Sunday, October 12, 2014

MJUMBE WA NCCR AWATESA VIGOGO...!!!


“Kutokana na alichofanyiwa kwa kupigiwa kura bila huku akiwa hajafanya hivyo tumemwandikia barua IGP tukimwomba amwekee ulinzi (Hamis) kwani kwa siasa za Pemba (anakoishi Hamis) wanaweza kumdhuru.” PICHA|MAKTABA 

Siku moja baada ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi- Zanzibar, Haji Ambar Hamis kutoa tuhuma za ‘kupigishwa’ kura ya kupitisha Katiba inayopendekezwa bila ridhaa yake, uongozi wa Bunge Maalumu la Katiba umethibitisha kuwapo kwa dosari hizo.
“Sikuwahi kushiriki kwa namna yoyote ile kwenye kupitisha katiba hiyo. Ukweli ni kwamba nimeumia sana na hadi sasa sielewi hatma ya maisha yangu na usalama wa familia yangu kwa ujumla” alisema Hamis alipozungumza na waandishi wa habari jijini hapa.
Akizungumzia tuhuma hizo za Hamis, Naibu Katibu wa Bunge Maalumu la Katiba, Dk Thomas Kashililah alisema: “Kwa taarifa zetu hakupiga kura siku zote tatu za zoezi hilo. Jina lake katika orodha ya wapiga kura lilikuwa namba 63 na hakupiga kura.”
Alisema hata hivyo wakati wa kuondoa majina ya Wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na wale ambao hawakushiriki jina lake lilisahaulika. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
“Tuligundua dosari hiyo na ndiyo maana hatukugawa vitabu siku ya sherehe, tumerekebisha kwa kuchapa vitabu vipya na vitakuwa tayari Jumatano.
“Aidha, majina yanayoonekana katika kitabu ukiacha hilo la Haji lililokosewa majina mengine yapo sawa kwa pande zote mbili na kwamba majina hayo siyo waliopiga kura tu hata wale ambao walishiriki, lakini hawakupata fursa ya kupiga kura majina yao yapo katika kitabu,” alisema Dk Kashililah.
Utata wa kura
Kwa upande wa Zanzibar kura mbili ndizo ambazo zilipitisha Katiba hiyo inayopendekezwa jambo ambalo wadau mbalimbali walihoji namna zilivyopatikana theluthi mbili.
Akitangaza matokeo hayo Oktoba 2, mwaka huu bungeni mjini Dodoma, Dk Kashililah alianza kutoa matokeo ya upande wa Zanzibar ambako wajumbe wengi walikuwa na wasiwasi kuwa huenda usipate akidi ya kura 146 iliyotakiwa.
Kwa jumla, kura za ‘ndiyo’ za Zanzibar zilikuwa ama 147 au 148 na ‘hapana’ ama saba au nane; wakati kwa matokeo ya Tanzania, wajumbe waliopiga kura walikuwa 335 na kura moja tu ndiyo ilikataa ibara zote na kura mbili zilichomoza kukataa baadhi ya ibara.
Akizungumza na gazeti hili jana, Kaimu Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Faustin Sungura alisema, kitendo kilichofanywa na uongozi wa Bunge hilo kinahatarisha usalama wa Hamis.
“Sitta alimkabidhi Rais Kikwete Katiba inayopendekezwa batili kutokana na mchakato wake kugubikwa na utata hususan upatikanaji wa theluthi mbili upande wa Zanzibar, wamepandikiza majina ambayo hayana uhalali kama hili la Hamis walivyomfanyia sasa mpaka hapo tunaendelea kutilia shaka uhalali wa theluthi mbili za Zanzibar. Na kuongeza kuwa;
“Kutokana na hatua hiyo, tumemwandikia barua Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Ernest Mangu kumuomba kumwekea ulinzi kiongozi wetu, kwani atakaporejea Pemba na siasa za huko zilivyo wanaweza wakamdhuru kutokana na taarifa kuwa amepiga kura ya ndiyo,” alisema.
Hata hivyo, Msemaji wa Jeshi hilo, Advera Senso alipotafutwa kutaka kujua kama barua hiyo imefika hakupatikana na alipotumiwa ujumbe mfupi wa maandishi hakujibu.
“Kutokana na alichofanyiwa kwa kupigiwa kura bila huku akiwa hajafanya hivyo tumemwandikia barua IGP tukimwomba amwekee ulinzi (Hamis) kwani kwa siasa za Pemba (anakoishi Hamis) wanaweza kumdhuru.”
Kuhusu kura za hapana zilizopigwa na baadhi ya wajumbe alisema kitendo kilichofanywa kinakandamiza uwepo wa demokrasia nchini.
“Haiwezekani mtu anapiga kura ya hapana halafu eti unasema tutajadiliana na hao waliopiga kura ya hapana kuona ni kwa nini...yote haya wameyafanya ili kuhalalisha kile walichokuwa wakikitaka,” alisema Sungura.
CUF na mbinu chafu
Siku mbili kabla ya Bunge hilo kupiga kura ya kuipitisha Katiba inayopendekezwa Septemba 29 mwaka huu, Chama cha Wananchi (CUF) kilibaini mbinu zilizopangwa kutumika ili kuongeza idadi ya kura zilizotarajiwa kupigwa kwa njia ya mtandao kuunga mkono Katiba iliyopendekezwa.
Hatua hiyo ilikuwa ni baada ya Bunge Maalumu kufanya marekebisho ya kanuni zake ili kuwaruhusu wajumbe waliokuwa nje ya Ukumbi wa Bunge wakiwamo waliokwenda Hijja kuipigia kura Katiba inayopendekezwa.
Chini ya marekebisho hayo, mjumbe aliye nje ya Bunge, ataruhusiwa kupiga kura ya wazi au ya siri kwa njia ya nukushi (Faksi) au barua pepe kama itakavyoelekezwa na katibu kwa kushauriana na mwenyekiti.
Akizungumzia njama hizo, Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CUF, Yusuf Salim Hussein, alizitaja mbinu hizo kuwa ni pamoja na kuingiza majina ya wabunge wa chama hicho na Chadema kwenye orodha ya waliopiga kura.
“Taarifa tulizo nazo sisi kutoka huko Dodoma ni kwamba yatawekwa majina yasiyopungua 10 ya chama chetu na 10 ya Chadema kwamba wamepiga kura katika njia ya mtandao,” alisema Hussein.
Alisema wabunge na wawakilishi wa chama cha CUF walikuwa na kikao cha pamoja na kukubaliana kwamba hakuna mjumbe yeyote atakayepiga kura kwa njia ya mtandao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na Mwananchi

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...