Producer maarufu bongo na mmiliki wa studio za
bongo record P funk Majan ametoa makavu kwa watu wanaochonga kuhusu
maendeleo yake husasani wale wote ambao wanapiga majungu kuwa mkali
huyo amepotezwa na vijana wadogo kwenye soko la mziki bongo. “Kuna watoto wadogo siku hizi wanakurupuka wanajiona wao baabkubwa juzi kati nikiwa kwenye club moja naskia kiproducer kinachonga kuhusu mimi kenyewe kana sijui nyimbo moja au tatu zimehit mimi nina yimbo zaidi ya 100 ambazo zimehit na hadi akina Mhe Mkapa enzi hizo, wametukubali we utaniambia nini” P funk alifunguka. Majani amefunguka kuwa kuna watu wanamtafuta chuki ili kumpachika skendo akitolea mfano msanii wa kizazi kipya Ney wa Mitego kuwa haelewi kitendo cha rapper huyo kumtukana kwenye nyimbo yake kulikua na lengo gani kwasababu msanii huyo hamkaribii hata kidogo kwa level zake. |
Friday, March 29, 2013
P FUNK AMCHANA MAKAVU MSANII NAY WA MITEGO
JACK PENTZEL ALONGA KUHUSU KUOLEWA KWAKE
MSANII wa bongo movie 'star 'wa bongo
asiyekauka vituko' Jackline Pentzel a.k.a Jack wa Chuzi ameibuka na
kuwataka mashabiki wake kuamini ameolewa na hajakurupuka kufanya
maamuzi hayo kwani ni jambo ambalo alikuwa akilifikiria kila wakati Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni Jack alisema kuwa anawataka mashabiki kuamini na kutowasikiliza watu wengine wanaotoa maneno ya uzushi juu yake kuwa maamuzi ya kuolewa ameyapanga na ameolewa na mwanaume wake wa siku nyingi hivyo anaamini anachokifanya ni sahihi kwake Alisema kuwa watambue mwanaume aliolewa naye si mume wa mtu bali ni mchumba wake wa muda mrefu na walikuwa wakiishi pamoja kbala ya kuoa na ndipo maamuzi ya kufunga ndoa yalipokuja kwa kutotaka kuendelea kufanya uzinifu wakati uwezo wa kufunga ndoa walikuwa wanao "Mimi nawashangaa kwani kuolewa ni kitu gani cha ajabu mpaka watu wasiamini mimi kufunga ndoa nimeamua kuolewa kwa sababu nampenda mwanaume wangu na nilikuwa naishi naye kwa kalibu hivyo tunajuana vizuri sijakulupuka" alisema Pentzel Akizungumzia sababu za kutotangaza harusi yake alisema ameamua kutofanya hivyo ili kuepusha maneno na vizuizi vya ndoa yake ambavyo vingeweza kuibuka na kupoteza mawazo ya mumewake huyo Alisema kuwa hakutaka hali hiyo itokee ndio maana akaamua kufanya iwe siri na ya kushutika ili wambaya wake wakose nafasi ya kufanya jambo lolote baya na kwa sasa baada ya harusi hiyo ndio vikao kwa ajili ya kufanya sherehe hiyo vinapangwa |
PICHA ZAIDI YA HALI ILIVYO SASA KWENYE JENGO LA GHOROFA LILILOANGUKA KATIKATI YA JIJI, DAR
Ni
moja ya Kifaa pekee kilichokuwepo eneo hilo Trekta, likifukua kifusi ili
kuokoa watu wanaodaiwa kufukiwa na kifusi hicho.
Baadhi
ya watu waliwahi kufika kujaribu kutoa msaada bila mafanikio hapa
wakiwa wamekwama baada ya kukosa vifaa vya kutosha.
Wahindi nao walikuwapo kutoa msaada hapa wakilielekeza Trekta kusogea
mahala walipo wao wakihisi kuwa kuna mtu mahala hapo.
BEAKING NEEEEEWZZZZZZZZ!!!!! GHOROFA LIMEANGUKA MITAA YA ILIGANDI K/KOO
Mpaka
sasa watu watu 12 wameshapoteza maisha,limedondokea msikiti wa SHIA.
Mpaka sasa eneo la tukio
kuna mkuu wa mkoa wa Dar es salaam na meya,Mmiliki wa jengo hilo bado
hajajulikana.Ndani ya jengo hilo kulikuwa na watu wasio pungua 60
wakiendelea na ujenzi.Watu zaidi ya 14mpaka sasa wameshakimbizwa
hospitali. Tutaendelea kuwajulisha zaidi.
UZINDUZI WA TAWI LA YANGA MAREKANI
TUNAPENDA KUWATANGAZIA RASMI MASHABIKI, WADAU NA WAPENZI WOTE WA TIMU YETU YA SOCCER YOUNG AFRICANS SPORTS CLUB MLIOPO MAREKANI KUWA TUNAZINDUA RASMI TAWI LETU HAPA MAREKANI LITAKALO JULIKANA KAMA YOUNG AFRICANS FAMILY USA. TUNAOMBA UKIPATA TANGAZO HILI MWARIFU NA MWENZIO.
TAREHE: JUMAMOSI 03/30/2013
MAHALI: KILIMANJARO PASSION RESTAURANT
ADDRESS: 2310 PRICE AVENUE, WHEATON,MD 20902
MUDA: 4:00 PM
KWA MAWASILIANO:
ALEX KASSUWI : TEL :301 305 9685
YOUNG AFRICANS "DAIMA MBELE NYUMA MWIKO"
SHIRIKISHO LA FILAMU TANZANIA LAMSHUSHIA PONGEZI WEMA SEPETU..
SHIRIKISHO la Filamu Tanzania (TAFF)
limempongeza msanii wa kike Wema Sepetu kwa moyo wa upendo aliouonyesha
kwa msanii mwenzie Kajala Masanja kwa kumlipia faini ya sh. milioni 13
alizotozwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutokana na kupatikana na
hatia katika kesi ya utakatishaji fedha iliyokuwa inamkabili mahakamani
hapo
Akizungumza kwa niaba ya viongozi
wengine rais wa shirikisho hilo Simon Mwakifwamba alisema kuwa imani na
moyo wa upendo aliokuwa nao msanii Wema ndio uliomsukuma kumlipia
kiwango hicho cha fedha bila ya kujiuliza mara mbili kitendo hiko
kimeonyesha jinsi gani wanavyohitaji kushirikiana katika matatizo.
LEO NI IJUMAA KUU
INAPOFIKA
saa
tisa alasiri, siku kama ya leo, maarufu kama Ijumaa Kuu, katika nyumba
za
ibada za Kikristo, kimya hutanda, mishumaa huzimwa na kuashiria kuwa ni
siku ya
majonzi.
Ijumaa
Kuu ni siku ambayo Wakristo duniani kote hukumbuka mateso aliyoyapata
Yesu
baada ya kusulubishwa msalabani yapata zaidi ya miaka elfu mbili
iliyopita.
Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimeipa thamani siku hii kwa
kuitangaza
kuwa ya mapunziko.
Siku
hii huadhimishwa kwa ibada inayoambatana na kusoma mistari ya Biblia
inayoelezea undani wa matukio yaliyosababisha kusulubiwa kwa Yesu
Kristo.
FILAMU YA SISTER MARRY KUINGIA SOKONI MUDA WOWOTE.
Ray amesema kuwa filamu yake ya SISTER MARRY iliyozua kasheshe na viongozi wa kidini kutoka kanisa katoliki hivi karibuni haijazuiliwa kabisa bali ameambiwa arekebishe baadhi ya vipande katika filamu hiyo hivyo mashabiki wake wakae mkao wa kula filamu hiyo itaingia sokoni kila kitu kikikamilika. The film stars Vicent Kigosi(Ray), Irene Uwoya, Blandina Chagula(Johari) and Grace Mapunda.
CAG akabidhi Ripoti ya ukaguzi wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2011-2012 kwa Rais Kikwete.
Mdhibiti
na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) Bwana Ludovick Utouh
akikabidhi Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2011-2012
kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo.(picha
na Freddy Maro).
Thursday, March 28, 2013
Mwanafunzi wa Kidato cha IV Kibaha Sekondari akamatwa kwa kuhusishwa na wizi wa meno ya Tembo.
Kamanda
wa Polisi kanda Maalum Dar es Salaam DCP Suleiman Kova akiwa
maeshikilia baadhi ya vipande vya meno ya Tembo vilivyokamatwa hivi
karibuni katika eneo la Kimara Wilaya ya Kinondoni.
Kamanda
wa Polisi kanda Maalum Dar es Salaam DCP Suleiman Kova akifafanua kuwa
Jeshi la polisi limeweka mikakati ya mpango kazi ikiwa ni pamoja na
kushirikiana na vyombo mbalimbali vya ulinzi na usalama pamoja na kikosi
cha zimamoto ili kuhakikisha kuna udhibiti wa matukio ya uhalifu au
fujo.
Aidha
amesema jeshi hilo pia limefanikiwa kukamata bunduki mbili aina
tofauti, moja ikiwa ni Shotgun yenye namba AB 44736 na ya pili ni
Greener yenye namba 10883 pamoja na risasi 17.
Jeshi
la polisi kanda Maalum ya Dar es salaam limefanikiwa kukamata vipande
vya meno ya Tembo vipatavyo 13 ambavyo thamani yake haikufahamika mara
moja. Tukio hilo limetokea katika eneo la Kimara wilaya ya Kinondoni
ambapo askari walipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema.
Pamoja
na kukamatwa kwa vipande hivyo pia amekamatwa mtuhumiwa Christopher
Julius mwenye umri wa miaka 18, mwanafunzi wa Kidato cha Nne – Kibaha
sekondari.
Katika
hatua nyingine kupitia misako mikali inayoendelea Jeshi la polisi
limefanikiwa kukamata noti bandia 32 za shilingi elfu 10,000/= zenye
thamani ya shilingi 320,000/= za kitanzania.
Akizungumza
na vyombo vya habari Kamanda wa Polisi kanda Maalum Dar es Salaam DCP
Suleiman Kova ametoa tahadhari kwa wananchi kuwa makini hasa katika
kuelekea siku kuu ambapo watu wasio na nia njema wanapenyeza pesa bandia
kwa nia ya kujiongezea kipato binafsi.
Na.Mo
Blog Team
Nelson Mandela hospitalini tena
Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela
amelazwa tena hospitalini baada ya kuugua ugonjwa wa mapafu kwa mara
nyingine.
Taarifa kutoka kwa serikali ya nchi hiyo,
ilisema kuwa Mandela mwenye umri wa miaka 94 alilazwa hospitalini muda
mfupi kabla ya saa sita usiku.
Mandela alilazwa siku kumi na nane
hospitalini mwezi Disemba mwaka jana kupokea matibabu ya ugonjwa wa
mapafu na kibofu.
Anasifika sana kama baba wa taifa hilo kwa
kuongoza vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi.
Kadhalika Mandela alihudumu kama rais wa kwanza
mweusi Afrika Kusini tangu mwaka 1994 hadi mwaka 1999, ingawa hali yake
ya kiafya imezua wasiwasi kwa muda sasa.
Rais Jacob Zuma alimtumia taarifa ya kumpa pole
na kumtakia kupona Mandela
"tunawataka watu wa Afrika Kusini pamoja na
duniani kote kuwa watulivu na kumuombea Madiba na familia yake. Tuna
imani kuwa kikosi cha madaktari wanaomtibu Mandela watafanya kila hali
kuhakikisha anapona,'' alisema Zuma katika taarifa yake.
Mapema mwezi huu bwana Mandela alilazwa
hospitalini mjini Pretoria baada ya kufanyiwa ukaguzi wa kiafya.
Pengo: Polisi nchini wanafuga uhalifu
Dar es Salaam. Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam,
Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amelitupia lawama Jeshi la Polisi kwa
kile alichosema kwamba limeshindwa kuzuia vitendo vya uvunjifu wa amani
na mauaji ya watu wasiokuwa na hatia.
Kadhalika kiongozi huyo alihoji ulipofikia upepelezi wa mauaji ya Padri Evarist Mushi wa Zanzibar aliyepigwa risasi mwezi uliopita huku akisema, “Siwezi kusema naridhika au siridhiki lakini tulitegema kwamba polisi wangetegua kitendawili cha wauaji wa padri huyo.
MENEJA WA KAMPUNI YA NDEGE YA FASTJET ATIWA MBARONI
MENEJA wa
Wafanyakazi wa Ndani ya Ndege wa Kampuni ya Fastjet Emma Donovan,
alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala Dar es Salaam kujibu
shtaka linalomkabili la kutoa lugha ya matusi.
Emma (40) alipandishwa kizimbani jana na
kusomewa shtaka hilo na Wakili wa Serikali Nassoro Katuga, mbele ya
Hakimu Joyce Minde.
Katuga alidai Machi 19 mwaka huu Emma alimtolea lugha ya matusi Samson Itinde jambo ambalo ni kinyume cha sheria. Emma alikana shtaka hilo ambapo Katuga alidai upelelezi umekamilika na kuomba kupangiwa tarehe kwa usikilizwaji wa awali.
Hakimu Joyce alisema kuwa dhamana ya mshtakiwa iko wazi
lakini kwa kuzingatia vigezo vya dhamana vitakavyotolewa kwa kuwa
mshtakiwa ni raia wa kigeni.
Alitaja masharti ya dhamana kuwa
mshtakiwa anatakiwa kuwasilisha hati yake ya kusafiria au kutoa fedha
taslim sh milioni tano na pia awe na wadhamini wawili ambao ni
Watanzania.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Aprili 9 ili kupangwa tarehe
ya kuanza kwa usikilizwaji wa awali.
|
BREAKING NEWS. MBUNGE WA JIMBO LA CHAMBANI AFARIKI DUNIA.
Mbunge wa Chambani Salim Hemed Khamis (CUF),amefariki dunia muda mfupi uliopita katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili .Taratibu za kuusafirisha mwili kuelekea Pemba kwa mazishi zinafanyika.
jambotz8.blogspot.com INATOA POLE KWA FAMILIA, WABUNGE, NDUGU NA JAMAA WA SALIM HEMED KHAMIS
CHANZO: ITV
KIKWETE ASIMULIA ALIVYOIBA WALI JKT......!!!!
RAIS Jakaya Kikwete
amesimulia maisha yake ya jeshini, huku akikumbuka namna alivyokamatwa
na mkuu wa jiko (afande ubwabwa) akiiba wali. Rais Kikwete alitoa
ushuhuda huo wakati akifunga mafunzo maalumu ya uongozi kwa wabunge na
kuzindua mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria.
Hafla hiyo ilifanyika juzi katika Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kikosi cha 832 KJ, kilichopo Ruvu, Kibaha mkoani Pwani, ambapo viongozi mbalimbali walihudhuria.
Rais Kikwete aliwakumbusha vijana hao kwamba yeye ni miongoni mwa watu waliochukua mafunzo ya JKT kambini hapo akiwa katika Operesheni Tumaini mwaka 1972.
Rais Kikwete alisema katika mafunzo hayo alijengwa vizuri, ingawa hadi leo bado anakumbuka matukio mawili ya kufurahisha na kusikitisha akiwa kambini hapo.
Alisema tukio la kwanza ambalo hawezi kusahau ni pale alipokamatwa akiiba wali na tukio jingine ni kuhusu kifo cha askari mwenzao aliyefariki dunia baada ya kukanyagwa na trekta.
“Nawashukuru kwa kunialika katika shughuli hii, nimetembelea na kujionea miradi mbalimbali inayoendelea kufanywa hapa kambini.
“Wakati tukiwa kule nilikuwa naangalia kwa makini, hasa nilikuwa naangalia lile bweni letu, sisi tuliokuwa Kombania A mwaka ule, nimepakumbuka ingawa sasa pamekarabatiwa vizuri.
“Yapo matukio mawili ninayoyakumbuka siwezi kuyasahu hadi leo wakati nikiwa hapa kambini…(kicheko) jeshi si mchezo, nawaeleza haya mjue maisha ya jeshi hayana mzaha.
“Nakumbuka namna nilivyokamatwa na bwana ubwabwa nikiiba wali kule katika bwalo la chakula,” alisema Rais Kikwete huku wananchi na askari wanafunzi (kuruta) waliokuwapo wakiangua kicheko.
UTAJIRI WA WEMA SEPETU HUU HAPA...........!!!!
Wema Sepetu ni tajiri kiasi gani? Ni
ngumu kusema exactly mrembo huyu ana shilingi ngapi benki, lakini mambo
anayofanya yanatupa jibu la wazi kuwa, Wema ana mkwanja mrefu.
So hebu
tuangalie mangapi makubwa yaliyohusisha fedha nyingi aliyoyafanya
kuanzia mwezi June, 2012.1.
Thamani ya nyumba yake
Wema Sepetu aliwaacha hoi watu wengi baada ya kuonesha
nyumba yake mpya exclusively kwenye kipindi cha Take One cha Clouds
TV.
Alisema thamani ya nyumba yake hiyo ilifikia shilingi
milioni 400 na hiyo ni tofauti na karibu shilingi milioni 30 za
kuipamba ndani. Hiyo ilikuwa ni tarahe za mwanzo za mwezi June, 2012.
Sebule
Sehemu
ya nje ya nyumba
Uzinduzi wa filamu yake Superstar Katika historia ya Bongo Movies,
hakuna filamu iliyowahi kuwa na uzinduzi wa nguvu kama wa filamu ya
Wema ambayo hata hivyo haijawahi kutoka, Supastar. Katika uzinduzi
huyo, Wema alimdondosha muigizaji namba moja wa kike nchini Nigeria,
Omotola Jalade ambaye alimpeleka kwenye event iliyofanyika Giraffe
Hotel Ocean View ambako watu mbalimbali walikutana kubadilishana mawazo
na Omotola. Hiyo ilikuwa ni baada ya kushindwa kufika kwa wakati.
Awali
ulifanyika uzinduzi wa filamu hiyo yenye mastaa kibao akiwemo yeye
mwenyewe, TID, Shetta, Mwinyi Machozi, Chaz Baba, Barnaba na wengine
kwenye hoteli ya Hyatt Kilimanjaro ambako mastaa wote wa orodha A
nchini walihudhuria huku Shaa na Shilole wakiwa miongoni mwa wasanii
waliotumbuiza.
Rais Kikwete azindua Taarifa ya Utafiti wa Viashiria vya Ukimwi na Malaria Mwaka 2012.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akikata ukanda kuzindua rasmi taarifa ya utafiti
wa viashiria vya ukimwei na malaria mwaka 2012 leo Machi 27, 2013 katika
ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam. Kulia kwake ni Waziri Mkuu Mhe
Mizengo Pinda na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadiki.
Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiri Ukimwi (TACAIDS) Mama
Fatma Mrisho na
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Mhe William
Lukuvi.
Rais Jakaya Mrisho
Kikwete akinyanyua juu baada ya taarifa ya utafiti wa viashiria vya
ukimwei na malaria mwaka 2012 leo Machi 27, 2013 katika ukumbi wa
Karimjee jijini Dar es salaam. Kulia kwake ni Waziri Mkuu Mhe Mizengo
Pinda. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiri Ukimwi
(TACAIDS) Mama Fatma Mrisho.
MBUNGE SALIM HEMED HAMIS AANGUKA GHAFLA
Mbunge wa chambani (CUF) Visiwani zanzibar Salim
Hemed Hamisi ameanguka ghafla akiwa katika kikao cha kamati ya mambo ya
nje na ushirikiano wa kimataifa katika ofisi ndogo za bunge jijini Dar
es salaam wakati kamati hiyo ikiendelea na kikao chake
Mbunge
huyo ambaye siku za hivi karibuni ametoka nje ya nchi kwa matibabu ya
afya yake amefikwa na dhahama hiyo na kubebwa na baadhi ya wabunge kwa
kushirikiana na baadhi ya wandishi wa habari kutolewa nje ya chumba cha
mkutano na kupelekwa hospital ya taifa ya Mhimbili kwa uchunguzi na
matibabu zaidi.
Mwenyekiti
wa kamati ya bunge ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Edward
Lowasa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Wednesday, March 27, 2013
SIKU CHACHE BAADA YA KUFUNGA NDOA JACK WA CHUZ YADAIWA KAIBA MUME WA MTU
Kama utakuwa mfuatiliaji mzuri wa blog hii
kribuni tulikuletea habari juu ya Jack wa Chuz kufunga ndoa na kubadili
dini kwa habri zilizoko ni kwamba baada ya saa 48 tu Jack kufunga ndoa
ymekuja mapya kabisa baada ya dada Mariam Omary anayedai Jack Chuz
kamchukulia baba(Gardner Dibibi) watoto wake akiwa na mwanaye.
Mwanamke huyu mwenye jina la Marium
Omary inadaiwa kuwa na mahusiano na Gadner Dibibi kwa muda wa miaka
mitatu sasa na kufanikiwa kupata mt0to mmoja wa kiume.
Dada huyu ambae anishi Kigogo jijini
dar es salaam alisema siku ya tukio ya ndoa ya Gadner alimuaga kuwa
anasafiri anaenda Morogoro hivyo hatakuwepo dar lakin baada ya muda dada
huyu alipata taarifa kutoka kwa watu kuwa mumewe anafunga ndo na
mwanadada Jack wa Chuz
Dada huyu alialamika na kusema kuwa
Jack wa Chuz anajua kila kitu kuhusu yeye na Dibibi na kusema
“Hakuna asichokijua kati yangu na
Dibibi, kwa usalama wake Jack aniachie mume wangu,” alilalama mwanamke
huyo.
Baada
ya Jack kulizwa swala hili alisema hivi ‘’baba wa mtoto anayemjua ni
mama peke yake na isitoshe kuzaa naye isiwe sababu kwani yeye hakumuoa’’
Na Dibibi naye alikuwa na haya ya
kusema
“Alikuwa demu wangu na kuzaa mtoto
isiwe sababu. Hata hivyo, ukweli wa baba wa mtoto anayejua ni mama.
Sikumtolea mahari wala kumvalisha pete ‘so’ hana kizuizi na ndoa yangu,”
alisema jamaa huyo kisha akakata simu’’
KWA WALE WAPENDA TATOO ANGALIA MADHARA YAKE KWENYE MIILI YETU
Hii ni kwa wale wote wapenda kujichora miili
ya kwa inayojulikana kama tattoo
UJUMBE WA FIFA KUSIKILIZA WAGOMBEA TFF APRILI 16
SHIRIKISHO la Kimataifa la Mpira wa Miguu
(FIFA) ambalo lilisimamisha mchakato wa uchaguzi wa Shirikisho la Mpira
wa Miguu Tanzania (TFF) kutokana na baadhi ya wagombea kulalamika
kuenguliwa sasa litatuma ujumbe wake nchini katikati ya mwezi ujao.
Ujumbe huo ambao moja ya shughuli zake
kuwasikiliza wote walioenguliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF
na hawakuridhika na uamuzi huo, utakuwepo nchini Aprili 16 na 17 mwaka
huu.
Kwa mujibu wa barua ya
Katibu Mkuu wa FIFA, Jerome Valcke kwenda kwa Rais wa TFF, Leodegar
Tenga, kazi ya ujumbe huo ni kubaini tatizo lililopo na kutoa ripoti kwa
mamlaka zinazohusika ndani ya FIFA kwa ajili ya kutoa mwongozo.
Ujumbe huo utakutana na pande mbalimbali
zinazohusika wakiwemo wagombea, kamati za uchaguzi za TFF. Lakini pia
ujumbe huo unatarajia kumtembelea Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo, Dk. Fenella Mukangara pamoja na watendaji wake wizarani.
Uchaguzi wa viongozi wa TFF ulikuwa
ufanyike Februari 24 mwaka huu, lakini ukasimamishwa na FIFA baada ya
baadhi ya wagombea walioenguliwa kulalamika kuwa hawakutendewa haki na
wangependa shirikisho hilo liingilie kati.
‘Siri ya Kuuawa Zitto Yafichuka’ – Sio Kweli.
Katika
gazeti la Mtanzania toleo na. 7269 la Jumatano Machi 27, 2013 kuna
habari yenye kichwa chenye maneno
‘ SIRI YA KUUAWA ZITTO YAFICHUKA’ na
vichwa vidogo ‘yadaiwa ilipangwa anyweshwe sumu hotelini’ dk. Slaa
atajwa kumtuma Saanane kummaliza’. Habari hii imeniletea usumbufu mkubwa
kwani ndugu, jamaa, marafiki na wapiga kura wangu, wamejazwa na
wasiwasi mkubwa sana kwamba ninaweza kuuwawa. Napenda kusema yafuatayo:
Moja,
sijawahi katika maisha yangu yote kukutana na mtu anayeitwa Ben Saanane
na hivyo hicho kikao ambacho inasemekana nilikuwa naye na akajaribu
kunipa sumu hakijawahi kutokea. Imetajwa Hoteli ya Lunch Time ambayo sio
tu sijawahi kufika, pia hata siijui ipo wapi. Haijawahi kutokea mimi
kufanya kikao cha pamoja na Ben Saanane, Juliana Shonza na Mtela
Mwampamba. Hivyo habari iliyoandikwa ni ya kufikirika na hivyo naomba
mwandishi ahakikishe kuwa vyanzo vyake vya habari vimempa habari sahihi.
TIGO yazindua Ofa ya bei moja kupiga simu kwenda mitandao yote
Meneja
wa Chapa ya Tigo bw. William Mpinga akiongea na waandishi wa habari
wakati wa uzinduzi wa huduma ya kupiga simu kwenda mitandao yote ndani
ya nchi kwa bei moja na punguzo la 20% kupiga nje ya nchi, kushoto kwake
Mtaalam wa ofa za bidhaa za Tigo Bi.Jacqueline Nnunduma .
Mtaalam
wa ofa za bidhaa za Tigo Bi.Jacqueline Nnunduma akifafanua jambo kwa
waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma ya kupiga simu kwenda
mitandao yote ndani ya nchi kwa bei moja na punguzo la 20% kupiga nje ya
nchi.
Albam ya Justin Timberlake yauza kopi 968,000 katika wiki ya kwanza
Albam mpya ya
Justin Timberlake, “The 20/20 Experience” imekamata nafasi ya kwanza
kwenye Billboard 200 chart, kwa kuuza kopi 968,000 katika wiki yake ya
kwanza, kwa mujibu wa Nielsen SoundScan.
“20/20,” ilitoka March 19, na ndio albam aliyouza zaidi katika wiki ya kwanza. Albam yake ya mwaka 2006 “FutureSex/LoveSounds,” iliuza kopi 684,000 na ile ya kwanza aliyoitoa mwaka 2002, “Justified,” iliuza kopi 439,000.
Mauzo huzo hayo ya “20/20′s” ni makubwa zaidi tangu SoundScan ianze kuchukua data za mauzo ya albam mwaka 1991.
Albam ya kundi la zamani la Timberlake, ‘N Sync, “No Strings Attached” iliuza kopi milioni 2.42 katika wiki ya kwanza na kukamata na kuongoza chart ya Billboard 200, April 8, 2000.
“20/20,” ilitoka March 19, na ndio albam aliyouza zaidi katika wiki ya kwanza. Albam yake ya mwaka 2006 “FutureSex/LoveSounds,” iliuza kopi 684,000 na ile ya kwanza aliyoitoa mwaka 2002, “Justified,” iliuza kopi 439,000.
Mauzo huzo hayo ya “20/20′s” ni makubwa zaidi tangu SoundScan ianze kuchukua data za mauzo ya albam mwaka 1991.
Albam ya kundi la zamani la Timberlake, ‘N Sync, “No Strings Attached” iliuza kopi milioni 2.42 katika wiki ya kwanza na kukamata na kuongoza chart ya Billboard 200, April 8, 2000.
Dk Slaa awatuhumu Usalama wa Taifa
Dar es Salaam.
Kwa ufupi
“Chadema
ni chama makini na hakiwezi kuyumbishwa na mtu yoyote wala idara
yoyote inayotumiwa na baadhi ya watu ili kutaka kukizohofisha,” alisema
Dk Slaa ambaye mara kwa mara amekuwa akilalamika kuchezewa rafu.
Dar es Salaam. Katibu Mkuu
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa
ameanza kuisakama Idara ya Usalama wa Taifa kuwa wanatumia mbinu
mbalimbali kuwahujumu na kwamba mbinu zinazofanywa na idara hiyo ni
kueneza propaganda walizodai za uongo dhidi yao.
Akizungumza jana makao makuu cha chama hicho jijini Dar es Salaam, Dk Slaa alisema: “Tumezibaini mbinu zinazofanywa na Usalama wa Taifa kwa kutumiwa na CCM kueneza propaganda za uongo dhidi yao kwa lengo la kukichafua chama, lakini haziwezi kufanikiwa kwani tayari tumegundua mbinu zao.
ROSE NDAUKA: KAJALA AJIPANGE KUTIMIZA NDOTO ZAKE
Habari na saluti5
NYOTA
wa filamu, Rose Ndauka amemzungumzia msanii mwenzie wa filamu, Kajala
Masanja aliyeponea chupuchupu kwenda jela miaka mitano na kusema kuwa,
anachoamini ni kwamba sasa Kajala atajipanga na kuyafanya maisha yake
yaende kama alivyokusudia hatimaye kutimiza ndoto zake.Saluti5
ilizungumza na Rose ili kupata maoni yake juu ya kuachiwa huru kwa
Kajala aliyekuwa jela kwa muda mrefu, ambapo alisema kuwa kikubwa ni
kushukuru mungu kwa kuweza kwake kurudi tena uraini, lakini pia sasa ni
wakati wa kuzijenga upya ndoto zake.
“Binafsi, siwezi kujua
kwa sasa Kajala mwenyewe amepanga kitu gani juu ya maisha yake, lakini
ninaamini atafanya yale anayayowaza katika akili yake, hususan
kuhusiana na kuendeleza mipango yake ya kimaisha,” alisema Rose.
Subscribe to:
Posts (Atom)