Friday, July 17, 2015

WANAJESHI WANNE WANAMAJI WAUAWA MAREKANI

Rais wa Marekani Barack Obama

Mtu mwenye silaha amewaua askari wanne wa jeshi la wanamajiwa Marekani katika shambulio lililofanywa kwenye majengo mawili ya jeshi hilo katika mji wa Chattanooga, Tennessee.

Wanajeshi hao wote waliuawa katika jengo moja. Maafisa nchini humo wameyaita mauaji hayo kuwa ni Shambulio la ndani. 

Shirika la Upelelezi la Marekani FBI linalochunguza mauaji hayo, limesema halijajua bado kilichosababisha shambulio hilo.

SIMBA KUCHEZA NA AFC LEOPARDS, SIMBA DAY 2015

Afisa Mtendaji Mkuu wa EAG Group, Imani Kajula akiwa Pamoja na Rais wa Simba Sport Club, Evans Aveva, wakati wa uzinduzi wa Simba Day. 

Dima ya Simba Sports Club ya kuendeleza mabadiliko ndani ya Simba bado inaendelea kushika kasi, Katika kipindi cha miezi mitatu sasa, mmekuwa mashuhuda wa Simba inayolenga kuleta mapinduzi makubwa katika jinsi mpira unavyoendeshwa, kujali wanachama, wapenzi wake na kukuza vyanzo vya mapato.

Akizungumza wakati wa kutangaza rasmi Simba Week 2015 Rais wa Simba, Evans Aveva, alisema ‘’Kila mwaka timu yetu ya Simba imekuwa na utaratibu wa kuwa na siku maalum kwa ajili ya kufurahi, kuwatambulisha rasmi wachezaji, jezi za timu na kujiandaa kwa msimu mpya, siku hii imekuwa maarufu kama Simba Day.

FIFA KUZIFANYIA MABADILIKO BAADHI YA KANUNI

Makao makuu ya FIFA

Shirikisho la soka ulimwenguni FIFA lina mpango wa kuzifanyia marekebisho kanuni zake ili kuzibana nchi zinazowania kuandaa Kombe la Dunia, zisitumie mwanya wa misaada ya kifedha kwa nchi nyingine kama rushwa.

Kipengele kile kinachoziruhusu nchi zinazoshindania nafasi ya kuandaa Kombe la Dunia kusambaza pesa katika nchi nyingine huenda kikafutwa. 

Aidha FIFA inazitaka nchi zote zinazowania nafasi hiyo kuzingatia haki za binadamu na sheria za kazi wakati wote. Hivi sasa nchi zinazotupiwa jicho ni Urusi inayoandaa kombe la dunia mwaka 2018 na Qatar inayoandaa 2022. 

ura za kuamua nchi gani italiandaa Kombe la Dunia la mwaka 2026 zitapigwa mwaka 2017 huko Kuala Lumpur, Malaysia. Nchi zinazoiwania nafasi hiyo ni Marekani,Canada, Mexico na Colombia.

Tuesday, July 14, 2015

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 14, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

MICHUANO YA KAGAME KUANZA KUTIMUA VUMBI

Rais wa Rwanda Paul Kagame
Michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati jumamosi wiki hii inaanza kutimua vumbi mjini Dar es Salaam Tanzania huku jumla ya vilabu 13 vikishiriki.

Rais wa Rwanda Paul Kagame anatarajiwa kutoa kiasi cha dola elfu 60 za marekani kama zawadi kwa washindi. Kundi A itajumuisha timu za Yanga yaTanzania, Gor Mahia ya Kenya, Kmkm Zanzibar, Telecom ya Djibout na Khartoum- Sudani Kaskazini.

Kundi B - APR Rwanda, Al Shandy ya Sudan, LLB FC Burundi naHeegan Somalia.
Wakati kundi C - Azam ya Tanzania, Malakia ya Sudan Kusini, Adama ya Ethiopia na KCCA ya Uganda.

Hata hivyo mgawanyo wa zawadi kwa kila mshindi ni kwamba mshindi wa kwanza atajinyakulia dola elfu 30, wa pili dola elfu 20 na wa tatu dola elfu 10. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

Monday, July 13, 2015

NEC YATANGAZA MAJIMBO MAPYA 26 YA UCHAGUZI

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva (wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari wakati akitangaza majimbo mapya ya uchaguzi katika Ukumbi wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam leo.

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza majimbo 26 mapya ya uchaguzi ambayo yatakuwa na wagombea katika uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema kukata kwa majimbo hayo wamezingatia idadi ya watu pamoja na Jiografia katika majimbo mapya.

Amesema katika upande wa Zanzibar majimbo yamebaki kuwa 50 kama awali hiyo inatokana vigezo vilivyowekwa na tume hiyo.

Majimbo yaliongezwa ni Handeni Mjini, Nanyamba, Makambako, Butiama, Tarime Mjini, Tunduma, Msimbo, Kavu, Geita Mjini, Mafinga Mjini, Ushetu, Nzega Mjini, Kahama Mjini, Kondoa Mjini, Newala Mjini, Bunda Mjini, Mbulu Mjini, Ndanda, Madaba, Mbinga Mjini, Mbagala, Kibamba, Vwawa, Monongo, Mlimba, Pamoja na Uliambulu.

Jaji Lubuva amesema baadhi ya wabunge wamekuwa wakiingia katika Halmashauri mbili hiyo kuweka mipaka katika maeneo ili mbunge aweze kushiriki katika Halmashauri moja tu.

Amesema baadhi majimbo yamebadilishwa majina na kuendelea kuwepo kwa majimbo hayo kisheria.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JULAI 13, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

POLISI WANNE WAUAWA KATIKA SHAMBULIO

Mkuu wa polisi Ernest Mangu amethibitisha uvamizi huo
Maafisa wanne wa polisi na raia wawili wameuawa baada ya watu wasiojulikana kuvamia kituo cha polisi mjini Dar es salaam Tanzania.

Shambulizi hilo limetokea katika kituo cha polisi kilichoko Ukonga, viungani mwa jiji kuu la Dar es salaam. Polisi wanasema kuwa wavamizi hao walitekeleza shambulizi hilo la kuvizia usiku wa kuamkia leo.

Waliwafyatulia risasi maafisa wa polisi katika kituo hicho na kuua wanne.
Kwa mujibu na raia wanoishi karibu na kituo hicho,makabiliano ya risasi yalidumu kwa zaidi ya saa moja.
Uchunguzi unaendelea kujua nani aliyetekeleza shambulizi hilo
Mkuu wa polisi Ernest Mangu amethibitisha uvamizi huo akisema askari 4 na raia 3 wameaga dunia. Hadi sasa haijabainika iwapo kuna majeruhi.

Aidha amesema kuwa walipora handaki ya kituo hicho na kuiba bunduki za polisi na idadi ya risasi isiyojulikana. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

KAMBI YA JESHI YAPOROMOKA YAUA 23

Takriban wanajeshi 23 wa Urusi wameuawa karibu na mji wa Omsk ulioko Siberia baada ya jengo la kambi ya kijeshi kuporomoka.

Wanajeshi wengine 19 waliokolewa kutoka kwa vifusi vya jengo hilo.
Mwanajeshi mmoja aliyeokolewa ameileza runinga ya Urusi kwamba wanajeshi walikuwa wamelala wakati wa ajali hiyo.

Picha za televisheni zilionyesha sehemu ya jengo hilo la ghorofa nne likiwa limeharibika kabisa huku wanajeshi wakishirikiana kuondosha vifusi.

Mwandishi wa BBC Moscow amesema inadhaniwa kwamba ukarabati duni uliofanyika mwaka jana ndio uliosababisha kuporomoka kwa jengo hilo. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

MAN CITY YAKUBALI KUMUUZA STERLING KWA LIVERPOOL


Raheem Sterling
Klabu ya Manchester City ya Uingereza imekubaliana na wapinzani wao Liverpool dau la pauni milioni £49 kumsajili mshambulizi Raheem Sterling.
Uhamisho wa mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 20 sasa unategemea makubaliano baina yao na vipimo vya afya. Sterling alikuwa ameomba kundoka Anfield kabla ya klabu hiyo kukataa dau mbili za Man City mwezi Juni.

Mshambulizi huyo atakuwa mchezaji aliyegharimu pesa nyingi zaidi raia wa Uingereza baada yake kukatalia mbali mshahara wa pauni laki moja kwa juma kutoka Liverpool.
Sterling aliyejiunga na Liverpool akiwa na umri wa miaka 15 kutoka QPR mwezi februari mwaka wa 2010 yuko katika kandarasi inayokamilika mwaka wa 2017. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

VAN PERSIE ATUA UTURUKI


Van Persie akipokelewa Uturuki
Mashabiki wa manchester United wengi walijua kuwa Van Persie anaondoka kuelekea Fenabashe lakini kwa mtoto mdogo mwingereza wa miaka minne Louis Diamond hakufahamu kuwa kipenzi chake Robin Van Persie anaondoka mpaka pale alipoambiwa na wazazi wake kwamba mpachika magoli Robin alikuwa tayari kuelekea uturuki. 

Hivi sasa waturuki wameanzisha kampeni ya kuchangishana pesa ili mtoto huyo ambaye video yake imesambaa mitandaoni na kutizamwa na watu wengi aletwe Uturuki kumshuhudia mchezaji huyo. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

Friday, July 10, 2015

MAPINDUZI MENGINE YAANDALIWA BURUNDI

Rais Pierre Nkurunziza
Mmoja wa viongozi katika mapinduzi yaliyozimwa nchini Burundi hivi karibuni ya kumpindua Rais Piere Nkurunziza ameiambia BBC kuwa waasi wao wamekuwa wakiwapa mafunzo polisi na askari kwa ajili ya jaribio jingine la kumwondoa rais Pierre Nkurunziza.

Akiwa uhamishoni Generali Leornard Ngenda Kumana amekanusha kuwa walisaidia na mataifa ya nje. Wamekuwa wakimshutumu Rais Nkurunziza kuwa kusababisha vurugu kaati ya jamii ya wahutu na watutsi na kuwapa silaha wapiginaji wa vijana waoiunga mkono serikali ambao wanaonekana wengi ni kutoka jamii ya wahutu.

Zaidi ya watu laki moja wamekimbia nchi hiyo wakihofia vurugu wakati wa uchaguzi wa rais unaotarajiwa kufanyika wiki ijayo.

Wanaompinga wanasema hatua ya kugombea urais kwa muhula wa tatu kwa rais huyo ni kinyume cha katiba. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

KIKWETE: "NILIACHA KUANGALIA MPIRA ILI NISIONEKANE NINA MKOSI"


Raisi Kikwete akipeana mkono wa mchezaji wa zamani wa Real Madrid walipoitembelea Tanzania
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amesema aliacha kwenda uwanjani kuiangalia timu ya taifa Stars kwa kuwa alionekana kuitia mkosi wa kufungwa timu hiyo kila ilipocheza.

Akiongea wakati wa kuvunja bunge na kuwaaga wabunge, Rais Kikwete alisema zamani alihudhuria sana mechi za Stars na baada ya kuonaa inafungwa mara kwa mara, aliamua kuacha kwenda uwanjani .

“Mwanzoni nilikuwa navaa hadi jezi kuishangilia timu yetu ilipokuwa inafanya vizuri, tulipoanza kufungwa fungwa wakasema mzee unaitia timu mkosi, nikaamua kuacha”, alisema Rais Kikwete huku akicheka katika hali ya mzaha.

Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

FIFA YATAJA VIWANGO VYA UBORA, TANZANIA YASHUKA

Tanzania na Uganda zimeshuka katika viwango ya FIFA vilivyotolewa Alhamis huku Kenya, Sudan na Rwanda zikipanda.

Uganda, ambayo ilikuwa nafasi ya 71, imeshuka nafasi mbili na sasa ni ya 73 wakati Tanzania, imeshuka nafasi 12 na sasa ni ya 139.

Licha ya kushuka, Uganda, ambayo hivi karibuni imeitoa Tanzania katika kugombania nafasi ya kucheza fainali za CHAN mwakani nchini Rwanda, ndio nchi iliyo juu katika viwango vya FIFA kwa nchi za Afrika ya Mashariki.

Kushuka kwa Tanzania kunatokana na kufungwa na Uganda 4-1 katika michuano ya CHAN na kufungwa na Misri 3-0 katika mechi ya kwanza ya kugombania kufuzu kucheza fainali za AFCON.
Kenya imepanda nafasi saba na sasa ni ya 116 katika viwango hivyo ya Dunia. Rwanda ipo nafasi ya 78, ikipanda nafasi 16 wakati Sudan ikiwa nafasi ya 90, ikipanda nafasi 18. Burkina Faso (72), Botswana (120) na Comoros (187).

Algeria ndio timu inayoongoza katika viwango vya FIFA kwa Afrika ikiwa nafasi ya 19. Timu ya Agentina, licha ya kufungwa na Chile katika fainali za Copa America, imepanda na kuwa timu ya kwanza katika viwango va FIFA, ikiitoa Ujerumani. Tano bora za viwango vya FIFA ni Argentina, Germany, Belgium, Colombia na Uholanzi.

Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

Monday, July 06, 2015

RUTO "KENYA HAITARUHUSU NDOA ZA JINSIA MOJA"

Naibu rais wa Kenya Mh. William Ruto ameonya kuwa ndoa za jinsia moja ni haramu na kuwa hazitawahi kuruhusiwa nchini humo.

Ruto amechukua msimamo huo mkali siku chache tu kabla ya ziara wa Marekani Barrack Obama nchini Kenya.

Friday, June 26, 2015

KAFULILA AKOMALIA MABEHEWA FEKI

Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila.

MBUNGE wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR Mageuzi) ameitaka Serikali kuwasilisha bungeni taarifa ya kashfa ya ununuzi wa mabehewa feki katika Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) na kusababisha hasara ya Sh bilioni 230. 

Baada ya kipindi cha maswali na majibu bungeni jana, mbunge huyo alisimama kuomba muongoza wa Spika kwamba kutokana na unyeti wa jambo hilo, ikiwa ni pamoja na madai kwamba Kampuni iliyopewa zabuni ya kuagiza mabehewa hayo haikuwa na uwezo huo, kwa nini suala hilo lisipelekwe bungeni kujadiliwa.

WATOTO WALIWA NA FISI

Watoto wawili wenye umri wa kati ya miaka miwili na mitano wameuawa na fisi katika Kijiji cha Mnkola, Kata ya Ibihwa wilayani Bahi Mkoa wa Dodoma katika matukio mawili tofauti.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Teya Kata ya Ilindi wilayani hapa, Paul Mwaja alisema kuwa watoto hao wameuawa katika matukio mawili ndani ya kipindi cha wiki moja.

Mwaja alisema tukio la kwanza lilitokea juzi ambapo mtoto mmoja wa kiume mwenye aliuawa na fisi wakati akiwa na wenzie wawili wamelala.

AL-SHABAAB YASHAMBULIA KITUO CHA AMISOM

Kituo cha kijeshi cha wanajeshi wa kimatifa wa kulinda amani nchini Somalia Amisom. 

Takriban watu 30 wamepoteza maisha yao baada ya shambulizi la kigaidi katika kituo cha kijeshi cha wanajeshi wa kimatifa wa kulinda amani nchini Somalia Amisom.

Walioshuhudia wanasema kuwa mlipuaji wa kujitolea mhanga aliendesha gari lake moja kwa moja hadi kwenye lango kuu la kituo hicho .

Kituo hicho kiko katika eneo la Leego, barabara kuu inayounganisha mji mku wa Mogadishu na Baidoa.

BURUNDI KUENDELEA NA RATIBA YA UCHAGUZI

Gervais Rufyikiri aliyekuwa makamu wa rais wa Burundi amekimbilia Ubelgiji. 

Serikali ya Burundi imesema haitashiriki katika mazungumzo yaliyodhaminiwa na Umoja wa Mataifa yakilenga kupunguza hali ya uhasama uliopo kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wenye utata.

MKWASA AWAOMBA MASHABIKI WA SIMBA WASIMZOMEE

Kocha wa timu ya soka ya Taifa ya Taifa Stars, Charles Mkwasa.

KOCHA mpya wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa amewataka mashabiki wa Simba kutomzomea pindi watakapomuona kwenye mazoezi au mechi, kwa vile atakuwa pale kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya wachezaji wake wa timu ya taifa. 

Akizungumza Dar es Salaam juzi, Mkwasa alisema mashabiki wanatakiwa kufahamu kuwa yeye ni kocha wa taifa, hivyo atakuwa akitembelea katika mechi za timu mbalimbali kuangalia wachezaji na maendeleo ya wale wanaocheza timu ya taifa.

“Mashabiki wa Simba mnaponiona kwenye mechi zenu msinikimbize kwa mawe mkadhani kuwa nimekuja kwa ajili ya Yanga, nitakuwa na utaratibu wa kutembelea timu kuangalia wachezaji, mnajua kazi ya kocha wa taifa ndio hiyo,” alisema Mkwasa ambaye pia ni Kocha Msaidizi wa Yanga.

TAMBWE AIPANIA KAGAME

Amissi Tambwe

MSHAMBULIAJI wa Yanga, Amissi Tambwe amesema anategemea kufanya vizuri zaidi katika michuano ijayo ya Kagame kuisaidia timu kuchukua taji katika michuano hiyo itakayofanyika nchini kuanzia mwezi ujao. 

Tambwe, ambaye aliwahi kufanya vizuri katika michuano hiyo iliyofanyika Sudan miaka miwili iliyopita kwa kuibuka mfungaji bora, aliliambia gazeti hili kuwa anajipanga kufanya vizuri zaidi.

Mchezaji huyo aliibuliwa na Simba katika michuano hiyo wakati akiichezea Vital’O ya Burundi iliyochukua ubingwa wakati huo, kutokana na kuisaidia timu yake kwa kiasi kikubwa na kufanya vizuri.

ENGLAND YATETEA WACHEZAJI CHIPUKIZI

Timu ya England U21 katika moja ya michezo yao ya michuano ya Ulaya

England imefanya uamuzi sahihi kuwaondoa katika michuano ya ubingwa wa Ulaya kwa wachezaji wa umri chini ya miaka 21, baadhi ya wachezaji wake ambao wanacheza ligi kuu ya nchi hiyo, amesema mkurugenzi wa chama cha soka wa maendeleo ya wachezaji Dan Ashworth.

Timu ya England chini ya kocha Gareth Southgate ilifuzu kucheza hatua ya makundi kwa kwenda Jamhuri ya Czech. "Tulifanya uamuzi na nautetea ," Ashworth amemwambia mwandishi mwandamizi wa BBC wa habari za mpira wa miguu Ian Dennis. 

"Timu za vijana zipo kusaidia kuwakuza wachezaji na kuwapa uzoefu kuingia katika timu ya wakubwa." Mchezaji wa ushambuliaji wa Liverpool Raheem Sterling, kiungo wa Everton Ross Barkley, viungo wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain na Jack Wilshere na mlinzi wa Manchester United Phil Jones ni miongoni mwa wachezaji waliokuwa wakihitajika katika timu hiyo, lakini hawakuitwa.

England, ambayo ilikuwa na wachezaji wa ligi kuu, akiwemo mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane, mlinzi wa Everton John Stones na mshambuliaji mpya wa Liverpool Danny Ings, ilipoteza kwa Ureno 1-0 , wakaifunga Sweden kwa idadi kama hiyo lakini ilipoteza 3-1 kwa Italia.

Wednesday, June 24, 2015

WAZIRI GHASIA, KAFULILA WATOFAUTIANA BUNGENI

Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila 

Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Hawa Ghasia jana walitofautiana bungeni kuhusu tuhuma za ubadhirifu wa fedha zinazomkabili Mkuu wa Wilaya ya Uvinza, Hadija Nyembo.

Tukio hilo lilitokea baada ya swali la nyongeza la mbunge huyo, aliyetaka kujua msimamo wa serikali kuhusu Nyembo aliyedai kutoa kauli ya kutaka Wabembe waende kwao Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) iliyosababaisha Wabembe kukamatwa na kupelekwa ubalozini, ambapo ubalozi wa DRC , uliwakataa na kusababisha wanyanyasike kwa karibu wiki mbili. 

Pia Mbunge huyo alidai Mkuu huyo wa Wilaya aliondolewa wilayani Chato akihusishwa na ufisadi wa mbolea yenye thamani ya Sh bilioni 1.5 na kwamba sasa ana kesi katika Mahakama ya Wilaya ya Chato, hivyo serikali haioni aibu kuwa na Mkuu wa Wilaya wa aina hiyo, ambaye anashitakiwa na serikali yenyewe.

IS YAPATA WAFUASI WAPYA WA KANDA YAO

Mpiganaji wa IS

Kundi la kigaidi la wanamgambo wa kiislam, maarufu kama Islamic State limekubali ombi na ahadi ya wanamgambo wa kutoka kusini mashariki mwa Asia na Ulaya kusini magharibi katika maeneo ya Chechnya and Dagestan.

Hii ni mara ya kwanza kwa kundi hilo la IS kukaribisha rasmi kundi la wanajihadi kutoka katika kanda yao kuingia katika shirika lake. 

Na hii inaelezwa kwamba imekuja baada ya Vyombo vya habari vinavyotangaza kwa lugha ya lugha ya Kirusi mwishoni mwa wiki iliyopita, kurushwa kwa kipande cha video kinachomuonesha kiongozi mkuu wa kijeshi kutoka Chechnya akiapa na kuahidi kujitoa sadaka na kuwa kuwa mtii kwa IS.

Taarifa za awali zinaeleza kwamba kundi kubwa la kigaidi lenye kujitoa muhanga la Chechnya lilikuwa likipinga harakati za Is.

MTUNZI WA FILAMU YA TITANIC AFARIKI DUNIA

James Horner, enzi za uhai wake.

James Horner mtunzi nguli wa eneo maarufu kwa watu maarufu la Hollywood ambaye aliandika na kushinda katika tuzo za Oscar juu ya filamu maarufu ulimwenguni ya Titanic, amefariki dunia mjini California kutokana na ajali ya ndege akiwa na umri wa miaka 61. 

James alipata mafunzo ya urushaji wa ndege, inaarifiwa alikuwa peke yake wakati alipopata ajali hiyo, na ndege binafsi ndogo ambayo alipata nayo ajali eneo la Kusini mwa Santa Barbara mwanzoni mwa wiki hii.

Mwandishi huyu na mtunzi wa tungo mbali mbali ametia mkono wake katika kazi tatu tofauti za filamu za msanii James Cameron, pamoja na filamu ya A Beautiful Mind, Braveheart, Troy na ile ya Apollo 13.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...