio kwa sababu za kisoka. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Saturday, November 22, 2014
CHAMA TAWALA ZAMBIA WAMTIMUA KAIMU RAIS CHAMANI
Chama tawala nchini Zambia (PF) kimemtimua kaimu rais wa nchi hiyo Guys Scott kutoka chamani na kuvunja utaratibu wa katiba.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa msemaji wa chama hicho.''Amekuwa akiwaajiri na kuwafuta watu kazi ovyo na pia bila ya kushauriana na kamati kuu ya chama,'' amesema Malozo Sichone.
Bwana Scott, ambaye licha ya hatua hiyo ataendelea kuwa mwanachama wa chama hicho, ataendelea kuhudumu kama kaimu rais hadi uchaguzi utakapofanyika tarehe 20 Januari.
Scott aliteuliwa kuwa kaimu rais kufuatia kifo cha hayati Rais Michael Sata aliyefariki mwezi jana. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
MTOTO ALIYEKUFA KWA AJALI AZIKWA UGANDA
Shughuli
za mazishi ya mtoto wa miaka miwili zimefanyika nchini Uganda, mtoto
ambaye kifo chake kimezua ghadhabu baada ya mtoto huyo kugongwa na gari
la halmashauri ya jiji la Kampala ,baada ya mama yake kukamatwa akiuza
matunda kinyume cha sheria.
Familia ya Ryan Ssemaganda na
wanasiasa wa upinzani walitishia kutomzika mtoto huyo mpaka maofisa hao
watakapo wajibika kwa kitendo hicho.Mwili wake ulichukuliwa wakati
wakiandamana kuelekea bungeni siku ya alhamisi.Raia wa Uganda wanaona kuwa halmashauri hiyo inatumia nguvu nyingi kupambana na wachuuzi wa mitaani.
Mama wa mtoto Ryan alikamatwa siku ya jumatatu baada ya kukutwa akiuza matunda huku akiwa hana leseni.
Siku iliyofuata, Bibi wa mtoto huyo alimpeleka katika Ofisi za Mamlaka ya mji wa Kampala ambako mama mtoto alikuwa akishiliwa , nia ilikua kumpa mama mtoto ili amnyonyeshe.
Maafisa wa Ofisi hiyo walikataa na wakati wakijadiliana kuhusu hilo, mtoto alichoropoka kutoka kwa mama yake na kugongwa na gari linalomilikiwa na Mamlaka hiyo.
Siku ya Alhamisi polisi ilizuia kupelekwa kwa mwili katika Bunge, wakisisitiza mwili huo uzikwe ili marehemu apumzike kwa amani, na kuwataka waepuka jambo hilo kushughulikiwa kisiasa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
MECHI ZA LIGI KUU UINGEREZA LEO JUMAMOSI
Mechi za Ligi kuu ya Uingereza siku ya jumamosi
Chelsea v West Brom18:00
Everton v West Ham18:00
Leicester v Sunderland18:00
Man City v Swansea18:00
Newcastle v QPR18:00
Stoke v Burnley18:00
Arsenaly v Man Utd 20:30
Mechi zote kuchezwa saa za Afrika Mashariki. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
WENGER: TULIJARIBU KUMSAJILI MESSI
Mkufunzi
wa kilabu ya Arsenal Arsene Wenger amethibitisha kuwa kilabu hiyo
ilijaribu kumsajili nyota wa kilabu ya barcelona Lionel Messi kama
mpango wa kutaka kuwanyakua wachezaji watatu wachanga wa kilabu hiyo.
Messi alikuwa na miaka 15 wakati huo na mwenzake Gerrad Pique pamoja na aliyekuwa kiungo wa kati wa Arsenal Cess fabregas.Wenger:''Tulitaka kumchukua Fabregas,Messi na Pique,lakini tukafanikiwa kumpata Fabregas pekee''.
Fabregas aliichezea kilabu ya Arsenal kwa miaka minane kabla ya kurudi Barcelona ,huku Pique akijiunga na Manchester United mwaka 2004.
Messi mwenye umri wa miaka 27,ameichezea timu ya Barcelona kwa muda wote na kuisadia kushinda mataji sita ya La liga pamoja na kombe la vilabu bingwa mara tatu baada ya mpango wa kujiunga na Arsenal kugonga mwamba.
Hatahivyo ,Wenger amepinga madai kwamba mpango huo ulifeli kutokana na makaazi ya Messi na familia yake.
Mchezaji huyo wa timu ya Argentina pia angelazimika kuwa na kibali cha kufanya kazi nchini Uingereza.
Wenger aliongezea:''Nadhani Messi mwenyewe hakutaka kujiunga nasi''. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Friday, November 21, 2014
NDERAKINDO AMKANA SAMUEL SITTA
Wakati Waziri wa
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta akisema ofisi yake
imewakutanisha na kumaliza mgogoro baina ya wabunge wawili wa Bunge la
Afrika Mashariki (Eala), mmoja wa wabunge hao, Dk Nderakindo Kessy
amesema hakuna kitu kama hicho.
Dk Kessy jana aliripotiwa na vyombo vya habari
akidai kupigwa na mbunge mwenzake, Shy-Rose Bhanji, akisema
alisababishiwa maumivu makali, lakini likapingwa na Sitta. Jana, sakata hilo lilitinga bungeni na Serikali ikitakiwa kutoa maelezo kwa nini wabunge wa Tanzania wanafanya mambo ya ajabu.
Akijibu swali hilo, Waziri Sitta alisema ilitokea
bahati mbaya Bhanji kupitia CCM akamgonga Dk Kessy (NCCR-Mageuzi) na kwa
kuwa mbunge huyo wa chama tawala alikuwa na haraka kwenda kuwahi gari,
hakusimama, hivyo baadhi ya wabunge wa Uganda wakamshauri Dk Kessy
kwenda kuripoti tukio hilo polisi. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
NAPE: WAPUUZENI WAPINZANI
Wananchi wametakiwa
kupuuza kauli alizodai kuwa za wapinzani za kuwataka wasishiriki kupiga
kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliopangwa kufanyika Desemba,
mwaka huu.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema hayo juzi alipozungumza na wakazi wa Nchingwea mkoani Lindi.
Alisema ni marufuku kwa vyama vya upinzani kuzuia wananchi kupiga kura na kumchagua kiongozi wanayempenda
“Tumepata taarifa kuna wapinzani wameanza
kuwatisha wananchi wasiende kupiga kura siku ya Uchaguzi wa Serikali za
Mitaa,” alidai Nape.
“Hizi ni salamu kwa wapinzani wenye mpango huo kuwa hatutawaacha, lazima tutawashughulikia.”
Alisema kupiga kura ni haki ya kila mwananchi,
hivyo kitendo cha kuzuia watu ni sawa na kubaka demokrasia, jambo ambalo
CCM haitalivumilia.
Nape alisema CCM imejipanga vizuri na kwamba ina uhakika wa kushinda kwa kishindo. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
POLISI WABAKAJI WAONGEZEWA ADHABU
Polisi
wawili nchini Tunisia walioshitakiwa kwa kumbaka mwanamke ndani ya gari
la polisi, wameongezewa adhabu katika kesi iliyowashtua wengi.
Maafisa hao walifungwa jela mwezi Machi huku kukiwa na malalamiko kwamba adhabu hiyo haitoshi.Hukumu hiyo, iliongezwa hadi miaka 15 Alhamisi baada ya rufaa kuwasilishwa mahakamani na mwathiriwa wa kitendo hicho cha unyama Meriem Ben Mohamed.
Wakili wake alitaja hatua ya mahakama kuwoangeza adhabu watuhumiwa kama jambo zuri, na pia kusifu ambavyo kesi za ubakaji zinashughulikiwa nchini Tunisia.
Aliambia shirika la habari la AFP, kwamba ameridhishwa na adhabu hiyo.
"lakini bado haitoshi, kwa maoni yangu kwa tendo la kukera kama hilo,'' aliongeza kusema wakili huyo.
Meriem Ben Mohamed alishambuliwa mwaka 2012 na maafisa wa polisi waliosimamisha gari lake alimokuwa na mpenzi wake mjini Tunis. Alikuwa na umri wa miaka 27.
Watuhumiwa walikanusha mashitaka wakisema kuwa waliwapata wawili hao wakiwa wanashirki tendo la ndoa ndani ya gari lao.
Maafisa wa polisi walijaribu kuwashitaki Meriam na mpenzi wake kwa kosa la kukosa maadili lakini maandamano yalifanywa kupinga hatua kama hiyo huku wengi wakiwatetea wawili hao.
Ilisababisha Rais wa Tunisia kumsamehe Meriam na mpenzi wake.
Afisaa mwingine wa tatu aliyejaribu kuwatoza hongo wawili hao, atatumikia kifungo cha miaka miwili alichokuwa amepewa.
Ripoti iliyotolewa na mtaalamu wa kisaikolojia ilisema kuwa yote yaliyotokea yalimsababisha Meriam kusongwa na mawazo.
Kesi hii inatokea wakati ambapo kumekuwa na shinikizo kali kwa serikali kuzingatia haki za wanawake kufuatia kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa Rais Zine al-Abidine Ben Ali.
Na BBC
MKANYAGANO HATARI WAWAUA 11 ZIMBABWE
Watu 11 wamefariki katika mkanyagano nchini Zimbabwe baada ya ibada ya kidini kufnayika katika uwanja wa soka.
Polisi wanasema kuwa watu wanne walifariki katika uwanja huo ulio mjini Kwekwe wakati wengine saba wakifariki hospitalini.
Mkanyagano
huo ulitokea wakati maelfu ya waumini wakikimbilia kuondoka uwanjani
humo baada ya ibada iliyoongozwa na mhubiri wa kipentekoste Walter
Magaya.
Mhubiri huyo anadai kuwaponya watu kwa kufanya miujiza.
Baadhi ya walioshuhudia mkanyagano huo wanatuhumu polisi kwa kufunga
baadhi ya milngo ya kuondokea uwanjani humo, huku watu wakiondoka
kupitia mlango mmoja tu.
Hata hivyo polisi wanakana kutumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya.
Bwana Mugaya ambaye ni mkuu wa kanisa la 'Prophetic Healing and
Deliverance' aliambia vyombo vya habari kuwa alipopata habari ya kutokea
vifo hivyo alihuzunika sana. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
RONALDO AOSHA VYOMBO BAADA YA KUSHINDWA
Duru ziliarifu kwamba kiini cha nyota hao wawili kukutana katika chumba kimoja ni chakula kilichoandaliwa katika hafla hiyo.
Hatahivyo kitu kilichowafurahisha wengi kulingana na wageni ni hatua ya Ronaldo kukubali kushindwa na kupewa kazi ya kuviosha vyombo vya Nadal alivyotumia kula. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
ADEBAYOR ADAI MAMAAKE NI MCHAWI
Mshambuliaji
wa kilabu ya Totenham nchini Uingereza Emmanuel Adebayor amekosana na
mamaake kwa madai kwamba anatumia uchawi kumharibia kazi yake.
Duru
zimearifu kuwa mama huyo tayari ameondoka katika nyumba ya familia huku
dadaake Adebayor akiambia radio moja ya mjini Accra kwamba Adebayor
ndiye aliyemfukuza.Lakini mchezaji huyo wa zamani wa kilabu ya Arsenal anadai kwamba mamaake aliondoka mwenyewe na kwamba hawana mawasiliano yoyote kati yao kwa kuwa amekuwa akitumia uchawi kutaka kumuharibia kazi yake.
'' Ninawezaje kuzungumza na mama ambaye yeye na dadaangu wamekuwa wakijaribu kuniroga''aliwauliza maripota.Mchezo wa Adebayor katika kilabu ya Tottenham umeathirika katika kipindi cha miezi kadhaa iliopita huku Tottenham ikidaiwa kujaribu kumuuza kwa mkopo mchezaji huyo katika dirisha la uhamisho mnamo mwezi January kufuatia kushuka kwa mchezo wake.
Thursday, November 20, 2014
OBAMA KUTANGAZA MABADILIKO YA UHAMIAJI
Ikulu
ya Marekani imesema Rais Obama atatumia muda ambao watazamaji wa
televisheni nchini humo wanaangalia zaidi matangazo siku ya Alhamisi
kutangaza mabadiliko makubwa ya mfumo wa uhamiaji wa nchi hiyo.
Inatarajiwa
kuwa Rais Obama atasema kuwa atatumia madaraka yake aliyopewa kikatiba
kuzuia wahamiaji wapatao milioni tano kurejeshwa makwao na badala yake
wapatiwe vibali vya kufanya kazi nchini humo.Rais Obama amesema hayo katika video iliyotumwa katika ukurasa wa facebook kabla ya hotuba yake.Tangu kuingia madaraka Obama amekuwa akipigania baadhi ya mabadiliko ikiwemo huduma ya utoaji wa huduma za afya kwa mfumo wa bima ya afya. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Subscribe to:
Posts (Atom)