Sunday, April 19, 2015

USALAMA WAIMARISHWA AFRIKA KUSINI

Ubaguzi dhidi ya wageni nchini Afrika kusini 
 
Maafisa zaidi wa polisi wametumwa katika maeneo yenye mashambulio dhidi ya raia wa kigeni nchini Afrika Kusini. Yamkini watu sita wameuawa na makundi yenye silaha, ambayo yanawalaumu wahamiaji wa kiafrika kwa kuchukua kazi zao nchini Afrika Kusini.

Rais Jacob Zuma amewatembelea watu hao walioathirika na ghasia hizo, mauwaji pamoja na kuibwa kwa mali zao huku akiahidi kukabiliana vilivyo na wimbi la mashambulio hayo.
Bwana Zuma alifutilia mbali ziara yake nchini Indonesia, ili kukabiliana na vurumai hizo zilizoanza majuma mawili yaliyopita.

Yamkini watu sita wameuawa na makundi yenye silaha, ambayo yanawalaumu wahamiaji wa kiafrika kwa kuchukua kazi zao nchini Afrika Kusini. Nchini Harare Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, alilaani ghasia hizo.

Ghasia hizo zilianza baada ya mfalme mmoja wa Kizulu, Goodwill Zwelethini, kusema kuwa raia wa kigeni sharti waondoke Afrika Kusini. Akiongea katika kambi hiyo iliyoko mjini Durban kiongozi mkuu wa jimbo la Gauteng, David Makhura, anasema kuwa uhasama na ghasia hizo zinazoshuhudiwa, haundamani na uhuru wa miaka mingi ambayo Afrika Kusini ilipigania. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Saturday, April 18, 2015

WATU 38 WAFARIKI KATIKA AJALI

 Basi dogo aina ya Hiace likiwa limetumbukia kwenye Mto Kiwira eneo maarufu kwa jina la Uwanja wa Ndege, wilayani Rungwe mkoani Mbeya.

Msiba mwingine mzito umelikumba taifa baada ya watu 38 kupoteza maisha katika matukio mawili tofauti, likiwamo la ajali ya basi dogo aina ya Toyota Hiace iliyoua watu 19 wakati ikifanya safari ya wizi mkoani Mbeya.

Tukio jingine limetokea mkoani Shinyanga ambako wachimbaji wadogo 19 wa dhahabu waliokuwa katika mgodi mdogo wa Kalole, wilayani Kahama wamekufa baada ya kufunikwa na kifusi usiku wa kuamkia jana kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

 Polisi wakiwa katika machimbo ya dhahabu ya Kalole wilayani Kahama jana baada ya machimbo hayo kuporomoka na kuua watu 19.

Matukio hayo ni mwendelezo wa majanga ya ajali ambazo zimekuwa zikitokea kwa takriban wiki mbili mfululizo na kuua mamia ya watu. Zaidi ya watu 980 wamefariki dunia katika ajali za barabara katika muda wa zaidi ya miezi mitatu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MENGI ATUHUMIWA KWA UHAINI, MWENYEWE AIBUKA NA KUNENA...!!!


MWENYEKITI wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi, ametuhumiwa kutaka kuiangusha Serikali ya Rais Jakaya Kikwete na kumshughulikia baada ya kumaliza uongozi wake Oktoba, mwaka huu.

Baada ya tuhuma hizo kuelekezwa kwake na gazeti la Taifa Imara lililochapishwa Machi 23, mwaka huu likiwa na kichwa cha habari kinachosema, ‘Zitto amchongea Mengi kwa JK? Mwenyewe ameibuka Dar es Salaam jana na kuzikanusha mbele ya waandishi wa habari akisema zimemshtua na kumuogopesha.

“Tuhuma zilizotolewa na gazeti la Taifa Imara la Machi 23-29, mwaka huu kwamba nina nia ya kutaka kuiangusha Serikali ya Rais Kikwete na kumshughulikia baada ya kumaliza muda wake wa uongozi, zimenishtua sana,” alisema Mengi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRILI 18, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC01472
DSC01469
DSC01470
DSC01471 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

GWAJIMA APANDISHWA KIZIMBANI

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima (45), akiwasili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, akiwasili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.

HATIMAYE Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima (45), amepanda katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akikabiliwa na mashitaka mawili, ikiwemo la kutumia lugha ya matusi dhidi ya Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam la Kanisa Katoliki, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.

Mbali na Gwajima, washitakiwa wengine ni Askofu msaidizi wa Kanisa hilo, Yekonia Behagaze (39), Geofrey Mzava (31) ambaye hakuwepo mahakamani hapo na George Milulu (43) mkazi wa Kimara Baruti.


Kesi hiyo ambayo ilianza kutajwa saa 9:30 alasiri hadi saa 11 jioni, ilisikilizwa mbele ya Hakimu Wilfred Dyansobera, ambapo mawakili wa Serikali; Wakili Mwandamizi Joseph Maugo, akisaidiwa na Shadrack Kimaro na Tumaini Kweka, walisoma mashitaka dhidi ya washitakiwa. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WASHUKIWA WA UGAIDI WAKAMATWA AUSTRALIA

Mshukiwa wa ugaidi nchini Australia
Polisi katika jimbo la Victoria nchini Australia wanasema kuwa wamewakamata wanaume watano kufuatia oparesheni kubwa ya kupambana na ugaidi kwenye mji wa Melbourne.
Wawili kati ya wanaume hao walio na umri wa miaka 18 walikamatwa baada ya kushukiwa kupanga mashambulizi ya kigaidi yaikiwemo ya kuwalenga polisi.

Mshukiwa mwingine naye alikamatwa kufuatia sababu zinazohusiana na silaha. Shughuli za kuwatafuta washukiwa wengine zinaendelea sehemu zingine za mji wa Melbourne. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WATU ZAIDI YA 30 WAUAWA AFGHANIISTAN

Eneo kulikotokea shambulizi
Shambulizi la kujitoa mhanga kwenye mji ulio mashariki mwa Afghanistan wa Jalalabad limewaua watu 33 na kuwajeruhiwa karibu wengine 100.

Ripoti zinasema kuwa shambulizi hilo lilitokea karibu na benki ambapo wafanyikazi wa serikali wanalipwa misharaha yao.

Maafisa wanasema kuwa mtu aliyeendesha shambulizi hilo alikuwa na pikipiki.
Kulitokea shambulizi la pili karibu na madhabahu mjini Jalalabad lakini haijulikani kama kulikuwa na madhara yoyote.

Hakuna kundi lililokiri kuhusika, lakini mji wa Jalalabad umekuwa ukilengwa kila mara na kundi la Taliban. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA

Hii ni kabla ya Mechi za leo Aprili 18, Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.


Rnk
Team MP W D L GF GA +/- Pts

1
Young Africans 21 14 4 3 39 12 27 46

2
Azam 21 10 9 2 27 14 13 39

3
Simba SC 21 9 8 4 27 15 12 35

4
Kagera Sugar 22 8 7 7 21 20 1 31

5
Mgambo JKT 21 8 4 9 17 19 -2 28

6
Stand United 22 7 7 8 19 24 -5 28

7
Mtibwa Sugar 22 6 9 7 21 22 -1 27

8
Coastal Union 23 6 9 8 16 23 -7 27

9
Ruvu Shooting 22 6 8 8 14 20 -6 26

10
Mbeya City 22 5 10 7 17 21 -4 25

11
Ndanda 22 6 7 9 18 24 -6 25

12
JKT Ruvu 23 6 7 10 17 23 -6 25

13
Tanzania Prisons 22 3 12 7 14 21 -7 21

14
Polisi Morogoro 22 4 9 9 13 22 -9 21

ETOILE WAPIGWE TU...!!!

Wachezaji wa Yanga wakishangilia bao katika moja ya mechi katika uwanja wa Taifa.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia goli katika moja ya mechi walizocheza Uwanja wa Taifa.
 
WAPIGWE tu hao Etoile Sportive du Sahel. Ndio kauli ambayo wapenzi wa Yanga na wa mpira wa miguu Tanzania wanaitoa kuelekea pambano la leo la Kombe la Shirikisho Afrika.
Yanga, moja ya timu kongwe nchini, inashuka kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kuikabili Etoile Sportive du Sahel (ESS) ya Tunisia katika mechi ya raundi ya pili ya michuano hiyo ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF).

Vijana hao wa Jangwani ndio timu pekee iliyobaki ya Tanzania katika michuano ya kimataifa na ndio maana wapenzi wake, mashabiki wa soka nchini na Watanzania kwa ujumla, wangependa kuiona inaipiga ESS na kujiweka katika mazingira mazuri ya kusonga mbele katika marudiano Mei Mosi, mwaka huu, mjini Sousse. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KOCHA ETOILE AINGIA MITINI...!!!

faouzibenzarti
Kocha Mkuu wa Etoile du Sahel ya Tunisia, Faouzi Benzarti

KOCHA Mkuu wa Etoile du Sahel ya Tunisia, Faouzi Benzarti, ameingia mitini baada ya kushindwa kutokea katika mkutano wa makocha na waandishi wa habari ulioandaliwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa ajili ya mchezo wao wa Kombe la Shirikisho Afrika utakaochezwa leo katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Benzarti alishindwa kuhudhuria mkutano huo kwa madai walichoka baada ya kuwa angani kwa saa tisa wakitokea Tunisia ambapo waliwasili Dar es Salaam jana alfajiri.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa TFF, Baraka Kizuguto, Benzarti aliwataarifu kwamba asingefika kwenye mkutano huo na kuwaomba radhi kutokana na hilo.

Pamoja na kushindwa kutokea kwa kocha huyo, Kocha wa Yanga, Hans van der Pluijm alisema amezikamata mbinu za Etoile du Sahel na atahakikisha wanashinda mchezo huo wa raundi ya pili wa Kombe la Shirikisho Afrika. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Thursday, April 09, 2015

WABUNGE 50 KUHAMIA ACT...!!!

 
Kiongozi wa Chama cha ACT - Wazalendo, Zitto Kabwe akizungumza na wahariri wa gazeti la Mwananchi alipotembelea makao makuu ya Mwananchi Communications Limited, yaliyopo Tabata Relini, Dar es Salaam jana.

Kiongozi wa Chama cha ACT - Wazalendo, Zitto Kabwe amesema zaidi ya wabunge 50 wa vyama mbalimbali vya siasa nchini watajiunga na chama hicho kipya na kugombea ubunge katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Zitto ambaye alijivua ubunge wa Kigoma Kaskazini baada ya kufukuzwa uanachama wa Chadema, amebainisha kuwa wabunge hao, wakiwamo wa CCM na Chadema, ni miongoni mwa watu wanaokichangia fedha chama hicho kilichopata usajili wa kudumu Mei, mwaka jana na kuzinduliwa mwezi uliopita.
Pia, amewatangazia vita wabunge wa majimbo manane ya Mkoa wa Kigoma, akijigamba kuwa ili waweze kuibuka na ushindi katika uchaguzi huo ni lazima wakubali kujiunga na ACT kwa kuwa chama hicho kimejipanga kuyabeba majimbo yote. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

'NATAZAMWA NA CCM KILA KONA' LOWASSA

 
Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara.

Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa amesema anashindwa kujitokeza kuzungumzia au kufanya mambo yanayohusiana na urais kwa kuwa Kamati ya Maadili ya CCM inamfuatilia kwa karibu.
Alisema hayo jana alipoulizwa kuhusu kauli ya Rais Jakaya Kikwete wiki iliyopita akiwa Marekani ambako alielezea mafanikio na changamoto alizokumbana nazo wakati wa uongozi wake wa miaka 10.
Kikwete alisema: “Wakati unaingia Ikulu unakuwa na shauku kubwa pamoja na furaha ya ushindi, lakini hakika urais ni kadhia kubwa. Ukipata fursa ya kuwa rais kwa awamu mbili kama mimi nadhani zinatosha kabisa. Nimefanya mengi kwa nchi yangu atakayekuja ataendeleza nilipoishia.”
Kauli ya Lowassa inakuja ikiwa ni siku chache baada ya makada wengine wanaotajwa kuwania urais kupitia CCM kueleza maoni yao juu ya kauli hiyo ya Rais.
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba ameshalieleza gazeti hili kuwa kauli hiyo inampa hamasa kwa nia yake ya kutaka kuwania urais na kwamba alitangaza nia hiyo huku akifahamu kwa asilimia 100 uzito wa jambo hilo akisema kufahamu changamoto hizo ndiyo moja ya vitu vilivyomsukuma kuchukua uamuzi huo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS APRILI 09, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC01106


DSC01107

DSC01108

DSC01109

DSC01110 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

AUAWA KWA KUPELEKA WAGANGA KIJIJINI

Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Geofrey Kamwela

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Godfrey Kamwela.

MZEE mwenye umri wa miaka 68, Celestine Mushi, mkazi wa kata ya Motamburu wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, ameuawa na wananchi wanaotajwa kukasirishwa na kitendo chake cha kupeleka waganga wa jadi kijijini kwa lengo la kuifanyia zindiko nyumba yake.

Mushi anadaiwa kuwatoa waganga hao wawili jijini Dar es Salaam na kuwapeleka Rombo kwa kazi hiyo maalumu.
Tukio hilo limethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Godfrey Kamwela aliyesema mauaji hayo yalitokea juzi saa 2.30 usiku nyumbani kwa Mushi katika kitongoji cha Mbomai Juu, wakati waganga hao wakiendelea na zindiko lao.
Kamwela aliwataja wanaodhaniwa ni waganga wa jadi kuwa ni Ashraf Mjengwa (22) na Peter Mmaka (25), wote wakazi wa Magomeni, Dar es Salaam. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

HII NDIO YANGA: YAIFUNZA COASTAL UNION ADABU, YAIFUNGA 8 - 0....!!!

Kiungo wa Yanga, Salum Telela, akimiliki mpira mbele ya
wachezaji wa Coastal Union ya Tanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara
uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana. Yanga imeshinda 8-0.

(Picha na Francis Dande).
Simon Msuva akishangilia bao aliloifungia timu yake.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

CHRISTIANO RONALDO AFUNGA GOLI LA 300

cr7

CRISTIANO RONALDO, jana alifunga goli katika ushindi wa magoli 2-0 wa Real Madrid dhidi ya Rayo Vallecano.
Kwa kufunga kwake jana, mchezaji huyo amefikisha magoli 300 tokea aanze kuichezea Real Madrid, na amekuwa mchezaji wa tatu kwenye historia ya timu hiyo kufikisha idadi hiyo ya magoli baada ya wakongwe waliomtangulia kina Alfredo Di Stefano na Raul Gonzalez.
Sasa Cristiano bado magoli manane amfikie Di Stefano na 23 amfikie Raul.
Raul ndie mfungaji bora wa kihistoria kwenye timu hiyo akiwa amefunga magoli 323 katika mechi 741, wakati marehemu Di Stefano anashika nafasi ya pili akiwa amefunga magoli 308 katika mechi 396.
Cristiano Ronaldo amefunga magoli 300 katika mechi 288. Hivyo wastani wake ni mzuri kuliko wachezaji hao wote wawili akiwa na wastani wa kufunga goli moja katika kila mechi na amefunga magoli mengi kuliko idadi ya jumla ya mechi alizocheza.
Di Stefano naye wastani wake ni mzuri kuliko Raul. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MICHUANO YA KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA

Taifa Stars ya Tanzania
Ratiba ya michuano ya kuwania kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika imetolewa leo na CAF huku Tanzania ikiwa kundi G pamoja na nchi za Nigeria, Misri na Chad.
Makundi ni kama ifuatavyo:

Kundi A: Tunisia, Togo, Liberia, Djibouti.
Kundi B: Congo DRC, Angola, Jamhuri ya Kati, Madagascar.
Kundi C: Mali, Guinea ya Ikweta, Benin, Sudan Kusini.
Kundi D: Burkina Faso, Uganda, Botswana, Comoro.
Kundi E: Zambia, Kenya, Congo Brazzaville, Guinea Bissau.
Kundi F: Cape Verde, Morocco, Libya, Sao Tome.
Kundi H: Ghana, Msumbiji, Rwanda, Mauritius.
Kundi I: Ivory Coast, Sudan, Sierra Leone, Gabon.
Kundi J: Algeria, Ethiopia, Lesotho, Shelisheli.
Kundi K: Senegal, Niger, Namibia, Burundi.
Kundi L. Guinea, Malawi, Zimbabwe, Swaziland.
Kundi M. Cameroon, Afrika ya Kusini, Gambia, Mauritania.

Fainali zake zitafanyika Gabon 2017 na droo imefanyika Misri, makao makuu ya CAF. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Thursday, April 02, 2015

MWIGULU KUFUTA MAADHIMISHO MBALIMBALI YA KITAIFA...!!!

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba juzi alijikuta akitamka kuwa anakusudia kufuta maadhimisho mbalimbali ya kitaifa yanayotumika kama kichaka cha kutafuna fedha za Serikali baada ya wabunge  wa upinzani kuitoa jasho Serikali wakati wa kupitisha Muswada wa Sheria ya Baraza la Vijana wa mwaka 2015.
Mwigulu alitoa kauli hiyo pale alipoingilia kati mjadala huo, akiponda kitendo cha watumishi wa Serikali kutumia magari na fedha lukuki katika wiki za kuadhimisha kumbukumbu mbalimbali za kitaifa.
Kilichoibua mjadala huo ni suala la uanzishwaji wa Mfuko wa Vijana na maadhimisho ya wiki ya vijana ambayo imepangwa Oktoba kila mwaka. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS APRILI 02, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TRENI DAR - KIGOMA KAMA NDEGE...!!!

 
 Mwonekano wa ndani ya treni ya kisasa ya abiria ya Kampuni ya TRL iliyozinduliwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk Shabaan Mwinjaka, Dar es Salaam jana.

Treni ya kisasa (Delux), kwenda Bara yenye mabehewa 22 ilianza safari yake ya saa 30 kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma ikiwa ni tofauti ya saa sita ikilinganishwa na safari ya treni ya zamani.
Kutokana na tofauti hiyo, abiria walioanza safari kwa furaha na matumaini jana saa tano asubuhi wanatarajiwa kufika Kigoma leo saa 11 jioni badala ya saa tano usiku.
Hata hivyo, abiria hao watalazimika kuingiza mikono yao zaidi mifukoni, kutokana na kiwango kipya cha nauli kuwa Sh79,400 badala ya Sh75,700 za awali kwa daraja la kwanza. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

RAIA WA YEMEN WAKIMBILIA SOMALIA

Raia wa Yemen wakikatika Ghuba ya Aden kwa boti ndogo
Mashirika ya umoja wa mataifa yamesema kuwa mamia ya raia wa Yemen wamevuka ghuba ya Aden kwa kutumia boti ndogo na kuingia nchini Somalia, Djibouti na Somaliland wakikimbia mapigano nchini mwao.

Shirika la umoja wa mataifa la UNHCR limesema kuwa linaangalia eneo zuri kwaajili ya kuweka kambi ya wakimbizi kwaajili ya raia hao. Wakati huo huo wakimbizi kutoka nchini Somalia bado wanaendelea kuingia nchini Yemen kuepuka njaa na machafuko nchini mwao.

Shirika hilo la UNHCR linasema kuwa Yemen inawahifadhi wakimbizi wapatao 238,000 kutoka Somalia. Mwandishi wa BBC Africa Mary Harper anasema wazo la Yemen kufikiria kuwa na kambi za wakimbizi nchini Somalia si la kawaida kwa kuwa ni kawaida kwa raia nchini humo kuikimbia nchi yao kutokana na machafuko ya mara kwa mara hali ambayo haiwezi kuwa eneo zuri kwa wakimbizi kuhifadhiwa. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

BUHARI AAHIDI KUTOKOMEZA BOKO HARAM NIGERIA

Muhammadu Buhari, Rais mteule wa Nigeria
Rais mteule wa Nigeria, Muhammadu Buhari, amezitaja vurugu zinazosababishwa na kundi la wanamgambo wa Kiislamu wa Boko Haram kuwa ni tatizo kubwa linalokabili nchi.

Katika mahojiano maalumu na BBC, kiongozi huyo mstaafu wa jeshi amesema anatarajia kulishinda kundi hilo baada ya dhamira mpya kutoka jeshini na msaada wa nchi jirani.

 "Kwa ushirikiano na majirani zetu Cameroon, Chad, Niger na jumuia ya kimataifa na dhamira ambayo tutapata kutoka katika jeshi, Nafikiri itachukua muda mfupi zaidi kukabiliana nao."

Jenerali Buhari amesema tayari ameainisha msingi wa tatizo linalokabili nchi ya Nigeria, lakini amewataka raia wa nchi hiyo kuwa wavumilivu.

"Tumebaini matatizo makubwa matatu. Ambayo ni kukosekana kwa usalama nchini, tatizo ambalo kila mmoja analifahamu na lingine ni ukosefu wa ajira, hii ina maana uharibifu wa uchumi ikiwa ni kutokana na vitendo vya rushwa na rushwa yenyewe. 

Matatizo haya matatu makuu, Wanigeria wote wanafahamu na tunaomba ushirikiano wa wananchi wa Nigeria, wasitarajie miujiza kutokea katika kuyapatia ufumbuzi matatizo haya katika kipindi cha miezi michache baada ya kutwaa madaraka kwa sababu uharibifu umechukua miaka mingi, miaka kumi na sita ya utawala wa chama tawala cha nchi hii."

 Anasema rais huyo mteule wa Nigeria. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...