Tuesday, May 27, 2014

MISRI WAMCHAGUA RAIS MPYA

Mabango yanayotangaza uwaniaji wa aliyekuwa Mkuu wa jeshi la Misri, Abdel Fatah al-Sisi, kama Rais
Raia wa Misri wanapiga kura kwa muda wa siku mbili kumchagua rais mpya chini ya ulinzi mkali kuhakikisha mchakato wa upigaji kura unafanyika kwa usalama.
Karibu maafisa wa usalama laki mbili wameshika doria kote nchini Misri serikali ikionya dhidi ya hatari za usalama zinazoweza kusababishwa na itikadi kali za kiislam .
Adbel Fatah al-Sisi Kiongozi wa kijeshi wa zamani aliyeongoza mapinduzi ya kijeshi dhidi ya rais wa awali Mohammed Morsi anatarajiwa kupata ushindi kwa u rahisi.
Oparesheni kubwa ya usalama inayoendelea nchini Misri ni ushahidi kamili kuwa utawala wa sasa unaoungwa mkono na jeshi unatambua kuwa ugaidi unaoungwa mkono na Waislamu wenye itikadi kali upo na unaweza kuteguliwa wakati wo wote.
Mbinu ya kukabiliana na ugaidi huo ya Abdel Fatah al-Sisi haijabadilika ila tu ni magwanda yake ya kijeshi ya field Mashel yaliyojaa medali yaliyobadilishwa na nguo za kiraia.
Ametangaza katika kampeni yake kuwa anaunga mkono kuangamizwa kabisa kwa kundi la Muslim Brotherhood ambalo limeshuhudia maelfu ya wanachama wake wakizuiliwa na mamia wakihukumiwa vifo.
Bwana Sisi ametoa wito kwa watu wanaotakia Misri amani na utangamano baada ya miaka kadhaa ya mapinduzi na ghasia na ameheshimiwa kiwango cha kusujudiwa na wengine hivi kwamba unaweza kununua peremende au chokoleti dukani iliyopachikwa picha yake.
Mpinzani wake mwenye mrengo wa kushoto, Hamdeen Sabbahi, anatajwa katika vyombo vya habari ambavyo vinaoenekana kuamua tayari kuwa yeye atashindwa katika Uchaguzi unaoanza leo.
Ingawa wapiga kura wana mazoea ya kubadilika dakika za mwisho kabla ya uchaguzi lakini wengi nchini Misri watashangaa iwapo Bwana Sisi hashindi uchaguzi huu, na tena kwa urahisi. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo: BBC

Saturday, May 24, 2014

MBUNGE NA BIBI HARUSI MTARAJIWA VICY KAMATA AUGUA GHAFLA SAA 36 KABLA YA HARUSI...!!!

Mbunge Vicky Kamata akiwa amelazwa Hospitali ya Tabata General, Dar es Salaam jana. Picha na Florence Majani 

Dodoma/Dar es Salaam. Ni matukio nadra kutokea katika maisha, lakini haya ndiyo yaliyomkuta Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Vicky Kamata, baada ya kuugua ghafla saa 36 kabla ya harusi yake.
Kuugua kwa bibi harusi huyo mtarajiwa, kumezua gumzo katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma na maeneo mengine nchini, kutokana na kile kilichoelezwa kwamba harusi hiyo ilipangwa kuwa ya kifahari ikitarajiwa kutumia Sh96 milioni.
Kamata ilikuwa afunge ndoa leo katika Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Mama wa Mkombozi, Sinza Dar es Salaam na tayari kadi za mialiko zilishasambazwa kwa watu mbalimbali wakiwamo wabunge.
Habari za kuugua ghafla kwa mbunge huyo ambaye pia ni msanii wa muziki aliyetamba na kibao chake cha ‘Wanawake na Maendeleo’ zilianza kuzagaa kwa kasi juzi jioni nchini. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

LIGI YA MABINGWA: SAMATA, ULIMWENGU KUIONGOZA TP MAZEMBE DHIDI YA MAHASIMU WAO AS VITA MJINI LUBUMBASHI


1
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
WASHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samata na Thomas Emmanuel Ulimwengu kesho jumapili wanatarajia kuiongoza TP Mazembe katika mchezo wa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya wapinzani wao wakubwa, AS Vita mjini Lubumbashi.
Timu hizi hasimu zitakutana katika mchezo wa kesho zikiwa na kumbukumbu ya kusababisha maafa ya vifo vya watu zaidi ya 15 katika mchezo wao wa ligi kuu ya DR Congo wiki za karibuni.
Tukio hilo baya lilitokea mjini Kinshasa baada ya mashabiki wa AS Vita kutoridhishwa na kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa wapinzania wao TP Mazembe.
Mchezo wa kesho umevuta hisia za mashabiki wengi wa soka, kwani timu hizi zinapokutana, upinzani unakuwabmkubwa mno nje ya uwanja na ndani ya uwanja.
TP Mazembe wataingia katika mchezo wa kesho wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kupigwa bao 1-0 kwenye mchezo wao wa kwanza wa kundi A na Al Hilal ya Sudan mnao mei 17 mwaka huu.
Mei 18 mwaka huu, AS Vita walitumia vyema uwanja wao wa nyumbani baada ya kuilaza Zamalek ya Misri mabao 2-1, hivyo wataingia katika mchezo huo wa kundi A wakiwa na morali kubwa ya kusaka ushindi wa pili.
Mechi nyingine ya kesho jumapili itakuwa ya Kundi B kati ya wenyeji ES Setif ya Algeria dhidi ya SC Sfaxine ya Tunia.
Mei 18 mwaka huu SC Sfaxine waliifumua Al Ahly Benghazi ya Libya mabao 3-1, wakati mei 17, 2014, ES Setif waliifunga mabao 2-1 Esperance ya Tunisia.
Mbali na mechi hizo za kesho, leo hii mitanange mingine inaendelea ambapo kundi A, wenyeji Zamalek watawakaribisha Al Hilal kutoka nchini Sudan.
Huu utakuwa mchezo muhimu kwa Mafarao waliopoteza mechi iliyopita. Al Hilal wao watakuwa wanahitaji ushindi wa pili katika michuano hiyo.
Mechi ya kundi B leo hii, wenyeji Al Ahly Benghazi ya Libya waliopoteza mechi ya kwanza kwa mabao 3-1 watakabiliana na miamba ya soka la Tunisia, Esperance ambao nao mechi ya kwanza walilala kwa mabao 2-1. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

CECAFA NILE BASIN CUP, MBEYA CITY FC KUTUPA KARATA YAO YA KWANZA LEO

IMG_1150 
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano mipya ya CECAFA Nile Basin Cup inayoendelea nchini Sudan , Mbeya City fc wanaanza kutupa karata yao ya kwanza leo hii majira ya 11:30 jioni kwa saa za Sudan dhidi ya Academie Tchite ya Burundi. Kuelekea katika mechi hii itakayopigwa uwanja wa Al-Merreikh mjini Khartoum, ushinidi ni muhimu kwa Mbeya City fc ili kupata morali ya mashindano haya yaliyoanza jana kwa mechi tatu kupigwa viwanja viwili tofauti. Kocha Juma Mwabusi ameuambia mtandao huu kwa njia ya simu kutoka nchini Sudan kuwa kikosi chake kipo salama na kipo tayari kwa ajili ya mechi ya leo jioni. “Tumewasili salama mjini Khartoum. Tulichelewa kufika huku ili angalau kuzoa hali ya hewa. Lakini haimaanishi hatuwezi kushindana. Sisi tumejiandaa vizuri na tulikaa Dar kwenye joto ingawa hailingani na Sudan”. “Mashabiki wetu wawe na imani na timu yao. Tunaiwakilisha nchi na tutapambana kwa nguvu zote. Wachezaji wana morali ya kufanya vizuri”. Alisema Mwambusi. Mbali na mchezo huo wa jioni, mechi nyingine ya usiku itakuwa baina ya AFC Leopard ya Kenya dhidi ya Enticelles ya Rwanda. Katika mechi zilizopigwa jana, kwa mujibu wa msemaji wa CECAFA Rodgers Mulindwa, Victoria University ya Kenya iliilaza Malakia FC ya Sudan kusini bao 1-0. Wenyeji Al-Merreikh waliibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Polisi ya visiwani Zanzibar. Nao Al-Shandi waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Dkhill ya Djibouti. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

CCM: "HATUWEZI KUWAVUMILIA WATENDAJI WA SERIKALI WANAOKWAMISHA UTEKELEZWAJI WA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI"

Katibu wa CCM wilaya ya kilolo Bw. Raphel Mahumba mwenye pama, akimuagiza Diwani wa kata ya ukumbi afuatilie nani anaye kwamisha ujenzi wa zahanati ya kitowo na hatua zichukuliwe haraka, aliye vaa skafu ni katibu mwenezi wa chama.
Wananchi waliongozana na katibu wa CCm wilaya ya Kilolo kuangalia ujenzi wa zahanati ya Kotowo ambayo imesimama bila sababu za msingi. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

ZIJUE KANUNI ZA SAYANSI ZA KUSAIDIA MTU KUISHI MAISHA MAREFU


Nyama nyekundu inaelezwa kuwa ni moja ya vyakula vinavyopunguza urefu wa maisha. 

Na Clifford Majani, Mwananchi


Kwa miaka mingi sana binadamu wa karne zote wamekuwa wakitafuta siri za maisha marefu, kuzuia uzee na hata kuzuia kifo. Lakini pamoja na jitihada nyingi mambo haya yameendelea kuwa changamoto kubwa kwenye maisha ya mwanadamu katika nchi mbalimbali duniani.  Kwa Tanzania, inakadiriwa kuwa umri wa kuishi kwa wanaume ni takriban miaka 58.2 na kwa wanawake ni miaka 60.5.
Muda huu wa kuishi ni mfupi sana ikilinganishwa na wenzetu katika nchi zilizoendelea kama vile Marekani ambako wastani wa kuishi ni unakadiriwa kuwa ni miaka 78.2. Wanasayansi wamekuwa na nadharia nyingi kuhusu sababu zinazosababisha binadamu azeeke na kufa mapema. Ila wengi hufikiri kuwa tunazeeka mapema kutokana na sababu za maumbile na vinasaba tunavyorithi kwa wazazi wetu.
Wengine husema kuwa tunazeeka haraka kutokana na kuwa na mtindo usiofaa wa maisha. Mtaalamu wa Afya, Dk Mark Stibich  anasema kwamba kuzeeka haraka na kuishi maishi mafupi ni suala mtambuka na linahusisha mambo kama vile vinasaba, kemia, fiziolojia ya mwili pamoja na tabia zetu kwa mujibu wa makala yake ya Mei 10, 2014 liyowekwa kwenye tovuti ya longevity.about.com.
Mtaalamu wa maabara nchini Ujerumani, Dk James Vaupel anadai kuwa vinasaba huchangia kasi ya kuzeeka kwa asilimia tatu pekee na sehemu kubwa ya visababishi vya kuzeeka haraka hutokana na mtindo wa maisha usiofaa pamoja na lishe duni. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MEI 24, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

ALIYEZAA MTOTO WA AJABU HANDENI ALONGA


Mwajuma Seif (50). PICHA|MAKTABA 



Tangu mwaka 2012 zaidi ya watoto 154 wamezaliwa na wanawake walio juu ya umri wa miaka 50. Miongoni mwao, wamo waliotokana na teknolojia ya upandikizaji. Pamoja na madaktari kuonya kuwa kuzaa katika umri mkubwa kunahatarisha maisha ya mama na mtoto, wanawake hasa matajiri wamekuwa wakizaa katika umri mkubwa. Wilayani Handeni Mkoa wa Tanga, Mwajuma Seif (50) aliweka rekodi ya kujifungua watoto mapacha katika umri huo.

Lakini Mwajuma ana kingine cha ziada tofauti na wanawake wengi wanaozaa katika umri huo; alizaa kwa njia ya kawaida na si kwa teknolojia ya upandikizaji. Tofauti nyingine ya mwanamke huyo si kwamba alizaa katika umri huo kwa kuwa hakuwa na mtoto; ujauzito huo ulikuwa ni wa 13. Daktari anayemwangalia Mwajuma, Elinisa Mushi anasimulia mkasa wa mwanamke huyo akisema pamoja na umri, kingine kilichomshangaza ni mtoto wa ajabu aliyemzaa .

Anaeleza kuwa walimpokea Mwajuma, ambaye ni mkazi wa Kata ya Sindeni zaidi ya mwezi mmoja uliopita akiwa na ujauzito, lakini walishangazwa na tumbo la mama huyo kwani lilikuwa kubwa sana kiasi cha kuhisi kulikuwa na tatizo fulani. Ndipo walipoamua kuanza kumfanyia uchunguzi. Baada ya kupima ujauzito huo kwa kutumia mashine ya ultra sound (kamera ya mionzi), waliona ni kweli tumboni kuna watoto wenye maumbo yasiyoeleweka hivyo walitaka kumsafirisha kumpeleka Hospitali ya Mkoa wa Tanga, Bombo lakini walishindwa kutokana na hali yake. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

UN: VATICAN INAPUUZA HAKI ZA WATOTO

Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis
Kamati ya Umoja wa Mataifa dhidi mateso imelaumu vikali kanisa Catholiki kwa kutoshughulikia ipasavyo suala la unyanyasaji wa ngono ndani ya kanisa hilo.
Katika ripoti iliyochapishwa hivi karibuni na Umoja huo mjini Geneva , Kamati hiyo imeushutumu utawala wa Vatican kwa kuwahamisha watawa kutoka parokia moja hadi nyingine kuwaepusha kushtakiwa, na kupuuza haki za waathiriwa za kupokea fidia .
Utawala wa Vatican uliithinisha mkataba dhidi ya unyanyasaji , ukatili na matendo yaliyo kinyume na utu.
Uchunguzi uliofanywa na kamati ya Umoja wa Mataifa dhidi ya Vatcan ni sehemu ya uchunguzi wa mara kwa mara wa kamati hiyo dhidi ya nchi wanachama ili kuhakikisha mikataba inatekelezwa. Kamati hiyo ya Umoja wa Mataifa ina hofu kuwa wakati utawala wa Vatcan umeelezea kutokubali kamwe kuwepo kwa unyanyasaji ndani ya kanisa, maneno hayaendani na vitendo.
Kamati hiyo imekasirishwa zaidi na kwamba Utawala wa Vatcan unasisitiza kuwa unahusika zaidi na wahudumu wanaofanyika kazi ndani ya Vatcan kwenyewe , kuliko makasisi wake wanaofanyika kazi kwingineko duniani.
Mwezi Januari mwaka huu utawala wa Vatican ulichunguzwa upya na kamati ya Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watoto, baada ya kupokea ukosoaji kama huo kwamba ulishindwa kuwalinda watoto waliokuwa chini ya uangalizi wake. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo: BBC

Friday, May 23, 2014

BIBI ANASWA AMEBEBA 'UNGA' UWANJA WA NDEGE DAR...!!!


“Huyu ni mzee, lakini tumeshangaa kuona bado ana nguvu za kutosha na tulishangaa baada ya kutoa kete 20 kwa mara moja katika awamu ya kwanza, jambo hili si rahisi kutokana na umri wake,” .PICHA|MAKTABA 



Dar es Salaam. Bibi mmoja raia wa Nigeria, Olabisi Ibidun Cole (65) amevunja rekodi ya umri wa watu wanaokamatwa wakiwa na dawa za kulevya katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

Cole alikamatwa Jumatatu akiwa amemeza kete 82 aina ya heroini zilizokuwa zimefungwa kwenye karatasi zinazofanana na ganda la sigara, ambazo si rahisi kuonekana katika mitambo.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Mkuu wa Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya, Alfred Nzowa zimesema pamoja na mbinu zake na kujiamini, mwanamke huyo alikamatwa kutokana na ushirikiano wa vitengo mbalimbali vya uwanja wa ndege.

Kamanda wa Polisi wa Uwanja wa Ndege, Hamisi Selemani alisema mwanamke huyo alikamatwa Mei 19, mwaka huu saa tisa alasiri akijiandaa kwenda Paris, Ufaransa kwa ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia.

Selemani alisema raia huyo aliwasili nchini Mei 15, mwaka huu na alikaa muda wote bila ya kuwa na shughuli yoyote, jambo ambalo lilitiliwa shaka na kumkamata. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

KAKA WA MTOTO ALIYEFUNGIWA KWENYE BOKSI NAYE 'APOTEA'

 Rashid Mvungi  akimuangalia mtoto wake Nasrah Rashid (4) ambaye ni mlemavu wa viungo aliyefungiwa chumbani na kufichwa kwenye boksi bila ya kufanyiwa usafi tangu akiwa na umri wa miezi tisa.  

Morogoro. Zimeibuka taarifa kwamba mtoto aliyekuwa amefungiwa kwenye boksi kwa miaka minne na mama yake mkubwa, Nasra Rashid (4) alikuwa na kaka aliyefahamika kwa jina la Nasoro ambaye hadi sasa hajulikani mahali halipo.

Wakati polisi ikisema imefurahi kupata taarifa hizo na kwamba itazifanyia kazi, habari zilizopatikana jana kuhusu hali ya Nasra zimesema atafanyiwa vipimo 18 ili kubaini hali ya afya yake. Vipimo vya awali, vimebaini kuwa amevunjika mifupa ya mikono na miguu na kwamba atapelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Kuhusu kaka yake, baadhi ya majirani wa nyumba aliyokuwa anaishi mama mzazi wa Nasra enzi za uhai wake walidai kuwa Mariamu alikabidhiwa watoto wawili kuwalea baada ya mama yao kufariki dunia.

Mmoja wa majirani hao, Ramadhani Mansuri alisema wakati mama mzazi wa Nasra akiishi eneo la Mjimpya alikuwa na watoto wawili akiwamo Nasoro ambaye aliachwa akiwa na umri kati ya miaka 14-15.

Vipimo

Ofisa Ustawi wa Jamii, Mkoa wa Morogoro, Oswin Ngungamtitu alisema taarifa alizopata kutoka kwa madaktari zinasema kuwa mtoto huyo atafanyiwa vipimo 18 ili kubaini hali ya afya yake.

Akizungumzia matokeo ya vipimo vya awali, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, Dk Rita Lyamuya alisema haijafahamika sababu za kuvunjika kwa mifupa hiyo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 23, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.

.
.
.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

DAVID MOYES AZUA BALAA, AMPIGA DOGO MMOJA BAADA YA KUMTUKANA KWA KUPOTEZA KAZI MAN UNITED

Investigation: Moyes was present at the bar in Clitheroe at the time of the assault
Incident: Joshua Gillibrand claims he was attacked at just after 10pm on Wednesday night
 Tukio: Joshua Gillibrand anadai alishambuliwa majira ya saa 10:00 usiku wa jana jumatano.
 
Inasemekana Moyes alikerwa na kijana huyo mlevi aliyemtukana kocha huyo baada ya kufukuzwa kazi hivi karibuni na kumuita ‘s*** (hatujaona haja ya kutafsiri kimaadili), akimaanisha hajawahi kushinda kombe, alisema shahidi.
Baada ya maneno hayo vurugu ziliibuka mezani ambapo glasi zote zimeanguka chini.
Mr Gillibrand, alikula vibao na alichubuka kwenye bega kutokana na ugomvi huo, lakini hakuhitaji kwenda hospitali kupata matibabu zaidi.
Leo polisi walithibitisha kufungua uchunguzi juu ya tukio hilo na wanatarajia kuongea na kocha huyo wa zamani wa Everton.
Location: The Emporium wine bar in Clitheroe, Lancashire, where the alleged assault took place

BOKO HARAM NI MAGAIDI WA KIMATAIFA - UN


Baraza la Usalama la UN
Baraza la usalama la umoja wa mataifa hatimaye limeidhinisha kuwekewa vikwazo kundi la Boko Haram baada ya utekaji nyara wa takriban wasichana 300 wa shule katika eneo la Chibok Nigeria.
Kundi hilo limeshutumiwa kuwaua maelfu ya watu nchini Nigeria katika miaka michache iliyopita.
Nigeria ni mwanachama wa baraza la usalama la Umoja wa mataifa kwa kipindi cha miaka miwili. Kwa nafasi hii imeweza kushinikiza baraza hilo kuimulikia tochi.
Hatua ya baraza hilo kuiorodhesha Boko Haram miongoni mwa magaidi wa kimataifa, wakipishana au hata kuhusishwa moja kwa moja na AL Qaeda, huenda isionekane kama hatua kubwa. Lakini hii ina maana kuwa sasa jamii ya kimataifa italichukulia kwa uzito mkubwa zaidi kundi hilo.
Baraza hilo limeidhinisha pia vikwazo kuwekewa kundi hilo, viongozi wake na yeyote anayehusishwa nalo. Hii ina maana kuwa hata mali zao zitazuiliwa na akaunti zao zote zinazojulikana kufungwa. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Thursday, May 22, 2014

UNYAMA: MTOTO AFICHWA KWENYE BOKSI NA KUFUNGIWA NDANI KWA MIAKA MINNE...!!!


Rashid Mvungi  akimuangalia mtoto wake Nasrah Rashid (4) ambaye ni mlemavu wa viungo aliyefungiwa chumbani na kufichwa kwenye boksi bila ya kufanyiwa usafi tangu akiwa na umri wa miezi tisa. Picha na Hamida Shariff 

Alikuwa akitoa maelezo hayo huku akiwa amemshikilia mtoto huyo aliyetapakaa uchafu ikiwamo haja kubwa na ndogo alizokuwa akitoa ndani ya boksi na kusema kwamba mara ya mwisho alimwogesha Julai mwaka jana.

Morogoro. Mwanamke aliyetambuliwa kuwa ni Mariamu Said mkazi wa Kiwanja cha Ndege, Morogoro juzi alishushiwa kipigo na wananchi kutokana na kumficha mtoto wa marehemu mdogo wake kwenye boksi kwa miaka minne.

Tukio hilo lilitokea juzi saa nne asubuhi baada ya majirani zake kutoa taarifa kwa Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kiwanja cha Ndege, Dia Zongo kuhusu mtoto huyo, Nasra Rashid, kufichwa ndani ya boksi tangu akiwa na umri wa miezi tisa. Zongo alisema majirani hao walimweleza pia kuwa jirani yao huyo hamfanyii usafi mtoto huyo wala kumtoa nje.

Baada ya kupata taarifa hizo, Zongo alimtafuta Mwenyekiti wa Mtaa huo, Tatu Mgagala na kuongozana naye hadi kwenye nyumba hiyo na kumhoji mwanamke huyo ambaye alikuwa akijibu kwa kubabaika. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 22, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

NGASSA, SAMATTA KUGOMBEA TUZO MOJA

 Mchezaji wa Yanga, Mrisho Ngassa pamoja na Mbwana Samatta wa TP Mazembe, wanaumana katika kuwania tuzo za mwanamichezo anayependwa zaidi na watu zinazoendeshwa na Kampuni ya Bongo 5 Media Group kupitia tovuti yake ya bongo5.com.
Wengine wanaowania tuzo katika kipengele hicho ni Ramadhan Singano (Simba SC), Juma Kaseja (Yanga) na bondia Francis Cheka.
Inaonekana kuwa Ngasa na Samatta watakuwa na ushindani mkubwa zaidi hasa ikizingatiwa kuwa wachezaji wote wana mashabiki wengi na pia kila mmoja anacheza mchezo unaopendwa na wengi.
Akizungumzia tuzo hizo, mhariri mkuu wa bongo5.com, Fredrick Bundala, alisema watu wengi walijitokeza kupigia kura kuchagua watu wanawataka kushinda tuzo mbalimbali.
Bundala alivitaja vipengele vingine na majina ya waliopendekezwa kuwa ni pamoja na Nisher, Adam Juma, Nick Dizzo, Mecky Kaloka, Jerry Mushala wanaowania tuzo ya Mwongozaji Bora wa Video za wasanii.
Video Bora kwa Wanaume ni My Number ya Diamond, Jikubali ya Ben Pol, Mirror ya Baby, Love Me ya Izzo Bizness, Barnaba na Shaa, Muziki Gani ya Nay wa Mitego na Diamond.
Alisema wanaowania Tuzo ya Video ya Mwanamuziki wa Kike ni Amani ya Moyo ya Feza Kessy, Closer ya Vanessa Mdee, Sugua Gaga ya Shaa, Yahaya ya Lady Jaydee, Nakomaa na Jiji ya Shilole.
Bundala alifafanua kuwa wananchi wanatakiwa kuchagua jina moja kutoka katika majina matano ya kila kipengele kilichotajwa.
“Wiki moja baada ya majina ya washiriki watano kutangazwa, mchujo wa kwanza utafanyika katika kila kipengele,” alisema Bundala.
Aliwataka Watanzania kuwapigia kura wale wanaowapenda kwa kutuma ujumbe mfupi na baadaye kufuata maelekezo rahisi ya kupiga kura pia kupitia tovuti www.tuzozetu.com. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

YAYA AITIA KIWEWE MANCHESTER CITY

Yaya Toure amekoleza moto kwenye sakata lake kutaka kuihama Manchester City akisema hajui hadi sasa atakapokwenda kucheza msimu ujao.
Wakala wa mchezaji huyo, Dimitri Seluk alibainisha kuwa Yaya anaweza kuondoka kwa sababu anadhani kwamba amekuwa akichukuliwa kama mtu asiyeheshimika na wamiliki wa klabu hiyo.
Hivyo kwa sasa, Toure ambaye ana miaka 31, hajaamua hatima yake kuhusu klabu atakayochezea msimu ujao.
Alipoulizwa kama anaweza kuichezea klabu nyingine msimu ujao, alijibu: “Ndio. Hatujui katika soka nini kitatokea. Kamwe hatuwezi kujua hilo.”
Katika mahojiano maalumu na mtandao wa BE IN SPORTS, nyota huyo wa timu ya taifa ya Ivory Coast alisema: “Kwa sababu ya msimu mzuri niliokuwanao klabu ya Man City, kila mtu ananizungumzia na kila kitu kiko wazi.
“Wakala wangu Dimitri, siku zote amekuwa akizungumza na watu kwa simu na anajua cha kufanya kwa sababu siku zote nimekuwa nikimuamini sana.
“Hatujui kesho itakuwaje, lakini kwa sasa akili yangu iko katika Kombe la Dunia na baada ya kumalizika kwake tutajua nini kimetokea.”
Toure alisaini mkataba mpya wa miaka minne kuichezezea City Aprili mwaka jana.
Hata hivyo, majaaliwa yake yamebaki kuwa na mashaka kutokana na wakala wake kuwalaumu wamiliki wa City kwa kutoonyesha heshima kwa kiungo huyo alipotimiza miaka 31. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

WAZIRI AJIUA BAADA YA KUSHINDWA KATIKA UCHAGUZI

Shughuli ya kuhesabu Kura Malawi
Naibu waziri wa serikali za mitaa wa Malawi amejipiga risasi na kujiua nyumbani kwake mjini Lilongwe.
Godfrey Kamanya alikuwa anayegombea kutetea kiti chake cha ubunge katika jimbo la Nzonzi Kusini amejiua alfajiri ya leo katika mojawapo ya vyumba vya nyumba yake iliyopo Area Ten mjini Lilongwe.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye hospitali kuu ya Kamuzu mjini humo, na jeshi la polisi litatoa taarifa rasmi ya kifo hicho baada kukamilisha uchunguzi.
Haijajulikana sababu za Kamanya kujiua japokuwa ameacha barua ya maelezo ambayo polisi wataitoa baadae.
Matokeo ya kura bado hayajatangazwa rasmi katika kile kinachosemekana kuwa uchaguzi wenye ushindani mkali sana.
Afisa mkuu wa uchaguzi, amesema kuwa mfumo wa elektroniki umeharibika na maafisa wanatumia matokeo kwa njia ya barua pepe. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Wednesday, May 21, 2014

MELI YA KIKWETE KUKAMILIKA 2016

http://jambotz8.blogspot.com/
Siku kama ya leo mwaka 1996, ilikuwa ni vilio kila kona ya nchi, lakini Kanda ya Ziwa iliathirika zaidi na kuzama kwa meli ya Mv Bukoba na kuteketeza mamia ya wananchi.
Kuzama kwa Mv Bukoba inaelezwa ni kutokana na kuwa ubovu. Tukio hilo ambalo haliwezi kufutika vichwani mwa wakazi wa Kanda ya Ziwa, lakini kilio chao cha kupatiwa meli mpya licha ya Rais Jakaya Kikwete kuahidi Serikali kununua mwaka 2010, haijanunuliwa hadi sasa.
Hata hivyo, inaelezwa kuwa ujenzi wa meli hiyo mpya iliyoahidiwa na Rais Kikwete kwa Ziwa Victoria unatarajia kukamilika mwaka 2016.
Akizungumza ofisini kwake wiki hii, Ofisa Masoko wa Huduma za Meli Mwanza Obedi Nkongoki alisema mjenzi wa meli hiyo Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Denmark (Danida) kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania.
http://jambotz8.blogspot.com/
“Ujenzi huu unahusisha meli nne ingawa Rais aliahidi tatu; Ziwa Victoria moja, mbili Ziwa Tanganyika na nyingine Ziwa Nyasa ambazo zinatarajiwa kukamilika 2018, huku ya Ziwa Victoria ikitarajiwa kukamilika 2016,” alisema Nkongoki. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO MEI 21, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

VIFO VYA BOMU NIGERIA VYAFIKIA 118

Maafisa nchini Nigeria wamesema kuwa wamepata maiti 118 kufuatia shambulio la bomu katika mji wa Jos.
Mabomu mawili yalilipuka mojawepo ikiwa imefichwa ndani ya gari na kulipuka katika soko moja kubwa. Dakika 20 baadaye mlipuko wa pili ulitokea karibu na hospitali.
Inahofiwa kuwa kuna maiti zaidi zilizonaswa kwenye vifusi vya majengo yaliyo poromoka kutokana na shambulio hilo.
Kufikia sasa hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulio hilo lakini wengi wanaamini kuwa Kundi la wapiganaji wa kiislamu la Boko Haram lilihusika.
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan amejitokeza kukemea mashambulio hayo na kusema kuwa amejitolea kuangamiza kabisa ugaidi. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Na BBC Swahili

JESHI LA KENYA LAWASHAMBULIA AL-SHABAAB

Wanajeshi wa Kenya wanaendelea kukabiliana na Al Shabaab Somalia
Jeshi la Kenya limeishambulia ngome ya Al Shabab ya Jilib huko Somalia.
Katika mahojiano na BBC, msemaji wa Jeshi la Kenya Willy Wesonga amesema kuwa oparesheni hiyo kutoka angani imefaulu kuwaangamiza baadhi ya wakuu wa Al Shabab.
Ngome hiyo inadaiwa kuwa eneo ambapo wapiganaji hao wa kiislamu wanafanya mazoezi na mikutano yao.
Kikosi cha Kenya kinadai kuishambulia ngome hiyo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wakaazi wa wilaya hiyo ya Jilib.
Wapiganaji wa Al shabab wamezidisha mashambulio nchini Kenya tangu nchi hiyo iingize wanajeshi wake ndani ya Somalia kuwasaka wapiganaji hao haramu mwaka wa 2011
Wesonga anasema jeshi la Kenya linalishambulia Al shabaab kama sehemu ya vita vikuu duniani dhidi ya ugaidi, na pia kuwazuia wafuasi wa kundi hilo kutekeleza mipango yao, yanayohatarisha usalama wa kieneo.
Hayo yanajiri wakati kundi la Al Shabab likidai kufanya shambulizi huko Mandera na kuwaua maafisa wa usalama wa Kenya. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Na BBC Swahili

Monday, May 19, 2014

VAN GAAL AMTEUA VAN PERSIE KUWA NAHODHA MPYA MAN UNITED

Double Dutch: Louis van Gaal (right) sees Robin van Persie as his perfect captain at Manchester United
 Waholanzi wawili: Louis van Gaal (kulia) anaona Robin van Persie ndiye nahodha aliyekamilika katika klabu ya Manchester United.
LOUIS van Gaal  anatarajia kumteua mshambuliaji wake hatari Robin van Persie kuwa nahodha wa kikosi chake mara atakapojiunga na Manchester United baada ya kumalizika kwa kombe la dunia majira ya kiangazi nchini Brazil.
Jumamosi iliyopita Van Persia aliifungia bao muhimu timu ya taifa ya Uholanzi katika mechi ya kirafiki dhidi ya Ecuador na kulazmisha sare ya 1-1.
Van Gaal amekuwa na mahusiano mazuri na RVP ambaye ni nahodha wa timu ya taifa na sasa anatarajia kumpa jukumu hilo katika klabu ya Man United na kumpiga chini Rooney ambaye angekuwa nahodha wa kudumu katika utawala wa David Moyes.
A sign of things to come? Van Persie (right) poses with Kluivert (left), Louis van Gaal's assistant manager
Class: Holland captain van Persie scored a fantastic volley in their 1-1 draw with Ecuador on Saturday

SAKATA LA IPTL LAZIDI KUWAVURUGA WABUNGE


KABWE_b5fd6.jpg
Dodoma. Sakata la fedha za IPTL limechukua sura mpya baada ya baadhi ya wabunge kudai kurubuniwa na wenzao kwa fedha ili wakwamishe Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini, wakidai balozi mmoja yuko nyuma ya mpango huo.
Katika sakata hilo, Sh200 bilioni zilizohifadhiwa kwenye akaunti ya Escrow zilitolewa na kulipwa kwa Kampuni ya Pan African Power (PAP), ambazo Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali amesema anachunguza akishirikiana na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru).
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Kabwe Zitto ameonya kuwa kuwaingiza mabalozi katika sakata la ufisadi wa zaidi ya Sh200 bilioni za IPTL ni kuibua mgogoro wa kidiplomasia na nchi husika.
Akizungumza na gazeti hili jana, mbunge huyo alisema kuwa kiongozi yeyote atakayegundulika kufaidika na hongo hiyo, kamati yake itaweka wazi jina lake na hakuna atakayeachwa bila kuchukuliwa hatua za kisheria.
Zitto alitoa kauli hiyo jana baada ya kubainika ujumbe mfupi wa maandishi (sms) unaodaiwa kusambazwa, ukifichua kile kinachodaiwa ni kuhongwa kwa baadhi ya wabunge ili wakwamishe bajeti ya wizara hiyo.
Ujumbe huo unasomeka: "Spika wa Bunge la Jamhuri, sisi wabunge waadilifu tunakiri kwamba Mhe. Mkono ametufuata na kutupatia fedha kila mmoja milioni 3 ili tukwamishe bajeti ya Nishati na Madini.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

COSMAS CHEKA ATAMBA KUTETEA UBINGWA WAKE WA TPBO

IMG_8710Cosmas Cheka ‘kulia’
Na Mwandishi Wetu BONDIA Cosmas Cheka anatarajia kupanda ulingoni juni mosi kwa ajili ya kutetea taji lake la ubingwa wa TPBO anaoshikilia kwa kupambana na Suma Ninja katika ukumbi wa vijana social hall wa Morogoro
Akizungumzia mpambano huo Cheka amesema amejiandaa kupigana kwa raundi kumi hivyo mashabiki waje kuona kazi anayoifanya akiwa ulingoni. Bondia huyo ambaye anatamba sambamba na kaka yake Fransic Cheka aliyekuwa bingwa wa WBF ambao alivuliwa kizembe amesema yeye anataka afike mbali zaidi ya kaka yake huyo.
Pambano hilo linalosimamiwa na TPBO litasindikizwa na mapambano ya utangulizi kati ya Kudura Tamimu atakaeevaana na Sadiki Yusufu, wakati Mohamed Matimbwa ataoneshana umwamba na Twaha Kassimu
Siku hiyo pia kutakuwa na uuzwaji wa DVD kali za ngumi wakiwemo mabondia wakali wanaotamba Duniani na hapa nchini kama Mohamed Matumla vs Fransic, Miyeyusho, Japhert Kaseba Vs Thomas Mashali , Floyd Mayweathar, Manny Paquaio, Saul ‘canelo’ alverez , Mike Tyson, Mohamed Ali, Ferex Trinidad, Miguel Cotto na wengine wengi
DVD hizo za ngumi kali zitakuwa zikiuzwa na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila ‘Super D’ Pamoja na kutambua sheria na taratibu za mchezo huo siku hiyo pia kutakuwa na vifaa vya mchezo huo wa masumbwi vitakavyotolewa zawadi kwa mabondia na Kocha Super D ambaye ameahidi kutoa, Gum Shit ,Clip Bandeji,DVD za Mafunzo kwa mabondia, Bukta, Protector na vifaa mbalimbali kwa mabondia watakaoonesha uwezo wa hali ya juu wa kutupiana masumbwi. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...