Sunday, October 12, 2014

NYARANDU: HAKUNA TEMBO ALIYEUAWA SELOUS HIVI KARIBUNI


Waziri wa Maliasili na Utaslii, Lazaro Nyalandu. PICHA|MAKTABA 

Serikali imesema vita vya kupambana na ujangili vinaonyesha mafanikio katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita na hakuna taarifa za kuuawa kwa tembo katika Pori la Akiba la Selous.

Waziri wa Maliasili na Utaslii, Lazaro Nyalandu alisema jana wakati akiaga wanafunzi zaidi ya 100 kutoka China na Tanzania Makao Makuu ya Mamlaka ya Reli Tanzania na Zambia (Tazara) waliokwenda kutembelea pori hilo kubwa kuliko yote barani Afrika kupata mafunzo ya uhifadhi.

Alisema baada ya serikali kuvalia njuga suala la ujangili wananchi wameelimika na sasa wamekuwa wakitoa taarifa za majangili ambazo zimesaidia kuwakamata watu wanaojihusisha na ujangili.

“Baada ya Rais Jakaya Kikwete kukerwa na kukithiri kwa majangili tulianza mapambano na taarifa nilizonazo hadi hivi sasa kwa kipindi cha miezi mitatu hakuna tembo hata mmoja aliyekutwa ameuawa,”alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Kasi ya uuaji wa wanyama hao kwa ajili ya biashara haramu ya meno ilikua kwa kasi katika miaka ya karibuni ambapo takriban tembo 10,000 walikuwa wakaiuawa nchini kwa mwaka.

Waziri Nyalandu aliwaasa Watanzania kushiriki kutokomeza ujangili nchini, kwani maliasili zilizopo ni za Watanzania wote.

na vizazi vijavyo.

Waziri Nyalandu aliishukuru serikali ya China ambayo imekuwa ikifanya jitihada za kusaidia sekta mbalimbali za maendeleo nchini ikiwamo uhifadhi na kwamba ushirikiano huo ni wa muda mrefu kutokana na waasisi wa nchi hizo Mwalimu Nyerere na Mao Tse Tung.

“Inafurahisha kuwa uhusiano wetu huu umekuwa wa tangu enzi hizo, ndiyo maana kiongozi huyo wa China alituzawadia hata reli hii kwa ajili ya kuimalisha uchumi wa Tanzania.

Kutokana na ushirikiano huo Waziri Nyalandu alisema kupitia wizara yake itaalika wanafunzi 100 kuja kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii na kuelewa umuhimu wa uhifadhi wa maliasili.

Hali kadhalika aliahidi wanafunzi wa Tanzania kutembelea China ili nao wapate fursa ya kujua masuala mbalimbali ya faida ya maliasili na uhifadhi ili kukuza idadi ya watalii kutoka nchi hiyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...