Friday, March 29, 2013

JACK PENTZEL ALONGA KUHUSU KUOLEWA KWAKE

MSANII wa bongo movie 'star 'wa bongo asiyekauka vituko' Jackline Pentzel a.k.a Jack wa Chuzi ameibuka na kuwataka mashabiki wake kuamini ameolewa na hajakurupuka kufanya maamuzi hayo kwani ni jambo ambalo alikuwa akilifikiria kila wakati

Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni Jack alisema kuwa anawataka mashabiki kuamini na kutowasikiliza watu wengine wanaotoa maneno ya uzushi juu yake kuwa maamuzi ya kuolewa ameyapanga na ameolewa na mwanaume wake wa siku nyingi hivyo anaamini anachokifanya ni sahihi kwake


Alisema kuwa watambue mwanaume aliolewa naye si mume wa mtu bali ni mchumba wake wa muda mrefu na walikuwa wakiishi pamoja kbala ya kuoa na ndipo maamuzi ya kufunga ndoa yalipokuja kwa kutotaka kuendelea kufanya uzinifu wakati uwezo wa kufunga ndoa walikuwa wanao


"Mimi nawashangaa kwani kuolewa ni kitu gani cha ajabu mpaka watu wasiamini mimi kufunga ndoa nimeamua kuolewa kwa sababu nampenda mwanaume wangu na nilikuwa naishi naye kwa kalibu hivyo tunajuana vizuri sijakulupuka" alisema Pentzel


Akizungumzia sababu za kutotangaza harusi yake alisema ameamua kutofanya hivyo ili kuepusha maneno na vizuizi vya ndoa yake ambavyo vingeweza kuibuka na kupoteza mawazo ya mumewake huyo


Alisema kuwa hakutaka hali hiyo itokee ndio maana akaamua kufanya iwe siri na ya kushutika ili wambaya wake wakose nafasi ya kufanya jambo lolote baya na kwa sasa baada ya harusi hiyo ndio vikao kwa ajili ya kufanya sherehe hiyo vinapangwa

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...