Thursday, April 09, 2015

CHRISTIANO RONALDO AFUNGA GOLI LA 300

cr7

CRISTIANO RONALDO, jana alifunga goli katika ushindi wa magoli 2-0 wa Real Madrid dhidi ya Rayo Vallecano.
Kwa kufunga kwake jana, mchezaji huyo amefikisha magoli 300 tokea aanze kuichezea Real Madrid, na amekuwa mchezaji wa tatu kwenye historia ya timu hiyo kufikisha idadi hiyo ya magoli baada ya wakongwe waliomtangulia kina Alfredo Di Stefano na Raul Gonzalez.
Sasa Cristiano bado magoli manane amfikie Di Stefano na 23 amfikie Raul.
Raul ndie mfungaji bora wa kihistoria kwenye timu hiyo akiwa amefunga magoli 323 katika mechi 741, wakati marehemu Di Stefano anashika nafasi ya pili akiwa amefunga magoli 308 katika mechi 396.
Cristiano Ronaldo amefunga magoli 300 katika mechi 288. Hivyo wastani wake ni mzuri kuliko wachezaji hao wote wawili akiwa na wastani wa kufunga goli moja katika kila mechi na amefunga magoli mengi kuliko idadi ya jumla ya mechi alizocheza.
Di Stefano naye wastani wake ni mzuri kuliko Raul. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...