Tuesday, October 14, 2014

WASICHANA WA CHIBOK NIGERIA BADO WANASHIKILIWA NA BOKO HARAM

Aliyekua kiongozi wa Boko Haram, Aboubakr Shekahu
Walikamatwa na kikundi cha kigaidi cha kiislam boko Haram kutoka shuleni kwao huko chibok. Ingawa kunaahadi nyingi kutoka serikali ya Nigeria kwamba wataokolewa na pia watapewa msaada kutoka dunia nzima lakini mpaka sasa bado hawajaonekana, ripoti ya mwandishi wa BBC Will Ross kutoka Lagos inasomwa na Regina Mziwanda
Miezi sita sasa na wasichana 219 bado wametekwa, ni ushaidi kidogo sana unaojulikana kwa kile kilichotokea kuhusu wao tangu walipoondolewa katika shule yao ya bweni huko chibok na boko haram, serikali ya Nigeria imepata wakati mgumu sio tu kuwaokoa lakini pia kwa kuonesha mwitikio mdogo wa umma..
Wazazi wa chibok wameiambia bbc kuwa wameachwa na maneno tu na ahadi zinazovunjwa kwamba watoto wao wa kike watarudi nyumbani hivi karibuni, baba mmoja amesema wanasiasa wamejikita kwenywe uchaguzi wa mwakani ujao zaidi yakuwaokoa watoto wao waliopotea.
Tangu mwezi April vijana wengi wa kike na wa kiume wametekwa nyara na kikundi cha kiislam cha Boko haram ambao wanaongoza mijini na vijijini karibu na mpaka wa Cameroon.
Serikali ya Nigeria imesema jeshi kwa sasa limepata mafanikio dhidi ya vita na boko haram lakini wamezidiwa nguvu kaskazini mashariki ambapo raia hawako salama na maelfu ya watu wamehama makazi yao katika wiki za hivi karibuni. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

YANGA WAWEKA KAMBI KUNDUCHI

Kuelekea kwenye mpambano wa watani wa jadi YANGA Vs SIMBA siku ya jumamosi Oktoba 18, kikosi cha timu ya Young Africans kimeingia kambini leo mchana katika hoteli ya Landmark iliyopo eneo la Kunduchi kujiandaa na mchezo huo ambao umeteka hisia za wapenzi wa soka nchini Tanzania na ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Kocha mkuu Marcio Maximo ameingia kambini na kikosi cha wachezaji 28 kujiandaa na mchezo huo ambapo kikosi chake kitakua kikifanya mazoezi katika Uwanja wa Boko – Veterani kila siku kujweka fit kwa kuzisaka pointi tatu muhimu siku ya jumamosi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Monday, October 13, 2014

NDENJELA AZINDUA MABASI MAPYA YA KISASA NDENJELA JET

MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro akikata utepe kuzindua mabasi ya kisasa ya kampuni ya Mwaji Group  jijini Mbeya.
Ndani ya mabasi ya Ndenjela jet.
MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro pamoja na Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Ahamed Msangi wakifurahia maelezo mafupi toka kwa Mkurugenzi mtendaji    wa Mwaji Group Allan Mwaigaga. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

LWAKATARE. DDP KUCHUANA UPYA LEO





Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare. PICHA|MAKTABA 


Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare leo anatarajiwa kuchuana upya na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) wakati Mahakama ya Rufani itakaposikiliza maombi ya marejeo ya hukumu ya Mahakama Kuu iliyomfutia mashtaka ya ugaidi.

Maombi hayo Namba 5 ya mwaka 2014, yalifunguliwa na DPP akipinga uamuzi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam kumfutia Lwakatare mashtaka ya ugaidi yaliyokuwa yakimkabili yeye na mwenzake, Joseph Ludovick.

Katika maombi hayo, DPP anaiomba Mahakama ya Rufani iitishe majalada ya kesi hiyo na kuchunguza uhalali wa uamuzi wa Mahakama Kuu kuwafutia washtakiwa hao mashtaka ya ugaidi na kisha ifute uamuzi huo wa Mahakama Kuu na amri zote ilizozitoa.

Pamoja na mambo mengine, DPP anadai kuwa haikuwa sahihi Mahakama Kuu kuamua kuwa mashtaka hayo hayakuwa halali, kwani hapakuwa na taarifa zilizowasilishwa dhidi ya washtakiwa ambazo Mahakama Kuu ingezizingatia katika kuamua uhalali wake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU OKTOBA 13, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAALIM SEIF: TUTAZUNGUKA NCHI NZIMA KUPINGA KATIBA INAYOPENDEKEZWA


 
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema chama chake kitazunguka nchi nzima kupiga kampeni ili wananchi waikatae Katiba Inayopendekezwa.
Alisema watafanya hivyo kwa kuwa Katiba iliyopendekezwa imepoteza uhalali kwa vile theluthi mbili (ya wajumbe wa Zanzibar) inayodaiwa kupatikana haiwiani na takwimu za wabunge waliokuwamo ndani na nje ya Bunge na wale waliopiga kura ya hapana na kuwataka wananchi kuikataa wakati ukifika.
Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza Zanzibar, alisema hayo jana akihutubia mkutano wa hadhara wa kwanza tangu Katiba hiyo inayopendekezwa kukabidhiwa kwa Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ikipendekeza mfumo wa Muungano wa serikali mbili badala ya tatu kama ilivyokuwa imependekezwa na rasimu iliyotokana na maoni ya wananchi yaliyokusanywa na iliyokuwa Tume ya Marekebisho ya Katiba. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MSOMI MKENYA PROFESA MAZURI AFARIKI

Profesa Mazuri alisifika sana kwa kuangazia tamaduni za kifarika kwa dunia nzima
Msomi mashuhuri wa Kenya,duniani Profesa Ali Mazrui ameaga dunia nchini Marekani.
Mazrui alikuwa msomi wa maswala ya kisiasa, utamaduni wa kiafrika na maswala ya dini ya kiisilamu.
Mazrui aliyekuwa na umri wa miaka 81 alifariki nchini Marekani ambako amaekuwa akiishi baada ya kuugua kwa mda mrefu.
Duru zinasema kuwa Profesa Mazrui atazikwa mjini Mombasa Pwani ya Kenya alikozaliwa.
Alitoa ombi la kutaka kusikwa Mombasa kabla ya kifo chake akisema angependa kuzikwa katika jumba la kihistoria la Fort Jesus.
Kabla ya kifo chake Marehemu Mazrui alikuwa anafunza katika chuo kikuu cha Binghamton mjini New York. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAKILI DAMAS NDUMBARO ‘ ATUPWA JELA YA SOKA’ MIAKA SABA

ndumba
Kamati ya nidhamu ya Shirikisho la soka nchi TFF, imemfungia wakili Damas Ndumbaro kujihusisha na mambo ya soka kwa muda wa miaka saba na faini ya kiasi cha pesa. Ndumbaro ambaye aliingia katika mzozo mkubwa na rais wa TFF, Ndugu, Jamal Malinzi wiki iliyopita baada ya TFF kuagiza kila klabu kukatwa asilimia tano za mapato yatokanayo na udhamini wa klabu hizo wanaoupata kutoka kwa Vodacom, wadhamini wakuu wa ligi kuu ya Tanzania Bara, na Azam Tv.
Ndumbaro alikimbilia katika vyombo vya habari na kusema wazi kuwa, klabu zimemuagiza kuwaambia TFF kuwa havipo tayari na havitakubali jambo hilo litokee, huku akijiamini na kuchambua baadhi ya vipengele na mambo ya sheria, Ndumbaro alivuka mipaka pale aliposema kuwa wanatafuta wastani wa wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF na kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais wa Shirikisho, Malinzi.
Kikao cha juzi cha kamati ya nidhamu kimefikia uamuzi wa kumfungia, Ndumbaro na kumlilipisha faini kwa sababu. Ndumbaro ambaye alizungumza kama wakili wa klabu za ligi kuu kupitia, Bodi ya Ligi amekanwa ‘ hadharani’ na vilabu huku vikisema kuwa ‘ havikumtuma’ kuzungumza yale ambayo alisema mbele ya vyombo vya habari. Klabu zimesema alizungumza kwa ‘ utashi’ wake mwenyewe, na si wao walimtuma.
‘ Kilichomuhuku’ ni yeye kutaka kubadilisha maamuzi ya kamati ya utendaji ya TFF bila kuthibitishwa na wajumbe wa Bodi ya Ligi na kukubaliana. Kupingana maamuzi ya kamati ya utendaji ni kosa la kinidhamu. Ndumbaro amehukumiwa kutokana na makosa hayo na kama angezungumza kwa niaba ya klabu basi adhabu hiyo ingekwenda kwa kwao, lakini yeye alijizungumzia tu kama vile alivyotaka iwe. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

AMRI KIEMBA AMEFIKISHA UJUMBE KWA PHIRI APANGWE KIKOSI CHA KWANZA, DAR-PACHA…!!!

20140913_160508
Simba SC itacheza na mahasimu wao Yanga SC katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara siku ya Jumapili katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Katika michezo mitatu iliyopita Simba haijapata ushindi, huku mahasimu wao wakiwa na pointi sita katika nafasi ya tatu ya msimamo. Yanga ni timu iliyokamilika kwa sasa, kwa maana ya kucheza kitimu, umoja na ushirikiano.
Screen Shot 2014-10-13 at 10.58.05 AM
Kabla ya safari ya Afrika Kusini, kikosi cha Simba kimeonekana kukosa ‘ utimamu wa mwili na akili’ kwa maana ya wachezaji wake kucheza mpira huku wakiwa na mambo yanayowasumbua, umoja, kiwango cha chini kutoka kwa baadhi ya wachezaji, majeraha, na ufiti wa mchezaji mmoja mmoja, kikosi cha Patrick Phiri kimekuwa katika ‘ majanga’ hayo, lakini kama, mwalimu hapaswi kutumia sababu hizo kufungwa na mahasimu wao ambao wanaingia katika mchezo wa tano mfululizo wakiwa katika ‘ umbo zuri’.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Sunday, October 12, 2014

MJUMBE WA NCCR AWATESA VIGOGO...!!!


“Kutokana na alichofanyiwa kwa kupigiwa kura bila huku akiwa hajafanya hivyo tumemwandikia barua IGP tukimwomba amwekee ulinzi (Hamis) kwani kwa siasa za Pemba (anakoishi Hamis) wanaweza kumdhuru.” PICHA|MAKTABA 

Siku moja baada ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi- Zanzibar, Haji Ambar Hamis kutoa tuhuma za ‘kupigishwa’ kura ya kupitisha Katiba inayopendekezwa bila ridhaa yake, uongozi wa Bunge Maalumu la Katiba umethibitisha kuwapo kwa dosari hizo.
“Sikuwahi kushiriki kwa namna yoyote ile kwenye kupitisha katiba hiyo. Ukweli ni kwamba nimeumia sana na hadi sasa sielewi hatma ya maisha yangu na usalama wa familia yangu kwa ujumla” alisema Hamis alipozungumza na waandishi wa habari jijini hapa.
Akizungumzia tuhuma hizo za Hamis, Naibu Katibu wa Bunge Maalumu la Katiba, Dk Thomas Kashililah alisema: “Kwa taarifa zetu hakupiga kura siku zote tatu za zoezi hilo. Jina lake katika orodha ya wapiga kura lilikuwa namba 63 na hakupiga kura.”
Alisema hata hivyo wakati wa kuondoa majina ya Wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na wale ambao hawakushiriki jina lake lilisahaulika. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NYARANDU: HAKUNA TEMBO ALIYEUAWA SELOUS HIVI KARIBUNI


Waziri wa Maliasili na Utaslii, Lazaro Nyalandu. PICHA|MAKTABA 

Serikali imesema vita vya kupambana na ujangili vinaonyesha mafanikio katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita na hakuna taarifa za kuuawa kwa tembo katika Pori la Akiba la Selous.

Waziri wa Maliasili na Utaslii, Lazaro Nyalandu alisema jana wakati akiaga wanafunzi zaidi ya 100 kutoka China na Tanzania Makao Makuu ya Mamlaka ya Reli Tanzania na Zambia (Tazara) waliokwenda kutembelea pori hilo kubwa kuliko yote barani Afrika kupata mafunzo ya uhifadhi.

Alisema baada ya serikali kuvalia njuga suala la ujangili wananchi wameelimika na sasa wamekuwa wakitoa taarifa za majangili ambazo zimesaidia kuwakamata watu wanaojihusisha na ujangili.

“Baada ya Rais Jakaya Kikwete kukerwa na kukithiri kwa majangili tulianza mapambano na taarifa nilizonazo hadi hivi sasa kwa kipindi cha miezi mitatu hakuna tembo hata mmoja aliyekutwa ameuawa,”alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

POSHO ZA BUNGE ZAIBUA MAPYA


Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta. PICHA|MAKTABA

Siku chache baada ya Bunge la Maalumu la Katiba kumaliza muda wake, matumizi ya fedha zilizobaki kwenye Bunge hilo yameibua mvutano baada ya kuwapo taarifa kuwa fedha hizo ziliisha, huku Wizara ya Fedha ikieleza kuwa bado zipo.
Idadi ya wajumbe wa Bunge hilo kisheria ni 629 na wajumbe ambao hawakuhudhuria vikao vya Bunge hilo tangu Aprili 16, mwaka huu, wanakadiriwa kufikia 140.
Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta, aliwahi kukaririwa akiwaeleza wajumbe wa Bunge hilo kuwa fedha zitakazookolewa zitatafutiwa utaratibu badala ya kurudishwa zilikotoka.
Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni, Katibu wa Bunge, Yahaya Khamis Hamad, alisema hakuna pesa zilizobaki na kwamba waliomba Serikali kuwaongezea fedha za siku nne zilizobakia kabla ya kukabidhi Katiba inayopendekezwa kwa Rais Jakaya Kikwete Jumatano wiki hii. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 12, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MABINGWA WA DUNIA UJERUMANI ‘ YACHAPWA’ KWA MARA YA KWANZA NA POLAND

Poland imeifunga UJerumani kwa mara ya kwanza na kukwea juu ya kilele katika kundi la Nne kuwania nafasi ya kufuzu kwa fainali za Ulaya, Euro, 2016 nchini Ufaransa. Mabingwa wa dunia , Ujerumani ilikuwa na rekodi ya kucheza mara 18 mfululizo bila kupoteza mchezo wowote dhidi ya majirani zao, Poland ambao walipata mabao yote mawili katika kipindi cha pili.
Mshambulizi kinda wa klabu ya Ajax Amsterdam, Arkadiusz Milik, 20 alifunga bao la kuongoza katika dakika ya 51, na dakika mbili kabla ya kumalizika kwa mchezo, Sebastian Mila aliwahakikishia wenyeji ushindi baada ya kufunga bao la pili katika mchezo huo uliopigwa jijini, Warsaw.
Mabingwa hao wa sasa wa dunia, walifungwa mara ya mwisho na Jamhuri ya Czech, Oktoba, 2007 katika michezo ya kufuzu. Ujerumani ilicheza michezo 33 ya kufuzu pasipo kupoteza. Kipa wa Ujerumani, Manuer Neur aliokoa mabao manne ya wazi katika mchezo ambao walishambuliwa sana. Poland iliyokuwa na mshambulizi wa Bayern Munich, Robert Lewandowski ilipiga jumla ya mashuti 19, huku mashuti 12 yakilenga bao.
Kocha wa Ujerumani, Joachim Loew alikwenda Poland huku baaddi ya wachezaji wake muhimu wakikosekana. Ujerumani ilibanwa hasa na walimudu kufanya mashambulizi machache . Walipiga mashuti saba tu ambayo yote yalilenga lango lakini nyota wa mchezo huo, golikipa, Wojciech Szczesny alikuwa imara, kipa huyo wa klabu ya Arsenal aliokoa mara 14. Tomas Mueller, Andre Schurrle na Mario Gotze walishindwa kufunga kwa muda wote waliokuwa uwanjani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UFARANSA YAICHAPA URENO NA C.RONALDO AKIWEMO

Mshambulizi Karimu Benzema alifunga bao la mapema na akatengeneza lingine kwa kiungo Paul Pogba katika kipindi cha pili na kuisaidia Ufaransa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ureno. RicaRrdo Quaresma alitokea benchi katika kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Luis Nani katika dakika ya 68, alifunga kwa mkwaju wa penalti dakika tisa baada ya kuingia uwanjamni .
Ufaransa ambao ndiyo wenyeji wa fainali zijazo za Ulaya waliifunga Ureno ambayo ilikuwa na mshambulizi wake mahiri na mchezaji bora wa dunia, Cristiano Ronaldo katika mchezo uliofanyika jijini Paris. Ronaldo alipiga mashuti manne katika mchezo huo lakini ni shuti moja tu ambalo lilikuwa na uhai. Timu zote zilicheza mchezo wa kufanana, Ufaransa walipiga mashuti 12 sawa na waliyopiga Ureno, lakini wageni walifanikiwa kupiga mashuti mawili tu ambayo yalimsumbua golikipa, Steven Mandanda.
Eliaguim Mangala, RAfaer Varane, Patrice Evra na Bacary SAgna walianza katika safu ya ulinzi na wanne hao hawakuwekwa majaribuni na kikosi kilichopoteza makali cha Ureno. Ronaldo alitoka uwanjani dakika ya 76 akimpisha Jose Mario alianza sambamba Danny na Nani katika safu ya mbele lakini watatu hao hawakuwa tishio kwa Ufaransa ambao walicheza jumla ya faulo 15 katika mchezo huo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SITI MTEMVU NDIYE REDD'S MISS TANZANIA 2014

Miss Tanzania 2014, Siti Abass Zuberi Mtemvu akipunga mkono mara baada ya kuvikwa taji hilo usiku wa kuamkia leo katika shindano lililoshirikisha warembo 30 na kufanyika ukumbi wa Mlimani City Dar es Salaam. Siti Mtemvu ametwaa taji hilo lililokuwa likishikiliwa na Happyness Watimanywa.

Mrembo wa Redd's Miss Tanzania 2014,Sitti Abbas Mtemvu akiwa katika picha ya pamoja na Mshindi wa pili,Lillian Kamazima (kulia) na Mshindi wa Tatu,Jihhan Dimachk mara baada ya kutawazwa rasmi usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City,jijini Dar es Salaam.Sitti Mtemvu alianza kwa kunyakua Redds Miss Chang'ombe na baadaye Redds Miss Temeke. Sitti ni binti wa Mbunge wa Temeke, Mhe. Abbas Mtemvu.

Redd's Miss Tanzania aliemaliza muda wake, Happiness Watimanywa akimpisha crown, Redd's Miss Tanzania wa sasa, Sitti Mtemvu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz




Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BOKO HARAM LAWAACHIA MATEKA 27

boko haram
Rais wa Cameroon amesema kuwa mateka 27 wakiwemo raia 10 wa Uchina wameachiliwa na kundi la wanamgambo wa Boko Haram.
Raia hao wa China walitekwa nyara mwezi mei wakati kampuni moja ya China ilipovamiwa karibu na mpaka wa Nigeria.
Wengine walioachiliwa ni pamoja na mke wa naibu waziri mkuu nchini Cameroon aliyetekwa nyara mwezi Julai.
Haijulikani iwapo fidia ililipwa.
Boko haramu wameeneza mashambulizi kutoka nchini Nigeria kwenda kaskazini magharibi mwa Cameroon. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, October 11, 2014

UTAFITI: VIAGRA HUSABABISHA UPOFU

Kipofu
Watafiti nchini Australia wanadai kwamba dawa inayotumiwa kuongeza nguvu za kiume VIAGRA husababisha upofu baada ya mda mrefu.
Kulingana na Watafiti hao kutoka Australia, kiungo fulani katika dawa hiyo inayotumiwa kukabiliana na ukosefu wa nguvu za kiume,huathiri uwezo wa kuona miongoni mwa wanaume ambao wana ugonjwa wa macho.
Kulingana na gazeti la Nation nchini kenya,Madaktari nchini Australia wamebaini kwamba kiungo fulani katika dawa hiyo kinaweza kusababisha upofu miongoni mwa wanaume wenye tatizo la ugonjwa wa macho.
Vilevile inadaiwa kuwa dawa hiyo pia inaweza kuwaathiri watumiaji ambao wanaona vizuri.
Utafiti huo uliofanywa katika panya,ulibaini kwamba hata watu wasio na ugonjwa wa macho wanaweza kuathirika. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

WENJE ABADILI UPEPO MKUTANO WA RAIS KIKWETE

 

Rais Jakaya Kikwete (katikati) akipita kwenye daraja la waenda kwa miguu la Mabatini, Mwanza jana, baada ya kulizindua, daraja hilo limeghalimu kiasi cha sh8bilioni litasaidia kuondoa tatizo la ajali zilizokuwa zikitokea mara kwa mara eneo hilo. kushoto ni Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuli.


Mbunge wa Nyamagana, Ezekia Wenje jana amebadilisha upepo kwenye mkutano wa Rais Jakaya Kikwete, kwa kueleza kuwa miradi yote ya Serikali ni fedha za wananchi.

Wenje alisema hayo alipopewa nafasi ya kuzungumza kwenye viwanja vya Mabatini mkoani hapa, akidai kuwa miradi yote inayotekelezwa na Serikali ni kodi za wananchi wala siyo fedha za CCM.

Wenje alitoa kauli hiyo mbele ya Rais Kikwete baada ya Waziri wa Ujenzi Dk John Magufuli kudai kuwa CCM ndiyo inayotekeleza miradi yote ya maendeleo kupitia ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2010.

Rais Kikwete alikuwa akizindua daraja ya Mabatini lililojengwa kwa gharama ya zaidi ya Sh1 bilioni na Kampuni ya Adivance Life.

Kabla hajazungumza Wenje alipopanda jukwaani hapo, mamia ya watu waliohudhuria uzinduzi wa daraja hilo walianza kupiga kelele huku wakishangilia kwa kuonyesha ishara ya vidole viwili juu na kuimba ‘Peoples Power’. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAOFISA POLISI 120 WATIMULIWA CCP

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Mangu  

Moshi. Maofisa wa Polisi wapatao 120 wa Jeshi la Polisi, waliokuwa wakihudhuria mafunzo ya kupandishwa vyeo katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Moshi (MPA), wametimuliwa chuoni hapo.
Habari za uhakika zilizopatikana jana kutoka ndani ya chuo hicho zamani kikijulikana kama CCP, zimedai uamuzi wa kuwaondoa chuoni ulitangazwa jana na mkuu wa chuo hicho, Matanga Mbushi.
Vyanzo mbalimbali vililidokeza gazeti hili kuwa, waliotimuliwa chuoni hapo ni maofisa ambao wana ulemavu wa aina mbalimbali walioupata wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kazi.
Habari hizo zilisema hadi jana saa 9:00 alasiri, maofisa hao walikuwa ofisi za mkuu wa chuo hicho wakisubiri kupatiwa maelekezo ya namna ya kurejea katika vituo vyao vya kazi mikoa mbalimbali. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 11, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, October 10, 2014

MAMBO HAYA: MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI AMTUNDIKA MIMBA MWALIMU WAKE....!!!


Hii ni moja ya picha mbalimbali za wajawazito kama inavyonekani siyo ya mwalimu muhusika kwa tukio hilo.

WAKATI ikiwa imezoeleka kuwa baadhi ya walimu wa kiume huwarubuni wanafunzi wao wa kike na hata kuwaharibia kabisa ndoto zao za kielimu kutokana na kuwapa ujauzito, hali imekuwa tofauti mkoani Rukwa ambako mwanafunzi wa Kidato cha Pili anadaiwa kumzalisha mwalimu wake.

Mwanafunzi huyo aliyemzalisha mwalimu wake ana umri wa miaka 17, wakati mwalimu huyo anayefundisha katika Shule ya Sekondari ya Umma ya Nkasi, iliyopo mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Nkasi, Rukwa, ana umri wa miaka 25.

Tukio hilo linalotajwa kuwa la kwanza kutokea wilayani hapa, limekuwa gumzo kubwa kwa wakazi wa Nkasi na wilaya jirani.

Hata hivyo, kwa wanafunzi, wamekuwa wakimpongeza mwenzao kwa kujaliwa kupata mtoto katika umri wake huo mdogo, huku mzazi mwenzake akiwa na uhakika wa maisha kutokana na kuwa ni mtumishi serikalini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NEC: HAKUNA KURA YA MAONI BILA DAFTARI JIPYA




Rais Jakaya Kikwete akipokea Katiba Inayopendekezwa kutoka kwa Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta wakati wa hafla iliyofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma juzi. Katikati ni Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein. 


Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema haitaendesha uchaguzi wa aina yoyote, wala kuitisha kura ya maoni hadi kazi ya kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura itakapokamilika.

Kauli ya NEC imekuja siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kukabidhiwa Katiba inayopendekezwa na Mwenyekiti wa lililokuwa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta na kulitaja suala la uboreshaji wa daftari la hilo kama mambo matatu yanayoiweka kura ya maoni kupitisha Katiba hiyo njiapanda.

Mambo mengine ni Sheria inayotaka kura hiyo ipigwe ndani ya siku 84 baada ya Katiba inayopendekezwa kuchapishwa na kufanyiwa marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.

Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva alisema jana kwamba kuendesha uchaguzi bila kuboresha daftari hilo ni kuongeza malalamiko kwa wananchi na wadau, hususan vyama vya siasa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WASHUKIWA 7 WA UCHAWI WAUAWA KIGOMA



Moja ya nyumba zilizoteketezwa katika Kijiji cha Murufiti ambapo watu saba waliuawa kwa kuchomwa moto.

Kigoma. Watu saba wameuawa kwa kuchomwa moto ndani ya nyumba katika tukio ambalo nyumba 18 ziliteketezwa na mbili kubomolewa na wananchi waliodai wanawaua wachawi katika Kijiji cha Murufiti, Kasulu, mkoani Kigoma.
Polisi wameeleza kuwa tayari watu 17 wamekamatwa kwa kuhusika kwenye tukio hilo.
Miongoni mwa waliouawa katika tukio hilo lililotokea Jumatatu iliyopita ni John Mavumba (68) na mkewe Elizabeth Kaje 55 ambao pamoja na wenzao walikuwa wakituhumiwa kuwa ni washirikina. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 10, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RAIS MUSEVEN AKATAA WATU KUSALIMIANA....!!!

shaking hands 
October 9 2014 nchi ya Uganda iliazimisha uhuru wake huku rais wake Yower Museven akizungumza mambo muhimu matatu kwa wananchi wake ambapo ishu ya kwanza ni kuwataka wananchi wake kuwa makini kutokana na tishio la magonjwa ya Marburg pamoja na Ebola hivyo waache kusalimiana kwa kushikana mikono pamoja na kukumbatiana bila kuwepo ulazima wa kufanya hivyo.
Alisema magonjwa hayo kwa sasa yameonekana kuchukua nafasi kubwa duniani na amewataka kuwa makini zaidi ili yasizidi kusambaa lakini pia kumekuwa na utamaduni wa baadhi ya watu hasa wanaoishi maeneo yenye misitu kula nyama za nyani ambazo magonjwa hayo yanaaminika kuanzia huko, nao pia amewataka waache ili haya magonjwa ya ajabu yasije kwa binadamu.
Kitu kingine ambacho rais huyo alizungumza ni kitendo cha mabosi wa mahakama ya The Hague  ya Uholanzi kumtaka rais mwenzake wa Kenya, Uhuru Kenyatta kuhudhuria kikao cha kujibu tuhuma dhidi yake kuhusiana na ghasia zilizotokea nchini kwake na kusema kililenga kudharau na kusitisha mkutano uliofanyika juzi nchini kwake.
Alisema pamoja na Serikali ya nchi hiyo kuomba rais Kenyatta kuhudhuria mkutano huo muhimu lakini mahakama hiyo ilionekana kukataa na kulazimisha ahudhurie katika kesi hiyo.
Hata hivyo Kenyatta alikanusha tuhuma za yeye kuhusika na ghasia zilizosababisha kupoteza maisha ya zaidi ya watu 1200 huku wengine zaidi ya laki sita wakikosa mahali pa kukaa mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu na jambo la mwisho alilozungumzia ni kuhusu timu ya Taifa ilo ambalo inakabiliwa na mchezo dhidi ya Togo ambapo aliwatakia kila la Kheri. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ENGLAND YASHINDA TENA, ROONEY BADO BAO MOJA AVUNJE REKODI YA CHARLTON

article-2786987-22162C8600000578-875_964x386
Mshambulizi wa England, Wayne Rooney anahitaji kufunga bao moja tu ili kufikia rekodi ya ufungaji mabao ‘ wa muda wote’ katika kikosi cha ‘ The Three Lions’. Mshambulizi wa zamani wa ‘ Simba Watatu’ Gwiji Sir Bobby Charlton alifunga mabao 49 rekodimbayo haijapata kufikiwa. Miaka lifunga moja yakumi iliyopita, Michael Owen alionekana kama mchezaji ambaye angeifikia rekodi hiyo lakini majeraha yalimfanya kuwa nyuma kwa tofauti ya mabao tisa.
Nahodha wa England, Rooney ‘ Baba Kai’ alifunga moja ya mabao matano ya England usiku wa kuamkia leo wakati England ilipochomoza na ushindi wa kishindo dhidi ya San Marino katika uwanja wa Wembley. Mlinzi wa kati, Phill Jargierka alifunga bao la kuongoza dakika ya 24 kabla ya Rooney kufun ga bao la 48 kwa England kwa mkwaju wa penalti.
Danny Welbeck alifunga bao lake la Tatu katika michezo miwili ya England mara baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, Andros Townsend alifunga bao la nne dakika ya 72, kabla ya wageni kujifunga bao la tano kupitia kwa Alessandro Della Valle dakika tano baada ya bao la Townsend. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Thursday, October 09, 2014

KATIBA INAYOPENDEKEZWA YAKABIDHIWA


Mwenyekiti wa Bunge maalum la Katiba Mhe.Samuel Sitta akikabidhi  katiba inayopendekezwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho kikwete na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt.Mohamed Ali Shein katika hafla iliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma Oktoba 08, 2014.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho kikwete na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt.Mohamed Ali Shein wakiwa wameinua…

Mwenyekiti wa Bunge maalum la Katiba Mhe.Samuel Sitta akikabidhi  katiba inayopendekezwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho kikwete na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt.Mohamed Ali Shein katika hafla iliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma Oktoba 08, 2014.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho kikwete na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt.Mohamed Ali Shein wakiwa wameinua juu  Katiba inayopendekezwa katika hafla iliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma Oktoba 08, 2014 Kulia ni Mwenyekiti wa Bunge maalum la Katiba Mhe.Samuel Sitta akifuatiwa na Makamu wake Mhe samia Suluhu Hassan. 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la katiba, Samuel Sitta amekabidhi Katiba inayopendekezwa  hafla iliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma Oktoba 08, 2014 kwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho kikwete na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt.Mohamed Ali Shein. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...